Muda huo Patrick nae alikuwa amefika nyumbani kwao, kusogelea mlango akawa anamsikia Tusa akisimulia.
Patrick roho ikamuuma sana kwani hakutaka mama yake ajue habari ile, akamuweka Tusa katika kundi la wanawake wapumbavu na wasio na akili, alibaki kusita pale mlangoni kwani hakujua sura yake itaangaliwa vipi atakapoingia ndani.
Akarudi nyuma na kutamani kuondoka hapo nyumbani kwao kwani vitendo alivyomfanyia Tusa wakati wapo Arusha hata yeye vilianza kumuumiza roho yake kwa sasa.
Akaanza kuondoka, wakati anapinda kona akakutana na Sele na Yuda ambao walikuwa wanakuja nyumbani kwao.
YUDA: Vipi Patrick?
PATRICK: Dah! Hakuna tatizo bhana, nyie nendeni tu.
YUDA: Ila mbona kama haupo sawa?
PATRICK: Aaah!! Ni Tusa bhana.
Sele kusikia vile hakutaka kuendelea kusikiliza ila alikimbia nakwenda moja kwa moja ndani kwani alihisi labda Tusa kapatwa na tatizo tena.
Patrick alizungumza kidogo pale na Yuda, halafu akaamua kuondoka.
Tusa aliendelea kuwaeleza namna ambavyo alitolewa mimba kinguvu na Patrick na jinsi ambavyo alikuwa akimfungia ndani hadi kubakwa na Maiko.
TUSA: Patrick alithubutu hata kuniingilia kinyume na maumbile bila ridhaa yangu.
DEBORAH: Mungu wangu, nini hiki!!! Yani Patrick ndio wa kufanya hayo mambo!! Dah.
Muda wote Deborah alionekana kusononeshwa tu na vitendo ambavyo aliambiwa kuwa Patrick amevitenda.
Tusa akaelezea pia alivyoteswa na wakina Maiko na kukombolewa na Patrick hadi kufika Mwanza.
Mara wakamuona Sele akiingia kwa kasi ya ajabu ndani.
MARIUM: Vipi na wewe?
SELE: Nilijua Tusa amepatwa na matatizo.
MARIUM: Kwanini?
SELE: Tumekutana na Patrick njiani anaondoka na akasema kuwa tatizo ni Tusa.
Deborah akashtuka sana na kujua kuwa kwa vyovyote vile lazima Patrick atakuwa amesikia mambo ambayo Tusa alikuwa akisimulia, ikabidi ainuke na kwenda nje ili akajaribu kumfatilia.
Wote mule ndani walibakia na mshangao kwani hawakuamini kama Patrick anaweza kufanya vitu alivyofanya kwa Tusa.
Ikabidi kikao kihairishwe na kupangwa tena kesho yake.
Pamela akamchukua mwanae Tusa na kwenda kuzungumza nae pembeni.
PAMELA: Pole sana mwanangu kwa yaliyokukuta.
TUSA: Asante mama, nimeshapoa.
PAMELA: Ila mwanangu tukiacha uovu wote huo ambao Patrick amekutendea ila inaonyesha anakupenda kwani alikukomboa.
TUSA: Hivi mama, kumbaka mtu ni upendo? Kumlazimisha atoe mimba ni upendo?
PAMELA: Sitayasemea hayo ila nadhani Patrick aliingiliwa na shetani wakati anayafanya hayo, Patrick anakufaa mwanangu usimchukie kiasi hicho. Yeye sio kama huyo Maiko wanayemsema.
TUSA: Mama, huyu Patrick hana cha kubadilika wala nini. Kama angebadilika basi asingenipulizia madawa wakati tuko hapa na kunibaka.
PAMELA: Inamaana hata wakati tuko hapa alikubaka?
TUSA: Ndio mama ila nilikaa kimya sikusema chochote.
Pamela alikuwa akitafakari mazuri na mabaya ya Patrick ili kuangalia wapi uzito umezidi.
Deborah akafata njia aliyopita Patrick bila ya mafanikio ya aina yoyote ile.
Deborah akaamua kurudi nyumbani kwake, alikaa chini na kumtafakari Patrick alivyokuwa wakati wa udogo wake.
"Alikuwa ni mtoto mchangamfu na mjanja, alikuwa mtundu sana ila ukimkataza anaelewa. Alipenda sana ibada, hakumchukia yeyote, alimpenda kila mtu. Alipokuwa na tatizo alinieleza, nilimpatia chochote alichotaka ilimradi afurahi. Kwanini Patrick umebadilika mwanangu!! Hivi hii ndio ahadi uliyoniahidi wakati mdogo kuwa utanisaidia!! Patrick, kwanini umebadilika baba?"
PAMELA: Usiwaze sana Deborah, kila mwanadamu na mapungufu yake na mara nyingine shetani hupitia kati.
DEBORAH: We acha tu Pamela.
PAMELA: Tusa ni mwanangu, na imeniuma sana kunielezea alichokuwa anafanyiwa na Patrick. Ila kwa upande mwingine Patrick ni mtu mwema, anahitaji kusamehewa tu ni shetani aliyempitia.
