Matukio ya ajabu yakasikika Singida, wanajeshi wapatao wanne walikutwa wamechinjwa sehemu tofauti tofauti. Kila mtu alipatwa na mashaka, msako ukaanza kwa kumtafuta mtu anayefanya matukio ya kusikitisha kama yake.
Wakati kila mwananchi akiwa na hofu, Hamisi alienda kumtembelea Mwita kama kawaida yake. Leo hii aliingia ndani bila hata ya kugonga hodi kwaajili ya kumpa taarifa ya vifo vya wanajeshi hao.
Ile ameingia tu akamuona Patrick akiwa na kisu mkononi tena kisu kilicho kuwa damu nyingi.
Ile anaingia tu mlangoni akamuona Patrick akiwa na kisu mkononi tena kisu kilichokuwa na damu nyingi.
Hamisi akapigwa na butwaa na kubakiwa na bumbuwazi,
HAMISI: Vipi tena Patrick?
PATRICK: Usishtuke Hamisi, njoo nikuonyeshe nilichokuwa nafanya.
HAMISI: Mwita yuko wapi?
PATRICK: Katoka kidogo kaenda kununua bidhaa, leo tumeamua kufanya mapishi hapa. Nilikuwa nachinja kuku.
HAMISI: Sasa ndio uchinjie ndani?
PATRICK: Sijachinjia ndani bhana, hiki ni kisu tu.
Hamisi alimtazama Patrick kwa macho ya wasiwasi na Patrick akaligundua hilo, akaamua kuweka kisu pembeni na kumkaribisha Hamisi ndani.
Hamisi hakutaka kuingia ndani kabisa ila kabla hajasogea kokote, Patrick alikuwa tayari yupo mlangoni. Hamisi akaogopa sana,
PATRICK: Wasi wasi wako ni nini Hamisi? Najua wewe ni mwadilifu na mwanajeshi imara katika kulitumikia taifa, sasa unaogopa nini kwa mtu kama mimi Hamisi?
HAMISI: Aaah..... Unajua..... Aaaah.....
Hamisi alishikwa na kigugumizi cha gafla.
PATRICK: Unawaza nini juu ya matukio ya vifo uliyoyasikia?
HAMISI: (Akashtuka kwanza), ndio nilikuja kumweleza bwana Mwita hapa ili nizungumze nae.
PATRICK: Na je iwapo unamjua mtu anayefanya hayo? Usiwe na shaka Hamisi, nataka kusaidia upelelezi.
HAMISI: Nikimjua nitachukua hatua ya kumripoti.
PATRICK: Je, hautapenda kupambana nae?
Hamisi akabaki kumuangalia tu Patrick huku akiwa hajui dhamira ya Patrick ni nini.
Mara akapigiwa simu kuwa mwanajeshi mwingine amekutwa amekufa. Baada ya simu kukatika, akajikuta akisema kwa hasira.
HAMISI: Hivi ni nani anayetenda haya?
PATRICK: Ni mimi Hamisi.
Halafu akaanza kucheka.
Adamu na Maiko kama walivyopanga, ikabidi Adamu afanye juhudi za kwenda kumchukua bi.Rehema ili Maiko apate kuzungumza nae.
MAIKO: Basi ukirudi njoo nae moja kwa moja huku.
ADAMU: Hakuna tatizo ila sielewi tu kwanini hutaki kwenda kule nilipokwambia.
MAIKO: Kuna muda utaelewa ila sio sasa, naomba tu nizungumze na mama kwasasa, niletee yeye tu ananitosha.
Adamu akaondoka na safari ya kwenda kwa Deborah ikaanza.
Deborah na Pamela walipatana sasa na kuendelea kufanya maongezi pamoja.
DEBORAH: Pamela rafiki yangu hata siku moja usikimbie tatizo ila kabiliana nalo na hapo utapata njia ya kuliondoa kabisa ila kulikimbia ni kujiongezea tatizo zaidi.
