Sele alipoona Mwita amebeba kisu ikabidi auwahi mkono wa Mwita, katika purukushani kile kisu kikamuangukia Tusa ila wenyewe hawakugundua hilo na kuendelea kupigana, kumbe pale chini Tusa alizinduka.
Katika kupigana Mwita akafanikiwa kumuangusha Sele na kuanza kumkaba, ndipo Tusa alipoinuka na kile kisu na kumchoma nacho Mwita mgongoni.
Tusa alifanya kitendo hicho kwa gafla sana na kujikuta anatetemeka, damu zilijaa kwani Mwita alitokwa na damu nyingi sana. Sele aliinuka na kushangaa lile tukio la gafla lililofanya Mwita atapetape.
Wakati wanashangaa na hawajui cha kufanya, mara alisikika mtu akigonga mlango wa Mwita.
Wakati wanashangaa na hawajui cha kufanya, mara alisikika mtu akigonga mlango wa Mwita.
Hofu ikawatanda Sele na Tusa.
SELE: Umeona sasa ulichofanya Tusa? Hii ni kesi tayari.
Tusa alikuwa akitetemeka tu kwani hakudhamiria kumchoma mtu kisu, ila alimchoma sababu ya maumivu aliyonayo moyoni juu ya kubakwa.
Yule mtu aliyekuwa anagonga aliendelea kugonga, ikabidi Sele aende kumchungulia, akamuona ni mwanajeshi akajua ni rafiki wa Mwita au anafanyakazi na Mwita kwani Mwita nae alikuwa mjeshi.
Sele akarudi kwa Tusa,
SELE: Hali mbaya Tusa, huyo anayegonga ni mwenzie na Mwita, nae ni mwanajeshi. Hata sijui itakuwaje.
Tusa hakujibu kitu, ila akajivika ujasiri na kwenda mlangoni, akawa anamuuliza bila kufungua mlango.
TUSA: Nani wewe?
MGENI: Mimi hapa Hamis, namtaka Mwita mara moja.
TUSA: Mwita ametoka na ameondoka na fungua, nadhani atarudi asubuhi.
MGENI: Mbona gari yake ipo?
TUSA: Kuna rafiki yake alikuja kumfata, sitaki maswali zaidi maana sina majibu yake.
Tusa alimjibu kwa ujasiri na kujiamini sana, ikabidi Hamis aondoke zake.
SELE: Mmh Tusa! Umekuwa mkavu kama hujafanya chochote vile, haya tuondoke hapa fasta kabla mambo hayajaharibika.
Wakachukua vitu vyao na pesa iliyopo ya Mwita halafu wakaondoka bila kujali kama Mwita yupo hai au amekufa.
Adamu akajiandaa kwaajili ya kwenda tena polisi.
REHEMA: Unatakiwa usimame kama baba, uitetee familia yako. Sasa ukikata tamaa unadhani itakufaidia nini?
DEBORAH: Mwambie ukweli mama, nadhani matendo uliyofanya nyuma unayajutia hata kama hayana madhara kwako. Ila uwe makini kwasasa usije ukajutia maisha yako yote.
ADAMU: Umakini gani unaousemea Deborah? Wewe ndo chanzo cha yote haya, tusingekuja Mwanza haya yasingetupata.
DEBORAH: Kunilaumu ni kawaida yako, kwahiyo sioni tatizo. Katika swala la ndoa, upendo ni kitu muhimu sana.
ADAMU: Sasa swala la ndoa na upendo vinahusika nini hapa? Deborah nadhani kuna kitu unahitaji toka kwangu wewe.
DEBORAH: Tena usitake kunikera mwanaume wewe, sina chochote ninachotaka toka kwako. Nikutake kwa lipi msaliti wewe!!
Ikabidi bi.Rehema aingilie kati.
REHEMA: Jamani jamani msije mkaanza kugombana bila sababu hapa, haya Adamu nenda polisi na utuache hapa.
