Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mume gaidi sehemu ya kumi (10)

 


Tina alikuwa amebaki na Yuda nyumbani.

TINA: Yuda, mbona nilikuwa siwaelewi. Mlikuwa mnamtaja Tusa Tusa, huyo Tusa ndio Tusa yupi?

YUDA: Ni Tusa ndugu yako.

TINA: Kapatwa na nini? Na je hapa Mwanza alikuwa anaishi wapi?

YUDA: Ametoroka na Sele, kwa hapa Mwanza alikuwa anaishi kwa mamdogo alipoenda mama.

TINA: Tafadhari naomba unipeleke.

YUDA: Mama mwenyewe hajarudi hadi leo hata sijui kuna nini.

TINA: Nipeleke hivyo hivyo bhana.

Yuda akaamua kujiandaa na Tina ili kwenda nae nyumbani kwa Deborah.


Sele na Tusa walikuwa kwenye mateso ya wanajeshi, watu hawa hawakuwa na huruma hata kidogo. Waliwatesa kama vile si binadamu, kwakweli wanajeshi huwa wanafanya mambo ya kikatili sana.

Wakati wa yale mateso, Tusa akaanza kuugulia tumbo, aliwaambia ila hawakumsikiliza.

Tumbo lilimuuma sana Tusa, kwakweli Sele alimuonea huruma sana. Akamuita mjeshi mmoja ili kuzungumza nae.

SELE: Tafadhari nawaomba, adhabu zote za huyu mwanamke nipeni mimi. Nitafanya pamoja na adhabu zangu.

Yule mjeshi akacheka sana na kuwaita wenzie kisha akamwambia

"hebu sema tena"

SELE: Nipeni mimi adhabu zote, mwachieni Tusa. Tazama anavyoteseka, muoneeni huruma jamani.

MJESHI: Je, yeye aliona huruma kumchoma Mwita kisu?

SELE: Ile ilikuwa ni gafla ukizingatia alikuwa amezimia, tafadhari nawaomba mmuhurumie.

MJESHI: Ngoja nikwambie kitu rafiki, sisi wanajeshi kwetu huruni ni no tena big NO. Hakuna kumuhurumia mtu, ni adhabu kwenda mbele hadi muonje mauti. Nyie si mnajifanya wababe? Hapa huwa hatuwafungulii kesi watuhumiwa, hapa ni adhabu tu.

Sele alijitahidi kuwasihi lakini hawakukubali.

Tusa aliendelea kuumwa na tumbo huku damu nyingi zikilowanisha gauni lake.


Patrick na Hamisi walifika nyumbani kwa Mwita ila hawakumkuta.

HAMISI: Sijui kaenda wapi huyu mgonjwa? Au kaenda kuwatazama wale watuhumiwa!

PATRICK: Watuhumiwa! Inamaana waliomchoma kisu mnawajua?

HAMISI: Tumewakamata kabisa, unajua wanajeshi huwa tunauwezo mkubwa sana wa kucheza na akili za watu. Eti walikuwa wanakimbilia Morogoro, yani huko huko tukawatia mbaroni.

PATRICK: Mmh! Kwani ni wengi sana?

HAMISI: Wawili tu, ni mwanamke na mwanaume.

PATRICK: Sasa kati yao nani aliyemchoma kisu Mwita?

HAMISI: Ni mwanamke ndo kamchoma Mwita, ila wote wanapata adhabu kwakuwa wameshirikiana kutoroka.

PATRICK: Unaonaje tukiwafata huko eneo la tukio, ujue nimemkumbuka sana Mwita.

HAMISI: Aah! Tuwangoje bhana. Kule atakupeleka Mwita mwenyewe.

Patrick alikuwa anaichezesha akili yake jinsi ya kuwaingia iawa wajeda kwani alijua lazima watakuwa wengi tu.

Akajisemea kimoyomoyo.

"maisha ya Tusa yapo mikononi mwangu. Huyu ni mke wangu lazima nimkomboe. Mmh! Sele nae ni ndugu yangu, siwezi kumuacha na hawa bora nimtoe hapa nikamshughulikie mwenyewe"

Patrick aliwaza mengi huku akimngoja huyo Mwita kujua ni mtu wa aina gani na vile vile kujua jinsi gani ya kumuingia.