DEBORAH: Shetani mwenyewe si mwingine bali ni Maiko, huyu jamaa ndiye aliyemuharibu Patrick.
PAMELA: Ni kweli Deborah, Patrick si mtu mbaya.
Pamela aliendelea kumpa moyo Deborah.
Tulo aliyeachwa porini na Patrick, alipata msaada kutoka kwa wakata kuni kule porini. Walimuhurumia sana kwani alikuwa amevimba na kutokwa na damu sehemu nyingi sana.
Wale watu walimchukua na kumuhudumia ili aweze kupona na kurudi katika hali yake ya kawaida.
Maiko aliendelea kupambana na Mashaka hadi wakachoka wote wawili.
Maiko akamkaba Mashaka sasa, na Mashaka nae akawa anamzuia Maiko kumfanyia vile kwahiyo alikuwa amekazana kuitoa mikono ya Maiko. mashaka alikuwa akiongea kwa shida.
"Tafadhari Maiko naomba nikwambie kitu cha ukweli."
Maiko akaamua kumuachilia amsikilize, ila akachukua bastola yake na kumuelekezea Mashaka ili asikimbie.
MASHAKA: Nina mengi ya kuzungumza Maiko, unatakiwa uyajue mambo mengi sana. Ila je utajiri wote tuliousumbukia miaka yote mwisho wake ndio huu?
MAIKO: Huu utajiri si wa halali, na ubaya zaidi tumeua watu wengi sana wasiokuwa na hatia.
MASHAKA: Ni kweli, na je ukinimaliza mimi utakuwa umemaliza tatizo?
MAIKO: Sitaki maswali Mashaka, wee sema tu unachotaka kusema.
MASHAKA: Sawa mimi si baba yako Maiko ila pia ni mjomba wako. Kumbuka hilo kuwa mimi bado ni ndugu yako.
Maiko aliona Mashaka anataka kumpotezea muda tu.
Marium alipokuwa kwake akaamua kuongea vizuri na mwanae Sele.
MARIUM: Sele mwanangu, leo nimeamua kurudia tena Sele. Tusa hakufai.
SELE: Jamani mama, Mimi nampenda sana Tusa.
MARIUM: Hakufai mwanangu, Tusa amekuwa kopo tena kopo la jalalani hafai hata kidogo.
SELE: Mama, usiseme hivyo bhana.
MARIUM: Mimi ni mama yako Sele usije kusema kuwa hatukukwambia. Tusa ashaingiliwa na wanaume wengi sana, muachie huyo Patrick anayemng'ang'ania ila kwa wewe hakufai mwanangu.
SELE: Nampenda sana Tusa mama.
MARIUM: Sijui umerogwa wewe, hebu kaa chini nikusimulie kwanza aliyofanyiwa Tusa wakati yupo Arusha.
Marium akaanza kumueleza Sele yale mambo waliyosimuliwa na Tusa.
Patrick alikosa raha na kujiuliza kuwa kwanini Tusa ameamua kufanya vile, hakuelewa kwanini Tusa aliamua kuelezea mambo yao ya Arusha.
"Nitamuangaliaje mama mimi, mama atanionaje mwanae? Kuwa nimekuwa mtu mbaya!!"
Patrick alitafakari sana na kuamua kukodi chumba hotelini atacholala kwa siku hiyo huku akiendelea kutafakari jinsi ya kumueleza mama yake.
Akiwa hotelini amelala, mzimu wa mzee Ayubu ukamtokea tena.
Akatokewa na mzimu wa mzee Ayubu.
Patrick akaanza kuogopa tena ingawa alikuwa ndotoni.
"Usikimbie kwenu Patrick, rudi nyumbani ukakabiliane na tatizo. Kukimbia tatizo sio suruhisho la tatizo, unatakiwa ulikabili tatizo"
Halafu akapotea, Patrick aliogopa sana na kushtuka, akaamua kukaa sasa pale kitandani akijadili na akili yake.
"Kwanini huyu mzee anapenda kunitokea? Je, anataka nikaseme ukweli kuwa nahusika na kifo chake mmh!! Mama yangu je atanionaje??"
Patrick akajiuliza sana ila akaona itakuwa vyema kama kesho yake atarudi tena kwao.
Tangu siku Mwita alipoona wanafamilia wameamua kukaa kikao na kujadili maovu ya watu, akajua lazima na yeye atajadiliwa kwahiyo aliamua kuondoka pale kwa Deborah.
Mwita nae aliona ukoo wake haufai ukizingatia kila shutuma zilimuhusu baba yake mzazi, akaona sasa hali si shwari kabisa ukizingatia yeye ni mwanausalama na mambo aliyofanya babaye ni makubwa sana.
Alijikuta akienda kulala hotelini kwa muda ila kumbe alipanga hoteli moja na aliyopanga Patrick.