Ikabidi Adamu atoke na kuondoka. Deborah akakaa chini huku machozi yakimlengalenga.
REHEMA: Tulia mama, hii ni changamoto ya maisha.
DEBORAH: Inaniuma sana kuona Jumanne anaona ni sawa tu hadi leo kitu alichonifanyia, ila mama Mungu ni mkubwa sana na anaendelea kunitetea ingawa ni mapito mengi niliyopitia.
REHEMA: Usijali mwanangu.
Rehema akaendelea kumpooza Deborah kwani alipandisha jazba sana.
Pamela alizinduka na kuanza kurudisha kumbukumbu, akakumbuka mara ya mwisho alikuwa anabishana na mumewe halafu mumewe akaenda kumsikiliza dereva wa bodaboda na kumuacha yeye amesimama, akakumbuka alisikia mikono ya baridi ikipita toka nyuma yake na kitambaa kilichomziba pua na kupoteza fahamu kabisa, ndio amezinduka sasa na yuko kwenye mikono ya adui ambaye ni Maiko.
MAIKO: Ulijiona umewin kwa kunikimbia na Patrick wako, haya sasa huyo Patrick wako alikupeleka wapi?
Pamela akawa anatetemeka bila ya kujibu chochote.
MAIKO: Nijibu bhana, Patrick alikupeleka wapi?
PAMELA: Kwa mama yake.
MAIKO: Unamaanisha Deborah eeh!
PAMELA: Ndio ni Deborah.
MAIKO: Haya sasa, pona yako ni kunielekeza mimi nyumbani kwa Deborah au tutaenda wote. Kwanza Patrick yuko wapi?
PAMELA: Hayupo kwao, nadhani wiki ya pili hii.
Maiko alifurahi kwa kupata kupajua nyumbani kwa Deborah kwa wepesi bila hata ya kutumia nguvu.
Tusa na Sele walienda kufikia kwenye hoteli moja wapo kwenye mji wa Dodoma kwani ilishindikana kusafiri zaidi kwa usiku ule.
SELE: Tusa, nadhani sasa umekuwa na tabia za Patrick.
TUSA: Kivipi?
SELE: Hivi Tusa wewe ni wa kuua mtu kweli? Mbona umefanya ukatili mkubwa sana.
TUSA: Yani mimi kukutetea wewe ndio unaniona kuwa nimekuwa katili? Yote haya umeyataka wewe Sele. Tungebaki Mwanza hata yasingetokea, vipi nikianza kutafutwa na polisi?
SELE: Tusa sina nia mbaya kukwambia kuwa umekuwa katili, nisamehe kwa hilo ila kumbuka yule Mwita ni mwanajeshi na sijui kama tutaweza kupambana na mtiti wa wajeshi.
TUSA: Tusitishane basi.
Kesho yake wakatoka kwaajili ya kuendelea na safari, walipokuwa stendi walimuona Hamis na baadhi ya wanajeshi wakikagua abiria wa pale stendi ikabidi waende kwenye choo cha pale stendi na kujificha kwani walikuwa hawajui wale wajeda wanatafuta nini.
Adamu alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, aliona mji wa Mwanza ukimchanganya sana.
Alipotoka polisi akaamua kwenda baa ili apate bia mbili tatu aweze kupunguza mawazo.
Huko baa akakutana na mtu mwenye kuitwa Mashaka na katika stori mbili tatu akaamua kumsimulia yanayomsibu.
Patrick aliona kuendelea kukaa na Fausta kutakwamisha mipango yake, kwahiyo akaamua kumchukua kama alivyopanga na kuanza safari ya kumpeleka kwa mama yake, pia alihitaji kumuona na kumsalimia mama yake. Alimkumbuka sana.
FAUSTA: Ndio unanipeleka kwa huyo mama yako?
PATRICK: Ndio, na kule utakuwa salama zaidi.
Hakutaka tena kumpelekea mzigo mamake mkubwa, aliona huyu ampeleke kwa mama yake tu.
