Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Beyond Love (Zaidi ya Mapenzi) Sehemu ya Kumi Na Sita (16)

 


“Tom?”

“Ndiyo!”

“Unataka kuonana na mimi?”

“Ndiyo!”

“Kuna nini?”

“Ni vizuri tuonane, siwezi kuzungumza kwenye simu!”

“Namba yangu ni nani amekupa?”

“Hilo siyo la muhimu kujua kama ambalo linanifanya nikuite!”

“Tukutane wapi sasa?”

“Nitakuja Mlimani City!”

“Wapi sasa?”

“Samaki Samaki!”

“Sawa, saa ngapi?”

“Saa mbili kamili usiku nitakuwa hapo!”

“Huwezi kufanya mapema zaidi?”

“Muda huo ni mzuri zaidi kutokana na aina ya maongezi niliyonayo!”

“Ok!”

“Kazi njema!”

Moyo wa Mariam ulilipuka sana, hakujua Tom alikuwa na kitu gani cha kumwambia hasa ukizingatia alikuwa akisikia kila kukicha juu ya maandalizi ya ndoa yake. Hata hivyo, aliisubiri jioni hiyo kwa hamu kubwa sana, alihisi kama mshale wa sekunde hautembei ipasavyo. Ikawa saa la kwanza, la pili hatimaye saa moja na nusu ilipofika alikuwa kwenye teksi akielekea Mlimani City kukutana na Tom.

Alifika Mlimani City saa 1:48 za usiku, akiamini alikuwa amewahi sana lakini cha ajabu alimkuta Tom akiwa anamsubiri kwa hamu kubwa sana. Mariam akamsogelea sehemu aliyokuwa amekaa akitetemeka kwa woga, hakuamini kama aliyekuwa amekaa mbele yake alikuwa Tom.

“Habari yako mrembo?” Tom akamsalimia.

“Nzuri! Mbona tumekaa sehemu ya wazi kiasi hiki? Kumbuka wewe ni mtu maarufu na isitoshe ndoa yako ipo mbioni kufungwa, huogopi wapiga picha wa udaku?”

“Wapo wanaosimamia hilo, siyo rahisi kupigwa picha, vijana wangu wapo kazini!”

“Sawa basi, sema ulikuwa unasemaje?” Mariam akauliza akiwa mtulivu sana.

Tom hakuongea chochote zaidi ya kutoa kadi na kumkabidhi. Mariam akaifungua na kuisoma, ilikuwa ni kadi ya mwaliko wa harusi yake ambayo ilikuwa inafanyika siku tatu zilizofuata.

“Umeamua kuja kunitukana? Hujatosheka na mateso uliyonipa?”

“Tulia mrembo huwezi kujua nina maana gani, lakini naomba usiache kuja, nina bonge la surprise kwa ajili yako!”

“Surprise?”

“Ndiyo, niamini tafadhali, naomba usipuuze!”

“Lakini wewe siku hiyo ndiyo unaoa na unafahamu kabisa ni kiasi gani nakupenda, unataka niumie moyo wangu kwa mara nyingine?”

“Sina maana hiyo Mariam, nakuomba uje halafu nakuhakikishia furaha. Amini siku hiyo itakuwa ya furaha kuliko zote zilizowahi kutokea katika maisha yako!” Tom alitumia kila aina ya maneno matamu kumshawishi, mwishowe akakubali.

Akatoa bahasha ya khaki ambayo ndani ilikuwa na milioni moja, akamkabidhi kama nauli. Mariam akakubali kufika kwenye harusi ya Tom.

******

Watu walikuwa wamefurika ndani ya meli, wakisubiria kwa hamu kubwa sana ndoa ya Julina na Tom ambayo ilikuwa ya aina yake. Ibada iliendelea kama kawaida, baadaye Mchungaji akawaita Tom na Juliana mbele kwa ajili ya kuwafungisha ndoa. Watu walipiga vigelegele na makofi wakiwashangilia.

