Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mume gaidi sehemu ya kumi na tano (15)



Patrick alishangaa kumuona Tulo pamoja nao.

Akajiuliza wamemtoa wapi na kwanini wameongozana nae.

Kufika karibu Tulo nae akamuona Patrick na hofu ikamjaa, Patrick alimfata Tulo na kumkunja ikabidi Deborah ndio amtete Tulo.

DEBORAH: Patrick mwanangu muache kijana wa watu hajafanya lolote baya.

Patrick kwa heshima ya mama yake akamuachia Tulo ila akataka kupewa maelezo xa kutosha kuwa yule Tulo ni nani yao.


Walipoingia sebleni, Pamela alienda moja kwa moja mahali ambako mwanae alikuwa amekaa na kujiinamia na machozi, ikabidi ainuke nae na kwenda nae chumbani.

PAMELA: Tatizo ni nini mwanangu?

TUSA: Mama, Patrick ameniambia maneno ya fedheha na kuumiza sana.

PAMELA: Kivipi na amekwambiaje?

TUSA: Yani kweli yeye wa kuniambia mimi kuwa ni mwanamke niliyechakaa, eti nimeshachoka anaendelea nami kwa kunihurumia tu, kwakweli mama sitaweza kuishi tena na Patrick naomba myasitishe mahusiano yetu ikiwezekana anipe talaka yangu tu.

PAMELA: Mmh mbona pagumu sana hapo mwanangu!! Unadhani Patrick atakubali?

Mara Deborah naye akaingia mule chumbani na kuwauliza kinachoendelea na shida ya Tusa ni nini.

DEBORAH: Tusa jamani, kwanini tusiyasuluhishe tu haya ili muendelee kuwa pamoja?

TUSA: Mama zangu, kiukweli sijisikii kuwa na Patrick na kamwe sitajisikia kwahiyo matatizo na migogoro hii haita isha kamwe, ataendelea kunibaka na kunipiga. Nimechoka sasa, kama hamtaki kunisambaratisha nae nitajua cha kufanya.

PAMELA: Unamaana gani Tusa?

Deborah ikabidi amwombe Tusa aende sebleni kwanza ili wao waweze kujadili.

DEBORAH: Unadhani tufanyeje Pamela?

PAMELA: Mimi sijui, sijui kabisa mwanangu ana matatizo gani kwani nionavyo mimi Patrick ni mtu sahihi kwake cha muhimu ni kuelewana tu.

DEBORAH: Kwavile leo wote wapo, basi twende tukajadili ili kujaribu kuwapatanisha kwanza.

Wakakubaliana kwenda kufanya mazungumzo kwaajili ya kutatua tatizo baina ya Patrick na Tusa kwanza kabla ya chochote.


Bi.Rehema aliendelea kumuomba Mashaka kuwa akubali waende nae kwa Deborah, ila Mashaka aliendelea kukataa kufanya hicho ambacho anaambiwa na dada yake kwa kuhofia usalama wake na maisha yake.

MASHAKA: Dada, huko nitakutana na mtu mmoja anaitwa Patrick. Mtu huyo ni khatari sana dada yangu, anaweza hata kunichinja.

REHEMA: Wasiwasi wako tu ila Patrick si muuaji, yeye hupenda kusaidia watu walioko kwenye matatizo.

MASHAKA: Dada, nadhani humjui vizuri huyu Patrick na kwanini nakwambia kwamba ni mtu khatari. Patrick hafai kabisa, bora mimi chui unayenijua kuwa chui kuliko huyo Patrick. Amevaa ngozi ya kondoo kumbe ni chui mla watu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

REHEMA: Mbona sikuelewi Mashaka!!

MASHAKA: Unajua Patrick kaua watu wangapi? Unadhani atashindwa vipi kunimaliza na mimi? Patrick hujifanya kuokoa mmoja na kuangamiza zaidi ya kumi.

