Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mume gaidi sehemu ya nane (08)

 


Yuda aliingia kwenye himaya ya wakina Maiko, alimkuta Mashaka na kuzungumza nae mawili matatu, halafu akamuulizia Maiko alipo.

Mashaka akamuelekeza Yuda ambaye alienda moja kwa moja karibia na kichumba alichoelekezwa.

Akawaona vijana wawili wakiwa nje, alipokaribia alisikia sauti ya mwanamke ikilia toka kwenye chumba alichoambiwa kuwa Maiko yupo ndani.

Alipoisiliza kwa makini sauti hiyo akajikuta akipatwa na jazba kubwa sana na kuanza kwenda kwa kasi kwenye kile chumba.


Alipoisikiliza kwa makini sauti hiyo, akajikuta akipatwa na jazba kubwa sana na kuanza kwenda kwa kasi kwenye kile chumba. Simu yake ya mikononi ikawa inaita ndani ya mfuko wa suruali, akaipokea na kuirudisha tena mfukoni kwani kadri alivyozidi kusogea ndivyo ile sauti ilivyozidi kupasua mawazo yake, akapatwa na hasira zaidi.

Alipofika mlangoni akataka kuingia wale vijana wakamzuia, akawasukuma pembeni na kuwafanya waanguke kwani alitumia nguvu nyingi kufanya hivyo, halafu akasukuma mlango kwa nguvu, akamkuta Maiko juu ya kifua cha Tina. Kwa gadhabu aliyokuwa nayo Yuda, akainama na kumnyanyua Maiko aliyekuwa kwenye ulimwengu mwingine uliyomfanya asijari zile kelele zilizopigwa na Tina.

Yuda alimnyanyua Maiko juu juu, na kumpiga ngumi moja ya haja iliyomfanya aanguke chini, halafu Yuda akainama chini na kumnyanyua yule binti.

Alipomtazama vizuri akashtuka na kumwambia "Tina!!"

Tina alikuwa analia tu.

Kabla Yuda hajafanya kitu kingine, wale vijana wawili aliowatupia pembeni nao wakaja mule ndani na kumkamata Yuda kwa nyuma.

Yuda alikukuruka na kuanza kupambana na wale vijana, wakaja na wengine wawili na kuweza kumdhibiti Yuda.

Tina nae akaona ule ndo upenyo wake kutoroka, wakati anakimbia akadakwa na Mashaka.

MASHAKA: Huna pa kwenda binti, hapa ndio umefika.

Tina akahisi kizunguzungu na kuanguka.


Pamela alienda kuwapokea wakina Adamu na kuweza kwenda nao kwa Deborah.

Adamu alifurahi sana kumuona mkewe, ila Pamela alishangaa kumuona dada yake na mkwewe nao wakiwa mahali hapo, akawasalimia na kuwakumbatia.

REHEMA: Usishangae Pamela, hata sisi tuna uchungu na wewe.

PAMELA: Yani mmenifanyia surprise kwakweli, sikutarajia kabisa.

FAUSTA: Tusa je yuko wapi?

PAMELA: Nimemuacha tulipofikia, nimeamua kumfanyia surpise na yeye hata hajui kama baba yake anakuja leo, mmh atafurahije.

REHEMA: Atafurahi na kuniona bibi yake ambaye hajawahi kuniona?

PAMELA: Atafurahi sana mama, unajua Tusa hakujui kabisa na kila siku anatamani kumjua bibi yake, nadhani leo itakuwa ni siku ya furaha kwake.

FAUSTA: Kama ulivyofurahi wewe kumuona mumeo.

PAMELA: Aaaah dada, mi nimewafurahia wote jamani.

Wote wakawa wanacheka na kufurahi, huku safari ikiendelea bila ya Pamela kuwaambia kuwa wanaenda kwa Deborah.


Deborah hakutoka ndani, alikuwa amejifungia tu hofu ikawatanda Sele na Tusa.

SELE: Tutafanyaje sasa?

TUSA: Ngoja nikamuangalie tena.

Tusa akaenda tena mlangoni kwa Deborah ila Deborah hakufungua mlango, akaenda dirishani kumchungulia ila hakuweza kumuona kumbe Deborah alikuwa amelala chini pembezoni mwa kitanda akilia kwa uchungu.

Tusa akarudi tena alipo Sele.

TUSA: Hali ni mbaya, hata haonekani humo chumbani.

SELE: Tusa, tuondoke hapa.

TUSA: Tuondoke! Twende wapi? Na hapa tutamuacha na nani?

SELE: Hali ni mbaya hapa Tusa, hivi unamjua Patrick vizuri? Akirudi hapa na kumkuta mama yake yupo hivyo eti sababu ni sisi, hali itakuwa mbaya ukizingatia hata hatujui alipo huyo Patrick.

TUSA: Sasa tutamuacha na nani huyo mama humo ndani? Maana hata mama yangu nae hayupo, ametoka.

