Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Beyond Love (Zaidi Ya mapenzi) Sehemu Ya Kumi Na Tatu (13)



 “Nini kipya unataka kunieleza Mariam? Nimeshakuambia wewe  ni mtu mbaya sana katika maisha yangu, sioni kama kuna sababu ya kuendelea kusumbuana. Haiwezekani kipindi nikiwa na matatizo unikatae halafu sasa hivi nina mafanikio ndiyo unajifanya unanililia. Huo naufananisha na unafiki! Acha unafiki Mariam!” Tom akasema kwa hasira ya wazi akimtizama Mariam machoni.

“Hapana Tom, nakupenda sana Tom wangu, Mungu ndiye shahidi wa ninac hokiongea. Nilitaka kupoteza maisha yangu kwasababu yako! Hujui kilichotokea!”

“Kwani ulipatwa na nini?”

“Siku ile wakati narudi kutoka hospitalini, nilipata ajali mbaya ya gari, nikakimbizwa hospitalini na kulazwa. Nilikuwa na hali mbaya sana maana nilipoteza kabisa fahamu kwa miaka mitano!

“Nililala kitandani kwa muda wote huo nikiwa sijui kinachoendelea, ni kama nilikuwa nimekufa! Nilipata majereha makubwa sana katika ubongo wangu hivyo kushindwa kupata fahamu katika kipindi chote hicho. Niliteseka sana, lakini nilipopata fahamu na hali yangu kurejea kawaida ndipo nikarudi tena hapa chuo, ndiyo maana unaniona nina umri mkubwa zaidi kuliko wanafunzi wengine!” Mariam alisema huku machozi yakitiririka machoni mwake kwa kasi sana.

“Pole sana Mariam, nakupenda sana Mariam!”

“Hata mimi Tom, sijaona mwanaume mwingine zaidi yako, sikuambii haya kwasababu ya utajiri ulionao sasa, kumbuka hata kipindi ulipokuwa huna kitu nilikuwa nakupenda kwa mapenzi haya haya ninayokupenda leo!

“Nirudishe moyoni mwako tafadhali, nipe nafasi nyingine Tom, naamini kwa kuwa na wewe  maisha yangu yatakuwa ya furaha tena baada ya kuishi bila kuwa na furaha kwa miaka mingi sasa!” Mariam akamwambia Tom.

“Lakini umeshachelewa!”

“Kivipi?”

“Subiri!”

Tom akatoa simu yake mfukoni kisha akabonyeza namba fulani, akaanza kuzungumza na mtu. Dakika moja baadaye, msichana mrembo sana mwenye sifa zote za kuitwa mrembo akaingia kwenye gari ya Tom. Alikuwa mrefu, mwenye hips pana, makalio makubwa yaliyobebwa na kiuno chembamba sana.

Msichana huyo alikuwa amevaa suruali nyepesi nyeusi, blauzi ya pink pamoja na viatu vya wazi vyenye rangi ya pinki. Macho yake yalifunikwa kwa miwani kubwa ya giza! Alikuwa na midomo minene, iliyopambwa na mafuta maalum ya kupambia midomo, nyusi zilizochongwa kwa ustadi wa hali ya juu zilizochorwa kwa wanja mweusi zilizidisha uzuri wake.

Alikuwa msichana mrembo kwelikweli, manukato yake yalikaribia kupasua pua za Mariam! Yalikuwa manukato ya bei mbaya yenye harufu nzuri kuliko kawaida. Alipofika aliketi na kumtizama Mariam kwa dharau.

“Unasemaje Tom?” Msichana huyo akasema akionekana kuchukizwa na Mariam kuingia kwenye gari la Tom.

“Nataka kukutambulisha!”

“Sawa...”

“Mariam huyu ni mchumba wangu mpenzi ninayempenda sana, anaitwa Juliana. Ndiye mwanamke niliyenaye kwasasa ambaye kwakweli nampenda sana. Tupo mbioni kufunga ndoa ili tuishi kama mke na mume!” Tom akamwambia Mariam. Alipomaliza akamgeukia Juliana.

“Juliana, huyu anaitwa Mariam, alikuwa mpenzi wangu wa zamani kabla sijakutana na wewe!”

