Kesho yake Patrick alitoka asubuhi sana na baada ya muda akarudi na daktari ndio hapo Tusa akaona kuwa kazi yake itaanza, Tusa akawa analia pale ambapo aliitwa.
Akapelekwa kwenye chumba kingine humo ndani, akaambiwa alale kwenye kitanda ili afanyiwe ile operesheni ndogo ya kutolewa mimba, Tusa akagoma ikabidi yule na daktari na Patrick wamfanyie kinguvu.
Wakatumia nguvu kumlaza Tusa kitandani, akafungwa kamba mikono na miguu yaani kila mguu upande wake na mikono hivyohivyo akiwa amelazwa chali.
Yule daktari alifanya kazi yake bila hata ya huruma na Tusa akapata maumivu makali sana kwani mimba yake ilikuwa kubwa kubwa.
Tusa alipiga kelele na kulia hadi akazimia.
Hata alipozinduka Tusa aliendelea kulia akiyajutia maisha yake.
PATRICK: Pole sana Tusa ila sikuwa na jinsi zaidi ya kufanya vile.
Tusa alikuwa analia tu, hakuona raha kabisa ingawa Patrick alikuwa akimuongelesha vizuri kama vile ni mtu mwema.
Tusa alitamani kufa, alikuwa akimuomba Mungu tu amchukue ili apumzike na yale mateso anayoyapata kwa Patrick.
Baada ya siku mbili kabla hata Tusa kupona vizuri, Patrick alikuwa akimuingilia Tusa kimwili kwa kasi ya ajabu ili tu kuhakikisha kuwa Tusa anapata mimba nyingine.
Siku zote Tusa alikuwa akilia na kujutia maisha yake.
Sele alirudi kwao Mwanza ambako walimzoea kwa jina lake la kuzaliwa la Sulemani, ambapo alipofika mjini alisikia wengine wakiitwa Selemani na kufupishwa majina na kuitwa Sele, akaona kuwa akifupisha jina lake la Sulemani na kuitwa Sule haitanoga na ndiomana akaamua kujiita Sele na watu wote mjini wakamjua kama Sele ila nyumbani kwao kabisa walimzoea kama Sulemani.
Mama yake bi.Marium alisikitika sana kumuona mwanae jinsi alivyokonda, kwakweli alimuhurumia.
MARIUM: Jamani mwanangu nini kilikupata huko mjini?
SELE: Nilitekwa mama.
MARIUM: Pole sana mwanangu, kumbe huko kuna utekaji loh! Halafu ulisema utaniletea mkamwana wangu, yukn wapi?
SELE: Mama, wee acha tu. Yani yaliyonipata dah!! Siku nikikaa na kutuliza akili yangu nitakusimulia vizuri mama.
MARIUM: Pole sana mwanangu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
SELE: Usijari mama, haya ni mapito tu ya dunia.
Marium akaenda kumwambia mdogo wake kuwa mwanae amerudi, kwakweli Deborah akafurahi sana.
MARIUM: Ila amekonda huyo, huwezi amini kama ndio yule Sulemani tuliyemzoea. Mwenyewe anajiita Sele siku hizi.
DEBORAH: Kumbe anajiita Sele, vijana bhana ila hilo jina linaendana na jina lake halafu linapendeza tu. Mwambie aje na huku basi.
MARIUM: Atakuja tu, nimemwambia akae kae kidogo nyumbani arudishe mwili.
DEBORAH: Basi nitakuja mimi dada, tena ikiwezekana aje akae huku si unajua mi nipo mwenyewe tena! Hakuna hata mtu wa kukaa nae.
MARIUM: Basi itakuwa vyema, uje umshawishi mwenyewe kuja huku.
DEBORAH: Hawezi kukataa bhana, sema rafiki yake kipenzi Patrick hayupo nadhani atakuwa amemkumbuka sana.
MARIUM: Na huyo Patrick atarudi lini?
DEBORAH: Mwenzangu hata simuelewi, kila siku nitakuja nitakuja hadi leo kimya.
MARIUM: Tumuombee mema tu mdogo wangu, natumaini atarudi.
Walimkumbuka Patrick walipomuongelea Sele, maana Patrick na Sele licha ya kuwa ndugu walikuwa ni marafiki waliokaribu sana. Na walipatana kupita kiasi kipindi wapo wote huko Mwanza.
Maiko akiwa na Patrick kwenye mipango yao.
MAIKO: Sasa Tusa yupo mikononi mwetu ila ni binti mrembo sana, nimeona picha zenu za harusi kwakweli pesa yetu imeenda kihalali.
PATRICK: Huwa sikosei kabisa katika kuchagua mimi, nachagua vilivyo bomba.
MAIKO: Nakuaminia Patrick, ila kuna kazi moja kubwa sana nataka ukaifanye wewe.
PATRICK: Kazi gani hiyo?
MAIKO: Ni kazi ya khatari halafu inahitaji tahadhari kubwa sana. Najua wewe utaiweza.
PATRICK: Mmh! Itachukua siku ngapi?
MAIKO: Kama siku tatu tu, vijana wangu watakuelekeza.
PATRICK: Mke wangu nitamuacha na nani? Si unajua kuwa ndoa yangu bado ni changa!
MAIKO: Naelewa Patrick, usijali kuhusu mkeo. Mimi nipo na nitamlinda, atakuwa salama kabisa. Wala usiwe na shaka.
PATRICK: Sawa nakuamini.
Patrick akajipanga kwaajili ya kufanya kazi aliyotumwa, kazi hiyo ilitakiwa kufanywa kwenye mkoa wa Morogoro.
Walifika Morogoro, Patrick akiwa na vijana watatu wa Maiko.
Patrick alipotajiwa kazi yenyewe alitaka kukataa kabisa kuifanya ila akatishiwa kuwa ameshakula kiapo kwahiyo kukataa kwake kutahatarisha maisha yake.
Patrick na kundi lake wakajiandaa kuifanye hiyo kazi hatari.
Patrick na kundi lake wakajiandaa kuifanya hiyo kazi hatari.
Kazi yenyewe ilikuwa ni kumteka mzee mmoja mwenye upara aliyeita Ayubu, mzee huyu alikuwa ni mlevi na alisifika kwa ulevi wake ila alikuwa ni mtu makini sana.
Wakamtumia Patrick kuweza kumshawishi mzee huyo ili afatane nae na wakammalize wanapopajua wao, kwavile Patrick alikuwa ni mtu aliyesoma na mwenye muonekano wa ukarimu na upole, ukimuona huwezi kumfikiria kama anaweza kutenda jambo lolote baya.
Patrick akatumia kama siku mbili kumzoea mzee huyo kwenye duka la pombe.
Tusa akiwa ndani ametulia kwani hakuweza kwenda popote kwavile alifungiwa ndani na Patrick, alishangaa siku nzima imepita bila ya Patrick kurudi.
Tusa akajiuliza kuwa Patrick yuko wapi ila hakuwa na jibu wala hakuwa na wa kumuuliza, kwa upande mwingine alishukuru kwa kutokumuona Patrick kwani alikuwa ni mateso mbele ya macho yake.