SELE: Sikia Tusa, twende kwanza nyumbani kwetu nikamshtue mama yangu aje hapa au kwa mamdogo Anna nadhani kidogo atawaelewa hao, halafu na sie tutokomee huko huko.

TUSA: Na mama yangu je?

SELE: Atatukutia Dar, nataka nikakukabidhi kwa baba yako Tusa. Utakaa utumwani hivi hadi lini? Unatakiwa kuwa huru Tusa.

TUSA: Sawa, au hata atanikuta Morogoro kwa babu. Najua kule Patrick hawezi kufika.

Tusa na Sele wakaondoka mahali hapo.


Patrick ndiye aliyempigia simu Yuda muda ule wakati Yuda anaenda kwenye kile chumba, kwahiyo alisikia baadhi ya maneno na purukushani, akahisi kuwa lazima Yuda atakuwa ameenda kufanya fujo tu.

Kwavile Yuda alishamtajia mahali penyewe ikabidi na yeye ajiandae kwenda.

Akabeba silaha zake vizuri na kujiandaa kwenda eneo la tukio.

"labda kuna jambo limetokea kule, itabidi niwe makini sana. Safari hii nikiwapata ni kuwafyeka tu wale sio watu kabisa"

Patrick akaondoka kwa ghadhabu huku akiwa amejiandaa vya kutosha.


Pamela na wageni wake wakafika salama nyumbani kwa Deborah ila palikuwa kimya sana kama vile hakuna watu.

Pamela akawakaribisha ndani, hata wao walishangazwa na ukimya ule.

Pamela alijaribu kumuita Tusa ila hakuitikiwa, akaamua kwenda chumbani kwa Deborah ambako alikuta mlango umefungwa, akabaki akishangaa pale mlangoni.

Wakati Pamela akishangb pale kwenye chumba cha Deborah, huku sebleni aliingia Anna akiwa na wasiwasi mwingi, hakuweza hata kuwasalimia wale wageni aliowakuta, alichofanya ni kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha Deborah ambapo alimkuta Pamela mlangoni.

ANNA: Kuna nini hapa? Kuna nini?

PAMELA: Hata sielewi.

ANNA: Huelewi kivipi?

PAMELA: Na mimi ndio kwanza nimekuja muda huu kwahiyo hata sielewi kitu.

Ana akaanza kugonga huku akiita "Deborah, Deborah"

Ila ikawa kimya, hofu zaidi ikamtawala Anna. Nae akazunguka dirishani kuchungulia ila hakuona chochote.

Ndipo Pamela alipoenda pale sebleni na kuwaeleza wote ukweli kuwa pale ni kwa Deborah, na hadi muda huo hawajui kilichompata na huku Anna akidai kuwa Deborah yupo chumbani.

Adamu na wote wakashangaa sana kusikia hivyo kwani hakutarajia kama hapo pangekuwa kwa Deborah.

Ikabidi Adamu atumie uanaume wake kwenda kukorokochoa ule mlango na kujaribu kuvunja kitasa.

Walifanya hilo zoezi kwa muda, hata wakina Tusa wakasahaulika kabisa kama nao hawapo.

Walipofanikiwa kuufungua, wakamkuta Deborah akiwa kalala chini, alikuwa amezimia.


Mashaka alipompatia Tina huduma ya kumwagia maji, Tina akazinduka.

MASHAKA: Usijaribu tena kutoroka hapa binti, utakufa unajiona wewe.

Tina akatokwa na machozi baada ya kukumbuka kilichomtokea kabla.

Akabahatika kuinuka huku akiwa ameshikiliwa na Mashaka, gafla Tina akapatwa na nguvu za ajabu na kuinua mguu halafu akampiga teke sehemu za siri Mashaka, kitu hicho kilimfanya Mashaka amuachie Tina na kuanza kuugulia lile Teke.

Tina akatumia muda huo kujaribu tena kutoroka, akakimbia sana na kuona Mashaka akimkimbiza, akafika mahali na kujificha.

Alipokuwa amejificha, mara gafla akatokea mtu nyuma yake na kumziba Tina mdomo.


Alipokuwa amejificha, mara gafla akatokea mtu nyuma yake na kumziba Tina mdomo.

Tina aliogopa na kutetemeka hadi mkojo ukamtoka safari hii kwani alijua kuwa yupo mikononi mwa adui na lazima atauwawa tu, kwahiyo Tina alikuwa akimwaga machozi huku akiombea muujiza utokee.

Mara Mashaka akafika eneo lile na kuanza kuangalia uelekeo wa Tina, yule mtu aliyemziba Tina mdomo akamuachia na kumrukia Mashaka kwa nyuma kisha akamkaba, Mashaka akakukuruka na kufanikiwa kumuangalia mtu huyo na kugundua kuwa ni Patrick, kabla Mashaka hajafanya chochote alishtukia Patrick akiruka hewani na kumpiga mateke mawili ya juu kwa juu, mateke hayo yalimfanya Mashaka aanguke chini, Patrick akamuinua pale chini na kumpiga teke moja matata lililomfanya Mashaka aanguke mbele zaidi kama mzigo, Mashaka akiwa hoi pale chini akamuona Patrick akimfata, akaamua kuinuka na kukimbia.

