Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mume gaidi sehemu ya nne (04)



Patrick akaamua kwenda kumuaga Maiko ila Maiko alitokea kuipinga safari ya Patrick.

MAIKO: sikia nikwambie Patrick, huyo binti ukimpeleka kwa Deborah sahau kabisa kurudi nae Arusha.

PATRICK: Haiwezi kuwa hivyo bhana, hata hivyo si atakuwa kwa mama yangu?

MAIKO: Kumbuka kuna kazi kubwa sana ambayo inatakiwa aifanye huyo Tusa. Labda tuifanye kwanza ndio uende nae.

PATRICK: Mama anataka kwenda kumuona mara moja tu, hakuna tatizo nitarudi nae.

MAIKO: Hapana Patrick, nimekataa. Namjua Deborah alivyo, tutamkosa kabisa huyo Tusa.

PATRICK: Mama yangu hayupo hivyo.

MAIKO: Hujui tu Patrick, Deborah kanipotezea mademu zangu wengi sana. Anajifanya mshauri wa wanawake kwavile tu yeye mambo yamemuharibikia. Usiende na Tusa hadi kazi yetu itakapokamilika.

Hayo majibu hayakumpendeza kabisa Patrick ukizingatia kashamwambia mama yake kuwa karibia anarudi.


Patrick aliporudi kwake akaamua kufanya kitu cha haraka, akaamua kupanga safari ya haraka bila kumshirikisha Maiko alitaka Maiko ashtukie tu kuwa alishaondoka.

PATRICK: Tusa jiandae kesho tuna safiri.

TUSA: Ndio ile safari uliyosema?

PATRICK: Ndio tunaenda kumuona mama.

Kesho yake mapema alfajiri wakaondoka na kwenda kupanda mabasi yaendayo Mwanza. Wazo la Tusa ni kumtoroka Patrick tu wakiwa safarini.


Kesho yake mapema alfajiri wakaondoka na kwenda kupanda mabasi yaendayo Mwanza. Wazo la Tusa ni kumtoroka Patrick tu wakiwa safarini.

Wakati gari inakaribia kuondoka, Tusa akaanza kuhangaika huku amejishika tumbo.

PATRICK: Nini wewe?

TUSA: Tumbo Patrick, nimebanwa vibaya sana.

PATRICK: Mambo gani hayo Tusa jamani? Haya fanya haraka basi uende chooni.

TUSA: Kiko wapi?

PATRICK: (Akimuelekeza kwa mkono) nyuma ya lile bus la bluu, fanya haraka mi nitakuwa hapa kuwazuia ili watusubiri.

TUSA: Sawa mume wangu.

PATRICK: Uwahi kurudi maana hizo haja zako zisije zikatuchelewesha hapa.

Tusa aliposhuka ndani ya lile bus, alikuwa na mpango mmoja tu kichwani nao ni kutoroka.

Akaenda kama alivyoelekezwa na Patrick, kufika karibia na choo akazunguka nyuma yake huku akichungulia chungulia pa kuelekea, mara gafla akatokea mtu nyuma yake na kumziba mdomo, Tusa akaanza kuangaika, akafanikiwa kumpiga teke la nyuma mtu yule, lile teke lilimfanya yule mtu amwachie Tusa ila Tusa kabla hajapiga hatua zaidi akadakwa tena na yule mtu halafu yule mtu akampiga Tusa ngumi za dabodabo tumboni kitu kilichofanya Tusa alegee kabisa halafu akambeba begani na kwenda kumuweka kwenye gari.

Patrick akiwa ndani ya basi akashangaa kuona Tusa harudi na basi ndio limeanza kutoka, aliwazuia mwishowe akachoka na kuamua kushuka kabisa.

Kitu cha kwanza alichofanya Patrick ni kwenda chooni, akatazama vyoo vyote lakini hakumkuta Tusa, hofu ikaanza kumuingia Patrick, akatoka na kuzunguka nyuma ya choo akashangaa kuona gari la Maiko linaishia, wasiwasi ukamjaa kuwa Maiko amemteka Tusa.

Akaamua kuchukua bodaboda na kuifatilia gari ya Maiko.


Pamela akiwa amelala na mumewe alijikuta akishtuka gafla na kusema kwa nguvu.

"Tusaaaaaaa......"

kitendo hicho kilimshtua na Adamu pia.