Akaona ni vyema amgeleshe yule Hamisi kwa kuondoka ila badae arudi mwenyewe na akutane yeye na Mwita tu.

PATRICK: Nimechoka kungoja hapa nje, ngoja nirudi kupumzika. Kwavile nishakujua nitarudi tena badae.

HAMISI: Basi ngoja tuondoke wote, maana na mimi nataka kwenda kwangu mara moja.

Patrick akaondoka na Hamisi kwa lengo la kumgelesha tu.


Fausta aliendelea kulia na kubembelezwa na wote.

DEBORAH: Nyamaza Fausta, yule Maiko ni shetani kila mmoja analijua hilo. Utaumia zaidi ukizingatia tayari una majeraha mengine ndugu yangu.

MARIUM: Hivi, mnajua kama yule ndio aliyemkata kichwa mume wangu?

PAMELA: Mungu wangu, nyie yule Maiko ni gaidi kweli. Yani alimkata kichwa?

MARIUM: (Akiongea huku machozi yakimbubujika), yani alimchinja huku na mimi nikishuhudia kwa macho yangu haya mawili, halafu akaondoka na kichwa chake na kuniachia mwili wake tu.

FAUSTA: Mimi je, alimkatakata mwanangu vipande vipande kama nyama buchani. Inaniuma sana tena sana, Maiko ni gaidi tena wa kishetani.

Walikuwa wakilia na kuomboleza huku Pamela akiwabembeleza kwani Deborah nae alikumbuka matukio aliyofanyiwa na Maiko na kujikuta akilia kwa uchungu.

Rehema nae aliomboleza sana baada ya kusikia matendo aliyoyafanya mwanae mwenyewe.

Yuda na Tina walipofika mlangoni mwa nyumba hiyo walishangaa kuona kilio kimetawala hadi wakapatwa na hofu kuwa huenda kuna msiba.


Maiko alipoingia chumbani mwake alimuona Adamu nae akimvamia bila hodi.

MAIKO: Unataka nini wewe?

ADAMU: Nahitaji kuzungumza na wewe.

MAIKO: Sina muda huo, nakuomba utoke humu ndani.

ADAMU: Tafadhari naomba unisikilize.

MAIKO: Toka kabla sijatenda dhambi tena.

ADAMU: Nisikilize kwanza basi.

MAIKO: (Akiongea kwa ukali) nishakwambia sina muda huo, nakuamuru utoke humu ndani.

ADAMU: Kutoka nitatoka ila naomba unisikilize kwanza.

MAIKO: Wewe ni mbishi eeh! Haya kwa mara ya mwisho toka. Nahesabu hadi tatu uwe umetoka. Moja... Mbili.... Tatu.... Hujatoka eeh ngoja sasa.

Adamu alikuwa kaganda pale pale akimshangaa huyu Maiko na matatizo yake.

Maiko akainama kwenye begi lake na kuchukua bastola kisha akamlengeshea Adamu.


Mwita aliporudi tu nyumbani kwake, Patrick nae alikuwa mitaa ile ile.

Akaenda kugonga mlango, Mwita akamfungulia bila hofu yoyote kwani alijua ni wenzie.

Ile kufungua tu, Patrick alikuwa tayari na bastola mkononi akamnyooshea Mwita, nae Mwita alipomtazama vizuri akamwambia.

MWITA: Aah! Patrick, tusifanyiane ubaya bhana.

PATRICK: Kumbe Mwita ndio wewe?

MWITA: Ndio mimi bhana Patrick.

Patrick alishangaa kuona kuwa Mwita ni mtu anayefahamiana nae.


Patrick alishangaa kuona kuwa Mwita ni mtu anayefahamiana nae.

Patrick akashusha bastola chini ili apate kuzungumza nae.

MWITA: Mbona hivyo ndugu yangu kunijia na bastola?

PATRICK: Unajua nini? Mimi nimekuzoea wewe kwa jina la Frank kumbe na Mwita ni jina lako?

MWITA: Ndio bhana, mi naitwa Frank M. Mwita na huku wamezoea kuniita jina la mwisho yani hili la Mwita.

PATRICK: Sawa sawa, kwanza nashukuru kuwa tunafahamiana. Nadhani kazi yangu itakuwa nyepesi.

MWITA: Kazi gani hiyo?