Maiko aliondoka na Pamela hadi nyumbani kwa Deborah, Maiko alijiandaa vya kutosha na shida yake ilikuwa ni moja tu, nayo ni kumchukua na kumteka Deborah.
Walipofika pale, walimkuta bi.Rehema akiwa nje.
Wakati Maiko anaingia kwenye nyumba ya Deborah, macho yake yakagongana na macho ya bi.Rehema.
Maiko alimuangalia sana bi.Rehema bila ya kufanya chochote, alihisi kuwa sura ya mama huyo si ngeni machoni mwake.
Maiko aliendelea kuduwaa huku akimtazama bi.Rehema.
Maiko aliendelea kuduwaa huku akimtazama bi.Rehema.
Alihisi kabisa kuwa anamjua mama huyo, Pamela nae akawa anamshangaa Maiko jinsi alivyozubaa kwa kumtazama bi.Rehema kwani hata yeye aliyekuwa ameshikiliwa kwanguvu kama mtuhumiwa aliachiliwa, ndipo alipouliza.
PAMELA: Mbona unamshangaa, kwani unamjua?
Maiko hakujibu chochote alikuwa ameganda tu.
Rehema nae alikuwa amepatwa na kitu kama mshtuko kwa kumuona Maiko, akamsogelea karibu, akamshika kichwa na kuanza kumkagua kagua mwilini, Maiko aliganda kama sanamu alikuwa kama mtu aliyepigwa bumbuwazi.
Rehema alimshika mkono Maiko na kumvutia ndani kwa Deborah.
Alipofika nae sebleni, Deborah nae alikuwa anatoka chumbani na kushangaa kumuona Maiko, akajikuta akisema kwa kustaajabu.
DEBORAH: Maiko!!!
Maiko alimtazama tu Deborah kamavile hakumfata yeye.
Deborah akamshangaa bi.Rehema kumkaribisha Maiko ndani.
DEBORAH: Mama tafadhari, simtaki huyo mtu ndani ya nyumba yangu.
MAIKO: (Akaongea kwa mshtuko) mama!!!
Maiko akaanguka chini na kupoteza fahamu, ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Deborah kumuona Maiko akipoteza fahamu.
DEBORAH: Kheee!! Na mashetani huwa wanazimia?
PAMELA: Hata na mie nashangaa!
Rehema hakujibu kitu zaidi ya kutokwa na machozi tu.
Tusa na Sele walikuwa hatiani sasa na hawakujua ni jinsi gani watajinasua kutoka kwenye tukio la kumchoma kisu mwanajeshi.
SELE: Tusa, hii ni hatari sasa, naomba tufanye kitu.
TUSA: Kitu gani?
SELE: Tusiende tena Morogoro Tusa, machale yananicheza kuwa hatutakuwa salama huko.
TUSA: Sasa unataka twende wapi?
SELE: Twende Songea kwa bibi.
TUSA: Aaah! Mi Songea siendi.
SELE: Ubishi sio mzuri Tusa kumbuka kuwa tumeshaharibu, basi twende hata Mbeya.
TUSA: Mbeya ndo hunipeleki kabisaaa, sitaki kwenda kokote zaidi ya Morogoro. Nahitaji kumuona babu.
SELE: Tusa, tafadhari naomba unielewe. Twende Mbeya tutakuwa salama zaidi, Morogoro tutaenda mambo yakitulia.
TUSA: Sele, tafadhari usinichanganye. Huko Mbeya kuna tofauti gani ya Arusha na Mwanza? Kuchunwa ngozi hukohuko, kupiga nondo na matukio yote ya ajabu halafu unipeleke mimi Mbeya! Nishakwambia siendi popote zaidi ya Morogoro kwa babu.
SELE: Ubishi hauna faida Tusa, basi chagua mkoa unaoupenda zaidi ya Moro.
TUSA: Nishakwambia siendi popote zaidi ya Morogoro, kwanza wewe ndo chanzo. Usinichanganye sasa, unataka twende wote Moro hutaki baki Dom au uende hiyo mikoa yako ya ajabu.