ADAMU: Vipi mama Tusa, umepatwa na nini?

PAMELA: (Huku akitetemeka na kuonyesha hofu), nimeota vibaya kuhusu Tusa.

ADAMU: Umeota kafanyaje?

PAMELA: Ameumia sana halafu anapiga kelele za kutaka msaada, maskini mwanangu jamani (akaanza kulia).

ADAMU: Nyamaza mama Tusa, haya ni makosa kweli tumeyafanya. Sasa tujadili namna ya kutatua maana kulia hakutasaidia.

PAMELA: Naelewa hilo mume wangu, namuhurumia mwanangu Tusa. Binti yangu ni mpole sana, kama anapata mateso si haki yake kwakweli. Mwanangu Tusa si mkorofi, ni mcheshi, mpole, mkarimu na anapenda watu wote. Mbona niote anateseka vile, halafu hakuna wa kumsaidia! Roho inaniuma kwakweli, naumia sana nikimkumbuka Tusa, inakuwa kama tumemtupa jamani.

ADAMU: Sio hivyo mke wangu, tumuombe Mungu tu mtoto wetu arudi salama.

PAMELA: Kwakweli ipo siku nitaenda Arusha kumtafuta mwanangu, roho inaniuma sana Adamu.

Pamela alihuzunishwa sana na ndoto mbaya aliyoota juu ya Tusa.

Alikosa raha na amani kila anapo mfikiria mwanae.


Patrick alimfatilia Maiko hadi nyumbani kwake na kumuona akimshusha Tusa kama mzigo toka katika gari yake halafu akaingia nae ndani, Tusa alikuwa kapoteza fahamu, hakuweza kujielewa kabisa.

Patrick aliingia kwa Maiko akiwa na ghadhabu sana.

MAIKO: Nilijua tu kuwa utakuja mwenyewe baada ya mkeo kuwa huku.

PATRICK: Kwanini umemteka mke wangu Maiko?

MAIKO: Tumekubaliana nini mimi na wewe? Si mpaka Tusa atakapokamilisha kazi yangu? Sasa kwanini uliamua kutoroka nae, unanisaliti Patrick?

PATRICK: Sikuwa natoroka Maiko.

MAIKO: Ila ulikuwa unafanya nini?

PATRICK: Nilitaka Tusa akamfahamu mama tu basi.

MAIKO: Namjua Deborah, Patrick huyu Tusa angeenda huko asingerudi tena.

PATRICK: Angerudi tu.

MAIKO: Mimi ndio ninaemjua Deborah, kumbuka amewahi kuwa mke wangu yule.

PATRICK: Na ulijuaje kama nimeondoka.

MAIKO: Sikia Patrick, mtandao wangu ni mkubwa sana. Ulidhani kuondoka na basi sitojua? Mimi ndio Maiko bhana, Tusa lazima afanye kazi yangu ili milioni kumi yangu irudi, ulidhani nimetoa bure?

PATRICK: Maiko wewe ni mtu mbaya sana, umembaka Tusa, umeona haitoshi sasa umemteka eti umfanyishe kazi. Mbona una roho mbaya hivyo jamani?

MAIKO: Sina roho mbaya ila mfanya biashara yeyote hutarajia faida sio kutoa kitu kwa hasara. Nilitoa milioni kumi kuchangia mahari ya Tusa, sasa nitamtumia Tusa kuingiza pesa zaidi.

Patrick alishindwa kuelewa kuwa ni kazi gani ambayo Maiko alitaka kumfanyisha Tusa, roho ya Patrick ilipatwa na hofu sana.

Tusa akawekewa ulinzi wa kutosha, aliposhtuka akaanza kutapika damu, Patrick akamuhurumia Tusa, akamsogelea na kuanza kumbembeleza Tusa ambaye alikuwa akilia tu.

Wakati Patrick akiendelea na hiyo kazi ya kumbembeleza Tusa, mara akaitwa na Maiko, ikabidi aende kumsikiliza.

MAIKO: Patrick, yule mtu uliyekuwa unamuulizia ameshawasili na muda mfupi ujao atakuwa hapa nyumbani.

PATRICK: Nani huyo?

MAIKO: Anaitwa Mashaka ndio huyo ambae ataenda na Tusa kwenye kazi.

Moyo wa Patrick ukalia paaaa baada ya kusikia mtu huyo ataenda na Tusa kwenye kazi.