Deborah aliendelea kumuwaza mwanae Patrick, alijikuta akitokwa na machozi kwani alihisi labda Patrick ameondoka moja kwa moja na hatorudi tena kutokana na yale maneno, kwani alimjua mwanae ni mtu wa hasira sana haswa akihisi mama yake amemchukia.
Debora akawa anajisemea,
"Nakupenda mwanangu, rudi nyumbani"
Pamela aliyekuwa pembeni alimsikia na kumfata.
PAMELA: Atarudi tu Deborah, hata usiwe na shaka. Ukizingatia Patrick ni mtu mzima sasa.
DEBORAH: Mtoto ni mtoto Pamela, haijalishi ukubwa wake. Patrick amekuwa mwanangu kwa muda sasa, nimepata nae tabu na shida ila sikumtupa kwani nilimuona kama vile ni faraja yangu kwa kipindi kile kigumu cha maisha yangu.
PAMELA: Sawa Debo, ila atarudi tu. Unapataje mashaka kwa mtoto mkubwa kama Patrick jamani!!
DEBORAH: Pamela hujui uchungu wa kupoteza mtoto ndugu yangu, ukiujua uchungu huo utasema.
PAMELA: Inamaana hata uchungu wa kuzaa si uchungu?
DEBORAH: Kuzaa ni kuchungu sana ila unafarijika pale kuona uchungu wa kuzaa kwako umefutwa na mtoto uliyempakatia. Kupotelewa na mtoto inauma sana, kufiwa ndio kabisa asikwambie mtu. Hata nawashangaa wanawake wenzetu wanaotupa vitoto walivyovizaa wenyewe.
PAMELA: Ugumu wa maisha hufanya hiyo kitu, hakuna mwanamke anayependa kumtupa mtoto wake.
Pamela nae akawa anatoa machozi.
DEBORAH: Inamaana unawatetea watoa mimba na watupa watoto? Nadhani utakuwa umepitia humo kwenye ujana wako ndomana machozi yanakutoka. Kupenda usichana wakati ushakuwa mama ni kubaya sana, ukishakuwa mwanamke hunabudi kuwa mama.
PAMELA: Na kwa wale wasiozaa je!
DEBORAH: Sikia Pamela, haijalishi mtoto umemzaa au hujamzaa ila ukimlea kiukamilifu na kwa mapenzi mema mtoto yule atakupenda tena atakupenda kushinda hata mama yake mzazi. Mama mlezi naye ni mama, mwanamke yeyote anatakiwa kuwa mama kwa mtoto aliyembele yake. Kubagua watoto ndio kunakofanya tusiheshimiane wakubwa kwa watoto, ila ukijiweka kama mama mbele ya mtoto yeyote itakufanya uweze kumsaidia hata pale anapopatwa na tatizo wakati wowote hata kama mama yake mzazi hayupo.
PAMELA: Umenifundisha kitu Deborah, ningempenda Sele kama mwanangu na kumwelewa basi yote haya yasingetokea. Ila nilimdharau sana na kumchukia.
DEBORAH: Hunabudi kumuomba msamaha hata kama ni mtoto kwako kwani chuki na dharau si kitu kizuri mbele ya mwanadamu mwenzio.
Pamela akakubaliana na Deborah kuwa kesho yake atamuita Sele ili aweze kuzungumza nae na kumuomba msamaha.
Kesho yake wakati Patrick anatoka kwenye chumba chake, Mwita nae alikuwa anatoka.
Wakajikuta wapo wote kwenye ngazi wanashuka, wakaangaliana na kusalimiana.
PATRICK: Natumaini yale yaliyotokea kati yetu yameisha.
MWITA: Yote yameisha Patrick.
Kwa kuonyesha kuwa yameisha, ikabidi waende mahali kukaa na kupata supu pamoja kama kifungua kinywa.
MWITA: Unajua nini Patrick, hakuna kitu kinachoniuma kama kumtendea vile Tusa. Nilikaa mule ndani hata kumtazama Tusa mara mbili mbili sikuweza na kumbe Tusa ni dada yangu dah inaniuma sana.
PATRICK: Mara nyingi watu hufanya mambo bila kufikiri, kama baba yako nae Maiko, alikuja kwangu na kumbaka Tusa kwa lengo la kunikomesha mimi kumbe alikuwa akimtesa mwanae nadhani hata yeye hilo swala linamuumiza.
MWITA: Ni kweli, hata mimi nilifanya vile kwa lengo la kumpiku Sele kumbe namtesa dada yangu.
PATRICK: Unajua mimi mwanzoni kabisa wakati namfahamu Tusa kupitia mtandao wa facebook, nilikuwa naona jamaa yake anafaidi sana ukizingatia Tusa alikuwa haachi kumtaja Sele kila unapojaribu kutupia ndoano kwake ndomana nikatumia gharama kubwa sana kumpata Tusa. Ila badae nilitekwa na mapenzi, nilitaka Tusa anione mimi kama huyo Sele aliyekuwa akimtajataja ndomana nikafanya kila njia kumuweka Tusa karibu bila kujua kama zile njia zilimuathiri Tusa kiasi gani na bila kujua kama Sele aliyetajwatajwa ni ndugu yangu.