PAMELA: Nakubaliana nawe Deborah, sitapenda tuendelee kurumbana. Maji yakishamwagika hayazoleki tena. Ngoja nikueleze nilichofanya huko nyuma na kinachofanya nijute hadi leo.
Mara wakamuona Adamu amerudi, wakabaki wanamshangaa kwani alishindwa kuwapa hata salamu zaidi ya kumfata mama yake ndani.
DEBORAH: Hivi mumeo ameanza kuchanganyikiwa? Inamaana hajatuona hapa nje?
PAMELA: Sijui.
Wakamuona akitoka na mama yake na kuanza kuondoka, ndipo Pamela alipoinuka na kuuliza.
PAMELA: Wee Adamu, unafika bila salamu unamchukua mama bila ya kusema chochote halafu unataka kuondoka nae ndio nini hivyo? Ustaharabu gani huo?
ADAMU: Yani wewe ndio usiongee kabisa, ngoja nirudi unieleze ulipokuwa hadi mimi nahangaika mapolisi kukutafuta.
Adamu na mama yake wakaingia kwenye gari ya kukodi aliyoenda nayo Adamu mahali pale na kuondoka.
Rehema hakutaka sema chochote kwani alishanong'onezwa na Adamu kuwa wanaenda kwa nani, akajua kuwa angesema tu basi wale wanawake wote wenye hasira na huyo mtu wasingekubali.
Deborah na Pamela wakaendelea na mazungumzo yao hawakuwa na shaka sana kwani wanajua kuwa bi.Rehema ameondoka na mwanae.
Hamisi kumsikia Patrick kuwa ndiye aliyefanya mauaji yote yake, kwanza aliogopa pili alishangaa ni jambo lipi lilimpelekea Patrick kuua kiasi kile.
PATRICK: Unataka kujua nimewaua kwanini?
Hamisi aliitikia kwa kichwa tu.
PATRICK: Nimewaua kwasabu wana roho mbaya kushinda yangu, sasa wale wakiendelea kuwa jeshini watawatesa sana wananchi.
HAMISI: Ila umelitia jeshi hasara.
PATRICK: Hilo nalitambua.
Halafu akamfata tena Hamisi na kumkaba, ikabidi Hamisi ajitetee kwa kupigana na Patrick. Ila Hamis alishindwa na kujikuta akiwa chini.
Akachukua kamba na kumfunga mikono na miguu kisha na kumchinja kawa kuku. Huku akisema,
"Hivyo ndivyo nilivyowamaliza wenzio wote. Nilipambana nao kwanza na kuwafunga kamba, kisha nikawachinja taratibu kama kuku ili wayapate mateso waliyowatesea watu wote hadi kifo"
Akainuka juu na kumwambia tena,
"Sina sababu ya kukumaliza ila ushahidi wako umefanya nikumalize ili usije ukaniripoti kabla sijamaliza kazi yangu nyingine. Nayo ni Maiko tu."
Patrick hakupoteza muda zaidi mahali hapo na usiku huo huo akasafiri kurudi Mwanza.
Bi.Rehema alipelekwa hadi alipo Maiko, yote haya yalishuhudiwa na Yuda.
Bi.Rehema alifurahi sana kumuona tena mtoto wake huku akimuangalia kwa umakini mkubwa. Maiko nae alifurahi kumuona mama yake na kwa mara ya kwanza tangia kukua kwake aliweza kutoa machozi siku hii ya leo.
REHEMA: Niambie mwanangu, kwanini imekuwa hivi?
MAIKO: Ni ndugu yako Mashaka ndiye aliyesababisha haya, alinifanya niamini kuwa ulikufa kitambo sana na hatuna ndugu tena. Na kwavile alirudi kama kachanganyikiwa tukaamini kuwa ni kweli.
REHEMA: Mmh! Jamani mwanangu!! Na kwanini ulibadili jina?