PATRICK: Kwanza niambie Tusa na Sele wamekufanya nini?

Mwita akaeleza ilivyokuwa jinsi Sele alivyorudi na kuanza kupambana nae hadi pale alipochomwa kisu na Tusa.

PATRICK: Unataka kuniambia Tusa alikuchoma kisu tu bila sababu?

MWITA: Si aliona nimemkaba Sele ndomana akanichoma.

PATRICK: Haya, mi nataka kitu kimoja tu hapa Frank.

MWITA: Kitu gani?

PATRICK: Namtaka huyo Tusa na Sele.

Mwita akashtuka na kuuliza,

MWITA: Sasa mimi nitawatoaje ilihali nishawaamuru wajeshi wenzangu wawafanye watakavyo?

PATRICK: Nadhani unanijua vyema Frank, sitaki kutumia nguvu tusije tukaumizana bure hapa. Ukinisaidia hilo jambo, nami nitakusaidia lile swala lako la baba yako.

MWITA: Kweli Patrick?

PATRICK: Huu ni ukweli, huwa sina ahadi za uongo mimi.

MWITA: Ngoja basi tutafanya kitu flani hivi. Kwani wewe ni nani zako hao?

PATRICK: Nitakwambia tu usiwe na shaka.

Ikabidi Mwita aamue kwenda na Patrick eneo la tukio, akapanga kwenda nae kesho yake kwani siku hiyo usiku ulishaingia.


Maiko aliendelea kumnyooshea bastola Adamu, na kuendelea kumuamuru atoke.

Ila Adamu hakutoka, aliendelea kung'ang'ania kuongea nae, Maiko akajaribu kufyatua risasi ili kumtishia, na ile risasi ikampata Adamu begani na kujikuta akianguka huku akisema,

"Umeniua Jumaaaa"

Maiko akajikuta akishtuka na kumfata Adamu pale chini ambapo alikuwa akitokwa na damu nyingi, ikabidi amchukue na kumpakiza kwenye gari na kumpeleka hospitali.

Kwakweli Maiko alikuwa hajielewi kabisa na alifanya vitu bila hata ya kufikiria.

Akawa anajiuliza kuwa yule mtu kwanini aseme umeniua Juma, au amesikia maongezi yake na Mashaka? Alijiuliza sana ila alikuwa anaombea apone tu ili aweze kumuuliza, alijilaumu sana kwa kitendo chake cha hasira na kukumbuka kuwa kweli hasira hasara.


Yuda na Tina waliingia ndani kwa Deborah ila hofu yao kubwa ni kuwa kuna msiba.

Walipoingia wakawaona hawa wanawake wa humu wote wakilia na kuomboleza. Yuda akaamua kuuliza,

"Kuna nini jamani?"

wakajikuta wakinyamaza na kuangalia watu walioingia ndani, ndipo walipomuona Tina na Yuda.

Tina kwanza hakuamini kuonana tena na familia yake, mama yake aliinuka na kumkumbatia mwanae kwa machozi.

FAUSTA: Jamani mwanangu, ulikuwa wapi siku zote?

Tina nae akaanza kulia.

TINA: Nilitekwa mama.

DEBORAH: Mmh! Jamani, naona hii Mwanza imeharibika sasa hadi nashikwa na hofu mwenzenu. Pamela alitekwa, Fausta alitekwa kumbe na huyo Tina nae alitekwa mmh!

REHEMA: (Akawa kama mtu aliyeshtuka usingizini), jamani Adamu!!

PAMELA: Kwani nae yuko wapi?

DEBORAH: Alienda kuripoti kupotea kwenu na ndio hajarudi hadi leo. Inamaana nae katekwa?

REHEMA: Mungu wangu, tutafanyaje sasa?

Yuda alikuwa akiwasikiliza tu huku nae akijiuliza anayefanya huo utekaji ni nani? Na kwanini atoke familia moja tu? Alikosa jibu kabisa kwani hakufikiria kama Maiko na Mashaka watakuwa wanahusika kwa wote.


Mashaka alijiona kuwa atakuwa amepoteza kila kitu asipofanya kitu.