Deborah alishangaa sana kuona mida inazidi kukatika bila kuwasili Patrick.

DEBORAH: Kwakweli nashangaa sijui mwanangu amepatwa na nini njiani jamani!

SELE: Hata me nimeshangaa ila tujipe moyo tu kuwa atafika.

DEBORAH: Ndio hivyo yani hadi akili haikai.

Muda ukaenda, usiku sana ukafika wakaamua kulala tu.

Hadi kesho yake hakuonekana Patrick wala mfano wake kitu ambacho kilizidi kumuumiza Deborah na kumtia simanzi moyoni.

DEBORAH: Simu yake haipatikani, sijui hata kapatwa na nini?

SELE: Mamdogo tumuwazie mema tu aweze kurudi, mawazo mabaya tuyaweke kando.

SELE: Sawa mwanangu.

Deborah aliendelea kujiuliza maswali mengi sana bila ya majibu.


Patrick akawafata baadhi ya vijana wa Maiko ili awaulize kuhusu huyo Mashaka.

Akamfata moja kwa moja kijana aliyeitwa Talo.

PATRICK: Eti Talo, huyu jamaa Mashaka anajishughulisha na nini huku?

TALO: Inamaana hujui? Huyu ndio hununua viungo vya binadamu.

PATRICK: Binadamu wa aina gani?

TALO: Mauaji mengi tunafanya kwaajili yake, kama la yule mzee mwenye upara.

PATRICK: Sasa yeye anafanyia nini hivyo viungo?

TALO: Huwa anapeleka Nigeria huko na kwingineko, ni jamaa mwenye pesa sana.

PATRICK: Mmh! Kwahiyo huwa anawapangia watu wa kuwaua?

TALO: Ni yule mzee tu ndio alitoa maelekezo ila mara nyingi huwa anaagiza tu labda nataka shingo ya mtu mnene basi sisi tunamzia yeyote mnene tunafyeka tu, malipo yake ni makubwa sana ndomana hatukaukiwi na pesa kwa ajili yake.

Patrick akapata picha ya kitu na kuanza kuingiwa na hofu kuhusu Tusa.


Maiko alimuita Patrick ili wazungumze kuhusu Tusa.

MAIKO: Sasa Patrick, huyu ndugu yangu ataondoka na Tusa kwaajili ya kazi.

PATRICK: Kwanini jamani? Mbona wanifanyia hivyo Maiko?

MAIKO: Usijari, nitakupatia milioni mia moja kwaajili ya hiyo kazi Patrick. Tunatengeneza pesa ya maana hapa.

PATRICK: Hapana bhana.

MAIKO: Hivi kazi gani Patrick ikupatie pesa yote hiyo? Tena hiyo milioni mia moja ni kianzio tu, kazi ikikamilika utapata milioni mia tano. Patrick hupendi utajiri wewe? Fikiria mambo mazuri hayo.

Moyo wa Patrick haukuafikiana kabisa na swala hilo kwani Tusa alikuwa na hali mbaya sana, halafu akatambua kwamba thamani ya Tusa ni zaidi ya hiyo milioni mia tano na pia ni zaidi ya pesa yoyote, huruma ilimjaa Patrick dhidi ya Tusa.

Patrick akaamua kupambana kwaajili ya kumtetea Tusa.


Patrick akaamua kupambana kwaajili ya kumtetea Tusa.

Wakati Patrick anajipanga kupambana huku Mashaka na Maiko nao wanapanga namna ya kuondoka na Tusa.

Patrick akamfata tena Maiko.

PATRICK: Kwahiyo umedhamiria kabisa Tusa aende na Mashaka?

MAIKO: Tatizo liko wapi Patrick? Fikiria mambo ya pesa kwanza.

PATRICK: Hapana, nampenda sana Tusa siko tayari kumpoteza kizembe hivyo.

MAIKO: Sasa unataka kufanyaje Patrick? Unataka kupambana? Unajua wazi huna la kufanya sababu unataka ataenda hutaki ataenda tu.

PATRICK: Lakini huo ni uonevu Maiko, Tusa ndiye binti pekee nimpendaye.

MAIKO: Duniani kuna wasichana warembo maelfu kwa maelfu, na ukiwa na pesa unampata yeyote umtakaye, sasa wewe kinakushinda nini kumtoa Tusa mmoja na kuingiza pesa nyingi zitakazofanya uwapate kama hao zaidi ya kumi! Fikiria mara mbili Patrick, mwanamke si ndugu yako ikitokea tenda uza mmoja uwapate wengi zaidi bila ya shida.