Patrick akaacha kumfatilia Mashaka na kurudi kwa Tina aliyekuwa anakimbia huku anachechemea, alipomfikia Tina akamnyanyua na kumuweka begani kisha akaifata bodaboda yake na kumpakia hadi barabarani ambako alisimamisha gari ya kukodi na kumpakiza Tina humo kisha akampa dereva maelekezo ya mahali pa kumpeleka Tina.

PATRICK: Ukifika waambie umeelekezwa na Patrick.

Tina akaitikia kwa kichwa huku akizidi kulia, na dereva akaondoka gari halafu Patrick akarudi eneo la tukio.

Kufika pale akawakuta vijana wa Mashaka wamejipanga tayari kwaajili ya kupambana nae, Patrick aliyekuwa na hasira, aliwafata na kuwavuruga vuruga, aliwapiga bila kujali sehemu.

Mashaka na Maiko kuona vile wakatoka kwenye chumba walichokuwemo na kukimbilia gari yao, wakapanda na kuondoka.

Patrick nae kuona vile hakutaka kupoteza muda na wale vijana, akaenda kuchukua bodaboda yake na kupanda ili awafate wakina Maiko.

Kabla ya kuondoka mara akasikia sauti nyuma yake,

"Patrick, nisaidie"

Alipogeuka nyuma, alimuona Yuda aliyekuwa anajikongoja huku anavuja damu, ikabidi Patrick aende kumchukua na kumpakia kwenye pikipiki yake na kuanza safari ya kwenda hospitali.


Deborah alipozinduka alikuwa anashangaa tu kwani hakujua chochote kilichoendelea, ikabidi wengine wapungue chumbani na kurudi sebleni ili Deborah apate muda wa kupumzisha mawazo.

DEBORAH: Patrick wangu yuko wapi?

ANNA: Hajarudi bado.

DEBORAH: Sele na Tusa je?

ANNA: Nao hawapo.

Debora akatingisha kichwa kama ishara ya kukataa au kusikitika.

ANNA: Tukuletee nini?

DEBORAH: Maji tu yatatosha.

Pamela akaenda jikoni na kumletea maji ambayo aliyanywa kidogo na kuyaacha.

Baada ya maongezi mawili matatu, Deborah alionekana kurudi katika hali ya kawaida na kuamua kwenda sebleni kukaribisha wageni.

DEBORAH: Karibuni sana, na pia naomba radhi kwa yote.

FAUSTA: Usijari Deborah, tunaelewa.

DEBORAH: Kumbe unanikumbuka?

FAUSTA: Ndio nakukumbuka, siwezi kukusahau Deborah.

DEBORAH: (Akacheka sana) sisahauliki kwasababu ya lile tukio nililofanya nini.

Wakamshangaa Deborah kuona anacheka kwa tukio la kusikitisha, hadi wakahisi kuwa huenda akili yake haipo sawa.


Mashaka na Maiko wakiwa wamechoka kwa tukio ambalo limewatukia siku hiyo.

Maiko ndio aliyemchoma kisu cha ubavu Yuda baada ya kugundua kuwa Yuda ni mshirika wa Patrick.

MASHAKA: Hapa Mwanza kishanuka, bora turudi Arusha tukaongezee jeshi.

MAIKO: Umeona mziki wa Patrick eeh!! Yule dogo hafai.

MASHAKA: Dah! Hafai kweli yule, anapiga kama anatwanga mmh!!

MAIKO: Si ulisema hakubabaishi wewe?

MASHAKA: Aaah wewe! Yule Patrick si mtu bhana, ana nguvu za ajabu. Ameharibu haribu vijana wetu wote wanne. Turudi tu Arusha.

MAIKO: Kabla ya kurudi Arusha, nina wazo kidogo.

MASHAKA: Wazo gani? Je litaweza kutusaidia?

MAIKO: Sikia, tumtafute kwanza Deborah yule mama wa Patrick hapo ndio itakuwa rahisi kumpata Patrick.

MASHAKA: Sasa huyo Deborah tutampataje?

MAIKO: Hiyo niachie mimi, ila itabidi tufanye kimya kimya na kwa umakini sana.

Mashaka na Maiko wakaanza kupanga mipango ya kumpata Debora sasa.


Tusa na Sele waliishia Singida ambapo pesa ya Sele iliishia hapo kwani nyingine aliibiwa njiani, ikabidi waende kufikia kwa rafiki wa Sele ambaye aliishi hapo Singida, huyu aliitwa Mwita.

Mwita aliwapokea na kuwakaribisha vizuri sana.

TUSA: Kwakweli haya ndio mambo nisiyoyapenda, yani safari ya Morogoro tu hapo hadi tuchukue mwezi!