MWITA: Mmh!! Sasa ulivyogundua kuhusu Sele ulichukua hatua gani?
PATRICK: Sikia Frank, Tusa nilishafunga nae ndoa kwahiyo hata nilipogundua kuwa Sele ni ndugu yangu na kuwa mimi na yeye tumegombea mwanamke mmoja sikuwa na la kufanya kwakweli na kumuacha Tusa siwezi ukizingatia nishamuharibu sana.
MWITA: Sasa Sele yeye anaichukuliaje hiyo hali?
PATRICK: Muda mwingine anakubaliana nayo na muda mwingine anahitaji kurudiana na Tusa hata namshangaa utafikiri wanawake wameisha duniani! Kwakweli mtindo wa kumgombea mwanamke mmoja siupendi ila namgombea Tusa sababu nishamuharibu na kumuumiza sana.
MWITA: Mmh! Khatari, je Tusa anakupenda sasa?
PATRICK: Haijalishi ananipenda au hanipendi ila mimi ni mume wake tu.
MWITA: Ila usisahau kwamba Sele naye anamgombea Tusa sababu wanapendana.
PATRICK: Aaargh! Tuachane na habari hizo bhana, ngoja tuzungumze mengine ya maana.
Wakakubaliana kurudi nyumbani ili kuweza kukabiliana na kile ambacho kinatokea.
Mashaka alimuomba Maiko karatasi na peni ili aweze kuandika anachotaka kuandika.
Maiko akamkabidhi daftari kabisa.
MAIKO: Haya, andika humo hayo matapishi yako.
MASHAKA: Usijari Maiko, mimi leo naandika ila kesho wewe utasema.
MAIKO: Sina cha kusema mimi.
MASHAKA: Utayasema tu maovu yako yote uliyoyatenda, mimi leo nitaandika maovu yangu yote niliyoyatenda na kwanini nimeyatenda. Ila wewe utasimama na kuyasema maovu yako kwani mengi yapo wazi na ubaya ni kuwa karibia wote uliowatendea wanakujua. Nakuhurumia sana Maiko.
MAIKO: Jihurumie wewe na nafsi yako, tena usiendelee kujiongelesha nisije nikafyatua huo ubongo wako, endelea kuandika hapo.
Muda wote Maiko alikuwa ameshika bastola kwani alikuwa na uchungu sana na Mashaka haswa kwa kitendo cha yeye kutumwa kwenda kumuua baba yake mwenyewe.
Sele alimuaga mama yake kuwa ameitwa na Pamela kwaajili ya mazungumzo.
MARIUM: Mwanangu narudia tena kukwambia, swala la wewe kurudiana na Tusa lipoteze kabisa. Tusa si mwanamke wa kuoa tena.
SELE: Jamani mama!
MARIUM: Ndio hivyo. Tusa ni kopo mwanangu hafai kabisa. Sitaki kabisa umuoe huyo binti, sitaki umrudie hata kama Patrick akisema mrudiane. Tafuta mwanamke mwingine atakayekufaa lakini sio Tusa.
Sele akaondoka nyumbani kwao na kuelekea nyumbani kwa Deborah.
Tulo alipopata unafuu aliwashukuru sana wale watu waliomsaidia na kuomba kurudi mjini ili aweze kurudi kwao Arusha.
Alifika mjini salama na kuanza safari ya kwenda stendi kukata tiketi ya kurudi Arusha kwani aliona mji wa Mwanza haumfai tena.
Tusa na Tina walichukuzana siku hiyo ili kwenda magengeni kutafuta udongo ambao Tina alikuwa akiuhitaji kwa sana.
Wakiwa njiani wakakutana na Tulo aliyeonyesha akimtambua Tina.
TULE: Kheee Tina!!
Mara gafla Tina akapatwa na kizunguzungu na kuanguka.
Mara gafla Tina akapatwa na kizunguzungu na kuanguka.
Ikabidi Tulo na Tusa waanze kumpa huduma ya kwanza.
Baada ya kumpatia huduma ya kwanza Tina akazinduka ila kabla hawajafanya chochote akazimia tena.
Ikabidi waombe msaada wa kumuwaisha hospitali, walipofika hospitali ikabidi Tusa aamue kwenda nyumbani ili kutoa taarifa ya kuanguka na kuzidiwa kwa Tina.
Akaamua kumuacha Tulo pale hospitali akiendelea kutoa maelezo huku yeye akichukua uamuzi wa kuwahi nyumbani kutoa taarifa ingawa hakumuelewa Tulo vizuri.
Sele alikuwa amefika nyumbani kwa Deborah kwaajili ya wito ambao ameitiwa na Pamela.
Aliwakuta wote kasoro Tina na Tusa.
Baada ya salamu akaamua kumuulizia Tusa kwanza.
SELE: Kwani Tusa yuko wapi?
PAMELA: Tusa katoka kidogo na Tina, ila ngoja tuzungumze yetu hapa.