Siku ya pili jioni tangia Patrick aondoke, Tusa akasikia mlango ukifunguliwa naye akajua kwavyovyote vile atakuwa ni Patrick tu ila ukweli ni kwamba hakuwa Patrick bali ni Maiko.
Maiko aliingia hadi sebleni na kuita 'Tusa'
kwavile Tusa alijua ni Patrick, akaitikia tu kule kule jikoni alipokuwa. Maiko akamfata Tusa hadi jikoni, Tusa akashtuka kuona sura ngeni ambayo hajawahi kuiona kabisa.
MAIKO: Mbona umeshtuka Tusa?
TUSA: Kwasababu sikujui.
MAIKO: Usiwe na wasiwasi, mimi naitwa Maiko ni kama baba mkwe wako. Njoo basi sebleni tuzungumze.
Tusa akatoka jikoni na kumfata Maiko pale sebleni, kwa upande mwingine Tusa alihisi kuwa labda ukombozi wake umefika.
TUSA: Abee.
MAIKO: Usiniogope Tusa, Patrick ni kama kijana wangu hata mahari yako nimemchangia.
Tusa alikuwa anakodoa mimacho tu, wala hakujua cha kujitetea.
MAIKO: Nimekuja tu kukusalimia na kujua unaendeleaje, vipi hali yako lakini?
TUSA: Niko salama, je Patrick yuko wapi?
MAIKO: Patrick ameenda kuchukua mzigo Nairobi, kwahiyo usijari.
TUSA: Atarudi lini?
MAIKO: Siku mbili tu zimepita ndio umemkumbuka hivyo!
TUSA: Hapana, nimeuliza tu.
Muda wote Maiko alikuwa akimuangalia Tusa kwa macho makali sana, macho hayo yalimuogopesha sana Tusa kiasi cha kuingiwa na uoga.
Maiko kuona vile kuwa Tusa anaogopa akaamua kuaga.
MAIKO: Kesho nitakuja tena kukuangalia kwahiyo usijari.
TUSA: Sawa nashukuru.
Maiko akainuka na kutoka, akafunga milango kama ambavyo aliikuta, kwahiyo Tusa akafungiwa ndani vile vile kama kawaida.
Maiko akiwa anaelekea nyumbani kwake sura ya Tusa ilimkaa kichwani bila kutoka, mara akapigiwa simu na Patrick.
PATRICK: Nadhani hii kazi itachukua kama siku tano na sio tatu tena, maana huyu mzee ni mtata sana.
MAIKO: Hakuna tatizo, nyie fanyeni kazi tu.
Maiko alifurahi kusikia hivyo ili na yeye apate wasaa mzuri wa kuzungumza na Tusa.
Kama ambavyo Deborah alihitaji, alimuomba Sele na kwenda kuishi nae nyumbani kwake.
SELE: Nimemkumbuka sana Patrick, hivi yuko wapi?
DEBORAH: Yupo huko kwenye miji ya watu, amepata kazi huko. Na yeye amekukumbuka sana.
SELE: Dah! Bora arudi anifanyie na mimi mpango wa kazi.
DEBORAH: Hilo ondoa shaka, Patrick na wewe mmh!! Lazima atakufanyia tu.
SELE: Ndio mamdogo najua Patrick hawezi kunitupa mimi. Nikikumbuka wakati tuko wadogo ilikuwa raha sana.
DEBORAH: Utoto raha, hata mimi namtamani Patrick wangu arudi utoto ili nikae nae muda wote ila ujana ukifikia mara kutafuta kazi mara kuoa ndio kunikimbia kabisa hapo.
SELE: Hivi Patrick ana mchumba mama?
DEBORAH: Awe nae wapi? Angekuwa nae angeniambia, Patrick anatafuta maisha kwanza si unajua wanawake wanavyofilisi mwanangu.
SELE: Kweli kabisa, ila lazima atakuwa nae wa kuzugia. Mmh ila Patrick na mambo ya mademu yuko mbali nayo kabisa, labda kama atampatia huko kazini.
DEBORAH: Hata kutongoza kwenyewe mwanangu yule hawezi.
SELE: Hahaha, mamdogo nawe loh!
Sele alitamani sana kumuona nduguye Patrick, alikuwa amemkumbuka sana.
Alikuwa akipiga stori nyingi na mamake mdogo za kumuhusu Patrick.
Sele alikuwa anaishi na Deborah kama ambavyo alizoea ila kwasasa hakuwepo Patrick, alingoja zipite siku mbili tatu ili aanze kuzunguka mitaani na kuwasalimia vijana wenzie aliowaacha.
Patrick alitumia lugha nzuri sana kumshawishi mzee Ayubu ili aweze kufatana nae.
PATRICK: Mzee kuna bia mpya imezinduliwa ila tulikuwa tunahitaji watu wa kuonja na kwavile nimekuona mzee wangu hapa ni mkarimu nimependelea uwe mmoja wapo kati ya watu watakaoionja na kutuambia ladha yake.
AYUBU: Hayo ndio mambo ninayopenda kijana, inaitwaje hiyo bia na je kuna malipo?
PATRICK: Hiyo bia bado haijapewa jina ila waonjaji ndio mtakaopendekeza jina la pombe hiyo. Ndio mtalipwa elfu ishirini ila leo nitakupa elfu kumi kama advance.
Mzee Ayubu alifurahi sana alipokabidhiwa hiyo pesa na kuambiwa kuwa atafuatwa badae kwaajili ya hilo zoezi.
Muda ulipofika Patrick alimfata mzee Ayubu na kuondoka nae.
Akampeleka huko kwa wenzake, wenzee huyo alidhania kuwa na wale wapo kwaajili ya kuonja hiyo bia mpya.
Mzee Ayubu akapewa glasi moja tu na kulala hapohapo, wakamfanya watakavyo na kuondoka.
Kwakweli kwa Patrick ilikuwa ndio mara yake ya kwanza maishani kuua mtu, siku zote alijua kuwa kazi haramu afanyayo yeye na Maiko ni madawa ya kulevya tu kumbe kuna kazi mbaya zaidi ya kuchukua baadhi ya viungo vya mwili wa binadamu na kuua kabisa, alitetemeka sana kuuangalia ule mzoga wa mzee Ayubu. Roho ya Patrick ikasinyaa, huruma ikamjaa ila hakuwa na jinsi zaidi ya kulikimbia hilo eneo la tukio.
Walirudi Arusha, na kwenda kwenye hilo jumba ila Patrick hakuweza kuingia kwani mawazo yake yalikuwa kwa Tusa, alihitaji kumuona Tusa, ingawa ilikuwa usiku ila Patrick alishaamua kurudi kwake ili akamuangalie Tusa.
Tusa akiwa katulia ndani kama ambavyo Maiko alimuahidi, na kweli siku hiyo akaenda tena kumuona Tusa. Mida ya jioni mlango ulifunguliwa na Maiko akaingia, Tusa akajiuliza kuwa iweje tena huyo Maiko kuja jioni vile, na hakutaka kuondoka wala nini.
Muda kidogo Maiko akaanza kumsifia Tusa.
MAIKO: Tusa, kweli wewe ni binti mrembo tena unayevutia machoni. Kweli pesa yetu imeenda kihalali kabisa.
