IMEANDIKWA NA : EDGAR MBOGO
#1. Kilikuwa kipindi cha ukoloni karne ya 15 katika ngome kongwe ya mfalme MWAMAKUNGE ilikuwa ni ngome iliyoogopeka kwa uendeshaji wa mfalme huyo kwani alikuwa katili kupita kiasi aliuwa watu na kuteka wakoloni kutoka ngome nyingine basi alijulikana mno na kuogopeka kipindi hicho kwani alikuwa na vijana wachapakazi na waliobobea kwenye mapambano na waioiva kisawasawa. Wafalme wenzake walikuwa wakija kununua watumwa kutoka kwake basi alitokea mfalme alie taka watumwa kazaa wenda kusaidia katika kijiji chake kwani kulikosa msaada basi ilimbidi aje kuomba msaaha kwa mfalme MWAMAKUNGE katiriiiii lao basi ilimpasa mfalme MGAZA kuja kuomba iliii aweze kumpa msahada wa watumwa wachache.
Ilikuwa asubui na mapema ndipo vijakazi wa mfame MWAMAKUNGE walipoona jahazi kwa mbali zikija kwenye eneo lao basi walipiga kengeree kuashiria kuwa makini kwa kila mtu aliyepo maeneo hayo au kwenye ngome hiyo basi vijana walijificha na kutazama msafara huo mpaka ulipofika.
Ulipofika mfalme MGAZA alishuka huku akiwa na mlinzi wake na ndipo alipoo omba akutanishwe na mfalme MWAMAKUNGE nae alijitambulisha na vijana walichomoka na kufikisha habari kwa mfalme wao na ndipo alipofika nae alipooo mwona mfalme MGAZA alimfahamu mara moja na aliruhusu vijana kuingia ndani ya ngome.
Basi alipofika kwa mfalme MWAMAKUNGE aliongea nae kuhusu msahada aliokuwa akiitaji kutoka kwenye falme yake.
MWAMAKUGE" karibu sana hapa nyumbani vipi kurikoni mbona asubui mnooo lete habari za hapa na pale huko utokako"
MGAZA "mmmmmh huku nitokako hali si shwari kwani naitaji msahada wako kwa garama zote utakazo"
MWAMAKUNGE "kitu gani hicho nijuze nami nitakusaidia wala usiwe na shaka"
MGAZA "haaah shida yangu ni kuniongezea watumwa wapatao 500 japo nikaongeze hata nguvu ya utenda kazi kwani vitu huko vimesimama kukosa watenda kazi"
MWAMAKUNGE "hooooh sawa lakini siunajua kuwa huwa natoa kwa pesa basi nikatie mafungu yangu nihamlishe wakuleteee huondoke mapema"
Walikubaliana na ndipo mfalme MWAMAKUNGE alipo wahamuru vijakazi wake wawa danganye watumwa kuwa wanarudishwa kwao.
Basi walifanya kama alivyooo sema mfalme MWAMAKUNGE huku wafalme hao wakigawana walicho kubaliana pembezoni kidogo huku wakielekezana
Ni njisi gani watawaingia kiurahisi, na kuamini wanarudishwa kwao bali
walikuwa wakiuzwa nakupelekwa sehemu nyingine, yote hayo hawakujua kwani kila
mtumwa alitoa tabasamu zuri, huku akiwaza kuonana na ndugu zake toka walipo
hachana muda mrefu, pindi walipo tekwa na ufalme wa MWAMAKUNGE katili lao.
Mfalme MGAZA alimpatia pesa zenye dhamani ya watumwa aliopewa, na huku kwa
urafiki wao mfalme MWAMAKUNGE alimpa watumwa wengine kidogo, kuonesha urafiki
wao huku akimwonesha kwenye majahazi waliokuwa wakipanda watumwa hao.
Basi mfalme MWAMAKUNGE ndipo alipo muaga mfalme mwenzake, kwa safari yake ya
kurudi kwenye ngome yake, na ndipo mfalme MGAZA ali amuru vijakazi wake waanze
safari mara moja, na safari ilianza kwa kasi msana, huku watumwa wakitizama
ngome ya mfalme MWAMAKUNGE, kuiacha na kufurahi sana, huku wengine wakishusha
pumzi nzito kwa uchovu wa kazi walizokuwa wakifanya, na mateso makubwa ya siku
zote, awakujua waendako, pia hawakujuwa kama kule wanako kwenda, ni kazi kama
walikotoka, hayo yote hawa kujua, laiti wangelijua waendako ndiko kuna mateso
zaidi, wangeli panga njia ya kutoroka pindi safari hiyo ilipokuwa ikishika
kasi baharini.
Watumwa wote waliamini ya kuwa nanarudi kwao, basi kila nyimbo zilipigwa ndani
ya majahazi hayo, waliotumia kusafilia huku furaha ikizidi na kutaamani kupaaa
ndani ya dakika chache tu wafike.
MGAZA mfalme alimuamuru kjakazi wake mmoja ajurikanae kama "YOROBI" kuangalia
wamebakiza kilomita ngapi kufika kwenye ngome yao nae alifanya haraka huku
akionesha juhudi zidi ya hamri aliyopewa na mfalme wake alitizama na ndipo
alipotamka na kusema.
YOROBI"mkuuuu wangu tumebakiza kilomita chache tu kwani hapa tulipo ni robo
tatu ya sehemu tuliyotoka matumaini ya kufika mapema nyumbani yapoooo"
MGAZA "Okey sawa yorobi nimekuelewa basi waambie vijana wenzako juuu ya
kuchochea vizuri hizo jahazi tuwahi kufika sawa"
YOROBI "sawaaa mfalme nafanya hivyo mara moja wala usijariiii mkuuu wangu"
yorobi aliamlisha vijana wenzake na ndipo walipotia juhudi kubwa kwa tamko
alilosema mfalme wao MGAZA basi ilimbidi yorobi awe msitali wa mbele
kuhakikisha hiyo shughuri ya kufanya vyombo vitembee haraka ilikuwa yake.
Kasi ilipokuwa kubwa basi vijakazi wote walianza kuchoka na ndipo hakiba ya
chakula ikaagizwa kwani kulukuwa na mikate na soda ili kufanya mwili uwe na
nguvu na kuendelea na kazi.
ITAENDELEA
0 Comments