Kwavile Sele alimpenda sana Tusa ikabidi akubaliane nae na hakutaka kumuona anaangamia.
Walipoona wale wanajeshi wameondoka wakaenda kupanda busi la kwenda Morogoro.
Marium akajiandaa kwaajili ya kwenda kumuona Deborah.
Akahitaji kwenda na Tina ili akamfahamu mdogo wake.
YUDA: Mmh! Mama, Tina muache achangamke kwanza halafu ndio utaenda nae.
MARIUM: Ila nilitaka akamfahamu mdogo wangu.
YUDA: Mama usijali, atamfahamu tu muda ukifika. Ila kwasasa muache hapa abaki na mimi.
MARIUM: Eti Tina, nikuache?
TINA: Usijali mama, nitaenda siku nyingine.
MARIUM: Sawa basi mbaki salama.
YUDA: Sawa mama, na wewe nenda salama.
Marium akaondoka kwaajili ya kwenda kwa Deborah.
Adamu alipokuwa anamuelezea Mashaka kuhusu matatizo yake, Mashaka akahisi moja kwa moja undugu uliopo kati ya Fausta na Adamu.
MASHAKA: Inamaana huyo Fausta ni ndugu yako?
ADAMU: Ndio, ni dada yangu kabisa.
MASHAKA: Halafu umesema kuwa Pamela ni mkeo?
ADAMU: Ndio ni mke wangu.
Mashaka akajikuta na maswali, kwani ajuavyo yeye ni kuwa Fausta na Pamela ni ndugu, sasa anamshangaa Adamu kusema kuwa mmoja na dada yake na mwingine ni mke wangu.
MASHAKA: Rafiki, pombe ulizokunywa zimekupeleka vibaya nini?
ADAMU: Kwanini?
MASHAKA: Yani ni kweli kabisa hayo maelezo uliyonipa?
ADAMU: Ndio ukweli mtupu huo.
Mashaka akahisi maelezo anayopewa na Adamu si sahihi, akafikiria labda watu anaowataja ni wengine.
MASHAKA: Itabidi ujiandae kurudi kwako.
ADAMU: Leo sirudi labda kesho, siwezi kulala nyumba ya mwanamke mimi.
MASHAKA: Hakuna tatizo basi, tushakuwa marafiki tayari. Utaenda kulala nilipofikia halafu kesho nitakusindikiza ulikofikia.
Mashaka aliamua kufanya hivyo ili apate kugundua ukweli wa maneno.
Patrick alifika karibia na kwao ila akasita kwenda kwani alijua wazi kuwa mama yake atamzuia kutoka wakati yeye bado alikuwa na mipango yake, na kikubwa alitaka kwenda kumjulia hali Tina, binti aliyemuokoa ili kujua maendeleo yake. Na ikiwezekana nae amlete kwao.
Akamwambia Fausta ashuke kwenye ile pikipiki na kumuelekeza.
PATRICK: Umeona ile nyumba yenye rangi ya maziwa?
FAUSTA: Ndio nimeiona.
PATRICK: Basi nenda pale waambie kuwa Patrick ndio ameniambia nije hapa, pale kuna mama yangu na mke wangu. Watakupokea vizuri tu hata usijali.
FAUSTA: Kwanini tusiende wote?
PATRICK: Usijali, mi nitakuja tu ngoja nikamalizie mambo flani kidogo halafu nitakuja.
Fausta akashuka na kutembea taratibu, kila alipokuwa anakwenda ndipo kumbukumbu zilipoanza kumrudia.
Deborah na Pamela walikuwa wakimshangaa bi.Rehema kutoa machozi kwaajili ya Maiko.
DEBORAH: Mama mbona hatukuelewi?
REHEMA: (Huku akilia), mwanangu huyu.
Wote wawili walisema kwa mshangao "mwanao!! Kivipi?"