Mara Maiko akaanza kumsogelea Tusa, Tusa akawa analia huku akipiga kelele na kumsihi Maiko asimfanye chochote.
MAIKO: Tusa, hata mimi ni halali kuwa na wewe kwani nimekulipia mahari kubwa sana. Kwahiyo hutakiwi kuninyima.
Tusa akawa anakimbia hovyo hovyo mule ndani, ila mwanaume ni mwanaume tu.
Maiko alimkamata Tusa na kumuingilia kimwili kwa nguvu, Tusa akawa analia na kuomboleza.
Mara mlango unafunguliwa, Patrick alikuwa anaingia ndani.
Maiko alimkamata Tusa na kumuingilia kimwili kwa nguvu, Tusa akawa analia na kuomboleza.
Mara mlango unafunguliwa, Patrick alikuwa anaingia ndani.
Maiko hakuweza kusikia mlango unavyofunguliwa kutokana na kelele za Tusa na pia hakufikiria kama Patrick anaweza kuja muda huo, aliendelea na yake mpaka pale alipohisi amejiridhisha.
Patrick alishangaa kumsikia Tusa akilia na kujiuliza maswali "Hivi huyu Tusa ni chizi nini? Yani anajiliza hata kama sipo." akaanza kufatilia sauti ya Tusa inapotokea na akagundua kuwa ni chumba cha mwisho kabisa, kile chumba ambacho walitumia kumtoa Tusa ujauzito aliobeba.
Patrick alipofika kwenye kile chumba alimuona Maiko kasimama na Tusa amejikunyata chini, Patrick akaelewa kuwa kwa vyovyote Maiko alikuwa amemuingilia kimwili Tusa, Patrick akachukia sana, kwa ghadhabu akamsukumia Maiko pembeni ambapo alikuwa hajafunga suruali vizuri, ile Maiko anainuka akashtukia anapigwa ngumi ya uso, kabla hajajiweka sawa akapigwa ngumi nyingine.
Maiko akaiona kuwa ishakuwa cheche, akaamua kukimbia.
Patrick alikuwa na hasira hadi mishipa ikamtoka usoni, hakuweza kuzungumza zaidi ya kutetemeka tu, alikuwa akimuangalia Tusa kwa macho makali na ya ghadhabu.
Maiko akafanikiwa kutoka na kupanda gari yake na kuondoka.
Sele alikuwa akimuwaza sana Tusa, alikosa raha kila alipomfikiria Tusa. Alijiuliza maswali mengi sana kuhusu Tusa.
"kwanini ulikubali kuolewa Tusa? Inamaana hukunipenda tena? Na vipi mimba yangu uliyobeba Tusa? Natamani nikuone mpenzi wangu ili moyo wangu uridhike"
Deborah akamuangalia Sele aliyejawa na msononeko machoni.
DEBORAH: Tatizo nini jamani? Eti Sulemani, una nini wewe? Kila siku mawazo.
SELE: Mamdogo, nilikuwa na msichana mzuri sana. Niliyempenda kwa dhati ila mapedeshee wamemuiba mpenzi wangu.
DEBORAH: Mmh pole sana, tatizo la mabinti si waaminifu.
SELE: Alikuwa mwaminifu ila wamemlaghai kwa pesa na mali. Mamdogo nikimfikiria moyo wangu unaniuma sana, sijui kama atatokea msichana yeyote nikampenda kama yeye.
DEBORAH: Usiwe na shaka mwanangu, kama ni wako basi ni wako tu. Tambua ipo siku atarudi kwako.
SELE: Natamani hiyo siku hata iwe leo, kwakweli tunanyanyasika sana maskini katika mapenzi.
DEBORAH: Usijari mwanangu, kila kitu kitakuwa sawa.
SELE: Asante mama.
DEBORAH: Uwe unaenda na kuzungukazunguka huko mtaani ukutane na wenzio, wakina Juma, John labda upunguze kidogo mawazo.
SELE: Sawa mamdogo.
Sele akaamua kwenda kutembea tembea kidogo pale mtaani kama alivyoshauriwa na Deborah ili aweze kupunguza mawazo kiasi.
Patrick akiwa na ghadhabu juu ya Maiko na Tusa.
PATRICK: Kwanini Tusa umelala na Maiko?
TUSA: (Huku akitetemeka), alinilazimisha, amenibaka.
PATRICK: Kwanini akubake Tusa? Umeshindwa kujizuia? Nadhani nawe ulipenda.
TUSA: Hapana Patrick, sijapenda.
PATRICK: Unataka na mimi nikuingilie wapi? Huko kwenye uchafu wa Maiko? Nijibu Tusa.
TUSA: Hapana Patrick.
PATRICK: Kiukweli nimekereka sana Tusa, umeichefua roho yangu.
Tusa akawa anatetemeka tu huku machozi yakimtoka.
Kwavile ulikuwa usiku ikabidi waende kulala, Tusa alilala kwa uoga na mashaka yaliyopitiliza.
Patrick akainuka na kumuingilia Tusa kinyume na maumbile, Tusa alitapatapa na kulia sana ila Patrick hakumuacha hadi pale alipojiridhisha.
Tusa hakuweza kulala hadi panakucha, alikuwa akilia tu. Siku hiyo alipatwa na ugonjwa wa kuhara gafla, alikuwa akiendesha tu na tumbo likimsokota.
Patrick alimuacha Tusa akiwa analia na kuondoka zake ile asubuhi.
Sele akiwa mtaani alikutana na marafiki wengi sana na kupiga story za hapa na pale, na ndipo alipotokea John na kukumbushana mambo yao ya zamani na kuambiana ya sasa.
JOHN: Mwenzio Patrick kaukata, maisha yamemnyookea ile mbaya. Ila wewe umechakaa balaa, vipi hata demu bongo hukuopoa?
SELE: Wee nilikuwa na msichana wangu mzuri sana John, yani huwezi amini.
JOHN: Nilitaka nishangae, kukaa kote bongo usiwe na demu. Labda kama uliwataka wa huku Mwanza.
SELE: Wewe, sijaona huku msichana mrembo kama Tusa wangu.
JOHN: Anaitwa Tusa? Ngoja nikuonyeshe mrembo mwingine mwenye jina hilo kwenye facebook.
John akafungua picha ya Tusa na kumuonyesha Sele.
Sele akashtuka kuiona picha ya Tusa.
SELE: Ndio huyuhuyu Tusa wangu, naye alikuwa anaipenda sana facebook.
JOHN: Mmh! Kaka, yani wewe ndio ulikuwa na huyu mrembo? Aliwahi kuniambia kuwa mpenzi wake anaitwa Sele, sasa wewe Sulemani na Sele wapi na wapi?
SELE: Mimi ndio huyo Sele, kule Dar wamezoea kuniita Sele jamani.
JOHN: Basi una bahati sana kama huyu mrembo ni wako.
SELE: Sipo nae tena, kuna pedeshee mmoja ameniibia mrembo wangu.
JOHN: Kivipi? Au ndomana siku hizi simuoni facebook.?