“Je, Bi. Juliana David Mongara, umekubali kuolewa na Bw. Thomas Chacha, awe mumeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Mchungaji Samwel Kiswele aliuliza.

“Ndiyo Mungu anisaidie!” Juliana akajibu akimtizama Tom machoni mwake, moyo wake bado ulikuwa na wasiwasi mwingi.

Baada ya hapo Mchungaji Kiswele akamgeukia Tom na kumuuliza; “Je, Bw. Thomas Chacha, umekubali kumuoa Bi.  Juliana David Mongara, awe mkeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Hilo lilikuwa swali gumu sana kwa Tom, akamwangalia Juliana usoni kisha akarudisha macho yake kwa waalikwa, yakagongana na ya Mariam.

Machozi yakaanza kumtoka.

“HAPANA MCHUNGAJI SIPO TAYARI!” Watu wote wakapingwa na butwaa. Juliana akiwa haamini alichokisikia, Tom akatoka mbio na kwenda kumshika Mariam mkono, ambaye mpaka wakati huo alikuwa haelewi kinachoendelea, akamwongoza hadi mbele. Akatoa pete iliyokuwa mfukoni mwake, kisha akachukua kidole cha Mariam na kumvalisha.

“Kuanzia sasa, wewe ndiye mchumba wangu na ninakuahidi sitakutesa katika siku zote za maisha yako! Tumuombe Mungu siku ya ndoa yetu ifike. Sherehe hii ni kwa ajili ya kumvalisha mchumba wangu Mariam pete ya uchumba, aliyonifanyia Juliana yanatosha!” maneno hayo yalipenya moja kwa moja masikioni mwa Juliana, hakuamini alichosikia,

Ghafla akahisi kizunguzungu, akaanza kuporomoka taratibu, mwisho akaanguka chini kama mzigo.




Ikiwa imebaki wiki moja tu kabla ya ndoa ya Juliana na Tom, Juliana anamsaliti Tom kwa kutembea na rafiki yake wa karibu sana aitwaye Joseph! Tom anashuhudia kwa macho yake jinsi mpenzi wake aliyempenda Juliana akifanya uchafu katika kitanda chao.

Haikuwa rahisi kuvumilika, Tom akaanguka chini kama mzigo! Baadaye akazinduka akiwa katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam. Muda mfupi baadaye anatoekea Juliana ambaye analia na kuomba msamaha.

Tom anakubali kumsamehe na wanakubalina kufungua ukurasa mpya! Taratibu za ndoa zinaendelea kama kawaida, ingawa akilini mwa Tom kulikuwa na kitu kingine zaidi, alipanga kumuumiza Juliana siku ya ndoa yao.

Alichokifanya ni kukutana na mpenzi wake wa zamani Mariam ambapo alimuomba sana asiache kuhudhuria hasuri yake ambayo ilipangwa kufanyikiwa ndani ya meli katikati ya Bahari ya Hindi. Mariam anakataa lakini baada ya kumshawishi kwa muda mrefu akakubali.

Siku ya ndoa, Juliana alipoulizwa na Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom alikubali, lakini Tom alipoulizwa kama alikuwa tayari kumuoa Juliana alikataa. Muda mfupi baadaye akamwita Mariam mbele na kumvalisha pete ya uchumba mbele za wageni waalikwa.

Watu walishangaa sana, Juliana akashikwa na uchungu mwingi sana, akashindwa kuzuia hisia zake, akaanguka chini na kupoteza fahamu. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....


Ukumbi mzima ulikuwa kelele tupu, utulivu uliokuwepo awali ulitoweka ghafla. Kulikuwa na makundi mawili katika kelele zile, wapo waliokuwa wakimsapoti Tom na wengine waliokuwa wakipingana naye. Waliokubaliana na Tom ni wale waliokuwa wakifahamu vizuri historia yake na Mariam.