REHEMA: Huyu ni mwanangu, huyu ni mtoto niliyemtafuta kwa kipindi kirefu sana.
Mara wakamuona Fausta akiingia mlangoni, Pamela alipomuona dada yake alifurahi sana na kuenda kumpokea ingawa alikuwa na bandeji kichwani.
DEBORAH: Jamani Fausta, imekuwaje?
Fausta aliwaangalia kwa sura ya huzuni huku akilia tu.
Ni muda huo huo Maiko nae akazinduka.
Tusa na Sele walipokaribia Morogoro ikambidi Sele ampigie simu Yuda ili tu kumpa taarifa kwani aliona usalama wao ni mdogo sana.
Wakati Sele anazungumza na Yuda ni muda huohuo ambao Patrick alikuwa nyumbani kwa wakina Yuda kwaajili ya kumuona Tina.
PATRICK: Vipi Yuda kuna nini?
YUDA: Mmh! Sele anasema anatatizo.
PATRICK: Kwani yuko wapi?
YUDA: Ameenda Morogoro.
PATRICK: Ameenda kufanya nini?
YUDA: Sijui.
PATRICK: Basi atajijua mwenyewe.
YUDA: Ila yupo na Tusa.
PATRICK: Nini?
Patrick akapandwa na hasira za ajabu.
Sele na Tusa wakati wanashuka kwenye basi wakakuta wanajeshi kama kumi wapo pale stendi
Ni Rehema tu ndiye aliyekuwa akishughulika na Maiko kwani Pamela na Deborah walikuwa makini kuongea na Fausta.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mara dada yake na Deborah akawasili na kuingia ndani, mtu wa kwanza kumuangalia ni yule Maiko aliyekuwa amekaa chini.
Marium alijikuta akienda pale chini na kumkaba Maiko bila hata ya kuwasalimia aliowakuta ndani.
MARIUM: Shetani mkubwa wewe, na lazima nikuue na wewe.
Marium alionekana kuwa na hasira sana dhidi ya Maiko.
Marium alionekana kuwa na hasira sana dhidi ya Maiko.
Aliendelea kumkaba Maiko huku Rehema akimtoa ile mikono, Deborah na Pamela walipoona lile tukio walistaajabu sana haswa Deborah, alishangaa dada yake amemjulia wapi Maiko.
Fausta nae alipotazama kinachoendelea akajikuta akimkumbuka vilivyo Maiko, naye akaenda kwa hasira alizo nazo na kuanza kumshambulia Maiko.
Rehema aliwasihi sana wasimshambulie vile, ikabidi yeye ajikinge juu ya Maiko.
DEBORAH: Hivi mama kwanini wamzuia huyo shetani asipigwe?
REHEMA: Jamani huyu si shetani, ni mwanangu jamani.
DEBORAH: Mungu wangu, na mashetani nayo huwa yanazaliwa na binadamu!!
Fausta na Marium walikuwa na hasira sana dhidi ya Maiko, Rehema nae alizidi kumzuia mwanae asipigwe.
MARIUM: Jamani mnaumzuia huyo mtu asipigwe? Ngoja niwaonyeshe sasa.
Marium akainuka na kwenda jikoni, alipotoka alitoka na panga. Maiko akaona hili sasa ni balaa, ikabidi atumie ujasusi wake kukimbia eneo hilo.
Hata wote mule ndani walishangaa amewaponyoka vipi.
MARIUM: Na ningemchoma nimkatekate na nyama, shetani mkubwa.
PAMELA: Mmh!! Kweli yule ni shetani jamani.
DEBORAH: Tena ni shetani mwenye mapembe.
Rehema alijiinamia akitoa machozi tu kwani kama mama ilimuuma sana kuona mwanae anaitwa majina ya ajabu kiasi kile.
Patrick akiwa pale kwakina Sele, akamuamuru Yuda awapigie simu wakina Sele ili wapete maelekezo ya kutosha.
YUDA: Mko wapi sasa?