SELE: Usijari Tusa, huyu Mwita ni rafiki yangu sana. Atanikopesha tu hiyo pesa na tutafika huko Morogoro.

TUSA: Aaaargh!!

SELE: Usichukie bhana Tusa, si unajua kuwa nimeibiwa pesa nyingine! Tutafika tu.

TUSA: Ila tusikae hapa sana.

SELE: Hakuna tatizo mama, usiwe na shaka.

MWITA: Karibuni sana na muwe huru.

Mwita nae alionekana kuvutiwa sana na Tusa.


Patrick akampeleka Yuda hospitali, ambako daktari alikataa kumuhudumia.

DAKTARI: Siwezi kumuhudumia bila PF3.

PATRICK: Tafadhari daktari, nakuomba utuhurumie.

Daktari akakataa kabisa, Patrick akajaribu kumuhonga napo akakataa. Ikabidi Patrick atumie nguvu, akamtolea silaha daktari.

PATRICK: Utamuhudumia au umuhudumii?

Daktari kuona silaha akaanza kutetemeka na kuamua kumuhudumia Yuda.

PATRICK: Na ole wako umlipue lipue, utaipata hii.

Daktari akamziba Yuda jereha, ila hakuumia sana sababu kisu hakikuingia chote, alipommaliza Patrick akatoka na mgonjwa wake na kuondoka bila ya kulipia gharama za matibabu.


Tina alifika mahali ambapo alielekezwa, akagonga mlango na akatoka mama wa makamo kumfungulia. Yule mama alimuangalia kwa makini sana Tina, kisha akamuuliza

"wee Tina, nini kimekupata? Mbona umekuwa hivyo?"

Tina akabaki anamshangaa huyu mmama kwani yeye hakumjua.


Tina akabaki anamshangaa huyu mmama kwani yeye hakumjua vizuri.

Yule mama akazidi kumkaribisha Tina ndani.

"karibu sana, na hata sijui umepatwa na nini jamani"

Tina alizidi kushangaa na kufanya huyu mama amuulize tena.

"mbona unashangaa! Kwani wewe sio Tina mtoto wa Fausta?"

Tina akaitikia kuwa ni yeye.

Huyu mama alikuwa ni Marium, mama yake na Sele. Patrick alimuelekeza huku kwavile alikuwa akipatana sana na mama zake hawa, pia hakutaka Tina aende kwao moja kwa moja kwa kuhofia kumpa presha mama yake kwa atakayoelezwa na Tina.

TINA: Mimi ni Tina ndio mtoto wa Fausta ila sijui umenijuaje?

MARIUM: Fausta ni rafiki yangu sana, kuna kipindi nilikuwa nafanya nae biashara ya kuchukua bidhaa Chini, yani wewe nakujua tangia....."

Kabla Marium hajamalizia kueleza, Tina alikuwa ameanguka chini na kuzimia, ikabidi Marium aombe msaada kwa majirani na kumpeleka hospitali.


Deborah akaamua kuongea kilichomchekesha.

DEBORAH: Msifikirie nacheka tukio nililofanya Dar, hapana. Bali namcheka Jumanne.

ADAMU: Unanicheka mimi? Kwani nimefanyaje?

DEBORAH: Hujui kituko ulichofanya mjini Jumanne?

PAMELA: Kituko gani tena?

DEBORAH: Kwakweli Jumanne umenipa sababu ya kucheka, hivi ni kitu gani kilichofanya ujifiche baada ya kuniona mjini?

ADAMU: Mmh! Inamaana uliniona?

DEBORAH: Umekua ila bado una fikra ndogo, nilikuona hadi mahali ulipojificha ila nikachuna sababu nilijua wapi pa kukupata tu. Haya sasa upo nyumbani kwangu, vipi wataka kujificha tena?

Deborah akawa anacheka, Adamu nae aliona aibu kwani hakujua kama alionekana wakati anajificha pale mjini.


Patrick alienda na Yuda kwenye hotel na kupumzika.

PATRICK: Tungerudi nyumbani, ila na alama hizo itakuwaje!! Tutawaelezaje?

YUDA: Dah!! Labda tuwaambie kuwa nilivamiwa na majambazi. Au unaonaje?

PATRICK: Basi sawa, hakuna tatizo.

YUDA: Au mama atamaindi? Basi tukae kama wiki ndo turudi nyumbani au vipi?

PATRICK: Vyovyote vile kwangu ni sawa.

YUDA: Dah! Samahani sijakuuliza, ulipokuwa unakuja pale kwenye himaya, je hujabahatika kumuona binti aliyekuwa anakimbia?

Patrick akamueleza ilivyokuwa kwa huyo binti.

PATRICK: Nadhani atakuwa kwenu sababu nilimuelekeza aende huko.

YUDA: Dah! Kama yupo nyumbani sina budi kurudi, nahitaji sana kuzungumza nae yule. Nashukuru sana Patrick kwa kumuokoa yule.