"Yani Maiko amenidanganya mimi? Yani siku zote hizi amekuwa akicheza na akili yangu? Inamaana akili yangu imepoteaje hadi nimsahau mwanangu mwenyewe? Inamaana Rehema yuko hapa Mwanza au Maiko amemuonea wapi? Lazima nifanye kitu, lazima nifanye kabla ya Maiko. Ngoja nikanywe kwanza ili akili ikae sawa"

Mashaka akaenda kununua konyagi za kumtosha kulewa ili anywe hadi alale kabisa na akiamka afanye analotaka kufanya.


Tusa na Sele walikuwa katika wakati mgumu bado, Tusa aliendelea kumwaga damu iliyotoa harufu kama kitu kilichooza.

SELE: Pole Tusa ila ungenisikiliza yote haya yasingetupata.

Tusa hakuweza hata kuzungumza kwa maumivu ambayo alikuwa akiyapata.

Alishindwa kabisa kuendelea na adhabu, akawa ameanguka chini. Wanajeshi wasio na huruma walikuwa wakimburuta Tusa.

Wakati wanajeshi hao wawili wakiendelea kumburuta Tusa wakamuona mbele yao Mwita na mtu mwingine ambaye ndio Patrick.

Patrick alipowaona akawapigia makofi sana,

PATRICK: Vizuri sana, huo ndio uanajeshi kwakweli mnastahili pongezi.

Wale wanajeshi wakafurahi sana na kuendelea kumpiga mateke Tusa aliyekuwa ameshindwa hata kutoa tena sauti ya kilio, Sele aliangalia lile tukio na kuumizwa sana moyo wake.

MWITA: Umeona kazi yao eeh! Wengine wapo kwa yule kijana.

PATRICK: Ila mimi nimewapenda hawa, jamani muacheni huyo dada hapo chini. Nyie wawili jioni nitawapa ofa.

MJESHI 1: Dah! Hiyo sitakosa bhana, utushtue basi.

PATRICK: Ngoja tupeane mawasiliano basi.

Patrick akachukua namba za simu za wale wajeshi ambao walikuwa wakimtesa Tusa huku wakifurahia.

PATRICK: Mwacheni huyo dada basi.

MJESHI 2: Wa nini sasa huyu?

MWITA: Nataka nikadeal nae.

Wakamuacha pale chini ambapo Mwita alimuamuru mjeshi mwingine amchukue na kumpakiza kwenye gari, mjeshi huyo aliyeitwa Musa alimbeba Tusa na kumtupia kwenye gari.

PATRICK: Kwakweli nimependa sana kazi yako kaka, na wewe jioni uje kwenye ofa.

Naye alifurahi na kupeana mawasiliano na Patrick.

Wakabaki wengine wawili ambao hawakupata ofa, ikabidi waonyeshe ujuzi wao kwa Sele, wakawa wanampiga na kumpondaponda kila mahali. Mwita akawaamuru wamuache halafu nae akapakizwa kwenye gari.

Patrick akawageukia wale na kuwaambia nao kuwa jioni ofa, akachukua na mawasiliano yao.


Maiko aliendelea kushughulika na Adamu pale hospitali, kwavile alikuwa na pesa basi kila kitu kikaenda kama anavyotaka yeye. Nia yake kubwa ikawa ni kumuona Adamu akiwa mzima ili apate kuzungumza naye.

Adamu alipoanza kufumbua macho Maiko alifurahi sana, alihitaji majibu ya maswali yake. Hakutaka kumpoteza mtu huyu tena, ukizingatia alimkuta na Mashaka akajua lazima kuna mambo mengi anayoyajua kuhusu yeye.


Hali za Tusa na Sele zilikuwa mbaya sana hasa Tusa ambaye alipoteza fahamu kabisa, kitu cha kwanza alichofanya Patrick ni kuwakimbiza hospitali.

Akawaacha wakihudumiwa pale hospitalini na yeye akarudi kwa Mwita.

MWITA: Mbona umewapongeza wale wanajeshi halafu bado umeenda kutupa pesa ya matibabu kwa Tusa na Sele?

PATRICK: Nimewapongeza kwasababu wamefanya kazi nzuri sana, na wale nimewapeleka hospitali kwavile nao nawahitaji wakiwa hai.

Mwita hakuwa na wasiwasi wowote na Patrick kwani aliujua vizuri ukatili alionao Patrick kwahiyo alihisi amewapongeza kwa nia njema, na kweli jioni hiyo aliwaita wale wanajeshi na akawanywesha sana pombe huku wakifurahia siku yao kuwa poa, hakuna hata mmoja aliyejua Patrick ana lengo gani nao.