REHEMA: Mmh!! Ila hata hivyo pale hawezi fanya chochote ukizingatia mama yake yupo tena na wengi tu.

Rehema aliendelea kumuomba Mashaka hadi akakubali.

Mashaka akamwambia Rehema kuwa aende nae huko kwa Deborah.

Kufika karibu na nyumba ya Deborah, Rehema akashuka huku akimngoja Mashaka nae ashuke waweze kwenda ila alichofanya Mashaka ni kushusha kioo cha gari kisha akamuaga dada yake kuwa atakuja siku nyingine na kuondoka zake.

Mashaka bado alikuwa na hofu ya kukutana na Patrick kwani alijua ni jinsi gani Patrick alivynkuwa na hasira juu yake.


Pamela na Deborah wakarudi sebleni na kumuulizia Tusa ili waweze kuanza hicho kikao ila wakaambiwa kuwa Tusa ameenda dukani.

PAMELA: Ameenda peke yake?

PATRICK: Ndio, ila hakuna tatizo lolote.

Ndipo hapo wakakumbuka na kitu kingine kuwa bi.Rehema hayupo, wakamuuliza Sele ambaye alifika na Tusa mwanzoni naye akasema kuwa hawakumkuta.

Hofu ikawatawala kuwa mmama yule wa makamo atakuwa wapi.

Wakaji wanajiandaa kutafuta, bi.Rehema nae akawa anarudi, wakamshangaa na kumuuliza alipokuwa.

REHEMA: Nimekuja na Mashaka hadi hapa ila amekataa kuingia ndani na kuondoka.

Patrick akashtuka kusikia Mashaka ukizingatia Tusa nae alikuwa dukani.

PATRICK: Mmekutana na Tusa?

REHEMA: Hapana, hata hatujamuona.

Patrick bado hakuridhiwa kwani alimjua vizuri Mashaka kwa Tusa, ni kama vile simba kwa swala ikabidi atoke kwenda kumuangalia ila kwa bahati akamuona Tusa anarudi ndipo hapo aliporudi tena ndani.


Marium alikazana na lengo lake la kuonana na mganga wa jadi kwaajili ya mwanae, akaenda kwa mzee mmoja aliyeambiwa kuwa anahusika sana na mambo ya asili kumuulizia.

MZEE: Mwanao na huyo mwanamke hawawezi kuachana kabisa tena hawawezi kuachana kirahisi hivyo kama unavyodhani.

MARIUM: Vipi? Mwanangu amerogwa eeh!

MZEE: Kuna kitu kati yao ambacho walikifanya huko nyuma kabla, siku moja mdadisi mwanao.

MARIUM: Kitu gani hicho?

MZEE: Jaribu kumuuliza mwanao akwambie.

MARIUM: Je, kinaweza kutenguka na wakaachana? Nisaidie mzee, kiukweli yule binti hamfai kabisa mwanangu. Naomba unisaidie.

MZEE: Kuachana kwao labda mmoja afe ila la sivyo itabidi ukubali tu matokeo. Mwanao kampenda sana yule binti na yule binti nae kampenda sana mwanao na ndiomana anapata shida hata kukaa na kutulia na mwanaume mwingine hawezi anataka kurudi kulekule na kwa mwanao nae ndio hivyohivyo. Nadhani watakuwa wanajutia juu ya walichofanya ila ndio hivyo hakiwezi kutenguka.

MARIUM: Jamani mzee nisaidie, yule binti kachoka kashabakwa na wanaume hamsini kidogo sitapenda awe na mwanangu nakuomba unipe msaada wako.

MZEE: Labda ukajaribu kwingine ila kwa mimi imeshindikana.

Marium aliondoka akiwa amenywea sana ila akasema kuwa hawezi kukubali hadi pale atakapofanikiwa kumtenganisha Sele na Tusa ili wasikumbukane tena na Sele aweze kuoa mwanamke mwingine.