Maiko akaamua kuwaelezea kilichotokea,
"Ilitokea tu mama, mimi ni Juma na mtoto wa Mashaka aliitwa Maiko. Kipindi tunaenda Mombasa alimpitia huyo Maiko tukaondoka nae. Tulivyofika kule yeye akarudi kwenu, ni kipindi hicho ambacho mimi na mwanae tulibadilishana majina.
Alikawia sana kurudi, alikaa kama miaka mitatu, sisi tulikuwa tukitumikishwa tu na yule mwenzie tuliyekuwa nae. Aliporudi alikuta tumeyazoea yale majina tuliyobadilishana na hakuweza kutambua kwavile wote tulikuwa rika moja, tukamuuliza kuhusu mama zetu akajibu kuwa walikufa, kwakweli nilishikwa na uchungu sana na machozi yakanitoka, yule mwenzangu alilia hadi kujigalagaza chini na hakukubaliana na maneno kuwa mama yake amekufa, wakati huo ukumbuke alikuwa hatujui vizuri kwahiyo alitutambua kwa majina tu, alikuwa akijua mimi ndio yule na yule ndio mimi.
Akamgeukia mwenzangu na kumwambia kuwa yeye ndio hata asijisumbue kulia kwani ameshapoteza ndugu wote, hana ndugu hata mmoja zaidi yake. Mwenzangu hakukubali aliendelea kulia kila panapokucha, Mashaka hakupendezewa na yale makelele ya kila siku.
Siku hiyo usiku alituita na kutukanya tena ila bado ilikuwa kazi bure kwa yule mwenzangu, nikamuona Mashaka akitoa kisu na kumchoma yule mtoto kifuani na kusema hataki watoto wazembe. Na huo ukawa ndio mwisho wa mwanae Maiko ila yeye alijua ni Juma.
Nikabaki mimi na yeye na akanifundisha kazi za kujipatia kipato huku akiamini kuwa mimi ni mwanae ndio hadi ukubwa huu nakuja kutambua uwepo wa mama na ndugu zangu"
ADAMU: Duh!! Huyo Mashaka hafai basi.
Rehema alikuwa akilia tu huku mwanae akielezea.
REHEMA: Mashaka sio mtu kabisa, ni ndugu yangu ila hafai. Tafadhari mwanangu Juma, nina swali moja tu nataka unijibu.
MAIKO: Uliza tu mama.
REHEMA: Hivi ni kweli umekuwa katili kama huyo Mashaka?
Maiko alibaki kumtazama tu kwasababu ni ukweli mtupu tena yeye ndio alipatwa na ukatili wa ajabu. Ila kabla hajajibu, Mashaka alikuwa ameshaingia ndani ya nyumba ile.
Hali ya Tusa haikuwa nzuri sana ila Sele akaona ni vyema aondoke nae hapo hospitali na aende nae Mwanza mjini ikiwezekana familia nayo ipate habari kwa mambo yaliyotukia.
Kwahiyo akaanza safari ya kuondoka na Tusa kwenda nae Mwanza mjini, wakiwa kwenye bus wanasikia habari ya vifo vya kusikitisha vya wanajeshi mkoani Singida, majina yao yanatajwa na kwaharaka haraka Sele anatambua kuwa ni wale wanajeshi waliowatesa.
Tusa nae aliposikia hivyo anahisi moja kwa moja kuwa aliyehusika ni Patrick tu. Hofu inawatawala wote wawili juu ya Patrick.
Patrick ameingia Mwanza na jambo la kwanza kufanya ni kumtafuta Sele ili aweze kujua ni wapi alipo Tusa.
Akaanza kumtafuta hewani, ila kabla hajapiga simu ya Sele inaingia simu ya Yuda kwake, ikimwambia aachane na shughuli zote ili waende kupambana na Maiko kwani ameshajua sehemu alipo.
Habari ile inamvutia Patrick kwani bado anahamu ya kuua watu wote wanaoharibu furaha yake.
Akiwa anatafakari la kufanya pale njiani kama akamuangalie Tusa kwanza au akashughulike na Maiko, mara akashikwa bega, kugeuka nyuma ni Mwita akiwa na wanajeshi wengine watatu.