“Mh! Kumbe ulikuwa na mwanamke mbaya hivi? Ulifikiria nini lakini kuwa na uhusiano naye? Huyu ni kama alikuwa anakusababishia nuksi tu, katika maisha yako? Huyu ni takataka tu, hastahili kabisa kuwa na wewe!” Juliana akasema huku akifungua mlango tayari kwa  kurudi kwenye gari lake.

“Tom mimi mbaya, takataka? Ndiyo umeamua kumuita mwanamke wako ili anitukane? Sawa bwana, Mungu yupo!” Mariam akasema akilia sana.

Muda huo huo akashuka kwenye gari na kukimbia akielekea mtoni. Hakuna aliyejua alichokifuata.




Maneno yale kutoka kwa Juliana yalikuwa sumu kali kwa Mariam, kwanza alijiangalia kuanzia chini hadi juu, kisha akamwangalia na Juliana baadaye akayarudisha macho yake kwa Tom, hakuamini alichosikia, aliona kama alikuwa katikati ya ndoto kali na huenda muda wowote angezinduka.

Alishuka haraka sana kwenye gari kisha akapiga hatua za haraka akielekea katika mto uliokuwa chini ya Jengo la Utawala. Kila mtu alimshangaa, alionekana kama mwendawazimu.

Kilichokuwa kikimuuma zaidi ni kitendo cha kumsaidia Tom kwa moyo wake, tena wakati akirudi kutoka kumpeleka baba yake na Tom hospitalini akapata ajali ambayo ilimlaza kitandani kwa miaka kadhaa.

Hakuona thamani yake tena, kila kitu alikiona kichungu, hakuwa na hamu ya kuendelea kuishi duniani. Alipofika mtoni alikaa chini akiwaza jinsi gani atakavyoweza kumaliza hasira zake, haikuwa rahisi kupata jibu la haraka. Tom alikuwa amempa kovu ambalo lisingepona kabisa.

“Nimemkosea nini mimi jamani, kosa langu ni nini? Kwanini ananinyanyasa kiasi hiki? Kwanini ananikosesha amani kiasi hiki? Amenionaje kwanza, yaani napoteza kabisa mwelekeo wa maisha yangu!” Mariam akawaza.

Aliendelea kulia akiwa hajui la kufanya, maisha yake sasa yalishakuwa machungu. Lakini baada ya kuwaza muda mrefu, akapata jibu; jibu lenyewe lilikuwa baya sana. Aliwaza kujiua!

“Ndiyo lazima nife...sioni sababu ya kuendelea kuishi katika dunia yenye tabu kiasi hiki, dunia yenye watu wenye roho mbaya ambao hawataki kuangalia thamani ya maisha ya wenzao, bora nife!” Mariam aliwaza akifikiria njia nzuri ya kujitoa uhai bila maumivu.

“Watu wanaojinyonga mara nyingi hutamani kukata kamba, lazima nifikirie njia nzuri ambayo haitaniumiza, lazima niondoke duniani kimya kimya, tena bila maumivu makali. Nataka kufa taratibu...ndiyo bora nife, hakuna sababu ya kuendelea kuishi nikiteseka!” Aliwaza Mariam.

Alidhamiria kufa, lakini hakutaka kusikia maumivu wakati roho yake ikitengana na mwili, lakini alikuwa akiwaza sana njia ya kujiua! Ni njia gani hiyo? Hakuwa na majibu, lakini ilikuwa lazima ipatikane.

* * * * *

Watu walikuwa wamezunguka gari la Tom wakisikiliza mzozo uliokuwa ukiendelea kati yake na Juliana, tayari Juliana alishaanza kuleta fujo baada ya kumuona Mariam, alilalamika kwamba eti alikuwa akidhalilishwa!

“Nimekwambia ni msichana wangu wa zamani, kwani kuna tatizo gani?”

“Wewe huoni tatizo?”

“Lipi? Sioni tatizo mimi!”

“Sasa sikiliza, wakati mwingine sipendi na sitaki unifanyie ujinga kama wa leo, tafadhali sana Tom, na kama hunitaki ni bora ukaniambia ukweli ili nijue moja!”

“Usiseme hivyo mpenzi wangu!”

“Kumbe nisemeje?”

“Sikiliza tuachana na haya mambo, tunaonyesha picha mbaya, nenda kwenye gari lako tuondoke!”