"wangapi wanaachana na kuoa na kuolewa na watu wengine tena mara nyingine ndoa hazidumu wanaoa tena na kuolewa tena na tena kwanini wao ishindikane? Sele lazima amuache yule mwanamke kwani hamfai kabisa kashachoka na kuchakaa, sijui Tusa alimpa limbwata mwanangu dah!! Limbwata lake kali sana ila lazima nitalitengua tu."


Maiko kuona mambo ya Mashaka hayaeleweki akapatwa na hisia kuwa huenda Mashaka amerudi tena Mwanza kwahiyo na yeye akaamua kufanya safari ya kwenda Mwanza kwani hakumuamini Mashaka hata kidogo, alihisi kuwa anaweza kuisambaratisha familia yake ndogo aliyoijua ukubwani.


Baada ya wote kukamilika, ikabidi wafanye mazungumzo ya kumpatanisha Patrick na Tusa, walizungumza mengi ila Tusa alionekana kulia na kujiinamia muda wote.

PATRICK: Jamani mimi sina tatizo, Tusa ni mke wangu na ninampenda. Ninachomuomba ni kuwa atulie na mimi tu, tatizo lake huyu Sele anamchanganya sana akili.

DEBORAH: Achana na hayo ya Sele Patrick, tuzungumzie haya kwanza. Sele ni muelewa na hawezi kuendelea kumfatilia mke wa mtu.

Deborah alimtetea Sele bila ya kujua kuwa Sele mwenyewe muda wote mawazo ni kwa Tusa.

PAMELA: Mi ninachoona Tusa atulie tu na Patrick.

ADAMU: Ngoja tumsikie na Tusa mwenyewe ana maoni gani.

TUSA: Mimi sitaki kuendelea kuishi na Patrick kwani matatizo baina yangu na yake hayataisha. Ingawa Patrick ni mume wangu ila nakiri wazi na mbele yenu kuwa simpendi.

FAUSTA: Jamani Tusa acha kuongea maneno makali kiasi hicho.

PATRICK: Mimi nampenda Tusa na pia nakiri wazi kuwa siwezi kuachana nae.

Wakaendelea kujadili na kumsihi Tusa awe na Patrick kwakuwa ni mumewe.

PATRICK: Nimefunga nae ndoa ya gharama sana, siwezi kuachana nae jamani. Tusa ni mke wangu cha msingi ni mumshauri kuwa atulie tu.

Tusa akainuka na kwenda jikoni.

PATRICK: Tusa ana kiburi sana na jeuri, mwambieni abadilike ili tujenge maisha yetu. Sipendi kurumbana nae kila siku wakati ni mke wangu.

PAMELA: Tumekuelewa Patrick, usijari Tusa nae atakuelewa tu.

Sele alipoona muda umepita bila Tusa kurejea akaamua kwenda jikoni na kumkuta Tusa chini, akamkimbilia na kumshika kisha akawaita waliokuwa sebleni.

Wote wakashangaa kumuona Tusa akitapatapa pale chini huku povu likimtoka mdomoni.

Tusa alikuwa amekunywa sumu.


Wote wakashangaa kumuona Tusa akitapatapa pale chini huku povu likimtoka mdomoni.

Tusa alikuwa amekunywa sumu.

Pamela alipomuangalia mwanae pale chini akaangua kilio,

"Jamani mwanangu, mwanangu amekufa jamani"

Patrick akadakia na kuwaambia,

"Kweli nyie akili ni fupi, sasa kulia kutakusaidia nini?"

Patrick akainama na kumbeba Tusa begani kisha akaianza safari ya hospitali, wengine wakamfata nyuma tu.

Sele alikuwa kama vile kachanganyikiwa, alikazana kuomba kuwa Tusa apone na awe mzima.

Wengine wakaenda hospitali na wengine wakabaki nyumbani.