Mara akashikwa bega, kugeuka nyuma ni Mwita akiwa na wanajeshi wengine watatu.
Patrick akashtuka hadi wale wakamshangaa kwani hakutarajia kuonana na Mwita kwa wakati huo ukizingatia ameshafanya mambo mabaya,
MWITA: Vipi Patrick mbona umeshtuka? Inamaana hukutarajia kukutana na mimi huku Mwanza?
PATRICK: Aah! Kumbe ulishakuja Mwanza!
MWITA: Patrick, umesahau jamani!! Si uliniambia mwenyewe kuwa nitangulie Mwanza? Na siku niliyoondoka nikakwambia, tangia hapo sijakupata tena hewani hadi nakuona leo.
PATRICK: Dah! Nilisahau bhana, kule nilipoenda hakuna umeme kabisa ndomana sikuwa hewani, nimechajia hapahapa Mwanza leo.
MWITA: Basi hawa ni wanajeshi wenzangu, wenyewe kikosi chao kipo huku Mwanza.
PATRICK: Basi vizuri kuwafahamu.
Patrick sasa akajisikia amani kidogo maana mwanzoni alidhania ameshtukiwa alichofanya.
MWITA: Sasa vipi kuhusu ile ahadi Patrick?
PATRICK: Ile ya kuhusu baba yako?
MWITA: Ndio.
Patrick akaamua kumuelekeza Mwita mahali alipoambiwa na Yuda ili yeye aendelee na mishe zake zingine kwanza, kwavile Mwita hakuwa mwenyeji mzuri wa Mwanza ikabidi aende na wale wenzie kule alipoelekezwa na Patrick.
Deborah na Pamela waliamua kuingia ndani ili kuongelea mambo mengine.
DEBORAH: Jamani hapa tumelia sana tena tumelia vya kutosha, hebu tuwashe na radio kwanza tujiliwaze na kupata habari tofauti tofauti.
PAMELA: Kweli kabisa Deborah ili tupunguze machungu yetu.
Deborah akainuka na kuwasha radio na muda huo huo wakasikia tukio la mauaji ya wanajeshi mkoani Singida.
PAMELA: Jamani majanga gani hayo?
DEBORAH: Zaidi ya majanga, ni binadamu gani mwenye roho mbaya kiasi hicho? Yani anachinja kama kuku!!
MARIUM: Ingekuwa Maiko yupo huko Singida ningesema ni yeye tu,
PAMELA: Kwanini Maiko na si mtu mwingine?
MARIUM: Kwasababu yeye ndio mwenye roho ya kinyama namna hiyo.
DEBORAH: Kwanza mimi ndio sielewi mwenzenu, kwanini Maiko kawa ndugu wa Adamu? Dah!
FAUSTA: Wote nadhani hilo swala haliwachanganyi, mimi mwenzenu ndio sielewi hata itakuwaje yani sielewi kabisa.
Maiko aliweka msiba mkubwa sana moyoni mwa wanawake hawa na hawataweza kumpokea kama mwanafamilia kwa aliyowatendea.
Tusa na Sele wakiwa Mwanza wanamuona Mwita na wenzie wakipita, Tusa anajibanza huku akimkumbatia Sele kwa nguvu kabisa.
Tusa hakutaka kumuachia Sele, alijikuta akiwaogopa wanaume wote kasoro Sele ambaye aliishi nae kwa kubembelezwa.
TUSA: Sele, nakuomba unirudishe kwa mama. Nataka nirudi nyumbani na mama yangu ili nikaishi tena na familia yangu.
SELE: Tulia Tusa, yote yana mwisho haya.
TUSA: Kwakweli Sele unanipenda na unateseka kwaajili yangu, tamaa imeniponza Sele. Nilidhani wanaume wote duniani ni Sele, kumbe kuna wakina Patrick, John, Maiko na Mwita. Sikulijua hilo, Sele una moyo wa kipekee, moyo wa tofauti. Nimeoza mimi Sele ila bado hutaki kuniacha, nanuka mimi ila bado upo karibu yangu.