PATRICK: Kwani wewe umemfahamia wapi yule?

YUDA: Dah!! Yule binti ndo aliyefanya hadi mimi kuamua kufanya kazi za ajabu ili nipate mkwanja.

PATRICK: Sijakuelewa bado.

Ikabidi Yuda amueleze Patrick jinsi ilivyokuwa hadi yeye akafahamiana na Tina.

"Kuna kipindi mimi nilitoka Mwanza na kwenda Dar kumtembelea Sele, na ndio huko nikajua kama anatumia jina la Sele.

Nilipokuwa kwake, nikamfahamu msichana wake aliyeitwa Tusa. Mara nyingine Tusa akawa anakuja na huyu msichana aitwaye Tina kumtembelea Sele. Kwakweli nikatokea kumpenda sana Tina, ikabidi nimwambie ukweli ila akanikataa kwa kigezo kuwa sina pesa. Nakumbuka kitu alichoniambia Tina ni kuwa nikatafute pesa kwanza ndio niende kumtongoza tena. Nilirudi huku Mwanza na kutafakari sana maneno ya Tina, nikapata kazi Mombasa ila nikapitia tena Dar kumuona Tina, akaniambia kitu kilekile kuwa nitafute pesa kwanza kwani yeye hawezi kuwa na mwanaume mwenye pesa za mawazo.

Tina ni msichana mwenye maringo sana ila nampenda sana, sikutaka kumkosa, nikasema nitafanya kazi yoyote ile ili niweze kuwa naye. Ndio nikaenda Mombasa ila kazi ya kule ilikuwa hailipi kivile, katika pitapita ndio nikakutana na Mashaka, akaniomba nikafanye nae kazi akanitajia mshahara mnono sana. Sikuweza kukataa kwani pesa niliitaka, ndio huko nikakutana na yale maswahibu ya kuona kichwa cha baba"

PATRICK: Dah! Pole sana Yuda, kumbe yule ndio Tina aliyeutesa moyo wako! Pole sana.

YUDA: Kwakweli nilishindwa kujizuia baada ya kusikia sauti ya Tina ikilia toka kwenye kile chumba, na ndiomana nikafanya gafla bila makubaliano.

PATRICK: Ndio hivyo mdogo wangu, pesa kwanza mapenzi badae. Bila pesa huthaminiki.

YUDA: Ila mbona Tusa anampenda Sele bila ya pesa jamani!

PATRICK: Dah! Pole sana Yuda, nadhani huujui ukweli. Tusa ni mke wa mimi sasa, nae alidanganyika kwa kitu kidogo tu nacho ni Pesa. Unatakiwa uiheshimu pesa kwani ukiwa nayo chochote utakacho unapata.

Yuda akabaki anashangaa tu kwani hakujua chochote kuhusu Sele, Patrick na Tusa.


Tusa na Sele wakiwa nyumbani kwa Mwita, wakiwa hawajui hili wala lile.

Mwita akamwambia Sele kuwa aende nae mahali ambako atampa pesa za kumuwezesha kuendelea na safari yao, ikabidi Sele amuage Tusa.

SELE: Nadhani kesho ndio tutaenda Morogoro, sababu leo Mwita ananipeleka kuchukua pesa.

TUSA: Sawa, ila nakuomba uwe makini sana.

SELE: Usijari Tusa.

Sele na Mwita wakaondoka huku Sele akiwa hajui wazo alilonalo Mwita.


Mashaka na Maiko wakaendelea na mipango yao na kuona kuwa karibia wanafanikiwa.

MAIKO: Kuna mtu nimeongea nae, amesema atanitumia details zote za alipo Deborah.

MASHAKA: Hapo ni safi sana, nangoja majibu tu.

MAIKO: Itabidi niende mjini nikakutane nae.

MASHAKA: Hakuna tatizo, nenda tu.

Maiko akajiandaa na kuondoka.


Marium aliendelea kumshughulikia Tina hospitali, akasahau kila kitu.

MARIUM: Nakuomba daktari, muhurumie binti yangu.

Daktari huyu alikuwa kimya tu kwani alikuwa na hasira na wakina Patrick, ila Marium hakujua kama huyu Daktari ametoka kufanya kazi kinguvu kwa watoto wake.

Daktari alijawa na hasira iliyoambatana na uoga kwani alihudumia wagonjwa huku akihofia ujio wakina Patrick tena.


Maiko alipokuwa mjini kwaajili ya kuonana na mtu aliyepanga nae. Mara gafla akashtukia amepigwa mtama na kuanguka chini.


Mara gafla akashtukia amepigwa mtama na kuanguka chini.

Maiko akashangaa sana, kabla hajajiweka sawa alijikuta akipigwa tena teke lilolomfanya aanguke tena, akaanza kufuatwa pale chini na Patrick,kwakweli Maiko akaona amepatikana kwasasa na hana ujanja tena.