Mama yake Tom hakuamini kilichotokea, akaenda mbele haraka akimfuata mwanaye. Wakati huo huo wengine walikuwa wakimchukua Juliana na kumpeleka kwenye chumba cha Huduma ya Kwanza kwa ajili ya kumhudumia.

Dakika moja baadaye mama Tom alikuwa ameshafika mbele baada ya kujipenyeza katikati ya watu waliokuwa wakizozana kutokana na tukio lililokuwa limetokea siku hiyo. Tom hakuwa na habari kabisa na mama yake, aliendelea kumkumbatia Marima huku machozi yakimtoka.

Mariam hakuamini kabisa kilichokuwa kikitokea, alihisi kama alikuwa katika njozi kali na pengine baada ya muda mfupi angezinduka. Hata hivyo baada ya kutingisha kichwa chake kwa nguvu aligundua kwamba hakuwa anaota kama alivyokuwa akifikiria.

“Tom mwananu, umefanya nini?” Mama Tom akamuuliza mwanaye.

“Unaaminisha nini mama?”

“Kwanini unatuharibia sherehe?”

“Sijaharibu sherehe mama, sherehe iliyopo hapa ni ya kumvalisha pete ya uchumba Mariam, hiyo ndoa yangu na Juliana haipo na wala sitaki kuisikia!”

“Kwanini hukusema mapema kuliko kuja kumuaibisha mwenzio na familia yake?”

“Ilikuwa lazima nifanye mama!”

“Kwanini unasema hivyo?”

“Naomba MC anipe kipaza sauti nitoe sababu za msingi za mimi kukataa kumuoa Juliana dakika za mwisho, najua mnanihukumu bure na hiyo ni kwasababu hamjui kilichotokea. Nipeni nafasi niseme ukweli!” Tom akasema akimtizama mama yake kwa makini sana.

Mama Tom akatoka na kumfuata MC ambapo alimuomba kipaza sauti na kumpelekea Tom ambaye bila kuchelewa alianza kuzungumza.

“Najua wengi mnanilaumu kwa kitendo changu cha kukataa kumuoa Juliana, lakini naamini nikiwapa sababu za msingi mtanionea huruma. Hata wewe mama yangu ambaye umekuja hapa mbele na kunisema kwamba nimekuabisha, utagundua kuwa Juliana ndiye aliyekuabisha.

“Naamini hata wazazi wa Juliana na ndugu zake wote watajua wazi kwamba mtoto wao ndiye aliyeleta aibu hii katika hii sherehe. Juliana hafai kabisa, ni mwanamke mwenye sura ya kike lakini siyo mke.

“Nilimpenda sana Juliana, moyo wangu nikamkabidhi yeye  nikiamini kwamba angekuwa furaha ya maisha yangu, lakini imekuja kuwa tofauti. Juliana ameniumiza sana, amenitesa na nina uhakika alidhamiria kuniua,” Tom alikuwa akizungumza kwa hisia sana huku ukumbi mzima ukiwa makini kumsikiliza atakachokiongea.

Mpaka wakati huo, bado Tom alikuwa hajataja sababu ya msingi ya kuachana na Juliana, hivyo watu walikuwa na shauku kubwa sana ya kutaka kujua atakachokiongea.

“Wengi wenu mnafahamu kwamba wiki moja iliyopita nilikuwa nimelazwa, lakini hamjui sababu ya mimi kulazwa, ila leo nataka kuwaelezeni ukweli kwamba Juliana ndiyo cha mimi kulazwa. Nilianguka na kupoteza fahamu baada ya kumfumania Juliana akifanya mapenzi na rafiki yangu wa karibu sana Joseph!” Tom aliposema hivyo ukumbi mzima ulipigwa na butwaa.

“Aaaaaah!” Wati wote walisikika wakiguna.