PATRICK: Mmh! Na mama yangu ulitaka kumuuza nini?

MAIKO: Deborah nilimpenda ila alitiwa uwaruwaru na wewe, alikuthamini wewe tu hadi kuniibia na kutoroka nawe.

PATRICK: Ila ingetokea kama hivi ungemuuza?

MAIKO: Patrick, weka hili kwenye akili yako, pesa kwanza mapenzi baadae. Mwanamke si chochote kwenye pesa, hawa ni viumbe dhaifu huwa tunawatoa sadaka tu kwanza wapo wengi sana humu duniani.

PATRICK: Kwahiyo nisimtetee Tusa?

MAIKO: Wazo lako la kumtetea Tusa lifute kabisa kwenye kichwa chako, Mashaka ni mtu hatari sana anaweza kukumaliza ingawa bado mimi nakuhitaji. Cha msingi fikiria pesa tu Patrick.

Patrick akawaza sana, akaona akitumia nguvu atashindwa kumtetea Tusa kwamaana Maiko ana kundi kubwa sana, akaamua kutafuta njia nyingine ya kumuokoa nayo ni kuwa karibu na Maiko.


Pamela alikaa na kufikiria sana kuhusu mtoto wake, alikosa raha kabisa, muda wote aliona sura ya Tusa ikimjia kwa huzuni.

PAMELA: Mama, lazima nifanye kitu kuhusu mwanangu.

REHEMA: Utafanyaje sasa?

PAMELA: Naenda Arusha kumtafuta mama.

REHEMA: Mmh utaanzia wapi sasa?

PAMELA: Popote pale lakini lazima nikamtafute kwakweli.

REHEMA: Nakuhurumia mwanangu mmh! Ni kweli roho inauma kuhusu huyo mtoto, lakini wewe kwenda Arusha naona kama utahatarisha maisha yako vile.

PAMELA: vyovyote itakavyokuwa mama lakini lazima nikamtafute mwanangu, nimepanga kati ya siku mbili tatu niondoke, nitaongea na Tina atakuja kukaa na wewe hapa mama.

REHEMA: Lakini mwanangu....

PAMELA: Usinizuie mama, nimeshaamua.

Pamela hakutaka ushauri zaidi, alishaamua kwenda kumtafuta mwanae, akawa anapanga safari ya kwenda sasa.


Patrick akiwa amewaza sana, akaenda tena kwa Maiko huku akionekana kufurahia kile kitendo cha Tusa kuchukuliwa na mashaka.

PATRICK: Hivi safari yenyewe lini?

MAIKO: Ni kesho kutwa bhana.

PATRICK: Natamani hata iwe kesho.

MAIKO: Kwanini?

PATRICK: Aaah mi nawaza mkwanja bhana, nataka niongeze magari mengine.

MAIKO: Umekuwa mjanja sasa Patrick, huo ndo uanaume. Sio kufikiria hawa wanawake wasio na faida.

PATRICK: Hivi ataenda nae wapi?

MAIKO: Dubai bhana ila analalamika kuwa mwanamke mwenyewe anatapika tapika damu kila mara.

PATRICK: Kama anataka kufa si afe tu.

MAIKO: Akifa kabla ya kazi ataharibu bhana, huyu atamalizwa kazi ikiisha halafu atakuwa bonge la dili.

Patrick akaanza kutambua tambua nia ya Maiko kuwa ni kummaliza Tusa kabisa ili asiwepo tena katika uso wa dunia.

Patrick akaenda kumuona Tusa ambaye alikuwa anatia huruma sana, ingawa Patrick alikuwa na roho mbaya kipindi hicho ila alimuhurumia sana Tusa na hakuweza kumuangalia kwa muda mrefu.

Patrick akaenda kuzungumza na Mashaka kwa mara ya kwanza.

PATRICK: Umemuonaje yule binti? Anafaa sana eeh!!

MASHAKA: Tena sana, yani yule binti ana vivutio vingi sana kwenye mwili wake.

PATRICK: Kumbe umejaribu kumchunguza kidogo?