SELE: Ila mama, mmewaacha vipi watoke peke yao wakati wote ni wagonjwa wale?
PAMELA: Tusa kapona bhana.
Mara wakamuona Tusa akirudi mwenyewe, mama yake akamuuliza kwa mshtuko alipomuacha Tina, ikabidi awaeleze ilivyokuwa na Tina alipo, wakashangaa kusikia yale maelezo.
Wakaamua kwenda huko hospitali kuona anaendeleaje. Ikabidi waondoke nyumba nzima kasoro bi.Rehema ambaye waliona kuwa itakuwa ni vyema kumuacha nyumbani.
Walipofika pale hospitali ambapo Tusa alimuacha Tina na Tulo hawakuwakuta wote wawili.
Hofu ikawatawala sasa, Tusa ndio hakuelewa chochote.
Wakajaribu kuulizia ila hawakupa jibu la maana.
FAUSTA: Tusa, una uhakika kweli kuwa Tina umemuacha hospitali hii?
TUSA: Ndio, nilimuacha hapa na kijana mmoja hivi aliyeonyesha kumjua Tina vizuri.
PAMELA: wewe huyo kijana unamfahamu?
TUSA: Hapana mama simfahamu.
PAMELA: Mbona unaakili mbovu mwanangu? Si unajua kuwa hapa Mwanza kuna watekaji! Iweje unamuacha mwenzio na mtu usiyemfahamu. Kama kamteka je?
TUSA: Unanilaumu bure mama, mimi nilichanganyikiwa.
PAMELA: Kuchanganyikiwa gani huko, yani Tusa hauko makini kabisa wewe.
Fausta nae akahisi kuchanganyikiwa kabisa kwa kutotambulika mwanae alipo, lawama zote zikamuendea Tusa.
SELE: Mnamkandamiza Tusa bure tu wakati mnatambua kuwa na yeye alikuwa hoi siku chache tu zilizopita.
PAMELA: Hata kama ila ana wajibu wa kutupa maelezo ya kutosha juu ya alipo Tina.
Walikuwa wakibishana tu bila ya maelewano kwani hakuna aliyeelewa alipoenda huyo Tina.
PAMELA: Na huyu Tusa anatuletea kiwingu tu bora arudi nyumbani na sisi tuendelee kumtafuta huyo Tina.
DEBORAH: Sele, basi wewe ndio urudi na Tusa nyumbani ngoja sie tujaribu kuulizia hospitali zote za hapa.
Sele akaamua kuondoka na Tusa.
Adamu ndiye aliyebaki na wale wanawake watatu katika kumtafuta Tusa
Mashaka na Maiko waliendeleza yale majibizano yao huku Mashaka akiendelea kuandika ule ujumbe wake, alipomaliza akauweka pembeni na Maiko akaenda kuuchukua ikawa muda huo huo ambapo Mashaka akamgeuka Maiko na kumpokonya ile bastora kisha akamdhibiti yeye.
MASHAKA: Ila mimi sina nia ya kukumaliza kama wewe ambavyo unataka kufanya.
MAIKO: Nia yako nini wewe?
MASHAKA: Nia yangu ni kukudhibiti ili niweze kufanya yangu.
Alipomaliza kunena hayo Mashaka alitoka kinyumenyume na kuondoka.
Na safari yake ilikuwa ni kurudi tena Mwanza, nia yake ni kuonana na dada yake tena kabla ya kufanywa chochote na Maiko au Patrick.
Aliamua kufanya safari ya haraka kwa kutumia usafiri wa ndege, kwavile alikuwa na pesa bado kwahiyo haikuwa tatizo kwake katika swala la kusafiri na ndege.
Yuda na yeye aliondoka kwao kama alivyofanya Sele ila yeye alienda mjini kwa mambo yake tu.
Ndipo alipomuona Tina akiwa anakokotwa na kijana mwingine ila alipomuangalia vizuri akamtambua kuwa yule ni mfanyakazi wa Maiko na Mashaka kwahiyo aliamua kumfatilia nyumanyuma ili ajue wanapoelekea.
Tusa na Sele walirudi nyumbani, Deborah aliamua kuwa Tusa arudi na Sele kwaajili ya usalama wa Tusa kwani aliona akili ya Tusa kuwa kama akili ya mtu aliyechanganyikiwa.
Walipofika nyumbani ikabidi Sele amuhoji vizuri kwanza.
SELE: Tusa, una uhakika kuwa hospitali mliyompeleka Tina ndio ile?
TUSA: Mara ngapi niseme jamani? Nashangaa hamniamini, nishawaambia kuwa kweli ni hospitali ile.
SELE: Tusa, usifikirie vibaya bhana ni kwamba tunahitaji uhakika tu. Sina nia ya kukukandamiza wala nini.
Tusa akashangaa kuona bi.Rehema hatoki ndani kuwauliza ikabidi aende kumuangalia ila alimtazama kote bila ya mafanikio.
TUSA: Sele, simuoni bibi. Atakuwa ameenda wapi?
Sele nae akaingia ndani kumsaidia Tusa kumtafuta bi.Rehema ila hakuwepo.