PATRICK: Kesho tena nitawapa ofa.

MUSA: Dah! Wee jamaa uko poa sana yani. Sisi ni makomando, vijitu kama vile huwa tunapiga hadi kufa.

PATRICK: Hapo ndio ninapowapendea wanajeshi, kazi nzuri sana. Nitakuwa nawapa ofa hadi nitakapoondoka Singida.

Wote wakafurahi sana kwa ofa walizopewa na Patrick.


Ikabidi Yuda nae aamue kufanya kitu kama mwanaume maana akaona kukaa tu na wanawake hakutamsaidia chochote.

Sasa aliamua kwenda kuzunguka mjini ili kujua kama kweli Maiko na Mashaka wameondoka au la.

Safari yake ilianzia moja kwa moja kwenye hoteli ambayo Tina alimuelekeza kuwa alifikia mwanzoni.

Kufika kule aliweza kugundua vitu baadhi kwani alipata kujua uwepo wa mtu aliyepigwa risasi ndani ya hoteli hiyo ila huyo mtu na aliyepigwa hawakujulikana walipo.

Wakati anasikiliza hayo maelezo mara akamuona Mashaka kwa mbali, akaamua kumfatilia.


Mashaka alishapanga vitu vyake kwenye akili yake, na kitu cha kwanza aligundua hospitali ambayo Maiko amempeleka Adamu, Mashaka aliamua kwenda kwani alijua kuwa lazima kuna kitu kilichofanya hadi Maiko ampeleke Adamu hospitali kwani Maiko hakuna na roho ya kumuhurumia mtu hata siku moja.

Mashaka akaingia chumba alicholazwa Adamu, kabla hajafanya chochote akamuona Yuda nae ameingia humo.

Mashaka akaingia chumba alicholazwa Adamu, kabla hajafanya chochote akamuona Yuda nae ameingia humo.

Wakawa wanatazamana sasa, Mashaka hakuelewa kwanini Yuda amemfata kwenye mishe zake kama zile.

Ikabidi atoke nje na kumpita Yuda pale mlangoni, Yuda nae akamfata Mashaka nje.

MASHAKA: Kijana, nini unataka kutoka kwangu?

YUDA: Hakuna ninachotaka.

MASHAKA: Sasa mbona wanifatilia? Naomba kaa mbali na mimi, nitakupoteza.

YUDA: Siku yako inakuja ya wewe kupotezwa.

Mashaka akamtazama Yuda kwa jicho kali sana, akatamani hati ampige makofi ila akaona hawapo sehemu nzuri ya kufanya hivyo ukizingatia kuwa Yuda nae ni kijana mwenye fujo.

Yuda akamuangalia Mashaka anavyoondoka, ila akavutwa zaidi kwenda kumtazama yule mgonjwa aliyefatwa na Mashaka.

Alipoingia wodini safari hii akamkuta Maiko akiwa pale kwa mgonjwa. Kwakweli Yuda alishindwa kuelewa kabisa kuwa Mashaka na Maiko wana nini na huyo mgonjwa.


Nyumba ya Deborah ilikuwa kama vile nyumba ya wanawake wenye huzuni na waombolezaji.

REHEMA: Kwakweli nashindwa kuelewa jamani, hivi kwanini mwanangu Juma akajiita hilo jina la Maiko?

DEBORAH: Mama, usimlaumu sana huyo Maiko. Sote hapa tunajua kuwa huyo Maiko ni shetani. Swala linakuja kwa huyu mwanao mwadilifu Jumanne, kwanini alibadili jina na kujiita Adamu?

PAMELA: Debo, hapa tunamuongelea Maiko, sasa Adamu anaingiaje hapa?

DEBORAH: Pamela huelewi na huwezi kunielewa. Nimeishi na Jumanne akiwa anaitwa Jumanne, iweje akabadili jina kwako. Au mlitaka kuficha maovu yenu Pamela?

PAMELA: Najua shida yako ni kunikandamiza mimi, nilishakuomba msamaha ila hutaki kunielewa Deborah. Tuongee ya msingi tu hapa, tumuongelee huyo Maiko.