“Ni maumivu kiasi gani aliyonipa Juliana? Ni nani ambaye angeweza kuvumilia maumivu hayo? Baada ya mambo hayo kutokea, niliamua kutulia, nikawaza kwa makini sana hatua ya kuchukua. Nilijua hakuna atakayenielewa kama ningehairisha ndoa.

“Kitu cha msingi ambacho kilikuwa kichwani mwangu ni kuacha taratibu zote ziendelee lakini akilini nikijua kwamba itakuwa ni sherehe ya kumvalisha Mariam pete ya uchumba na siyo ya ndoa yangu na Juliana. Nilikumbuka mengi aliyonifanyia Mariam, nikasikia uchungu sana.

“Mariam alinisaidia sana wakati nikiwa na shida, aliiba gari lao na kumpeleka baba yangu hospitalini akiwa hoi usiku wa manane. Kwa bahati mbaya wakati anarudi  nyumbani, alipata ajali mbaya na kulala kitandani akiwa hajitambui kwa zaidi ya miaka minne!

“Yote hayo alifanya kwa ajili yangu, sikuwa na zawadi nyingine ya kumpa zaidi ya penzi la kweli kwake. Hiyo ndiyo zawadi ya pekee ambayo naona inamfaa kwa wema wote alionitendea. Mariam alikuwa katika hatari ya kufa, kupoteza fahamu kwa zaidi ya miaka minne ni nusu ya kufa, inawapasa wote mfahamu kwamba Mariam alikuwa katika hatari hiyo kwa ajili ya penzi lake kwangu!

“Kwanini nimuumize tena? kwanini nimtese tena? Pamoja na utajiri nilionao sasa, usaliti wa Juliana ulinifanya nikumbuke maisha yangu ya dhiki na taabu. Ni kitu gani alichokikosa kwangu hadi aanze kutembea na Joseph? Huyo Joseph ana nini ambacho mimi sina? Kwa hakika Juliana alinipa kidonda kikubwa sana katika moyo wangu lakini sasa nimeshapata tiba.

“Mariam ni tiba tosha katika maisha yangu. Naomba sherehe iendelee lakini ikumbukwe kwamba ni sherehe ya kumvalisha mchumba wangu Mariam pete, ni matumaini yangu kwamba siku chache zijazo, mtashuhudia ndoa yetu nzuri sana, itakayopendeza!” Tom alisema watu wakiwa kimya kabisa kumsikiliza.

Maneno aliyoongea yalikuwa makali san, watu wote walimwonea huruma, lakini wapo waliompongeza kwa ujasiri wake.

“Ana moyo sana huyu mtoto!” Mama mmoja aliyealikwa alimwambia mwenzake.

“Ni kweli, kama ni mtu mwingine asingeweza kuvumilia!”

“Lakini kuna kitu nahisi!”

“Kitu gani?”

“Unajua kwa jinsi Mariam alivyomsaidia, ilikuwa lazima arudiane naye siku moja!”

“Kwanini unasema hivyo?”

“Mapenzi yana nguvu sana ndugu yangu, kama mtu aliweza kuhatarisha uhai wake kwa sababu ya mapenzi, unadhani uhusiano wa aina hiyo unaweza kufa hivyo?”

“Kweli kabisa, mwacheni Mungu aitwe Mungu!”

“Yeye ni kila kitu, akisema iwe na inakuwa hivyo, akisema hapana, inakuwa hapana. Hakika yeye ni mwema!” Kila mtu alikuwa akiongea lake latika ukumbi huo uliokuwa kwenye Meli.

Sherehe ikaendelea kama kawaida, ingawa utaratibu haukuwepo na hakuwa na utaratibu wa kutoa zawadi. Walishauriwa warudi nazo kwanza hadi siku ya ndoa ya Mariam na Tom. Watu walikunywa, kula na kusaza.

“Tom!” Mariam alimwita walipokuwa wamejibanza kwenye eneo lenye giza totoro.

“Nakusikiliza mpenzi!”

“Umenishangaza sana!”

“Kwanini?”