Sele akaamua kumueleza John kinagaubaga ilivyokuwa kwake na Tusa hadi pale alipokuta Tusa kaolewa na huyo pedeshee Patrick.
Stori hiyo ikafungua akili ya John na kumfanya afikirie kwa kina kama awazacho ndicho au sicho.
Safari ya Patrick asubuhi hiyo ilikuwa ni moja kwa moja kwa Maiko.
PATRICK: Kwanini umenifanyia hivi Maiko?
MAIKO: Mmh! Hata ubaba umekufa sababu ya mwanamke!
PATRICK: Sina baba kama wewe, na bora wewe si baba yangu wala ndugu yangu. Binadamu mwenye roho mbaya kama ya simba.
MAIKO: Jamani Patrick, tusameheane tu ni mambo ya kupitiwa.
PATRICK: Unayajua maumivu ya mke wewe? Umenituma kufanya kazi ya kinyama na bado unanisaliti na mke wangu, kwanini Maiko?
Patrick alikuwa na hasira sana, wakati anaongea alimsogelea Maiko na kumkunja.
MAIKO: Tafadhari Patrick usinitende vibaya, najua wewe ni kijana jasiri. Usiniumize tafadhari, ila kumbuka hata mimi mahari ya Tusa nimechangia tena nimetoa pesa nyingi kushinda wewe.
PATRICK: Kwani nilikuomba unichangie pesa? Kumbe ulikuwa unatoa kwa shingo upande? Dah najuta kukufahamu Maiko.
MAIKO: Niachie Patrick, tuzungumzie kazi niliyokutuma.
PATRICK: Sina muda huo.
Akatoka nje na kuingia kwenye gari yake na kuondoka.
Maiko akawa anajisemea,
"alitaka afaidi peke yake yule binti mrembo! Hajui kuwa kizuri kula na nduguyo, toto choyo kama mama yake loh! Mke kitu gani wakati nimechangia mahari!!"
Maiko kazi yake ni kuharibu tu, kwanza huwa hapendi kuona mtu anaishi kwa furaha mwanzo mwisho.
Akajiandaa na yeye ili akaone kazi yake aliyowatuma wakina Patrick.
Nyumbani kwa kina Tusa, mama yake bi.Pamela akiwa anafua, mara akamuona Tina akija mbio mbio huku anahema kwa kasi ya ajabu.
PAMELA: Tina kuna nini?
TINA: Kuna tatizo mama.
PAMELA: Tatizo gani?
TINA: Tumepatwa na msiba mama.
Pamela alihisi kuchanganyikiwa kabisa kwani hakujua ni msiba wa nani.
Pamela alihisi kuchanganyikiwa kwani hakujua ni msiba wa nani.
PAMELA: Jamani Tina, nani tena?
TINA: Mamdogo, ni babu yao na wakina Tusa.
PAMELA: Wee Tina wewe, unamaanisha mzee Ayubu? Nani amekupa taarifa?
TINA: Ndio mzee Ayubu, nimeona kwenye taarifa ya habari. Tena amekufa kifo cha kusikitisha sana.
Pamela alishapagawa kusikia habari za huyo mkwe wake, ikabidi aende kumtaarifu mumewe na wajaribu kuwapigia ndugu zao ili kujua ukweli wa habari hiyo.
Pamela akaamua kumpigia simu wifi yake aliyeitwa Amina, ambaye naye alimwambia kuwa ndio wamepata habari muda huo.
Ilikuwa ni huzuni sana kumpoteza mtu mcheshi kama mzee Ayubu.
Patrick alirudi nyumbani kwake na kumkuta Tusa yupo palepale alipomuacha asubuhi.
Patrick akamuangalia Tusa na kukaa kwenye kochi, Tusa akamtazama Patrick na kumfata pale alipokaa, Tusa akaanza kuongea kwa maombolezo na kwa uchungu.
TUSA: Hivi Patrick, wewe ni mume wa aina gani? Mume usiyemjali mkeo na unasema unampenda? Hivi ulinioa ili unitese? Nimekukosea nini mimi jamani?
Patrick alimuangalia Tusa kwa jicho kali ila lililojaa huruma.
TUSA: Nasema ya moyoni, kiukweli natamani kufa kuliko kuishi na wewe Patrick. Kukupa namba yangu ndio kosa kubwa la kunifanya niteseke hivi? Unanifanya kama mbwa jike nisiye na thamani, kila anayetaka anachukua tu. Patrick umeniharibia maisha yangu, pesa zako ndio za kunitesa kiasi hiki!! Nimewahi kukuomba pesa mimi?
Tusa akainama na kuendelea kulia.
PATRICK: Nisamehe Tusa mke wangu, kiukweli nimejaribu kufanya mambo mengi ili unipende cha kushangaza huna mapenzi nami kabisa, kama vile sio mumeo. Hata mimi inaniuma Tusa, lini utajifunza kunipenda?
TUSA: Sikupendi na sitakupenda kamwe hadi naingia kaburini.
PATRICK: Kwani Tusa nina kasoro gani mimi? Kwanini usinipende kama yule bwanako?
TUSA: Siwezi kukupenda Patrick, wewe ni gaidi uliyejificha. Nampenda Sele na sikuzote nitaendelea kumpenda, najua sitaweza kuwa nae tena ila nitampenda milele. Nani akupende wewe Patrick? Mwanaume mwenye roho mbaya, usiyejali wengine, mtu mwenye roho ya shetani.
PATRICK: Ni kweli nina roho mbaya ndiomana nimeua.
TUSA: (Akashtuka sana) umeua?
Patrick hakumjibu Tusa ila akaenda chumbani, Tusa akaona maisha yake hapo ni ya mashaka, akabaki anajisemea.
"Eeh Mungu, naomba unitetee katika maisha haya"
Baada ya kutafakari sana, John akaamua kumfata Sele ili amwambie anachofikiria yeye.
JOHN: si uliniambia kuwa huyo pedeshee aliyemchukua Tusa anaitwa Patrick?
SELE: Ndio anaitwa Patrick.
JOHN: Mmh! Hivi sio Patrick ndugu yako kweli?
SELE: Acha masikhara bhana John, kwanini umuhisi yeye?
JOHN: Sikia nikwambie, Patrick ana hela sana kwa sasa halafu anaishi Arusha.
SELE: Hata kama, hawezi kuwa yeye.
John akaamua kumueleza Sele kuwa kwanini amemuhisi Patrick.
JOHN: Sikia nikwambie, kipindi Patrick amerudi hapa alinishangaa kuona nashinda facebook.
SELE: Kwani kukushangaa kuna tatizo John?
John akamueleza Sele ilivyokuwa, na jinsi Patrick alivyotaka kufunguliwa akaunti ya facebook na jinsi alivyomuulizia Tusa.
JOHN: Aliniuliza kwa makini jina analotua Tusa, nikagoma kumtajia ila akaomba kuona picha yake nadhani hapo ndipo alipojua jina lake na kumuomba urafiki.
SELE: Hayo uyasemayo John yananiingia sana halafu inaonyesha kama kuna uhusiano, ila kiukweli nakataa. Patrick hawezi kufanya vile, majina yanafanana John tena hayo majina ya Patrick wako wengi sana duniani.