DEBORAH: Sikia Pamela, nimeishi na Jumanne na nimeishi na Maiko. Uchungu niupatao sasa moyoni mwangu huwezi kuudhania wewe.

REHEMA: Inamaana wote umeishi nao kama mke?

DEBORAH: Ndio ila kwa wakati tofauti.

REHEMA: Mungu wangu, mbona mimi sielewi kitu jamani. Mbona naona kizunguzungu?

DEBORAH: Mama sikiliza nikwambie, huu muda ni wa kutuliza akili ili ijulikane ni wapi palipokosewa. Yote haya chanzo chake ni kutokufahamiana. Mimi sikujua kama Maiko ni ndugu wa mume wangu wa kwanza. Maiko ni shetani mkuu halafu huyo Adamu atakuwa msaidizi wake.

FAUSTA: Mnajua hata mimi nimechanganyikiwa hapa, kama Maiko ni ndugu wa Adamu inamaana Maiko ni ndugu yangu pia, Deborah ni mke mwenzangu. Yani nilizaa na ndugu yangu? Hapana, kwanini huyo Juma asiwe mtu mwingine zaidi ya Maiko?

Fausta akawa analia.

PAMELA: Naona hapa kila mtu ana msiba wake, na kilio kikubwa ni Maiko mmh!

DEBORAH: Ndio, hapa kila mtu ana msiba wake kasoro wewe Pamela.

REHEMA: Mabishano si mazuri jamani, yote haya yataisha siku moja.

Maelewano ya Pamela na Deborah tangia ujio wa kina Adamu yalikuwa hafifu sana kwani walikuwa watu wa kutupiana maneno tu.


Patrick alienda kuwatizama Sele na Tusa hospitali ambapo Sele alikuwa akiendelea vizuri, ila Tusa hali yake haikuwa nzuri.

Daktari akamwambia Patrick kuwa Tusa alikuwa mjamzito ila mimba yake imetoka kutokana na misukosuko, Patrick roho ilimuuma sana kwani alijua wazi kuwa ile mimba ilikuwa yake. Upande mwingine alimlaumu Sele kwa kumchukua mkewe bila ruhusa ila aliwalaumu zaidi wale wanajeshi waliomtesa Tusa kwani alijua ndio wamesababisha yote yale.

Akamfata Sele ambaye alikuwa anaendelea vizuri na kuongea nae.

PATRICK: Hivi wewe ndugu yangu, kilichokutuma kutaka kuondoka na mke wangu ni nini?

SELE: Hatukuwa na nia mbaya Patrick ila Tusa aliitaji kumuona babu yake.

PATRICK: Kwanini msingesubiri mimi nirudi? Ngoja Tusa apate nafuu, nitawasafirisha wewe na yeye mrudi Mwanza. Sasa ole wako umtoroshe tena, nakuhakikishia kichwa chako nitakitenganisha na mwili. Watu husema mchawi mpe mtoto akulelee, sasa mimi nitakukabidhi Tusa urudi nae Mwanza. Sawa.

Sele aliitikia kwa kichwa huku moyoni akiumia kwani aliona akiteswa na mapenzi aliyonayo kwa Tusa.


Adamu nae alikuwa anaendelea vizuri na hiyo ikawa furaha kwa Maiko.

Maiko aliondoka pale hospitali na Adamu akaenda nae sehemu aliyofikia, Yuda sasa akaanza kufatilia nyendo zote za Maiko ili kujua anapojificha.

Maiko alimuomba msamaha Adamu aliyekuwa na bandeji kwasasa,

MAIKO: Hasira zilinifanya nifanye yale, nisamehe kwanza.

ADAMU: Hakuna tatizo ndugu yangu.

MAIKO: Eeh! Niambie, ulijuaje kuwa mimi naitwa Juma?

ADAMU: Sikia ndugu yangu, wakati unaongea na yule baba nilisikia vizuri maelezo yako kuwa mama yako anaitwa Rehema si ndio?

MAIKO: Ndio ni kweli?

ADAMU: Hata mimi mama yangu anaitwa Rehema, halafu mimi jina langu lingine ni Jumanne. Nilipokusikia nikahisi labda wewe ni pacha wangu ambaye mama aliniambia kuwa yupo Mombasa na anaitwa Juma.