“Sikutegemea!”

“Hata mimi pia, lakini leo nimeamini kwamba Mungu yupo na akipanga lake hakuna yeyote chini ya jua anayeweza kupangua. Nakuhakikishia Mariam, Mungu alipanga mimi niishi na wewe!”

“Ni kweli mpenzi wangu, tumetoka mbali!”

“Kweli kabisa, nakuhakikishia utafurahia maisha siku zote za uhai wako ukiwa na mimi. nataka kulipa fadhila zote kwako, nataka kukuonyesha kulala kwako kitandani kwa zaidi ya miaka minne ukiwa huna kumbukumbu ya chochote kinachoendele haikuwa bure!”

“Nitashukuru sana mpenzi wangu!”

“Mariam mpenzi!” Tom akaita kwa sauti iliyojaa mahaba.

“Naomba unifanyie kitu kimoja....”

“Sema tu, mpenzi!”

“Naomba unibusu!”

“Hilo tu, sema lingine!”

“Siyo zaidi ya busu lako!”

“Haya bwana! Mmwaaaaaaaaa...” Mariama akamuangushia Tom busu maridhawa kabisa.

“Ahsante sana mpenzi!”

Baada ya sherehe kuisha, meli ilirudi hadi Bandarini na kutia nanga, watu wakashuka na kutawanyika. Tom akampeleka Mariam Hotelini kwake. Mapenzi yao yakarudi upya, yalikuwa motomoto.

******

Mwezi mmoja baadaye taratibu zote zilikuwa zimeshakamilika. Tom alitambulishwa rasmi nyumbani kwa akina Mariam kama mchumba wa Mariam, wazazi wa Mariam hawakuwa na kipingimizi. Waliruhusu watoto wao waendelee na mapenzi yao kutoakana na ukweli kwamba walianza kupendana muda mrefu kabla wakati wanasoma.

Mipango ya ndoa ikafanyika haraka sana, ilipangwa kufanyika ndoa ya kifahari kuliko kawaida. Kama ilivyokuwa wakati akitaka kufunga ndoa na Juliana ndivyo alivyofanya pia safari hii, aliamua kufunga ndoa yake katikati ya Bahari ya Hindi, wakiwa kwenye meli.

Ndivyo ilivyokuwa, siku ya harusi ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa ilifika, waalikwa walikuwa ni wengi sana. Mariam na Tom walikuwa haamini kabisa kilichotokea, walikuwa na nyuso za furaha sana kufunga ndoa yao.

Mchungaji akawaita mbele wakiwa na wapambe wao, ambapo mara moja shughuli ya kuwafungisha ndoa ikaanza.

“Je, Bw. Thomas Chacha, umekubali kumuoa Bi.  Mariam Isaya, awe mkeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Hilo lilikuwa swali rahisi sana kwa Tom, akamwangalia Mariam usoni kisha akarudisha macho yake kwa waalikwa, baada ya hapo akajibu.

“Ndiyo, Mungu anisaidie!” Ukumbi mzima ukapiga vigelegele na makofi kwa furaha.

Baada ya Tom kujibu, Mchungaji aliyekuwa akifungisha ndoa akamgeukia Mariam na kumuuliza; “Je, Bi. Mariam Isaya, umekubali kuolewa na Bw. Thomas Chacha, awe mumeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?”  Mchungaji akamuuliza lakini Mariam hakujibu.

Mchungaji akaamua kuuliza kwa mara ya pili, bado Mariam alikuwa kimya. Ghafla Mariam akaanza kutoa miguno ya taratibu, baadaye akashindwa kujizuia na kuanza kuangua kilio. Tom akashtuka sana, hata waalikwa nao walipigwa na butwaa.

“Mariam kuna nini?”

“Hakuna!”

“Mbona hujibu maswali ya Mchungaji!”

“Hapana...”

“Hapana nini?” Tom akazidi kumuuliza akiwa haelewi kinachoendelea. Mariam alizidi kulia.