JOHN: Kwahiyo haiwezekani kuwa ni yeye ingawa alimuulizia Tusa?
SELE: Kumuulizia mtu ni jambo la kawaida John, sidhani kama anaweza kuwa Patrick huyu.
Sele alipinga kabisa hisia za John za kudhania kwamba Patrick wanaemjua ndio muhusika.
Wakiwa msibani, hadi wanazika kila mmoja alisikitishwa na kifo cha mzee Ayubu, kwani kilikuwa ni kifo cha kusikitisha sana.
Mzee Ayubu alikutwa ametolewa upara na kunyofolewa sehemu za siri, kila mtu alihuzunika kwa kifo cha mzee huyo.
Hata baada ya mazishi habari ilikuwa ni hiyo hiyo ya juu ya kifo cha mzee Ayubu, hakuna aliyetambua mtu aliyemfanyia unyama mzee huyo, watu walikuwa wakisikitika tu.
Amina kama mtoto mkubwa wa kike wa mzee Ayubu akaamua kumuulizia Tusa kwani Tusa ndie mjukuu mkubwa wa mzee huyo na hakuonekana msibani.
AMINA: Wifi, Tusa yuko wapi?
PAMELA: Tusa yupo kwa mumewe, ameolewa.
AMINA: Yani mnamuoza mtoto bila ya kutushirikisha na wengine?
PAMELA: Ilikuwa ni haraka wifi, naomba utusamehe.
AMINA: Na mbona hajaja msibani au hamjampa taarifa? Unajua Tusa ni mtu muhimu sana kwa babu yake, angepaswa kuwepo mahali hapa.
PAMELA: Kwakweli Tusa hapatikani kwenye simu, huwa tunawasiliana na mumewe tu. Ila tangu msiba utokee naye hapatikani.
AMINA: Mmh! Wifi mmeuza mtoto nyie, yani hapatikani na hata kumfatilia hamumfatilii?
PAMELA: Mumewe kasema wanaendelea vizuri, hata hivyo mtu mwenyewe ana pesa.
AMINA: kupenda pesa uache wifi dada, ila mfanye juu Tusa apate habari na aje kutembelea kaburi la babu yake.
PAMELA: Sawa tutafanya hivyo.
Baadhi ya maneno yalimuingia vizuri Pamela, akawaza sana moyoni kuhusu mtoto wake Tusa kwani ilikuwa kama amemtupa vile.
Patrick alikuwa nyumbani kwake kama vile mtu aliyepagawa.
Akaitazama simu yake na kugundua kuwa alibadilisha laini ya simu, aliweka laini inayojulikana na watu wachache ili kuepuka usumbufu, wakati anatazama simu yake, ilianza kuita muda huo na mpigaji alikuwa Maiko.
PATRICK: Sema.
MAIKO: Mbona umekuwa hivyo Patrick? Unataka kuharibu kazi mwishoni? Uje kufanya kazi, kesho asubuhi nakuhitaji kuna mpango flani wa pesa uje tupange.
PATRICK: Poa.
Bado Patrick hakujisikia raha kuzungumza na Maiko ni kwavile tu ameshakula kiapo cha kufanya kazi ya Maiko hadi mwisho.
Tangia Patrick aropoke kwa Tusa kuwa aliua, Tusa alijikuta akimuogopa zaidi Patrick.
PATRICK: (Kwa ukali), una nini wewe Tusa? Unaniogopa mimi nimekuwa jini? Nakusemesha hujibu, umekaa kama sanamu. Nina hasira zangu hapa naweza nikakubutua ukiendelea kuwa kimya.
Tusa hakuweza kujibu zaidi ya kujipeleka kulala tu, ndipo Patrick nae alipoamua kulala.
Patrick akiwa usingizini, akamuona mzee Ayubu akimjia kwa sura ya huruma, na kuanza kuongea.
"kwanini umeniua Patrick?"
Patrick akiwa usingizini, akamuona mzee Ayubu akimjia kwa sura ya huruma, na kuanza kuongea.
"kwanini umeniua Patrick?"
Patrick akabaki akimtazama na kukosa jibu, mzee Ayubu akasema tena,
"Laiti ungelijua mimi ni nani yako! Usingethubutu kuniua."
Patrick akashtuka na kupiga kelele, "mzee Ayubuuu..."
Tusa nae akashtuka na kujisemea.
TUSA: Mzee Ayubu!!
PATRICK: (Huku akihema sana), nilikuwa naota Tusa.
TUSA: Huyo mzee Ayubu ni nani na ana mahusiano gani na wewe?
PATRICK: Ni rafiki yangu tu.
TUSA: Kivipi?
PATRICK: Aaargh, hayo mengine hayakuhusu bhana. We endelea kulala tu, nishakwambia ni rafiki yangu inatosha.
TUSA: Sawa bhana.
Tusa akaamua kujilaza tena, ila muda ule ule Patrick akaanza kumlazimisha Tusa kuwa anataka kumuingilia kimwili, kwakweli kile kitendo kilikuwa ni kero kwa Tusa kwani hakuwa na la kufanya, na siku zote Patrick huwa anamuingilia Tusa kwa kumlazimisha tu kitu kinachomfanya Tusa aumie na kulia sana kwani hakupewa maandalizi yoyote.
Kulipokucha Patrick aliwaza sana juu ya mzee Ayubu, na akajiuliza kuwa ana mahusiano yapi na mzee huyo kwani ile sauti kuwa angejua ni nani yake asingemuua ilimrudia mara kwa mara.
Alipoamua kwenda kwa Maiko alihitaji kumuuliza baadhi ya maswali ili apate kujua kwanini Maiko alimtuma kwenda kumuua mzee Ayubu, na pia aweze kujua kuwa yeye na mzee Ayubu wana mahusiano gani.
Sele aliendelea kuichuja kauli ya John katika akili yake, alishindwa kuamini kabisa kuwa inawezekana akawa ni Patrick ingawa kuna uthibitisho wa kutosha kuwa ni yeye.
Sele aliwaza sana bila ya kupata majibu, akawa anajiuliza tu,
"Hivi ni kweli Patrick anaweza kunitenda vile? Mmh!! Hapana, hata kama angekuwa mtu mwingine Patrick hawezi kuwa na roho mbaya ya kiasi kile"
Akamfata alipokaa Deborah ili amuulize maswali mawili matatu kuhusu Patrick.
SELE: Hivi mamdogo, ulisema kuwa Patrick yupo mkoa gani?
DEBORAH: Patrick yupo Arusha.
SELE: Anafanya kazi gani?
DEBORAH: Alisema yupo mgodini.
SELE: Ana pesa sana eeh!
DEBORAH: Mbona leo maswali mengi kama polisi? Ana hela ndio, nadhani kazi yake ina kipato sana.
SELE: Maswali kawaida tu mamdogo, mpigie basi nimsalimie.
DEBORAH: Yani ni kama wiki mbili sasa simu yake haipatikani, ngoja nimjaribishe.
Deborah akaamua kuchukua simu na kumpigia Patrick ila napo hakupatikana.
SELE: Vipi hapatikani?
DEBORAH: Ndio hapatikani, hata sijui amepatwa na matatizo gani maana sio kawaida kabisa.