Tusa alizidi kumkumbatia Sele huku machozi yakimbubujika.
Muda ambao Mwita na wenzie walipita mahali hapo ni muda huo pia Patrick nae alikatisha mahali hapo, wakina Mwita hawakuwaona Tusa na Sele ila Patrick aliwaona na kuwashangaa kilichowafanya wakumbatiane pale njiani, akaanza kuwafata pale walipo.
Mashaka aliumia sana moyo na kuendelea kumfatilia Maiko.
Akafika hadi mahali ambako Maiko alikuwa akifanya maongezi na mama yake na pacha wake pia.
Mashaka alifika na kuingia huku akiwa na hasira sana.
MASHAKA: Maiko, kitu ulichonifanyia nakwambia ipo siku utalipia.
Kuangalia pembeni akamuona dada yake bi.Rehema.
REHEMA: Hivi wewe Mashaka, mambo yako mangapi umeyalipia? Maovu uliyoyatenda unadhani yamesahaulika?
Mashaka akamuangalia sana dada yake hakutaka kuongea kitu cha zaidi ila akaondoka na kwenda kutafakari.
"Yani mimi ndio nikose kila kitu? Ila Maiko kwa maovu yake yote bado apate furaha ya maisha? Labda kama Mashaka nitakufa lazima nifanye kitu"
Mashaka alikuwa na hasira sana juu ya Maiko ukizingatia alikuwa anajua ndiye mwanae wa pekee.
Mwita alipelekwa na wanajeshi wenzie hadi mahali walipohisi ndio penyewe walipoelekezwa.
Mwita akagonga mlango, Maiko akajua Mashaka amerudi ikabidi ajiandae kwaajili ya kupambana.
Ila alipofungua mlango akamuona Mwita, naye Mwita akaingia ndani na kumwambia.
MWITA: Nimekutafuta sana baba, kwanini unanifanyia hivi?
MAIKO: Mmh!! Unanijua mimi vizuri?
MWITA: Nakujua ndio na picha zako ninazo baba.
MAIKO: Picha zangu? Alikupa nani?
MWITA: Alinipa mama, ngoja nikuonyeshe picha yake.
Mwita akatoa picha ya mama yake na kumkabidhi Maiko, akaitazama ile picha na kumkumbuka vizuri huyo mwanamke.
MAIKO: Kweli wewe ni mwanangu.
Maiko akamkumbatia Mwita, bi.Rehema na Adamu wakabaki wanashangaa tu. Ikabidi Maiko awatambulishe kwa ufupi.
Akawapatia na picha ya mwanamke aliyezaa nae.
MAIKO: Huyu ndiye mwanamke niliyezaa nae ila sikuwa naishi nae ilitokea tu tukampata huyo mtoto.
Maiko alificha ukweli wa mambo juu ya huyo mwanamke.
Bi.Rehema alipoangalia picha ya mwanamke huyo sura yake ilimjia vilivyo.
REHEMA: Mbona kama....., hebu ona na wewe.
Akamkabidhi na Adamu aitazame vizuri.
ADAMU: Mmh!! Ni huyu huyu mama.
Adamu na bi.Rehema wakajikuta wakitazamana kwa mshangao.
Tusa na Sele wala hawakumuona Patrick anavyowafata, Sele akasimamisha gari ya kukodi halafu wakapanda na kuondoka, Patrick nae akawafata kwa nyuma, yeye alikodi bodaboda.
Walienda moja kwa moja hadi karibia na nyumbani kwa Deborah wakashuka, wakawa wamesimama huku wakiongea, Patrick nae akashuka na kuwafata kwani wivu ulishamshika kwa jinsi alivyowaona.
Nia yake ni kujua kuwa kwanini walikuwa wamekumbatiana pale njiani.
Nia yake ilikuwa ni kujua kuwa kwanini walikumbatiana pale njiani.
Patrick akawasogelea pale walipo, kumuona wakashtuka sana.