Tom haamini macho yake alipomkuta mpenzi wake ambaye walikuwa na mipango ya kufunga ndoa, Juliana akimsaliti, tena na rafiki yake wa karibu aliyeitwa Joseph.

Lilikuwa tukio lililomsononesha sana, hali iliyomsababishia simanzi, kabla ya kuanguka chini na kupoteza fahamu. Baadaye anazinduka akiwa katika Hospitali ya Ocean Road, ambapo Juliana anakuwa wa kwanza kuonana naye na kumuomba msamaha.

Tom anakubali kumsamehe na wanakubaliana kufungua ukurasa mpya! Taratibu za ndoa zinaendelea kama kawaida, ingawa akilini mwa Tom kulikuwa na kitu kingine zaidi, alipanga kumuumiza Juliana siku ya ndoa yao.


Akafanya mpango wa kukutana na mpenzi wake wa zamani Mariam ambapo alimuomba sana asiache kuhudhuria harusi yake ambayo ilipangwa kufanyikiwa ndani ya meli katikati ya Bahari ya Hindi. Mariam anakataa lakini baada ya kumshawishi kwa muda mrefu akakubali.


Siku ya ndoa, Juliana alipoulizwa na Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom alikubali, lakini Tom alipoulizwa kama alikuwa tayari kumuoa Juliana alikataa. Muda mfupi baadaye akamwita Mariam mbele na kumvalisha pete ya uchumba mbele za wageni waalikwa.


Siku chache mbele, Mariam na Tom wakaamua kufunga ndoa! Kama ilivyokuwa awali,  ndoa yao ilifungwa katikati ya bahari, kwenye meli. Kitu cha kushangaza, Mariam alipoulizwa na Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom, alinyamaza.


Baadaye akaanza kulia kabisa. Tom alipomuuliza kama kulikuwa na tatizo lolote, Mariam hakujibu. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....


Kitendo cha Mariam kukataa kujibu swali la Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom au lah, kilimchanganya sana Tom, alishaanza kuhisi mchezo mchafu ulikuwa ukichezwa nyuma ya pazia. Ukimya wa Mariam ukazidi kumchanganya.


Hata hivyo alikosa raha zaidi baada ya kushangaa Mariam akianza kulia, hapo akili yake ikaenda mbali zaidi, alianza kufikiria kwamba, inawezekana Mariam alilazimishwa kumuumiza siku ya ndoa yao ili ampe maumivu lakini yeye hakuwa tayari.


Zote hizo zilikuwa hisia zilizoutawala ubongo wake, lakini mwenye majibu sahihi alikuwa ni Mariam pekee, alitakiwa kutumia kila njia anayoifahamu ili aweze kujua kilichokuwa kikiendelea. Akamgeukia Mariam wake ili amuulize kwa ajili ya kupata uhakika zaidi, tayari akili yake ilishabadilika, alipoteza matumaini ya kuwa na Mariam tena.


“Kuna nini Mariam?”


“Nishakujibu Tom.”


“Kwamba?”


“Sina tatizo.”


“Mbona unashindwa kumjibu Mchungaji, hujui kwamba ni wewe ndiye unayesubiriwa ili ndoa iweze kufungwa?”


“Najua...”


“Sasa?”


“Nashindwa kuamini kabisa.” Marim akasema akionekana kuwa na hofu sana na maneno aliyokuwa akiyaongea.


“Huamini nini tena? Kwani kuna nini?”


“Nashindwa kuzuia hisia zangu Tom, nimeshindwa kabisa.”


“Hisia za nini tena?”


“Machozi Tom, unajua wewe ndiye mwanaume pekee ambaye nilikukabidhi moyo wangu, siamini kabisa kwamba nimeweza kuwa na wewe tena katika ndoa!” Mariam akasema machozi yakizidi kumtoka.

INAENDELEA

Post a Comment

0 Comments