MASHAKA: Nimemchunguza ndio, kwanza ile michirizi yake ile saivi ndio dili, nimefurahi sana kumkuta nayo, halafu ule mwanya pia ni dili na ile shingo yake ya kujikata mmh! Alikuwa demu bomba sana, isingekuwa biashara hata na mimi ningemchumbia.

PATRICK: Michirizi ndio nini kwani?

MASHAKA: Mistari flani hivi kwenye mwili, wengine huwa wanasema ni mistari ya unene sijui ingawa si kila mwenye nayo ni mnene. Basi ile nayo wameagiza sasa.

PATRICK: Hii biashara ni nzuri sana, halafu mimi nawajua wengi tu wenye hiyo mistari.

MASHAKA: Tatizo ile imejificha, vipi unaweza kunilengeshea mmoja ili niondoke na viungo vyake wakati naondoka na Tusa?

PATRICK: Hakuna tatizo, kesho nitawapatia mmoja mkashughulike naye.

Patrick alitafuta njia ya kuweza kushughulikia kile anachokiwaza kwenye akili yake.

Akamfata na Maiko,

PATRICK: Nimeongea na Mashaka kasema kuwa mwanya nao ni dili saivi.

MAIKO: Sasa utasaidiaje kwa hili?

PATRICK: Kuna mdada nimemzoea huyo, nae pia ana mwanya. Unaonaje nikuunganishe naye ili tummalize na tujitengenezee pesa zaidi?

MAIKO: Wazo zuri sana, sasa itakuwaje?

PATRICK: Kesho kama vipi nitakuunganisha nae.

MAIKO: Hayo ndio mambo ya kufikiria, kitu pesa tu.

PATRICK: Ila wapo wengi tu.

MAIKO: Ni kweli, ila huwa poa kama mtu akiwaunganishia. Unafanya kazi haraka hapo.

Patrick akaonao ngoja ajaribu bahati yake.


Pamela akajiandaa kwaajili ya safari ya kwenda Arusha.

PAMELA: Mama, kesho asubuhi na mapema naondoka na Mtei kwenda Arusha, na tiketi nimeshakata.

REHEMA: Yani umedhamiria kabisa Pamela?

PAMELA: Yani hii ndio sirudi nyuma, najua Adamu atashangaa akirudi toka huko Bagamoyo ila ndio hivyo akija mwambie tu.

REHEMA: Kwanini usingemngoja mshauriane?

PAMELA: Mama, naona anakawia tu, ngoja niende itajulikana hukohuko Arusha.

Kesho yake asubuhi na mapema, Pamela akasafiri na kuelekea Arusha.


Patrick akaenda kuzungumza na machangudoa wawili na kuwanunua.

Akaenda kuwaweka hotel tofauti na kuwaahidi pesa nyingi baada ya huduma, walichotakiwa kufanya ni kumsubiri tu, aliwakabidhi pesa kidogo kama kianzio ili wasiondoke, kila changudoa mmoja aliamini kuwa Patrick yuko kwa mwenzake kwahiyo akawa anangoja amalize kule ili nae aje kufanya kazi yake.

Patrick alipofika karibia na nyumba ya Maiko, akampigia simu Mashaka kwanza na kumuelekeza alipoacha funguo, kitendo hicho kilimfanya Mashaka ajiandae na kuchukua baadhi ya vijana na kuondoka nao, halafu akampigia simu Maiko, nae ikawa hivyo hivyo kwa mawazo yao watamkuta Patrick eneo la tukio.

Patrick akaingia getini kwa Maiko na gari yake, chumba alichowekwa Tusa alibaki mlinzi mmoja tu, ikabi Patrick amlaghai mlinzi huo na kumtuma huku akidai kuwa atabaki yeye, yule mlinzi akaenda alipotumwa.

Patrick akaingia ndani na kumbeba Tusa begani akampakia nyuma ya gari na kuondoka, mlinzi wa getini hakujua lolote, kwahiyo alimfungulia geti na kutoka.

Patrick hakutaka kupoteza muda sehemu yoyote, akaendesha lile gari kwa mwendo wa ajabu ili mradi afike mahali ambapo ataweza kujificha na Tusa kwanza huku akitafuta usafiri wa haraka wa kuwaondoa kabisa eneo hilo.


Pamela akiwa ndani ya Arusha, hatambui hili wala lile.