MAIKO: Mmh!! Kwakweli sijui chochote, inawezekana ni kweli.

ADAMU: Kwani wewe mama yako ulimkutia wapi hapa Mwanza?

Maiko akamuelekeza Adamu nyumbani kwa Deborah.

ADAMU: Basi huyo huyo ndio mama yangu.

Maiko hakuamini wala kuelewa kwavile alichojua yeye ni kuwa hana ndugu kabisa. Ikabidi aongee na Adamu na wapenge jinsi atakavyomkutanisha tena na bi.Rehema.


Deborah aliamua kumuita Pamela pembeni ili apate kuzungumza nae.

DEBORAH: Pamela wewe ni rafiki yangu sana, kiukweli sipendi tunavyorumbana. Hebu tuongee ya maana sasa.

PAMELA: Nakusikiliza Debo.

DEBORAH: Hivi kwa mara ya kwanza kabisa Patrick alivyokuleta hapa, ulikuwa umetoka nae wapi?

Pamela akamsimulia Deborah jinsi alivyotekwa na wakina Maiko hadi kuja kuokolewa na Patrick.

PAMELA: Kwakweli Deborah, mtoto wako Patrick ni mtu mzuri sana.

DEBORAH: Inamaana Patrick anajuana na wakina Maiko?

PAMELA: Itakuwa maana walikuwa wakimtajataja sana.

DEBORAH: Mmh! Kazi ipo. Patrick atakuwa ameshaharibika tayari.

PAMELA: Kivipi Debo? Na hivi huyu Patrick ulizaa na nani?

DEBORAH: Mmh! Historia ndefu ila nitaisema Patrick akirejea. Kwanini umeniuliza hivyo?

PAMELA: Umempata mtoto shujaa sana Deborah, na mimi isingekuwa.....

Akaanza kulia, Deborah akambembeleza bila ya kujua anacholilia.

DEBORAH: Isingekuwa nini Pamela?

PAMELA: Mapenzi yaliniponza Debo, ingawa nimeolewa na Adamu ila kuna tukio ambalo kila nikifikiria halitaki kutoka kwenye akili yangu. Roho yangu inaniuma na kunisuta pia.

DEBORAH: Yote maisha na mapito, kuna wakati huwa tunafanya mambo bila kufikiri ila badae hugeuka na kuwa majuto, na ndio hapo kauli ya ningejua hutokea. Niambie nini tatizo ndugu yangu.

PAMELA: Nitakwambia Debo, inaniuma sana kwakweli.

Deborah alitulia kumsikilizia Pamela kitu ambacho anataka kusema.


Tusa alipopata nafuu kidogo, Patrick hakutaka kupoteza muda akafanya kama alivyopanga. Akawasafirisha Tusa na Sele warudi Mwanza ili Tusa akapate matibabu mengine kwenye mkoa wa Mwanza.

Patrick akaenda nyumbani kwa Mwita,

MWITA: Nilitaka nikutafute Patrick maana ahadi ni deni, nieleze basi kuhusu baba yangu.

PATRICK: Unamsema huyo baba yako Maiko?

MWITA: Ndio huyo huyo, kwakweli natamani kumfahamu.

PATRICK: Usijari utamfahamu.

MWITA: Anaishi wapi nimfate basi.

PATRICK: Anaishi Arusha ila nadhani kwasasa bado yuko Mwanza. Ukitaka tangulia Mwanza, nitakuja kuwakutanisha mfahamiane kabla sijafanya yangu.

MWITA: Yapi tena?

PATRICK: Ni siri ndomana nimesema yangu ingekuwa sio siri ningesema yetu.

MWITA: Sasa vipi huko Mwanza hatuendi wote?

PATRICK: Tangulia tu, mimi nataka nifike Manyoni mara moja halafu ndio nitaenda Mwanza moja kwa moja.

Mwita hakumuelewa Patrick anampango gani hapo Singida.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Sele aliposafiri na Tusa walienda vizuri ila walipokaribia kufika Tusa akazidiwa sana ikabidi ashuke na kumuwaisha hospitali, hali ya Tusa ilikuwa mbaya sana kiafya kwani alinyong'onyea na kunyorodoka zaidi.

Hawakuweza tena kufika nyumbani.

INAENDELEA......

Post a Comment

0 Comments