SELE: Au ameenda dukani?
TUSA: Dukani kufanya nini? Huwa haendagi.
SELE: Mmh! Atakuwa wapi sasa?
TUSA: Labda kweli ameenda dukani, hebu tungoje kidogo kama atarudi.
Ikabidi wavute subira kidogo kuangalizia kama bi.Rehema atarudi.
Wakina Deborah ikabidi wagawane katika kumtafuta Tina, ikabidi wawili waende upande huu na wawili upande mwingine.
DEBORAH: Nadhani itakuwa vyema kama Adamu ukifatana na Fausta halafu mimi nikifatana na Pamela. Ila uwe makini sana safari hii.
Wakiwa wanaendelea kujadili, Fausta akamuona kijana ambaye alikuwa anamfahamu na kuanza kumuita.
FAUSTA: Tulo, Tulo.
Tulo akageuka na kutazama nani anamuita kwani safari yake ilikuwa ni kuingia ndani ya hospitali hiyo.
Tulo akamfata muitaji na kuwasalimia.
FAUSTA: Khee! Unafanya nini huku?
TULO: Tena bora nimekuona mama, nilipokuwa njiani nilikutana na Tina na mwenzie mmoja hivi ila Tina akaanguka...
Fausta hakungoja amalize, aliamua kumuuliza haraka.
FAUSTA: Yuko wapi huyo Tina?
TULO: Yupo hospitali ya chini hapo.
Ikabidi waanze safari ya kwenda nae huko hospitali.
DEBORAH: Sasa mbona Tusa alituonyesha hospitali ile?
TULO: Ni kweli tulifikia pale na Tusa akaja kuwaambia ila huduma pale ni mbovu, kuna mtu akatushauri twende pale chini kwahiyo nimempeleka Tina pale na kashafanyiwa vipimo ndio nikaja huku kumuangalia Tusa kama amerudi ili nimpe taarifa.
PAMELA: Hakuna tatizo ili mradi tumewapata.
Wakaenda hadi kufika hospitali.
Patrick na Mwita wakaongea mengi na kukubaliana kurudi nyumbani.
MWITA: Kama ulivyosema Patrick, kukimbia sio muafaka bora kurudi tu na kukabiliana na tatizo.
PATRICK: Ndio hivyo, bora kuwa nyumbani kwanza mengine yataeleweka tukifika.
Wakachukua usafiri na kwenda nyumbani.
Anna nae aliamua kwenda nyumbani kwa Marium ili kuzungumza nae kuhusu mambo yanayojiri.
ANNA: Hivi unaelewa kinachotokea kweli dada yangu?
MARIUM: Hata sielewi yani sielewi kabisa na huyo mwanangu Sele ndio ananichanganya zaidi.
ANNA: Kwani amefanyaje?
MARIUM: Nahisi amerogwa maana kule sio kupenda jamani, atakuwa amerogwa tu.
ANNA: Acha imani mbaya dada, amroge nani bhana?
MARIUM: Amerogwa na ule ukoo, kwanza haueleweki halafu yeye amekazana kung'ang'ania itabidi nimtafute mganga wa jadi nikaulizie kwanini mwanangu yuko vile.
ANNA: Utajisumbua tu dadangu, mapenzi hayaingiliwi na wala hayashauriki.
Ila Marium hakutaka kabisa kukubaliana na dhana kuwa yale ni mapenzi tu, alihisi lazima kutakuwa na kitu cha ziada.
Tusa akawa anajilalamisha kwa Sele kuwa lazima lawama zote atapewa yeye tu.
TUSA: Yani na huyu bibi asiporudi, basi mimi tu ndio nitaonekana mbaya siku zote utadhani mimi ndio mpangaji wa haya.
SELE: Usijari Tusa, yote haya yatapita na wote watarudi nyumbani.
TUSA: Ila Sele unajua kuwa mimi sistahili tena kuwa na wewe? Ila pia sitaki kuwa tena na Patrick.
SELE: Achana na hizo habari kwanza Tusa. Mimi bado nakupenda na nitakupenda siku zote za maisha yangu ila kwasasa sinabudi kukubaliana na ukweli kuwa wewe ni mke wa ndugu yangu.
TUSA: Roho inaniuma sana, najiona mkosaji siku zote sijui kwanini mimi. Ila kwa yote bado wewe unaonyesha kunipenda na kunijari.
Tusa akaenda na kumkumbatia Sele, muda huo Patrick na Mwita nao wanaingia ndani.
Tusa akaenda na kumkumbatia Sele, muda huo Patrick na Mwita nao wanaingia ndani.
Patrick aliwatazama kwa jicho kali sana na wote wawili wakashtuka.
PATRICK: Mnashtuka nini? Endeleeni.
Sele na Tusa wakabaki kutazamana tu.
PATRICK: Hivi Sele, kwanini hupendi kunielewa? Nikikufanya chochote nitakuwa nimekuonea? Je upo tayari kufa kwa mapenzi?