Alipofika alilala nyumba za kulala wageni na kesho yake akaanza kumsaka Tusa, katika pitapita zake akakutana na mwanaume wa makamo ambapo Pamela alimuona ni mwanaume mwenye heshima zake kumbe alikuwa ni Maiko ambaye yupo katika harakati za kuwatafuta Patrick na Tusa.

Pamela akaamua kumuuliza kuhusu Tusa.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Pamela akaamua kumuuliza kuhusu Tusa.

Akasalimiana nae kwanza na kumuuliza.

PAMELA: Samahani baba naomba nikuulize kidogo.

MAIKO: Bila samahani mama, uliza tu.

PAMELA: Nina binti yangu ameolewa huku Arusha ila sijui anapoishi halafu sina mawasiliano nae.

MAIKO: Sasa wewe hujui kama Arusha hii ni kubwa sana? Hujui anaishi wapi wala huna mawasiliano nae, unadhani utampata kweli? Au huyo binti yako ni mtu maarufu?

PAMELA: Hapana sio maarufu ila mi naulizia tu labda unaweza ukawa umewasikia sehemu.

MAIKO: Anaitwa nani kwani?

PAMELA: Anaitwa.....

Kabla hajataja, simu ya Maiko ikaita nae Maiko akaipokea.

MAIKO: Nipe taarifa Tulo.

TULO: Kuna mahali ambapo Tusa na Patrick walionekana ndio nataka nikaangalie.

MAIKO: Hebu nenda haraka na mimi nakuja, huyu Patrick ni mshenzi sana.

Pamela akashtuka kusikia hilo jina la Patrick, Maiko alipomaliza kuongea na simu akasahau kabisa kama kuna mtu alikuwa anaongea nae, alichofanya ni kufungua gari yake na kuingia, kitendo kilichofanya Pamela amfate dirishani na kumwambia.

PAMELA: Hata mimi, huyo mume wa mwanangu nae anaitwa Patrick.

MAIKO: Wee mama wewe hebu niondolee maswahibu mie, wakina Patrick wamejaa wengi sana hapa Arusha bhana.

PAMELA: Labda unaweza kumjua mkewe anaitwa Tusa.

Maiko alishaanza kuondoa gari, aliposikia jina la Tusa ikabidi asimamishe gari na kushuka, kisha akamfata Pamela.

MAIKO: Umesema anaitwa nani?

PAMELA: Mwanangu anaitwa Tusa na mumewe anaitwa Patrick.

MAIKO: Ooh!! Mama hao nawafahamu sana, panda kwenye gari nikupeleke kwao.

Pamela bila kutambua akapanda kwenye gari ya Maiko.


Tusa alikuwa akishindwa hata kutembea kwani damu nyingi ilikuwa inamtoka sehemu za siri ni bora walikuwa na gari.

Patrick hakujua afanye nini na Tusa kwani alikuwa ananuka damu mwili mzima, ndipo alipoomba mahali ambapo Tusa aliweza kuoga na Patrick akamtolea nguo nyingine ambapo Tusa aliweza kubadilisha, jambo zuri alilofanya Patrick ni kubeba baadhi ya nguo zake na nguo za Tusa kwenye gari kabla ya kutoroka kwao.

PATRICK: Haya tuondoke Tusa.

TUSA: Tungekaa kaa kidogo hapa kwakweli nimechoka halafu najisikia vibaya sana.

PATRICK: Twende bhana, utapumzika kwenye gari. Tatizo lako hujamjua vizuri Maiko.

TUSA: Kwani wewe na huyo Maiko mna tofauti gani? Mi naona mko sawa tu, wote mna roho mbaya tena za shetani.

Patrick akaona kubishana na Tusa ni kupoteza muda, alichofanya ni kumnyanyua kwa lazima na kumuweka kwenye gari halafu safari ikaendelea, baada ya muda kidogo tu Tulo alifika eneo lile akiwa na vijana wengine wawili, wakajaribu kuwaulizia wakaambiwa kweli walikuwepo eneo lile ila wameshaondoka, walichukia sana na kuendelea kuulizia maeneo tofauti tofauti yani pale panapoonekana uwepo wa gari ya Patrick.


Adamu alisikitishwa sana na habari kuwa mkewe kaenda Arusha kumtafuta Tusa.

ADAMU: Kwanini asingeningoja jamani?

REHEMA: Hata mimi nilimshauri hivyo ila hakutaka kunielewa.