SELE: Tupo hapa stendi ya Morogoro na tumezungukwa na wanajeshi nadhani tutakamatwa maana hatuna pa kukimbilia.
YUDA: Wawakamate kwa kosa lipi?
SELE: Siwezi kueleza ila wakitukamata nadhani watatupeleka Singida kuna tukio tumefanya kwa mjeda mmoja.
YUDA: Mbona nashindwa kukueleweni kaka?
SELE: Kuna mjeshi mmoja anaitwa Mwita tumeharibu kwake, sasa huyu rafiki yake Hamisi na wajeshi wengine ndio wanatufatilia yani hapa......
Kabla hajamaliza kusema anachosema alisikika Tusa akipiga kelele na gafla simu ikakatika.
Patrick alisikia yote kwani simu iliwekwa sauta kubwa, Patrick alichukia sana kusikia vile na kujikuta akisema "Tusa!!"
YUDA: Kaka haya majanga sasa.
PATRICK: Lazima nikamuokoe Tusa.
YUDA: Kwa wanajeshi kaka!! Utamuokoaje? Na utajuaje alipo?
Patrick alikaa kimya na kutafakari huku akili yake ikimcheza vizuri.
Maiko alikimbia na kwenda hotelini moja kwa moja, ilikuwa ni usiku ila hakujali alienda kwenye chumba cha Mashaka kwanza.
Alipofika jambo la kwanza ni kwenda kumkaba Mashaka bila ya kujali mgeni wake mule ndani.
MAIKO: Niambie ukweli Mashaka, mama yangu yupo hai au amekufa?
MASHAKA: Usinikabe basi, hayo si mambo ya kukabana bhana. Kwani vipi?
MAIKO: Sielewi, ila leo nimemuona mama yangu kwa macho yangu haya mawili.
MASHAKA: Kwani wewe mama yako unamjua?
MAIKO: Ndio namjua, mama yangu namjua vizuri sana. Ni mwanamke mpole, mcheshi na mkarimu.
MASHAKA: Mama yako ni nani?
MAIKO: Hilo sio jibu la swali langu, nijibu kwanza Mashaka.
MASHAKA: Mbona wanikosea adabu Maiko! Mimi ni nani yako?
MAIKO: Unataka kujua wewe ni nani yangu eeh!! Subiri nikuonyeshe.
Maiko akatoka chumbani kwa Mashaka na kwenda kwenye chumba chake.
Adamu alibakia kaduwaa na pombe pombe zake.
ADAMU: Kwani kuna nini?
MASHAKA: Usijali rafiki, wewe pumzika tu.
ADAMU: Maana mmenitisha.
MASHAKA: Usiwe na shaka bhana.
Adamu akaendelea kulala kwani akili ya pombe bado ilimtawala.
Wakina Deborah ilibidi wamuulize vizuri bi.Rehema kuhusu Maiko.
DEBORAH: Unajua mama hata hatujakuelewa, kwani Maiko ni mwanao kivipi?
REHEMA: Yule haitwi Maiko, ni mwanangu Juma yule. Mtoto anayenitoa machozi sikuzote nikimkumbuka.
PAMELA: Inamaana huyo ndio pacha wa Adamu?
REHEMA: Ndio, niliwazaa mapacha siku ya Jumanne. Ndipo mmoja nikamuita Juma na mwingine Jumanne. Hata nashangaa hilo jina la Maiko limetokea wapi!
DEBORAH: Ila tu hushangai jina la Adamu limetokea wapi!! Ama kweli ni mapacha mmh!!
PAMELA: Jamani Deborah, kwani tupo kwenye marumbano hapa?
DEBORAH: Na wala sijarumbana ila nimeongea ukweli, Juma amekuwa Maiko na Jumanne amekuwa Adamu. Mapacha wasiofanana hao.
Fausta alikuwa akilia tu, ndipo Marium alipogundua kuwa yule ni Fausta.