Patrick alipomkutia pale chini na kumkunja . Halafu akakunja ngumi kwaajili ya kumshindilia nayo usoni, ndipo Maiko alipoanza kuongea,

MAIKO: Unatafuta kesi bure Patrick.

PATRICK: Unajua maana ya kesi wewe? Ungekuwa unajua ungeua watu hovyo.

MAIKO: Anaeua watu si mimi Patrick.

PATRICK: Najua, kazi yako si kutuagiza vijana tusio na hatia kutenda dhambi.

MAIKO: Hapana sio hivyo ni Mashaka ndiye anayetoa maagizo, hata mimi huwa naagizwa tu.

Patrick akamshindilia ile ngumi usoni

PATRICK: Hata kama, wewe ni muuaji tu Maiko huna cha kujificha. Haya huyo Mashaka wako yuko wapi?

Mara simu ya Patrick ikaanza kuita, mwanzoni akaipotezea ila ilipoanza kuita tena akaamua kuipokea na Maiko nae akatumia muda huo kukimbia kwani alichota mchanga pale chini alipokuwa na kumrushia Patrick usoni, kitendo kilichofanya Patrick amuachie Maiko na kuanza kupekecha macho.

Maiko akakimbilia gari yake na kuondoka.


Deborah na wote pale nyumbani wakaamua kufanya harakati.

DEBORAH: Kama hivyo unavyosema kuwa huyo Tina hajulikani alipo, itabidi tukatoe taarifa polisi.

PAMELA: Nadhani tufanye hivyo, ila vipi kuhusu Tusa?

DEBORAH: Tusa hajapotea ila wamejipoteza na Sele wake nadhani watarudi tu.

ADAMU: Ila huyo mtoto ndiye anayenipa presha jamani, sijui hata atakuwa wapi?

DEBORAH: Mmoja mmoja ndio mpango, anzeni na huyo Tina kwanza halafu wakina Tusa watafuata.

Ikabidi Adamu na Fausta wafanye safari ya kwenda polisi.


Maiko alirudi kwa Mashaka akiwa na alama za kudundwa usoni.

MASHAKA: Vipi tena?

MAIKO: Nimekutana na Patrick.

MASHAKA: Dah! Nilishakwambia mimi, hapafai huku bora turudi Arusha tukajipange upya bhana.

MAIKO: Kwakweli Patrick amenidhalilisha sana, wala sikufikiria kama angenifanya vile sehemu kama ile. Nakwambia sukubali hadi nimkomeshe, nitakapotoka tena hapa ni moja kwa moja hadi kumchukua mama yake, yani nimechukia sana.

MASHAKA: Sasa na huyo mama yake utampataje?

MAIKO: Nitampata tu, kwasasa sitaki kuwaagiza watu kukutana mjini, ila nitakutana nao hapahapa.

MASHAKA: Haya bhana, ila na mimi leo nitatoka kidogo. Kuna mahali naenda.

MAIKO: Kuwa makini sana huko uendako.

MASHAKA: Usijari chochote.

Mashaka nae akatoka kwenda alipopanga.


Patrick alirudi kwa Yuda akiwa na hasira sana.

PATRICK: Simu uliyonipigia imeniharibia kila kitu. Haya unataka nini?

YUDA: Samahani kaka, ila leo nilipowasha simu nimepigiwa na mama kuwa niende nyumbani kuna matatizo.

PATRICK: Sinilishakwambia kuwa huyo Tina nilimuelekeza aende huko! Sasa tatizo ni nini kuambiwa kuwa kuna matatizo?

YUDA: Hapana tatizo Patrick ila ningependa twende wote.

PATRICK: Aaah!! Wewe nenda tu kawachek, mimi nitakuja hata kesho.

YUDA: Kwahiyo umeniruhusu?

PATRICK: Ndio, nenda tu kawachek.

Yuda akaamua kwenda kwao ili kumuona Tina na mama yake.

Patrick nae akatoka kwaajili ya kuendelea kuwasaka wabaya wake, alitoka na bodaboda yake kama kawaida.


Tina alipopata unafuu akaruhusiwa na kurudi na Marium, kufika nyumbani kwake akafurahi kumuona mwanae Yuda. Na Yuda nae akafurahi kumuona Tina, akaenda kumkumbatia na kumpa pole.

Marium akawashangaa,

MARIUM: Kwani mnafahamiana?

YUDA: Usijari mama, nitakueleza tu.

Wakaingia ndani, na kuanza mazungumzo.

MARIUM: Nimekuita mwanangu kwavile nilishachanganyikiwa kabisa, Tina alikuwa na hali mbaya sana. Mbona hukuja moja kwa moja hospitali niliyokuelekeza?

YUDA: Aaah mama, niliona bora mje mnikutie nyumbani tu.

Yuda hakuweza kwenda kwenye hospitali aliyotajiwa kwakuwa ndio hospitali aliyofanya nayo majanga yeye na Patrick.

Tina nae akaamua kumuuliza Yuda.

TINA: Na yule aliyeniokoa na kunielekeza hapa, yule Patrick yuko wapi?