SELE: Basi tungoje siku atapiga mwenyewe.
DEBORAH: Ndio ila nitaendelea kumjaribisha mara kwa mara kama nitampata hewani.
Sele hakuweza kumwambia mamake mdogo juu ya maneno ya John kuwa uenda Patrick ndio muhusika kwani aliona ni kumpa presha mamake mdogo na pia hakuwa na uhakika bado.
http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Patrick alienda kwa Maiko na kufanya nae shughuli za hapa na pale, baada ya hapo akaamua kutulia nae na kumuuliza maswali aliyoyakusudia.
PATRICK: Hivi kwanini ulinituma kumuua mzee Ayubu? Kwani unamfahamu au unamahusiano naye?
MAIKO: Kiukweli simfahamu kabisa huyo mzee Ayubu, ila haya ni mambo ya biashara. Kuna mtu alitoa oda ya kufanya hivyo na tumeingiza pesa nyingi sana.
PATRICK: Huyo mtu ni nani na ana mahusiano gani na wewe?
MAIKO: Huyo mtu ni ndugu yangu ila haishi hapa, yupo nje ya nchi ni huko hufanya hiyo biashara ya viungo vya wanadamu. Hapa anakujaga mara moja moja sana.
PATRICK: Viungo vya wanadamu vina kazi gani?
MAIKO: Akija tena nitakutambulisha kwake umjue halafu utamuuliza hayo maswali yako.
PATRICK: Je, kuna uhusiano wowote kati ya mimi na mzee Ayubu?
MAIKO: Acha kuota Patrick, wewe mtu wa Mwanza, mzee Ayubu wa Morogoro huo uhusiano wenu unatokea wapi? Una ndugu Morogoro wewe?
PATRICK: Hapana.
MAIKO: Ndugu zako wako Mwanza, mzee Ayubu hakuhusu wewe wala mimi.
PATRICK: Unajua nini? Mi najiuliza, kwanini iwe mzee Ayubu na si mwingine yeyote?
MAIKO: Hayo maswali utamuuliza mwenye kazi, labda ana kisasi nae.
Patrick aliondoka kwa Maiko na kutambua kwamba mtandao wa Maiko ni mkubwa sana kwani hata yeye ana bosi wake, yote hayo yalimchanganya Patrick.
Walipomaliza matanga ya kwenye msiba, Pamela na mumewe walirudi kwao wakiwa na mwanamke mmoja wa makamo akidai kuwa yeye ni mama mzazi wa Adamu.
Mwanamke huyo aliitwa Rehema, hata Adamu alimshangaa kwani hakuweza kumuona tangia alipokuwa mdogo na yote hayo ilitokana na kwamba Adamu aliachwa na mama huyo akiwa na miaka miwili.
PAMELA: Mama, kwanini ulimuacha mwanao akiwa mdogo hivyo?
REHEMA: Nilijifungua mapacha, wazazi wangu hawakutaka niolewe na Ayubu ila Ayubu alihitaji watoto wake ikabidi tugawane mmoja nikawa nae na mwingine akaondoka na Ayubu. Kwa kipindi kirefu nimemtafuta Ayubu bila mafanikio mpaka pale nilipoona taarifa ya kifo chake kwenye luninga. Kwakweli nimesikitishwa sana, nikaamua kufunga safari hadi Morogoro.
PAMELA: Kwahiyo umetokea mkoa gani?
REHEMA: Kigoma mwanangu, kwakweli ilikuwa safari ndefu sana.
PAMELA: Pole sana mama.
REHEMA: Asante, na mbona kule wanapenda kukuita wifi dada?
PAMELA: Mama, kuna kaundugu flani hivi kapo kati yangu na Adamu ila mwanzo hatukugundua hadi tumeoana na kufunga ndoa. Ila undugu wenyewe hauna nguvu sana, ni undugu wa mbali.
REHEMA: Undugu gani tena?
PAMELA: Nitakwambia tu mama usijari ila kwanza turekebishe tofauti yako wewe na Adamu. Natumaini kuna muda atakuelewa mama yetu, hata usijari.
Pamela alipatana sana na huyu bi.Rehema kutokana na ucheshi wa bibi huyo hata akashangaa kwanini hakuweza kuishi na mzee Ayubu.
Patrick kabla ya kurudi nyumbani kwake alipitia baa kwanza ambako alikunywa pombe hadi akaridhika.
Aliporudi kwake alimkuta Tusa amelala, akaanza kumuamsha kwa nguvu, tofauti na walevi wengine ambao wakilewa wanakuwa legelege ila Patrick alikuwa na nguvu sana.
Akawa anamsumbua Tusa hadi akafanikiwa kumuingilia anakokutaka yani kinyume na maumbile, Tusa hakuweza kulala tena zaidi ya kulia tu.
Patrick akaanza kumwambia Tusa.
PATRICK: Unajua ile siku ya kwanza nimekufaidi sana huko nyuma na nimeona kutamu zaidi, siku hizi itakuwa hukohuko na safari hii hadi utapata mimba ya mgongo.
Halafu akalala, Tusa alilia sana na kuombea ukombozi wake ufike.
Kulipokucha Patrick aliamka kama kawaida ila alijikuta akimkumbuka sana mama yake, akaamua kuchukua simu yake na kumpigia ila iliita kama mara tatu bila ya kupokelewa.
Patrick akaweka simu mezani na kwenda kuoga, kwakweli siku hiyo alijisahau kwani huwa haachi simu yake, kila mahali anakuwa nayo.
Patrick akiwa bafuni ile simu yake ikaanza kuita, Tusa aliposikia akasogea kuitazama akaona jina 'mama' Tusa akaona kuwa kwa vyovyote vile huyo lazima atakuwa mama yake na Patrick, akaamua kuipokea ili amueleze matatizo yake.
Patrick akiwa bafuni ile simu yake ikaanza kuita, Tusa aliposikia akasogea kuitazama akaona jina 'mama' Tusa akaona kuwa kwavyovyote vile huyo lazima atakuwa mama yake na Patrick, akaamua kuipokea ili amueleze matatizo yake.
Tusa akaipokea ile simu na kuisikia sauti iliyosema 'hallow' kuwa ni ya mwanamke wa makamo.
TUSA: Mama, mimi ni mke wa Patrick. Ananitesa na kuninyanyasa sana.
DEBORAH: Patrick kaoa?
TUSA: Ndio na mimi ndiye mkewe.
DEBORAH: Unaitwa nani binti?
Mara Patrick akatoka bafuni na kumkuta Tusa yupo na ile simu sikioni, akaenda na kumpokonya halafu akaiweka sikioni mwake.
Deborah aliendelea kuongea kwani kilio cha Tusa kilimuingia masikioni mwake vilivyo.
DEBORAH: Niambie binti, halafu niambie anachokufanya hadi ulie hivyo.
Patrick akaikata ile simu na kumgeukia Tusa.
PATRICK: Nani kakutuma upokee simu yangu? Hujui mama yangu ana presha, akifa je? Nijibu, nani kakutuma?
Tusa aliendelea kulia bila ya kutoa jibu, Patrick akamuuliza tena.