“Siendi kabla haya mambo hayajaisha!”

“Unataka yaisheje?”

“Kwani wewe unafikiriaje?”

“Basi twende tutazungumza nyumbani!”

“Sawa!” Juliana akajibu kwa hasira kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake.

Kila jicho la watu waliokuwepo mahali pale lilikuwa likimwangalia Juliana. Alikuwa mwanamke mzuri sana kwa mwanaume yeyote rijali. Alikuwa mrefu, mwenye hips pana, makalio ya kumtosha na mwendo wake ulizidi kuwakosha raha wanaume.

“Mh! Huyu msichana mzuri sana jamani!” Mmoja wa watu waliomuona akipita alisema.

“Ni kweli kaka! Kweli pesa ni kila kitu, yaani ukiwa na pesa unaweza kuwa na mwanamke yeyote umtakaye!”

“Hivi umemuona vizuri usoni?”

“Ndiyo, ana macho mazuri ajabu, halafu anajua kuyatumia! Hakyanani huyu nikimpata chumbani, hakuna kulala yaani usiku mzima ni kupeana maraha tu!”

“Mh! Mshkaji sasa wewe umefika mbali!”

“Hakuna umbali wowote, ni mambo ya kawaida sana kwa mwanaume yeyote mwenye viungo vyote vizima mwilini!”

“Umeshinda kaka!” Hayo yalikuwa mazungumzo ya vijana wawili waliokuwa wakimtizama Juliana aliyekuwa akitembea kwa maringo akielea gari lililokuwa limeegeshwa karibu na la Tom.

Alipolifikia akafungua mlango na kuingia, Tom akafunga mlango wa gari, kisha akamwambia dereva aondoe gari! Tom akaondoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

******

Utajiri wa Tom ukawa gumzo kwa wanafunzi wa chuo, stori zote siku hiyo zilikuwa zikimhusu Tom! Kila mtu alikuwa akimmiminia sifa kutokana na uwezo mkubwa kifedha aliokuwa nao. Tom alikuwa mfano wa kuigwa.

“Lakini ana maendeleo sana!” Mmoja wa wasichana waliokuwa wakijadiliana kuhusu Tom alisema.

“Sana, halafu ana mwanamke mzuri sana!”

“Yaani acha tu, yaani ndiyo upate bahati ya kuwa na boyfriend kama yeye mh! Yaani mji mbona ungechimbika?”

“Lakini hapana bwana, watu wenye fedha wana matatizo yao bwana, waone hivyo hivyo!”

“Matatizo gani?”

“Kufungua zipu!”

“Tena ni viboko ile mbaya!”

“Ukiamua kuwa naye, lazima ukubali kuteswa, kutukanwa na kuchangia na wengine, lakini ukiwa na yale mambo ya kupenda umependa utake kuwa mwenyewe, thubutu haiwezi kutokea! Wanaume wenye pesa zao tabu tupu, asikudanganye mtu!” Walizungumza kwa muda mrefu sana wasichana hao, lakini baadaye mmojawao akamkumbuka Mariam.

“Halafu nilimuona kama Mariam akimfuata mbele wakati jamaa akitoa mada!”

“Eti alikuwa anamwambia anamkumbuka!”

“Mh! Mie sikuona jamani, ikawaje?”

“Jamaa akamtolea nje!”

“Si nilisikia baadaye alipotoka nje alimfuata tena?”

“Enhee! Lakini yaliyomkuta huko balaa!”

“Ilikuwaje?”

“Alimfuata jamaa, akamfungulia mlango, baadaye Tom akamuita mwanamke wake! Mzuri huyo asikuambie mtu. Basi bwana, sijui walikuwa wakizungumza nini, nikashangaa Mariam akitoka kwa hasira na kuondoka zake!” Lilian, mmoja wa wasichana hao alisema.

“Akaenda wapi?” Pamela akauliza.

“Kakimbilia huko chini!”

“Wapi?”

“Mtoni!”

“Alikuwa katika hali gani?”

“Kama amekasirika hivi, maana inaonekana aliambia kitu kilichomuuza sana!”

“Mungu wangu!”

“Mbona umeshtuka?”

“Yaani mnaona ni jambo dogo hilo, tunaweza kumpoteza mwenzetu kwa mzaha hivi hivi!” Pamela akasema huku akikimbia.