YUDA: Yupo nimemuacha mjini ila atakuja tu.

MARIUM: Mbona mnanichanganya, inamaana Yuda ulikuwa na Patrick? Siku zote ulipotoweka hapa ulikuwa na Patrick? Hivi unajua kama.... Aaargh!!

Marium akaingiwa na hofu kwani alishaambiwa na Sele kuwa Patrick ni jambazi na anapotoweka kwao basi huenda kufanya ujambazi, mwanzoni alishindwa kuamini ila imani ilimjia pale Sele alipopigwa na kuumizwa sana na Patrick.


Mwita alienda na Sele sehemu ya mbali sana, akamuacha hapo na kumwambia amsubirie ili arekebishe baadhi ya vitu.

Ila Sele alisubiri na kusubiri bila ya Mwita kutokezea. Ikabidi atafute utaratibu mwingine wa kuweza kurudi nyumbani kwa Mwita, na akaona kuwa Mwita hakuwa na lengo zuri, hivyo nia yake ilikuwa ni kurudi na kwenda kumchukua Tusa tu.

Mwita alirudi nyumbani kwake na kumkuta Tusa sebleni, akasalimiana nae na kwenda chumbani. Tusa akashangaa bila ya kumuona Sele, Tusa alipokuwa akitafakari mara Mwita akarudi tena sebleni ikabidi Tusa aulize.

TUSA: Kwani Sele yuko wapi?

MWITA: Yupo tu, unataka kujua alipo?

TUSA: Ndio, niambie ulipomuacha.

Mwita akainuka na kumwambia Tusa amfuate alipo Sele.

Tusa akainuka ila akasita kumfuata kwani aliona akielekea chumbani.

MWITA: Mbona umekwambia njiani? Twende ukamuone.

TUSA: Mbona huko ni chumbani?

MWITA: Hapana si chumbani ila kule kuna mlango mwingine, Sele ameamua kukusurprise.

Tusa akabaki akishangaa tu.

MWITA: Twende Tusa, usiwe na hofu. Mimi sio mtu mbaya.

Tusa akamfata, walipoingia tu, Mwita akafunga mlango na kuanza kumwambia Tusa.

MWITA: Binti mrembo kama wewe ni halali ya watu kama mimi wenye pesa na si mtu kama Sele, atakupa nini Yule eeh!

TUSA: (Huku akiogopa), mimi nampenda Sele sitaki mwingine.

MWITA: Kuwa mpole tu Tusa maana hapa hutaki utataka, unataka utapata.

TUSA: (Akaanza kutokwa na machozi), mimi sitaki, tafadhari usinifanye vibaya.

MWITA: Na mimi siwezi kumuacha mrembo kama wewe uende, hapa utanipa tu.

Mwita akaanza kumng'ang'aniza Tusa, ikawa purukushani. Tusa akampiga teke Mwita sehemu za siri ili apate kutoroka, ile anafika mlangoni tu Mwita akamkamata tena Tusa na safari hii akampiga hadi Tusa akazimia halafu akambaka wakati amezimia.

Watu wa namna hii wanaweza kubaka hata maiti kwa uchu wao.


Adamu na Fausta walipokuwa wanarudi toka kituo cha polisi, Adamu alimuomba Fausta amsubirie ili akatoe haja ndogo.

Fausta akawa amesimama akiwa hajui hili wala lile, mara akatokea mtu nyuma yake na kumziba mdomo kisha akampakia kwenye gari na kuondoka nae.

Tukio lile lilionwa na Patrick aliyekuwa kwenye bodaboda.

Patrick akaamua kuifatilia ile gari.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Patrick akaamua kuifatilia ile gari.

Dereva wa ile gari alikuwa akiendesha kwa kasi sana ila Patrick nae alikuwa na kasi ya ajabu kwenye bodaboda yake kwasababu hakutaka ile gari impotee.

Kwenye ile gari alikuwemo Mashaka na akagundua kuwa kuna bodaboda inamfatilia ila hakujua ni nani kwavile mwendeshaji alivaa helementi, ila hofu ikamjia kuwa huenda akawa ni Patrick, maneno ya Maiko yakamrudia kichwani kuwa anatakiwa awe makini sana.

Kila akizidi kuongeza kasi ndipo na ile pikipiki ilivyoongeza kasi.

Mashaka akajua kuwa anafatiliwa sababu amemteka Fausta, kwahiyo akaamua kufanya uamuzi wa gafla, akafungua mlango wa gari wakati ipo kwenye kasi na kumsukumia Fausta nje. Ni hapohapo kikatokea kitendo cha gafla pia toka kwa Patrick, kwani alichukua bastola na kulenga tairi moja wapo la gari ya Mashaka, kitu kilichofanya gari kukosa muelekeo na kuseleleka hovyo na mwisho kusimama.