PATRICK: Mbona mmeshtuka?
SELE: Hatukutarajia kukuona hapa muda huu.
PATRICK: Vizuri sana, haya umetoka wapi na Tusa?
SELE: Nimetoka naye hospitali.
PATRICK: Inamaana humo ndani kwetu hakuna watu wote wa kwenda nao zaidi ya wewe?
SELE: Ndio tunafika leo Patrick, hali ya Tusa ilikuwa mbaya sana.
PATRICK: Hata kama, mlitakiwa kufika nyumbani kwanza. Hilo ni kosa la kwanza, haya na kwanini mlikumbatina njiani?
Ikabidi Sele amweleze walivyowaona wakina Mwita na Tusa akapatwa na uoga na kujificha.
PATRICK: Kwanini Tusa unamuogopa Mwita? Nipe sababu sasa.
Tusa huku akiogopa na kutetemeka,
TUSA: Alinibaka.
Sele alishtuka ila Patrick alishtuka zaidi na kumuuliza tena na jibu likawa lile lile.
PATRICK: Kwanini alikubaka? Kwani alikubakeje?
TUSA: Sijui ila alinipiga sana halafu akanibaka.
Hasira zikampanda Patrick na kuona Mwita nae ni sawa na Maiko.
Akataka kuondoka ila mama yake mdogo akamuona na kumuita.
"Patrick, Patrick"
Alikuwa ni mama yake mdogo ambaye ni Anna.
Deborah bado hakuridhishwa na hali ya kuwa ni Patrick ndiye aliyemkomboa Pamela.
FAUSTA: Ila Deborah hata mimi nimekombolewa na huyo kijana maana alisema kuwa nikifika hapa niseme ni yeye kanielekeza.
DEBORAH: Yani na wewe unamaanisha Patrick!!
FAUSTA: Ndio huyo huyo, kwakweli Deborah unastahili pongezi kwa kumpata mtoto wa aina ile.
Deborah alicheka machoni ila moyoni aliumia sana haswa akifikiria huo uhusiano wa Patrick na Maiko.
TINA: Hata na mimi ameniokoa Patrick.
DEBORAH: Kheee! Kumbe hadi wewe!!
TINA: Ndio, kwakweli yule Patrick ana moyo wa tofauti sana.
DEBORAH: Nyie wote mlitekwa halafu wote mmeokolewa na Patrick mbona nashindwa kuelewa hapa, je kuna mahusiano yoyote kati ya ho waliowateka na Patrick?
FAUSTA: Kwa hilo mi sijui labda utamuuliza mwenyewe siku akirudi.
Wakiwa wanaendelea na maongezi wakamuona Anna, Patrick, Tusa na Sele kwakweli hawakuamini kuwaona waliwafurahia sana na kuwakumbatia kwa furaha.
Deborah alifurahi sana kumuona mwanae.
DEBORAH: Jamani Patrick mwanangu, ulikuwa wapi siku zote baba?
PATRICK: Nisamehe mama, ni historia ndefu sana.
DEBORAH: Unanipa presha na mawazo mwanangu kwanini jamani?
PATRICK: Nisamehe mama.
Patrick hakupanga kabisa kurudi kwao muda huo kwani hakutaka kukumbana na lawama za mama yake.
Pamela alilia kwakweli kwa muonekano wa mwanae aliyekuwa amefifia na kukonda zaidi.
Huku Deborah kichwa kikikosa kumuelewa vizuri Patrick.
Akamgeukia na Anna kumuuliza.
DEBORAH: Na wewe Anna siku zote hizi ulikuwa wapi?
ANNA: Nilisafiri kidogo dadangu, nisamehe sikukuaga. Siku niliyoona umepata nafuu ndipo nilipoamua kuondoka.
Wote wakawa wanafurahi sana kasoro Patrick ambaye alikuwa na mawazo mengine kichwani huku wengine kama Pamela, Fausta na Tina wakimpa pongezi kwa kazi aliyowafanyia.

0 Comments