Wenzake nao walimfuata wakikimbia hadi mtoni. Baada ya kutafuta kwa muda, walifanikiwa kumuona Mariam akiwa amelala chini akilia. Wakati mwingine alikuwa akjipigiza chini kwa hasira.

“Mariam vipi?” Pamela akamuuliza.

“Niache rafiki yangu!”

“Kwanini nikuache, niambie kuna nini?”

“Nina matatizo makubwa sana!”

“Matatizo gani tena?”

“Si unakumbuka niliwahi kukusimulia kuhusu maisha yangu?”

“Nakumbuka sana!”

“Unakumbuka kwamba nililala kuitandani kwa zaidi ya miaka minne nikiwa nimepoteza fahamu!”

“Nakumbuka!”

“Sijui kama unakumbuka sababu iliyonisababuishia matatizo yote hayo!”

“Ulisema...nakumbuka Mariam!”

“Ilikuwa ni nini?”

“Mapenzi...” Pamela akasema kwa sauti ya taratibu sana.

“Mwanaume mwenyewe ni Tom!”

“Tom?!”

“Ndiyo! Tom ndiyo chanzo cha matatizo yote hayo, lakini leo hii naambulia matusi!”

“Tom amekutukana?”

“Siyo yeye!”

“Sasa mbona umesema ni Tom?”

“Ni Juliana!”

“Juliana ndiyo nani?”

“Mwanamke wake, yule aliyekuja naye!”

“Mbona siamini kama anaweza kukutukana? Amekuambiaje?”

“Eti mimi mbaya, sina hadhi ya kuwa na Tom, yaani mimi mbaya...mimi mbaya? Sina hadhi ya kuwa na Tom? Siamini macho yangu, siamini kabisa, naona ni bora nife!” Mariam alipomaliza kusema maneno hayo akaanguka chini kama mzigo!

Akapoteza fahamu. Wakajaribu kumtingisha lakini hakushtuka, macho yake yakaanza kulegea pole pole kisha akayafumba kabisa, ute mwepesi ukaanza kumtoka kinywani mwake, shingo yake ikalegea kabisa. Mariam hakujigusa tena.

Wakapiga kelele za kuomba msaada.




Dakika kumi tu baadaye tayari watu walikuwa wameshajaa katika eneo lile. Hawakuwa na sababu ya kuuliza kilichotokea kwani hali aliyokuwa nayo Mariam pale chini iliwahuzunisha sana, mara moja akabebwa juu juu na kupelekwa eneo la Utawala.

“Nini kimetokea?” Mmoja wa wanafunzi aliuliza.

“Hayo siyo maswali kinachotakiwa sasa hivi ni kumuwahisha hospitali kwanza!”

“Lakini ni vizuri tukafahamu!”

“Ndiyo maana nimesema tumpeleke kwanza hospitali!” Pamela akaendelea kusisitiza.

Pamela na wenzake wakaongoza moja kwa moja hadi ofisini  kwa Mkuu wa Chuo ambapo alitoa taarifa na  gari likatolewa mara moja. Muda mfupi baadaye safari ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikaanza. Hawakuchukua muda mrefu sana kufika hospitalini hapo wakitumia Barabara ya Sam Nujoma baadaye Ali Hassan Mwinyi kisha walipofika eneo la Daraja la Salender wakakata kulia wakielekea Hospitali ya Muhimbili.

Hawakuwa na sababu ya kukaa mapokezi, moja kwa moja  aliweka juu ya machela na kusukumwa  kuelekea wodini.

“Nini kimempata?” Mmoja wa wauguzi aliuliza.

“Alianguka!”

“Kwanini?”

“Alipatwa na mshtuko!”

“Wa?”

“Ni mambo ya uhusiano!”

“Kawaida ya wasichana!”

“Naomba utusaidie apone!”

“Usijali hii ndio kazi yetu, mmesema mnatokea wapi?’

“Chuo Kikuu!”

“Tulisikia Papaa Bill alikuwa anatoa semina ya Ujasiriamali pale!”

“Ndiyo,  tena yeye ndiye amesababisha yote haya!”

“Kivipi?”

“Aliwahi kuwa mpenzi wa Mariam!”

“Mungu wangu!”

INAENDELEA

Post a Comment

0 Comments