PAMELA: Fausta, mbona unalia tu kwani yule shetani alikufanyeje?
FAUSTA: Yule alikuwa mume wangu.
Wote mule ndani wakajikuta wakistaajabu na kusema kwa mshangao.
"mume wako!!!"
Fausta aliendelea kulia huku akikumbuka matukio aliyofanyiwa na Maiko.
DEBORAH: Mmh! Mbona haya majanga jamani!!
REHEMA: Mungu wangu, huu ni msiba wa familia sasa.
Rehema nae aliendelea kulia kwani hakujua ni jinsi gani atafanikiwa kutatua hilo tatizo.
Patrick aliondoka usiku uleule kwani kila walipompigia tena simu Sele alikuwa hapokei, simu iliita tu bila ya kupokelewa.
Patrick akarudi alipokuwa amehifadhi vitu vyake na akajiandaa na kuianza safari ya usiku kwa usiku ili kesho yake imkutie Singida na ajue jinsi gani ya kufanya atakapofika huko.
Yuda aliyekuwa na hofu juu ya Patrick, akaamua kumpigia simu.
YUDA: Kuwa makini sana kaka, na ukumbuke hao ni wanajeshi.
PATRICK: Usijali.
YUDA: Siwezi kukuzuia kwavile wewe ukiamua kitu umeamua ila umakini ni wa muhimu sana ndugu yangu.
Patrick alikuwa na nia moja tu nayo ni kumuokoa Tusa.
Alipokuwa anasafiri na gari yake usiku ule, akakutana na majambazi njiani waliozoea kupora na kuwaibia watu usiku, majambazi yale huwa yanangoja mabasi ya abiria barabarani ili wapore mali za abiria na magari ya kawaida ili wapore magari hayo. Ila Patrick alikuwa ni makini sana kwani kashapitia maovu mengi.
Akawaona njiani wakisimamisha gari yake, alichofanya ni kupunguza mwendo halafu akatoa bastola yake na kuwapiga majambazi wawili waliokuwa wanamsimamisha halafu akamwamuru yule jambazi aliyebaki kutoa mawe waliyoyapanga barabarani. Yule jambazi akaona kweli wamepatikana safari hii kwani walikutana na jambazi mwenzao, alipangua yale mawe na kumuacha apite.
Patrick aliporudi kwenye gari yake, akachukua bastola yake na kummalizia yule jambazi aliyebaki halafu akaendelea na safari.
Tusa na Sele walikuwa kwenye mikono ya wanajeshi, na yote ilitokana na kelele alizopiga Tusa kwani zilifanya wajulikane ni wapi wamesimama.
Sele alikuwepo kumtetea Tusa ila juhudi zake ziligonga mwamba na wote wawili kukamatwa kwani wanajeshi walikuwa kumi pale stendi.
Tusa aliendelea kupiga kelele baada ya kukamatwa, kitendo kilichomfanya apigwe vibao vingi na wale wanajeshi waliokuwa na hasira.
Wakawapakia kwenye gari yao na safari ilikuwa ni kuelekea Singida. Kwani muda ambao Sele na Tusa walitoroka, ni muda huo Hamisi alirudi tena kwa Mwita na kumuona akitapatapa na kuvuja damu nyingi, ikabidi amuwahishe hospitali ambapo alipopata nafuu kidogo akasema kuwa waliomfanyia hivyo ni Tusa na Sele, kwavile Hamisi alishawaona alikuwa ameshika sura zao vilivyo, na Mwita aliwaambia kuwa watu hao walikuwa na mpango wa kwenda Morogoro, kitendo hicho kiliwafanya wale wanajeshi kuzingira kila kituo cha basi Morogoro ili kukagua abiria wanaoshuka. Na kama wanajeshi walivyo na ushirikiano hiyo haikuwa kazi ngumu hata kidogo kwao, kwani walishapata maelekezo ya kutosha juu ya jinsi walivyo Sele na Tusa.
Hawakutaka kuchelewesha wakati, walisafiri nao jioni ile ile ili wawahi kufika nao Singida.