Pale hospitali wakaanza kumuhudumia Tusa na kugundua kuwa amekunywa sumu, ikabidi wafanye kazi yao ya kukata ile simu kwanza kisha kumuwekea dripu.

Daktari akawafuata ili azungumze nao ila Patrick akasogea na daktari pembeni ili azungumze nae yeye,

DAKTARI: Inaonyesha kuwa mgonjwa wenu amekunywa sumu.

PATRICK: Hilo tunalitambua labda useme lingine, kwani anaendeleaje?

DAKTARI: Maendeleo yake si mabaya, nadhani atapona.

PATRICK: Apone bhana ndio tunachokitaka.

DAKTARI: Mambo haya huhusiana na ripoti ya polisi sababu kujiua ni kosa kisheria na inahitajika mtuhumiwa awe chini ya ulinzi sasa.

PATRICK: Sawa nimekuelewa, kwahiyo unataka kufanya nini?

DAKTARI: Tunahitajika kuandika ripoti na kuipeleka polisi kabla hawajapata taarifa hii toka kwa wengine.

PATRICK: Wewe daktari unajipenda kweli?

DAKTARI: Ndio najipenda kwani vipi?

PATRICK: Kama unajipenda, tafadhari achana na hizo habari. Nyie muhudumieni akipona turudi nae nyumbani basi.

Daktari akashangaa kauli ya Patrick kwani yeye alikuwa anamuelezea kwaajili ya kupoozwa na vitu kama rushwa ila akashangaa jibu alilopewa na Patrick.


Yule daktari aliwafata madaktari wenzie wawili na wao wakaenda kumchungulia Patrick, daktari mmoja wapo alipomuona Patrick alishtuka sana kwani alikuwa ni yule daktari aliyetishiwa silaha na Patrick kwa kudai PF3.

DAKTARI 1: Dah! Kumbe ni yule jamaa, muacheni kama alivyo mafia yule.

DAKTARI: Kwani unamjua?

DAKTARI 1: Ndio namjua, kwanza pale usimuone vile anatembeaga na mguu wa kuku yule. Mi simo kabisa, kama mtaamua kuchonga kachongeni wenyewe tu.

DAKTARI 2: Hata mi mwenyewe namjua, akiamua kukupiga hutathubutu kuamka.

DAKTARI: Sasa kama anatumia ubabe kama huo, hajui kuwa sisi tunauwezo wa kumpoteza mgonjwa wake?

DAKTARI 1: Thubutu kama hujazikwa pamoja na huyo mgonjwa wake, jamaa yule ana machale balaa. Yule ni mafia nakwambia.

DAKTARI: Mmh! Jamani mi najipenda, naipenda kazi yangu na familia yangu naipenda, tuachaneni na mambo haya twendeni tukamuhudumie tu huyo mgonjwa.

Madaktari wakaamua kuendelea na kazi yao.


Pamela alijisikia kulia tu kwani uamuzi ambao mwanae ameuchukua uliwatisha sana, familia nzima ilijikuta ikiogopa.

Tusa akalazwa kwa takribani siku mbili ili kurejeshwa katika hali ya kawaida.


Anna alipopata habari ya Tusa ikabidi amfate dada yake Marium kwenda kumwambia na kumuuliza.

ANNA: Au kuna kitu umefanya dada yangu?

MARIUM: Kwanza mi mwenyewe hiyo habari ya Tusa kunywa sumu inanitisha na kunishangaza. Ni kweli sipendi Tusa awe na mwanangu ila siwezi kuwatenganisha kwa kifo bhana mdogo wangu.

ANNA: Basi hofu ikanishika, nilijua umeenda kwa hao waganga wako na kuwaomba wamuue maana watu hao nao wana njia nyingi kweli za kumaliza watu.

MARIUM: Itabidi twende tukamuone, haya sasa majanga ndiomana mwanangu Sele hajarudi kabisa. Yuda nae yupo kama mwizi mwizi vile haonekani nyumbani hata sijui anakuwa wapi siku hizi.