Sele akabaki kimya huku akimsikilizia Patrick ambaye teyari alishakuwa na hasira.
Patrick akamsogelea Sele na kumpiga ngumi moja ambayo ilimpeleka hadi chini, Tusa akamfata Sele pale chini na kumuinua.
SELE: Halafu wewe jamaa sio kabisa yani huulizi wala nini unafikia kupiga tu sio vizuri bhana.
PATRICK: Sio vizurh eeh!! Haya Tusa muachie huyo mtu wako.
Tusa akabaki amemshika mkono Sele tu, sasa Patrick akaongea kwa ukali.
PATRICK: Nimesema muachie.
Tusa akatetemeka na kwenda pembeni.
Patrick akataka kumpiga tena Sele, Mwita akamsihi asifanye hivyo.
SELE: Mwache anipige bhana si kashazoea kutumia mabavu bila hata ya kujua nini tatizo.
PATRICK: Unajua Sele nitakuumiza wewe, sipendi tugombane ila wewe ndio unahitaji tugombane. Kuanzia leo, sitaki kukuona karibu na Tusa, hiyo ni amri na wala sio ombi.
Halafu Patrick akaenda chumbani kwake na kumuacha Mwita, Sele na Tusa pale sebleni.
Tina alipokuwa pale hospitali alipopelekwa na Tulo, baada ya Tulo kuondoka Tina akafatwa na Yuda.
YUDA: Tuondoke mahali hapa, hapakufai. Yule mkaka aliyekuleta ni mfanyakazi wa wakina Maiko.
TINA: Hapana Yuda, yule Tulo ni mtu mzuri tu na amekwenda kuwaita ndugu zangu.
YUDA: Tina, mi namjua yule hafai kabisa. Ni mtu mbaya, ni mfanyakazi wa wakina Maiko. Tuondoke hapa.
TINA: Hapana Yuda. Yule si mtu mbaya.
Yuda hakuelewa kuwa Tina anamjulia wapi Tulo na kwanini anamkatalia kile ambacho yeye anamwambia kuwa anamjua huyo Tulo.
YUDA: Ila basi kwa usalama wako tumuombe nesi akuweke sehemu nyingine ya mapumziko kwa muda, halafu mimi nitakuwa hapa kuangalia kama akija na ndugu zako niwalete.
TINA: Wasi wasi wako tu Yuda, ila ngoja tufanye usemacho.
Wakamuomba nesi naye akambadilisha chumba cha mapumziko.
Tulo alipofika pale alipomuacha Tina hawakumkuta na wote kushangaa.
ADAMU: Michezo gani ambayo mnatufanyia jamani!!
TULO: Jamani nilimuacha humu kweli, ngoja tuwaulize manesi.
Tulo akaenda kuuliza manesi na huku akafika Yuda na kuwaambia alipo Tina, ilibidi Fausta aulize kuwa tatizo ni nini.
YUDA: Sio mtu mzuri yule.
Wote wakabaki wanatazamana.
Yuda akaanza kuwaongoza alipo Tina na wao kumfuata ila Tulo nae alipowaona akaamua kuwafuata.
Bi.Rehema ambaye alikuwa mikononi kwa Mashaka sasa akakumbuka kuwa mara ya mwisho alikuwa nje.
MASHAKA: Sina nia mbaya dada, ila shida yangu ni kukiri kila jambo ambalo nilitenda kabla.
REHEMA: Kama nia yako ni nzuri, mbona ukaniteka sasa?
MASHAKA: Sikutaka wanione kwanza, najua wapo wenye hasira kali sana na mimi ingawa hawajawahi kuniona nikitenda huo uovu.
REHEMA: Hebu niweke wazi nijue, mwanangu tangia ameondoka pale nilipofikia hajaja tena je uko nae?
MASHAKA: Yeye yupo Arusha, mimi nataka nikiri mbele yako dada. Wewe ni ndugu yangu pekee uliyebaki, wote wameteketea sababu yangu.
REHEMA: Mmh!! Nitaweza kukusikiliza mwenyewe kweli mambo makubwa kama hayo ya kuteketeza ndugu wote? Naomba twende tukazungumze na hawa wachache waliobaki, kila mwanadamu ana haki ya kusamehewa najua hata wewe utasamehewa.
MASHAKA: Sidhani kama itakuwa rahisi hivyo.
REHEMA: Usijari mdogo wangu, kwani mimi umenifanyia mangapi mabaya na makubwa? Mbona nimekusamehe sasa, usiwe na shaka wote watakusamehe.
Bi.Rehema alikuwa akimvuta Mashaka kwa maneno ili aweze kuwa karibu nao ila kiukweli bado alikuwa na hasira kali sana dhidi ya Mashaka.
Wakaenda na kumuona Tina aliyekuwa katika mapumziko, wakati wanazungumza nae mara Tina akaanza kulalamika tumbo linamuuma, kuja kuinuka akawa amelowa damu.
Ndipo manesi wakaitwa na kuanza kumshughulikia huku ndugu zake wakiwa nje.