PATRICK: Kitu gani kinakuliza sasa wakati umeshafanya makosa?
TUSA: Unanionea Patrick, unaninyanyasa, unanitesa. Nini kosa langu jamani?
PATRICK: Kosa lako ni kupokea simu isiyo kuhusu.
Patrick akamsogelea Tusa akiwa anahitaji la kumzabua kibao, mara simu yake ikaita tena. Patrick akashindwa kupokea kwani hakujua cha kumjibu mama yake kwa muda huo.
PATRICK: Unaona sasa Tusa, mimi namwambia nini mama? Unadhani atanielewa? Yani we Tusa una akili mbovu sana.
Patrick alikuwa na hasira sana akaona kuwa akiendelea kukaa hapo atamuumiza huyo Tusa, akaamua kuvaa na kuondoka zake.
Tina alimkumbuka sana ndugu yake na rafiki yake kipenzi Tusa, kama kawaida yake alikuwa mara kwa mara nyumbani kwa kina Tusa ili kujua kama kuna taarifa yoyote kuhusu Tusa.
Akiwa amekaa na mamake mdogo wanaongea.
PAMELA: Hivi Tina dadangu bado hajarudi?
TINA: Anarudi leo mamdogo, halafu amesikitishwa sana na kifo cha babu. Kama angewezaa kupaa kutoka china basi angekuja msibani.
PAMELA: Kwakweli kifo chake kimetushtua wengi.
TINA: Vipi kuna taarifa yoyote kuhusu Tusa?
PAMELA: Hakuna mwanangu, tuzidi kumuombea tu.
TINA: Sawa mamdogo, mi naenda ila akija mjomba msalimie.
PAMELA: Sawa usijari.
Bi. Rehema akajikuta akiwa na maswali mengi kichwani.
REHEMA: Huyo mjomba wa Tina hapa kwako ni yupi?
PAMELA: Adamu mama ndio mjomba ake.
REHEMA: Adamu si mumeo na Tina wewe ni mamake mdogo iweje mumeo awe mjomba ake?
PAMELA: Utajua tu mama kwanini imekuwa hivyo, hata usijari.
Bi. Rehema alikuwa akishangaa tu bila kuelewa.
Deborah alishindwa kuelewa kabisa, akabaki anajisemea mwenyewe.
"Hivi kweli Patrick anaoa bila hata ya kunitaarifu? Dharau gani hii?"
Sele alimuona mamake mdogo huyo akiwa anajisemesha mwenyewe.
SELE: Nini tena mamdogo?
DEBORAH: Kwakweli nashindwa kumuelewa Patrick.
SELE: Kafanyaje tena?
DEBORAH: Asubuhi nilipotoka kuoga nikakuta kwenye simu yangu kuna missed call tatu, ile kupiga sasa mmh.
SELE: Kwani ikawaje?
Deborah akamsimulia Sele alichoambiwa kwenye simu.
SELE: Mmh! Yani Patrick kaoa? Kamuoa nani? Na kwanini hakusema?
DEBORAH: Hayo yote sijui, najaribu kumtafuta kwenye simu hapatikani halafu ile namba haipokelewi, nadhani ni namba yake anaogopa kupokea kwavile mimi nimeshajua ukweli.
SELE: Sasa itakuwaje mamdogo?
DEBORAH: Usijari Sele, mimi namjua Patrick. Natambua wapi pa kumkamatia, atanitafuta mwenyewe.
SELE: Sawa mamdogo.
Akili ya Sele ikawaza mengi sana, akaanza kuhisia kuwa huenda huyo binti akawa Tusa ila tu hakuwa na uhakika.
Deborah hakuacha kumtafuta Patrick kwenye simu ila simu yake haikupokelewa. Akaamua kumtumia ujumbe, alijua utafika na atausoma tu.
Mama yake na Tina aliyeitwa Fausta alienda nyumbani kwa mdogo wake Pamela ili kumsalimia bi. Rehema.
FAUSTA: Karibu sana mama.
REHEMA: Asante ingawa nimefika kipindi cha majonzi.
FAUSTA: Kwakweli huu msiba wa baba umetugusa sana, ingawa sijaishi nae sana ila namkumbuka sana baba alikuwa mcheshi na mpenda watu. Yeyote aliyemfanyia hivi baba na alaaniwe milele.
REHEMA: Inaonyesha unamjua sana mzee Ayubu.
FAUSTA: Ndio namjua, ni baba yangu mzazi kwakweli nimeumia sana.
REHEMA: Mmh!! Baba yako mzazi? Wewe na Pamela si mtu na mdogo wake? Iweje mzee Ayubu awe baba yako mzazi?
FAUSTA: Mama, sijui kama utanielewa.
REHEMA: Nieleweshe tu nitakuelewa.
FAUSTA: Mama, mimi na Pamela tumechangia mama halafu mimi na Adamu tumechangia baba kwahiyo Pamela ni ndugu yangu na Adamu ni ndugu yangu.
REHEMA: Mmh! Ndiomana Pamela wanamuita wifi dada!! Sasa nimeanza kuelewa, kwamaana hiyo Adamu na Pamela ni kama ndugu.?
FAUSTA: Wenyewe wanakataa kuwa si ndugu, ila walioana bila kujua. Hata hivyo undugu wao hauna nguvu sana.
REHEMA: Yani umenielewesha kwakweli, ndomana mwanao anamuita Adamu mjomba. Mmh! Kazi ipo. Eeh na wewe ulikuwa wapi kwani hadi msiba umeisha?
FAUSTA: Nilikuwa China, huwa naenda mara kwa mara kuna mizigo naitoaga kule naileta huku.
REHEMA: Hongera kwa hiyo kazi, kila siku namngoja Adamu kumwambia kuhusu pacha wake ili aende akamtafute huko Mombasa.
FAUSTA: Mombasa? Alienda kutafuta nini huko?
REHEMA: Aliondoka na kaka yangu ila hawajarudi hadi leo halafu huyo kaka yangu mwenyewe ana akili mbovu huyo balaa hadi kuna kipindi alipelekwa Milembe halafu akatoroka.
FAUSTA: Mmh! Kazi ipo, ila hakuna tatizo mama tutampata tu.
REHEMA: Eeh! Na huyo mama yenu yuko wapi?
FAUSTA: Alishakufa na hivi baba nae amekufa basi tumebaki yatima.
Rehema na Fausta wakaongea mambo mengi ya maisha na kuweza kutambuana kwa undani zaidi.
Patrick akiwa kwa Maiko huku akiendelea kuzipotezea simu anazopiga mama yake.
Mara akaona meseji imeingia kwenye simu yake kutoka kwa mama yake.
"Patrick mwanangu, hutaki kunitafuta, simu zangu hupokei! Nashukuru sana najua hiyo ndiyo fadhira yako kwa malezi yote niliyokupa. Umeona maisha ya huko Arusha ni bora kuliko mimi, basi endelea na maisha hayo ila usahau kabisa kama una mama anayeitwa Deborah"
Patrick alisoma ujumbe huo mara mbili mbili, neno la mwisho likawa linamrudia mara kwa mara kuwa asahau kabisa kama ana mama anayeitwa Deborah. Patrick akajihisi ni mkosaji, akatambua alichofanya hapo hakipendezi, akaamua kwenda sehemu iliyotulia na kumpigia simu mama yake ili amwombe msamaha.