Ikabidi wajiandae na kuanza safari ya kwenda nyumbani kwa Deborah wakijua labda Tusa ameshatoka.


Yuda ambaye alibaki na Tina pale nyumbani siku hiyo ambayo bi.Rehema naye aliomba kwenda hospitali kumuona Tusa.

Yuda akaamua kuutumia muda huo kuzungumza na Tina.

YUDA: Tina natumaini sasa matatizo yako yameisha, mimi swala langu kwako lipo palepale. Nataka kuwa na wewe.

TINA: Ingawa nimebakwa na unalijua hilo, bado wataka kuwa na mimi?

YUDA: Ndio Tina, nakupenda niamini hivyo Tina. Ukikubali kuwa na mimi nitakuoa Tina.

TINA: Mmh!! Hapana, bora niolewe na mwanaume ambaye hafahamu ukweli. Wewe Yuda unajua kila kitu lazima badae utanitusi kwa kejeli tu.

YUDA: Hapana Tina, siwezi fanya hivyo. Nimekuwa nikikufatilia kwa muda mrefu sasa. Uliniambia nitafute pesa kwanza, Tina utajiri ni majaaliwa ya mwenyezi Mungu nikubalie kwanza na tutafunga ndoa na kufanya sherehe kubwa uitakayo. Nikubalie Tina, nateseka mwenzio.

Tina akamuangalia sana Yuda na kushangaa kwanini bado ana moyo wa kutaka kuwa na yeye, Yuda nae akamsogelea vizuri Tina ili apewe jibu la uhakika.

YUDA: Tafadhari Tina nijibu nakupenda sana.

Tina akatikisa kichwa kama ishara ya kukubali.

Marium na Anna walipofika kwa Deborah wakaingia sebleni moja kwa moja bila hata ya kubisha hodi kwani walishapozoea.

Wakawakuta Tina na Yuda wamekaa mikao ya kihasara hasara, jambo la kwanza alilouliza Marium ni kuwa.

MARIUM: Nini kinaendelea kati yenu?

Yuda na Tina wakabaki kumtazama tu.

MARIUM: Mbona hamnijibu?

YUDA: Mama, kwasasa Tina ni mchumba wangu mtarajiwa.

MARIUM: Mmh!! Aliyenirogea wanangu kwakweli atakuwa amekufa.

Wakati wakiendelea kuzungumza, wale waliokuwa hospitali nao wakarejea, Tina akafurahi sana kumuona Tusa. Akainuka na kwenda kumkumbatia, kisha wote wakainuka na kusalimiana kisha kukaribishana.


Maiko aliingia jijini Mwanza akiwa na lengo moja tu la kumtafuta Mashaka kwani alijua kwa vyovyote vile atakuwa amekimbilia mkoa huo.

Nia yake kubwa ilikuwa ni kummaliza Mashaka popote pale atakapo muona atakuwa halali yake.


Tulo na Mwita nao wakazoeana kutokana na lile seke seke la kumpeleka Tusa hospitali. Wakajikuta wakiongea mambo mengi sana, wakati wenzao wamerudi nyumbani wao walielekea mjini kwa kupata vinywani na kuongea mambo mbalimbali.

MWITA: Unajua kinachonishangaza ni kwanini Patrick hataki kumuacha Tusa na kwanini Tusa hataki kuishi na Patrick.

TULO: Patrick ni gaidi bhana, hastahili kuishi na Tusa. Yule binti ni mpole sana halafu hajui kuzungumza, Patrick anatakiwa aishi na wale mabinti mcharuko ila Tusa hamfai. Na kama kumtesa dah!! Amemtesa sana, yule binti usimuone vile kateseka yule hadi kawa sugu.

MWITA: Sasa kwanini hataki kumuacha?