ADAMU: Mama, hivi mimi ukiniangalia unaniona ni mtu wa ajabu sana?

REHEMA: Hapana, upo kawaida tu mwanangu.

ADAMU: Mbona hawa wanawake wananichukulia tofauti? Najua kwa yule mke wangu wa kwanza nilikosea sana, sikutaka kufanya makosa hayo kwa Pamela ila mbona nae ameniogopa hivyo? Ameondoka bila kusikia kauli yangu.

REHEMA: Mwanangu, swala ni kwamba ameumizwa na upotevu wa mtoto wenu. Usimlaumu sana na wala usimfikirie vibaya.

ADAMU: Sasa mimi nifanye nini kwasasa?

REHEMA: Hakuna la kufanya zaidi ya kusikilizia majibu ya Pamela tu.

ADAMU: Na akipatwa na matatizo je?

REHEMA: Tumuombe Mungu tu amuepushie mabalaa yote.

Kwakweli Adamu hakupendezewa kabisa na kitendo cha mkewe kuondoka bila ya kushauriana nae.


Patrick alipofika mbele zaidi akamuona mtu mwenye gari pia, akamuomba wabadilishane, yule mtu alikubali haraka kwavile gari ya Patrick ilikuwa ni mpya na ya gharama zaidi. Wakabadilishana kila kitu halafu Patrick akaondoka na gari ya mtu huyo.

Wakiwa njiani, Tusa akaanza kumlalamikia Patrick.

TUSA: Binadamu gani wewe una roho mbaya kiasi hicho, unashindwa hata kunipeleka hospitali!

PATRICK: Wee Tusa funga domo lako chafu hilo, mi nahangaika hapa kwaajili yako halafu wewe unataka kuniletea maneno yako machafu nitakubadilikia sasa hivi nakwambia.

Tusa ikabidi akae kimya kwani anamjua Patrick alivyo kwahiyo akahofia kubadilikiwa pale. Akaamua kuongea kwa upole tu.

TUSA: Ila Patrick damu zinanitoka nyingi sana.

PATRICK: Sasa hizo damu zako mimi zinanihusu nini? Kama zinatoka acha zitoke tu.

TUSA: Nadhani mimba itakuwa imetoka.

PATRICK: Kama imetoka, thanks to God maana hiyo mimba yenyewe hata haijulikani ni ya nani.

TUSA: Ni ya kwako Patrick.

PATRICK: Ya kwangu wapi bhana! Mwanamke mwenyewe umebakwabakwa hovyo, uzuri wote umekupotea Tusa, umekongoroka vibaya sana.

Tusa alichomwa sana na yale maneno, ingawa Patrick alikuwa akiyaokoa maisha ya Tusa ila Tusa aliendelea kumuona Patrick kama mtu mwenye roho mbaya sana duniani.


Maiko akampeleka Pamela hadi nyumbani kwake, Pamela akashangaa kufika humo ndani akawekewa kizuizi cha kutoka.

MAIKO: Nisikilize kwa makini wewe mwanamke, mwanao kajifanya mjanja na kutoroka hapa na mumewe kwahiyo wee hutoruhusiwa kutoka hapa hadi mwanao apatikane.

PAMELA: Lakini hukuniambia hivyo mwanzo, huku si kunitendea haki jamani.

MAIKO: Tena utulie kabisa, ukizingua nakufumua fumua.

PAMELA: Ila mi sina makosa.

Maiko akampokonya Pamela kila kitu alichobeba hadi simu.

PAMELA: Basi naomba simu nimwambie hata mume wangu kilichonipata.

MAIKO: Hivi wewe mwanamke una kichaa? Hapa mahali sio pa mchezo kabisa unatakiwa utulie tuli.

Maiko akaondoka na kumuacha Pamela na baadhi ya walinzi, yeye akaenda kuzungumza na Mashaka.

MAIKO: Yule malaya tumempata mama yake mzazi.

MASHAKA: Vipi wanafanana?

MAIKO: Labda makalio tu ila vingine hawafanani sana.

MASHAKA: Sasa itakuwaje?

MAIKO: Tumtumie huyu mama kuwapata Patrick na Tusa au kama vipi tummalize yeye bhana.

MASHAKA: Ila je tutapata chochote toka kwake?

MAIKO: Tutapata tu kwamaana hata na yeye ni mrembo pia, njoo badae umchek.