Patrick aliongea kwa kutubu kwa mama yake ambapo Debora alimpa chaguo moja tu.
DEBORAH: Ukitaka nikusamehe basi chagua moja kati ya haya.
PATRICK: Yapi hayo mama? Niko tayari kwa chochote ilimradi tu nipate msamaha wako mama.
DEBORAH: Mlete huyo binti uliyemuoa Mwanza aje nimuone au mimi nije huko Arusha kumuona.
Patrick akajikuta anawaza jibu la kumpa mama yake.
Patrick akajikuta anawaza jibu la kumpa mama yake.
Deborah akamuuliza tena Patrick na kumsisitiza ampe jibu.
PATRICK: Mama, naomba kama masaa mawili nifikirie majibu ya kukupa.
DEBORAH: Kwani ni mtihani huo?
PATRICK: Hapana mama ila nahitaji muda kidogo.
DEBORAH: Kwahiyo utanipa jibu saa ngapi?
PATRICK: Nimekwambia baada ya masaa mawili mama.
Patrick akajikuta akiwaza sana na kujiuliza maswali mengi, kuwa akimwambia mama yake aende Arusha itakuwa msala kwa Maiko na akiamua kwenda yeye Mwanza atamuagaje Maiko kipindi hicho wakati walikuwa na kazi nyingi za kufanya, akajikuta akijiuliza sana. Akaamua kurudi kwake ili akatafakari kwa kina.
Bi. Rehema alikuwa akitafakari mara kwa mara juu ya mtoto wake Adamu na mkewe Pamela.
REHEMA: Hivi Pamela mwanangu hukujua kabisa kama una undugu wa mbali na Adamu?
PAMELA: Tulijua wakati tumeshapendana sana ila hata hivyo undugu wetu hauna nguvu sana.
REHEMA: Hata kama, nyie ni sawa na dada na kaka ila ndo hivyo maji yashamwagika. Vipi huyo binti yenu atarudi lini?
PAMELA: Hata sijui mama, maana tangu ameolewa huko Arusha hatujapata kuzungumza na yeye hadi leo. Mwanzoni tulikuwa tunazungumza na mumewe ila sasa kimya.
REHEMA: Hivi mnajua kama Arusha kuna ujangili sana? Mnajua wanapoishi?
Akatokea Adamu nae na kuchangia.
ADAMU: Na huko Mombasa alipoenda mwanao je? Unadhani atakuwa mzima? Kama akiwa mzima basi shoga.
REHEMA: Sina maana mbaya, ila nyie kama wazazi mlipaswa kutambua kwanza anapoenda mtoto wenu kabla hajaenda. Mlipaswa kuwatambua ndugu wa mkwe wenu, mlipaswa kuwa na mawasiliano nao. Ila hapo mlipo hamjui chochote.
PAMELA: Usemayo mama ni kweli kabisa, tumefanya makosa sana kumuozesha mwanetu kwa mtu tusiyemfahamu vizuri. Ila hakuna la kufanya sasa, labda tungoje arudi tu.
REHEMA: Cha msingi ni kumuomba Mungu arudi salama, sinamaana kwamba mji wa Arusha ni mbaya hapana. Ila Arusha ina watu flani ambao hupenda sana kufanya mambo ya ajabu.
ADAMU: Sio Arusha tu, hata Mbeya kuna wachuna ngozi. Shinyanga kuna machinjachinja.
PAMELA: Mmh!! Na wewe Adamu unataka kuleta mada zako za mikoa hapa.
Adamu alipenda sana kumpinga mama yake huyu kwani alimuona ni mwenye upendeleo, kwa kumchukua pacha mmoja kumlea yeye na kumuacha yeye kwa baba yake ambapo alilelewa na mashangazi.
REHEMA: Unanichukia bure mwanangu, ila ni baba yako aliyetaka tugawane watoto. Sio kwamba sikukupenda mwanangu.
Pamela alimuhurumia bi. Rehema aliyejaribu kumuelekeza Adamu kila leo japo amuelewe.
Patrick akiwa nyumbani kwake na kuendelea kutafakari, akamuita Tusa, naye Tusa alishajiandaa kwa majibu yaliyonyooka iwapo akiulizwa chochote na huyo mumewe.
PATRICK: Hivi siku ile ulipopokea simu yangu ulimwambia nini mama?
TUSA: Sijamwambia chochote zaidi ya kujitambulisha tu kuwa mimi ni mkeo.
PATRICK: Na kwanini ulipokea Tusa?
TUSA: Kwanza sikujua kama ni mama yako, nilihisi ni mwanamke wako ndomana nikapokea nisikie atasemaje.
PATRICK: Inamaana Tusa umeanza kuwa na wivu na mimi?
TUSA: Ndio ninao, wewe ni mume wangu lazima nikuonee wivu.
Kauli ya Tusa ilimfanya Patrick ajisikie vizuri sana.
PATRICK: Vipi ukionana na mama yangu utamwambiaje?
TUSA: Sitamwambia chochote zaidi ya kufurahi kumuona.
PATRICK: Eeh ungependa mama yangu aje hapa umuone au nikupeleke alipo ukamuone?
TUSA: Nadhani itakuwa vizuri tukimfata yeye, kwani itanifanya hata mimi kutambua miji mingine.
PATRICK: Sawa sawa Tusa, naona leo umekuwa mke mwema. Usijari tutapanga safari hivi karibuni.
TUSA: Sawa mume wangu.
PATRICK: Aaaah! Umeniitaje Tusa?
TUSA: Mume wangu.
PATRICK: Umenifurahisha sana, siku zote ungekuwa hivi ningenenepa jamani.
Patrick aliona kuwa ameanza kupendwa na Tusa na hiyo ndio ikawa furaha yake.
Deborah bado alitafakari kwa kina mambo ya Patrick. Alimuona Patrick kuwa mtoto wa ajabu tofauti na malezi aliyompa.
Alipoona muda umepita sana akaamua kumpigia simu tena Patrick ili ajue jibu lake.
PATRICK: Mama usijari, nitakuja nae Mwanza.
DEBORAH: Kweli Patrick?
PATRICK: Kweli mama, nitakutajia siku ya kuja. Ni hivi karibuni kati ya siku mbili tatu mama.
DEBORAH: Mungu akutangulie mwanangu ili muweze kufika salama huku wewe na mkeo.
PATRICK: Asante mama.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Deborah akafurahi kwani akahisi ni yule Patrick aliyemzoea kwani amejirudi sasa.
Sele akatokea na kumuuliza mama yake mdogo.
SELE: Mama, Patrick amekutajia jina la mkewe?
DEBORAH: Hapana ila anakuja nae huku Mwanza.
SELE: Lini hiyo?
DEBORAH: Kasema ataniambia hiyo siku.
Sele akabaki na lindi la mawazo huku maswali lukuki yakimuelemea kuwa je kama huyo mwanamke akiwa Tusa wake atafanyaje. Alikosa jibu kabisa.
ITAENDELEA

0 Comments