TULO: Pesa Mwita, Patrick amemgharamikia sana Tusa na ameshafanya mambo mengi mabaya kwaajili ya yule binti ndiomana hataki kumuacha ila sidhani kama anampenda tena sababu kama angempenda basi angemuacha apumue kwanza ila yeye kamng'ang'ania kama ruba.

MWITA: Na ilikuwaje hadi akamuoa?

TULO: Yote hayo ni mambo ya pesa, aliyesema pesa ni shetani hakukosea. Pesa ni mdudu mbaya sana kwani huharibu utu wa mtu kwa sekunde tu. Patrick anaumizwa na gharama zake juu ya Tusa, kule Arusha wanawake wengi wanampenda na kumuhitaji kwa sana ila yeye amekazana na Tusa tu. Labda kuna kitu cha ziada zaidi ya pesa kinachomvuta kwa Tusa.

MWITA: Mmh!! Khatari.

TULO: Ungemuona yule binti mwanzo kwakweli hata ungekuwa wewe ungemuhurumia kwa sasa. Alikuwa mzuri, mrembo na wa kuvutia. Ila sasa yupo kama wale misukule, dah anatia huruma. Ila Patrick mbabu na hashauriki sijui hata itakuwaje, labda atamuhurumia kwasasa baada ya kutaka kujiua.

MWITA: Basi itabidi Tusa akubali kutulia na Patrick.

TULO: Kwa mateso aliyopitia hawezi nakwambia, hata ingekuwa ni mimi ningekataa pia.

Walizungumza mengi, yale yote waliyoshindwa kuyazungumza mbele ya Patrick sasa waliyasema.


Nyumbani kwa Deborah waliona itakuwa vyema kwa Tusa kupata muda wa kupumzika kabla ya kuzungumza mambo yote yaliyojiri ila safari hii waliona kuwa itakuwa vyema kukaa karibu na Tusa ili kujua tatizo lake haswa ni nini hadi anakataa kiasi kile kuishi na Patrick. Ingawa alishawaeleza mambo mengi ila walihisi kuna kitu cha ziada ambacho Tusa anakificha.

DEBORAH: Jamani inatakiwa kila mmoja afunguke ili tujue jinsi ya kuokoa tatizo hili.

Wakakubaliana kuweka tena kikao cha familia ili wawekane sawa.


Mashaka nae aliendelea na mipango yake kama kawaida, wakati yupo mjini alionwa na Maiko.

Mashaka hakujua kama anafatiliwa.

Alirudi kwenye hoteli aliyofikia, alipoingia chumbani tu akasikia mtu akigonga mlango wa chumba kile.


Alipoingia chumbani tu akasikia mtu akigonga mlango wa chumba kile.

Mashaka akaenda kufungua huku akitarajia kuwa mgongaji atakuwa ni muhudumu wa hoteli ile.

Ila alivyofungua tu, Maiko alizama moja kwa moja ndani na Mashaka akamshangaa kuwa amejuaje kama yuko hapo.

MASHAKA: Umejuaje kama niko hapa?

MAIKO: Swali gani hilo? Nimekufatilia mwanzo mwisho.

MASHAKA: Najua umekuja kutimiza ahadi yako.

MAIKO: Ndio na leo sitazitaka hizo porojo zako.

MASHAKA: Maiko, hivi umejaribu kufikiria kuwa tumepoteza kazi ngapi, tumepoteza hela ngapi kwa huu upuuzi na ujinga? Hivi unajua kama ipo siku utakuwa masikini wa kutupwa sababu kwasasa unajua kutoa na si kuingiza. Fungua macho Maiko, ingawa ni mambo ya khatari ambayo tuliyafanya ila ndio mambo hayo yanayofanya tujidai na kutanua. Kila mmoja anafanya atakacho kwa pesa tuliyo nayo. Pata picha kama tungekuwa hatuna kitu.