Maiko akarudi nyumbani kwake na kumkuta Pamela akifanya fujo za kutaka kutoka, Maiko hakuwa na huruma kabisa, alichofanya ni kumshindilia mingumi hadi Pamela akapoteza fahamu na kuanguka chini, mara muda kidogo Mashaka akafika kumuangalia Pamela kama analipa.

Mashaka alipomtazama Pamela alishtuka sana, kitendo hicho kilimshtua hata Maiko kuwa kwanini Mashaka kashtuka kumuona Pamela pale chini?


Mashaka alipomtazama Pamela alishtuka sana, kitendo hicho kilimshtua hata Maiko kuwa kwanini Mashaka ameshtuka baada ya kumuona Pamela?

Mashaka akainama chini, kama vile akimkagua Pamela mara gafla akainuka na kutoka nje. Bado Maiko hakumuelewa Mashaka kwanini amebadilika gafla, akashindwa kumuuliza kwa muda ule, akangoja atulie kwanza ndipo amuulize.

Maiko nge akatoka nje na kumuona Mashaka amekaa mahali akiwa na mawazo sana, akaona asimsogelee kwanza. Alichoamua kufanya muda huo ni kumpigia simu Patrick na kumpa habari za mama mkwe wake, ila simu iliita bila kupokelewa. Tangia Patrick alivyotoroka na Tusa, hakutaka kabisa kupokea simu ya aina yoyote.


Patrick akiwa na Tusa kwenye gari na baada ya kuona kwamba simu inaita sana, akamwambia Tusa aichukue ile simu na kuizima.

Tusa alipochukua ile simu na kuona mpigaji ni Maiko, akataka kujua kuwa Maiko anataka kusema, akapokea simu ile na kuiweka sikioni.

MAIKO: Umejifanya mjanja sana Patrick kuondoka na Tusa, sasa huku tumempata mama yake na Tusa na hatutamwachia mpaka pale utakapotuletea Tusa, tutamtesa na kumtumikisha huyu mama.

Maiko alikuwa anaongea huku anacheka sana, Tusa alijikuta akishusha simu chini na kusema "mamaaa!!"

PATRICK: Vipi wewe Tusa?

TUSA: Maiko anasema amempata mama yangu na atamtesa hadi pale nitakapopatikana.

Patrick akasimamisha gari na kumuuliza Tusa.

PATRICK: Umepata wapi hiyo habari?

TUSA: Nimepokea simu yako hapa wakati Maiko anapiga.

PATRICK: Haya lete hiyo simu.

Tusa akamkabidhi Patrick ile simu na Patrick akaizima kabisa, kisha akamgeukia na kumuuliza tena.

PATRICK: Nani kakutuma upokee simu Tusa?

TUSA: Sijui ila nimejikuta tu nimepokea.

PATRICK: Tatizo lako Tusa una akili ndogo sana, nilikuwa nakuangalia tu unapopokea hii simu. Unapenda mi nionekane mbaya kwako muda wote, siku zote ubishi wako ndio huwa unakuponza wewe.

TUSA: Jamani Patrick, sasa itakuwaje kuhusu mama?

PATRICK: Unataka iwaje? Unataka turudi tukamatwe?

TUSA: Siwezi vumilia kuona mama anakufa kwaajili yangu, ni vyema nirudi mimi ili yeye apone.

PATRICK: Ndiomana nyie wanawake huwa hamsaidiwi nyie, akili zenu ni fupi sana. Hapa nahangaika kukuokoa wewe halafu unaniletea habari za mama yako, unaugua nini wewe? Safari inaendelea hakuna kurudi nyuma.

TUSA: Jamani mama yangu atakufa, hakuna wa kumtetea.

PATRICK: Mungu atamtetea.

Patrick akawasha gari na kuendelea na safari.

TUSA: Nishushe Patrick, niache nirudi nikamsaidie mama yangu.

PATRICK: Ukitaka kuona nina roho mbaya ya kiasi gani endelea kufanya fujo ujute, nitakufumua fumua vibaya vibaya bila kujali nakupenda kiasi gani. Usinione fala kuwasaliti wenzangu kwaajili yako, nimeamua tu kukuokoa toka kwao sasa jitulize tufike salama.

Ikambidi Tusa atulie kwani alimjua wazi Patrick kuwa si mtu wa mizaha.

INAENDELEA


Post a Comment

0 Comments