Ingawa Sele alikuwa amefungwa kamba vya kutosha ila nae alikuwa na mipango ya kumuokoa Tusa, alikuwa anaona bora yeye afe kuliko Tusa.
Maiko akarudi kwa Mashaka na picha ndogo mkononi yenye watoto wawili.
MAIKO: Haya mtambue mwanao hapo?
Mashaka alishika zile picha na kuziangalia kwa makini sana.
MASHAKA: Wewe ndio mwanangu Maiko.
MAIKO: Punguani kabisa wewe, hata mwanao humjui. Mimi sio mwanao Mashaka.
MASHAKA: Unasemaje Maiko?
MAIKO: (Akacheka sana), ulijiona mjanja eeh!
MASHAKA: Mbona sikuelewi Maiko?
MAIKO: Mwanao ulimuua kwa mikono yako mwenyewe bwege wewe, si ulisema kuwa alikuwa mzembe mzembe? Na uchizi wako toka milembe.
MASHAKA: Sikumuua mwanangu, niliyemuua ni Juma.
MAIKO: (Akacheka tena), kwa taarifa yako mimi ndio Juma. Huyo mwanao Maiko ulimuua mwenyewe. Mimi ndio mtoto niliyekuwa mjanja bhana.
Mashaka akampokonya ile picha Maiko, kumbukumbu zikamjia akapatwa na gadhabu kubwa sana, iliyopelekea yeye na Maiko kuanza kupambana mule ndani.
Patrick aliingia ndani ya Singida, alipomuona mwanajeshi akavutiwa nae na kupenda kufahamiana, mtu yeyote akikutana na Patrick hawezi kusita kuzungumza nae kwani alikuwa na kauli za kuvutia sana. Baada ya salamu na maneno mawili matatu, akaanza kujitambulisha.
PATRICK: Samahani kaka, naitwa Patrick sijui mwenzangu unaitwa nani?
MJESHI: Aah! Upo na Hamisi hapa ndugu yangu.
Patrick aliposikia hilo jina hakutaka kujua zaidi kama ndio Hamisi huyu au mwingine ila aliamua kushughulika na huyu kwanza.
Patrick aliposikia hilo jina hakutaka kujua zaidi kama ni Hamisi huyu au mwingine ila aliamua kushughulika na huyu kwanza.
Alianza kumvuta vizuri Hamisi ili aweze kupata uelekeo.
PATRICK: Dah! Nina rafiki yangu mwingine naye ni mwanajeshi, yani nimemkumbuka balaa ila sijui anapoishi.
HAMISI: Anaitwa nani?
PATRICK: Anaitwa Mwita.
HAMISI: Dah! Namjua huyo ni rafiki yangu pia. Yupo anauguza kidonda alichochomwa kisu.
PATRICK: Kachomwa kisu!! Mungu wangu, hebu Hamisi nipeleke nikamuone.
Hamisi akaanza safari ya kumpeleka Patrick nyumbani kwa Mwita.
Adamu alikuwa akisikilizia ugomvi wa Maiko na Mashaka kwakweli maneno yao yakamchanganya na yeye.
MASHAKA: Haya, huyo mama yako unayejivunia ni nani?
MAIKO: Ni dada yako Rehema, kichwa hiki kina kumbukumbu zote wewe. Usinitanie hata kidogo.
Kwakweli Mashaka aliishiwa uelewa na alijuta kwenda Mwanza na Maiko.
MASHAKA: Mmh! Maiko basi yaishe mwanangu.
MAIKO: Achana na mimi kabisa, ngoja niangalie ustaarabu wa kumpata mama yangu tu hapa.
Maiko akaamua kutoka, ndipo Adamu nae alipoinuka na kumfata Maiko kwa nyuma kwani alishindwa kumuelewa.
Mashaka alikaa chini huku akitawaliwa na mawazo kwenye akili yake.
INAENDELEA

0 Comments