MAIKO: Nina uhakika, kama tusingekuwa na kitu sasa ingesaidia sana kwani ingemaanisha kuwa hatufanyi kazi haramu, kazi ambayo imetuingizia pesa haramu na kazi hizo ndio zinazofanya tugombane sasa.

MASHAKA: Najua Maiko utanilaumu mimi kwa kazi zetu, na kama hivyo wataka kunimaliza. Ila jua kwamba wewe utamalizwa na Patrick kwani atakulaumu wewe siku zote. Umejipanga vipi kukabiliana na Patrick??

Maiko akaona kuwa Mashaka anamuwekea usiku tu, akajaribu kufikiria kuhusu swala la Patrick.

MASHAKA: Tena Patrick kama vile kwaajili yako, kumbuka kuwa wewe ndiye uliyemfundisha ujangili.

MAIKO: Ila mimi nilifundishwa na wewe.

MASHAKA: Atakuamini vipi, je kile kichwa ambacho Yuda alikikuta kwako ni mimi nimekufundisha? Hivi hujishangai Maiko kama wewe si binadamu wa kawaida?

MAIKO: Mimi ni mtu wa kawaida tu kama walivyo binadamu wengine.

MASHAKA: Unajua binadamu wa kawaida hawezi kulala hata usiku mmoja pembezoni mwa maiti? Wewe sasa, una vichwa vya marehemu wengi tu ndani kwako tena bila hofu nawe unalala kwenye nyumba hiyo hiyo. Mi huchukua viungo na kwenda kuviuza ila sio kwamba nitakaa navyo ndani kwangu kama wewe ufanyavyo Maiko. Sijui kama unaweza kusamehewa duniani na huko akhera, tena bila aibu unataka kujidai kuwa umebadilika kwa kuua tena! Unataka kuniua mimi, hayo si mabadiliko Maiko bali unajiongezea dhambi mbele za Mungu tu.

MAIKO: Kumbe hadi wewe unatambua uwepo wa Mungu? Ila bado sijaridhika, upo muda ambao kichwa chako hicho kitakuwa halali yangu.

MASHAKA: Na hakuna atakaye shangaa kwani kutunza vichwa vya marehemu ni kawaida yako.

Maiko alijifanya kupotezea ila maneno mengi aliyoambiwa na Mashaka yalimuingia sana. Akaamua kuondoka kwanza huku akijiuliza kuwa kwanini anasita kummaliza Mashaka wakati yeye akiamua kitu ameamua na huwa lazima akitekeleze kitu hicho.


Mwita na Tulo walilala kwa rafiki wa Mwita siku hiyo, mahali kule alipofikia Mwita kwa mara ya kwanza.

Mjeshi huyo aliyeitwa John ndiye aliyemuhabarisha Mwita juu ya kifo cha rafiki yake Hamisi.

MWITA: Inamaana Hamisi alikufa?

JOHN: Ndio, katika wale wajeshi sita waliouwawa kikatili na yeye alikuwa mmoja wao.

Mwita alisikitika sana kwani hakupata habari yoyote ukizingatia hakuwa na mawasiliano na watu wa Singida tangia siku aliyoondoka kwani aliacha na simu kabisa kwa kuhofia kutafutwatafutwa kabla hajampata baba yake.

Baada ya ile taarifa akaamua kuwasiliana na watu wa Singida, nao wakampa taarifa rasmi huku wakimwambia kuwa wamemtafuta sana kwa mahojiano ila hakupatikana kwani Hamisi alionekana mara ya Mwisho akienda nyumbani kwa Mwita na mwili wake ulitupwa mahali ambako si mbali sana na nyumbani kwa Mwita.

Alipokata simu akamgeukia John na kumuuliza.

MWITA: Inamaana Hamisi ameuwawa nyumbani kwangu?

JOHN: Itakuwa maana hata watu wanasema kuwa kwako ilisikika harufu ya damu ingawa damu hiyo haikuonekana.