Badae wakaja kuambiwa kuwa mimba ya Tina imetoka, walimuhurumia Tina ila ile ikawa ni habari njema kwani aibu ambayo ingepatikana kwa mtoto ingekuwa ni kubwa sana.
DEBORAH: Kweli Mungu mkubwa, bora tu hiyo mimba imetoka.
FAUSTA: Ndio afadhari, nadhani sasa mwanangu ataishi kwa amani.
Wakatulia kungoja muda ambao Tina ataruhusiwa ili warudi nae nyumbani.
Patrick alitoka tena sebleni na kuhitaji kuzungumza na Tusa hivyo Sele na Mwita wakaamua kutoka nje kwani Tusa aligoma kwenda kuzungumza na Patrick chumbani kwake.
PATRICK: Hivi wewe Tusa unataka upendwe vipi? Unajua mambo mangapi nimefanya kwaajili yako? Hivi kweli mema yangu yote huyakumbuki? Yani wewe unakumbuka mabaya tu!
TUSA: Sio hivyo Patrick.
PATRICK: Hivi kweli isingekuwa hivyo, ungethubutu kukaa na umati wote ule humu ndani huku ukizungumza mabaya yangu? Ukafurahi sana kuzungumza maneno yale ulitaka wanione vipi?
Tusa alikuwa kimya tu kwani alikosa cha kujibu.
PATRICK: Eti alikuwa ananilazimisha mapenzi, sijui aliniingilia kinyume. Sasa hayo yanawahusu nini? Hata kama nilikulazimisha mapenzi wewe ni mke wangu na nina haki ya kupata penzi toka kwako.
TUSA: Una haki ndio ila si kwa kunilazimisha.
PATRICK: Hivi wewe Tusa lini umekubali kwa hiyari yako kunipa penzi? Lini? Ningekuwa nangoja ukubali haja zangu ningemalizia wapi wakati wewe upo! Halafu swala la kinyume unajua kabisa chanzo kilikuwa ni nini, hivi ni mwanaume gani atakayeweza kuishi na mkewe bila ya kufanya chochote ndani? Wewe ungekuwa mke au picha tu?
TUSA: Na kunitoa mimba kinguvu je?
PATRICK: Tumia akili Tusa, uliondoka na mimba yangu ukaenda na kuitoa halafu unakuja kwangu na mimba ya mwanaume mwingine ukitegemea mimi nilee! Mi sio mpumbavu kiasi hicho, ungekuwa hujawahi kutoa kweli hilo lingekuwa tatizo langu ila ulishatoa mimba kabla ulitegemea nini?
TUSA: Na kunipiga je?
PATRICK: Mwanamke yeyote jeuri dawa yake ni kipigo tu, Tusa wewe ni jeuri na kiburi. Ulitaka nikulee kama yai kuwa utavunjika? Kwangu ukileta ujeuri utasubiri dawa yako ya kipigo.
TUSA: Na kunifungia ndani je?
PATRICK: Na ule urembo wako wa kipindi kile ningekuachia vipi utembee nje? Ulitaka wajanja wa Arusha waniibie eeh!! Kwasasa nikienda nawe siwezi kukufungia ndani tena kwanza umeshachoka na huna urembo tena na mvuto wako wa mwanzoni wote umepotea. Tena ushukuru Mungu kuwa mimi bado nakujali mwanamke uliyechoka kama wewe.
Tusa alijisikia vibaya sana na machozi yakawa yanamtiririka kuona kuwa Patrick anaona kila alichomfanyia mwanzoni ni sawa.
PATRICK: Tena ngoja nikwambie, hata huyo Sele anayekufata hapa usifikiri ni mapenzi bali anakufata kwa kukuhurumia tu.
TUSA: Kwani mimi kosa langu ni nini jamani?
PATRICK: Kosa lako ni tamaa, tamaa ya mali, magari na pesa na tamaa waliyonayo wazazi wako haswaa mama yako.
Tusa akawa analia huku akikumbuka mambo ya nyuma, alimkumbuka Sele ambapo alipokuwa analia alikuwa akimbembeleza ila Patrick hakuwa hivyo na wala hakufanya hivyo.
TUSA: Kweli Patrick wewe una roho mbaya, hivi ni mwanaume gani wewe usiyejua hata kubembeleza jamani? Hata siku moja hujawahi kunifuta machozi halafu unadai unanipenda mmh!!
PATRICK: Wewe Tusa huwa unalia ujinga wako, kwahiyo mimi huwa nakuacha ulie hadi pale utakapotosheka utanyamaza.
TUSA: Hadi mamako humfanyia hivyo?
PATRICK: Mama haliagi ujinga wewe. Akilia basi ni mambo ya maana sio kama wewe unayelia ujinga ujinga.
Tusa akazidi kujiona mpumbavu.
Patrick akainuka na kutoka nje huku Tusa akiwa analia pale ndani.
Walipokuwa nje wale walioenda hospitali nao walikuwa wanarudi.
Patrick alishangaa kumuona Tulo pamoja nao.
INAENDELEA

0 Comments