Mwita akawa na maswali mengi sana kichwani mwake, akajikuta akimuhusisha Patrick kwenye yale matukio ila upande mwingine wa akili yake ukakataa kuwa si Patrick aliyefanya yale.


Maiko aliyawaza maneno ya Mashaka kwa kina na kujiuliza kama anastahili kutubu.

"Hivi nastahili kutubu kweli? Mungu atanisamehe kweli? Sijulikani Msikitini wala Kanisani, wapi nitaenda na kupokelewa mimi? Nawachukia Mashekhe na Wachungaji, nishawafanyia mengi mabaya. Sidhani kama nitasamehewa mimi binadamu ambaye sieleweki wala sina uelekeo. Nimewaumiza wanawake wengi sana, watoto wengi na sikuwa na huruma yoyote hadi nimewabaka na wanangu na kumuua baba yangu. Nitasamehewa kweli? Huyu Mashaka huyu nae anastahili kuuwawa tu, sio kila dhambi kunigeuzia mimi tu. Lazima auwawe ila je nikimmaliza itakuwa mwisho wa utajiri wetu? Ni kweli wanausalama watalijua hili swala la mauaji ambayo nimewahi kufanya? Wapi mimi, nimekuwa mtu mbaya sana"

Alikuwa akijilalamisha tu na kuamua jambo moja kwenda kuzungumza na Patrick alijua huyo lazima amlainishe na kujaribu kufanya kitu kizuri kwa wao na familia inayoonekana mbele yao.


Hali ya Tusa sasa haikuwa mbaya sana ila walipomuhoji bado aliendelea kuwa na msimamo wake uleule wa kukataa kuishi na Patrick, na Patrick nae alipohojiwa msimamo wake ukabaki uleule wa kuishi na Tusa.

Pamela alichanganywa kabisa na maamuzi ya Tusa kwani alijua wazi Tusa akiendelea na maamuzi yale basi umasikini unawanukilia yeye na mumewe kwani Adamu hakutaka kuona mwanae akiendelea kuteseka kisa pesa ambayo Patrick alimgharamia.


Kesho yake Mwita na Tulo waliondoka nyumbani kwa John, leo hii Mwita alivaa kijeshi.

Tulo alimuuliza Mwita kama wanauhusiano gani na ile familia ya kina Patrick, Mwita akamueleza kuwa baba yake ni Maiko kwakweli Tulo alishtuka sana.

TULO: Je, unajua kazi ambayo Maiko anaifanya?

MWITA: Sijui chochote, baba mwenyewe nimemfahamu ukubwani.

TULO: Wewe ni mwanausalama wa nchi hii Mwita, hata sijui itakuwaje ukigundua.

Mwita akajaribu kumdadisi Tulo ili amuelezee ila Tulo akapotezea kwa kumletea story zingine.

TULO: Unajua mimi nimecheza sana utotoni na Tina, halafu nimesoma nae tulikuwa kama dada na kaka ila kiukweli nampenda sana.

MWITA: Unampenda kimapenzi?

TULO: Ndio, tena sana.

MWITA: Je, umewahi kumwambia?

TULO: Hapana sijawahi ila hata yeye Tina inaonyesha kuwa ananipenda, nadhani napaswa kumwambia ukweli hisia zangu.

MWITA: Ndio mwambie ajue, chelewa chelewa utamkuta mwana si wako. Wasichana wengi ni wagumu kumuanza mtu kuwa wanampenda hubaki na yao moyoni, na wewe ukijigelesha anaweza fika mjanja na kukupiku. Changamka kijana.

Wakakubaliana kwenda kwa Deborah, huku Mwita akiwa na lengo la kuzungumza na Patrick ili amdadisi kuhusu vile vifo na Tulo nae akiwa na lengo la kuzungumza na Tina.

INAENDELEA......

Post a Comment

0 Comments