Mashaka alikuwa mashakani sasa, akaamua kufanya uamuzi mwingine wa kukimbia, akatoka ndani ya gari, kwa bahati alitokea mwendesha bodaboda na bodaboda yake, alichofanya Mashaka ni kumsukuma yule wa bodaboda kwa mti, kitu kilichofanya bodaboda iwe upande wake na mtu upande wake. Mashaka akaikimbilia ile bodaboda na kuondoka nayo. Ikawa bahati kwa Mashaka na mkosi kwa mwendesha bodaboda.

Patrick hakuweza kumkimbiza tena Mashaka kwani alimuhurumia mwanamke aliyetupa pembeni na Mashaka.

Patrick aliinama na kumuangalia mwanamke huyo aliyekuwa anavuja damu hasa sehemu ya kichwani kwani aliangukia kichwa.

Ikabidi amnyanyue na kusimamisha gari ya kukodi akampakiza na kwenda naye hospitali.


Adamu alipotoka kujisaidia, akashangaa bila ya kumuona Fausta, akamtafuta sana bila ya mafanikio yoyote, ikabidi arudi nyumbani kwa Deborah.

Wote wakashangaa kumuona Adamu amerudi peke yake, na kumuuliza alipo Fausta. Akawajibu anachojua yeye.

DEBORAH: Sasa atakuwa ameenda wapi jamani? Maana Mwanza yenyewe hata haijui.

REHEMA: Isije ikawa amepotea kama mwanae Tina!!

PAMELA: Mmh! Mama, hata hakuna skendo za ajabu hapa Mwanza. Sasa huko kupotea watakuwa wanapoteaje?

ADAMU: Kwakweli mimi ndio sielewi kabisa, tumeandikisha vizuri pale polisi. Ila kitendo cha mimi kwenda kujisaidia tu yeye katoweka.

PAMELA: Au kuna mahali kapita atarudi.

ADAMU: Sidhani kama Fausta anaweza kushika njia kwa siku moja, ubaya ni kuwa nikimpigia simu inaita tu bila ya kupokelewa.

DEBORAH: Mmh! Huo mtihani, yani mengine hayajaisha yanakuja mengine mweeeh!! Sasa itakuwaje?

REHEMA: Mimi nadhani wewe Adamu na Pamela muende pale ambapo ulimuacha huyo Fausta, anaweza akawa amerudi pale ila amekosa uelekeo.

ADAMU: Ngoja tukajaribu basi.

Ikabidi Adamu na Pamela waende kumuangalia Fausta pale alipoachwa mwanzo na Adamu.


Mashaka alirudi hotelini akiwa anahema juu juu.

MAIKO: Vipi tena?

MASHAKA: Si yule mpumbavu wako, dah amenidhalilisha sana yani hadi nimeacha gari yangu.

MAIKO: Ila si nilikwambia uwe makini? Patrick ni khatari.

MASHAKA: Yani leo nilimpata mbaya wangu niliyemtafuta kwa muda mrefu, halafu Patrick kanizingua dah!!

MAIKO: Pole sana, gari umeiacha kabisa?

MASHAKA: Nitaifata tu, ila nimechukia sana leo. Yani yule mtoto wa kike ningemtesa leo na kumchinjilia mbali, ana bahati sana.

MAIKO: Mtoto wa kike gani huyo?

MASHAKA: Fausta huyo.

Maiko akashtuka na kushangaa kuwa Fausta yupo Mwanza.

MAIKO: Bora Patrick alivyotokea, dah yani wewe sijui hata ukoje! Unataka kuua watu wasio hata na hatia.

MASHAKA: Mimi ndiye ninayeijua hatia ya Fausta, yani Patrick namuandalia kisasi cha kufa mtu si anajifanya yeye ni bingwa wa kutetea watu wa Mwanza! Ngoja nitamkomesha tu.

MAIKO: Huna jipya Mashaka, ngoja nitoke mie ila mwenzio niko makini sana kwanza sitoki hovyo kwenye gari.

MASHAKA: Haya bhana, kunya anye kuku akinya bata....malizia mwenyewe.

MAIKO: Methali mbele ya Patrick!! Mbona utazijua zote mwaka huu, mtoto mdogo anatujambisha.

Maiko akatoka kwenda sehemu nyingine kwaajili ya kukutana na watu wake.


Tina akawa amepata unafuu kiasi pale nyumbani kwa Marium.

Ikabidi Marium amtume mwanae Yuda kwenda kumtembelea Deborah.

MARIUM: Yuda, ufanye uende kwa mamako mdogo ukamuangalie maana nikimpigia simu hata hapatikani. Si unajua atakuwa mwenyewe pale.

YUDA: Sele je yuko wapi?

MARIUM: Nimesahau, Sele aliniambia anaenda Singida mara moja. Mamako mdogo nasema yuko mwenyewe sababu huyo Tusa mwenyewe pale kwake ni kama mgonjwa tu.

YUDA: Yupo na mama yake Tusa.

MARIUM: Nimekwambia uende ukamuangalie, porojo sitaki sijui yupo nani na nani sitaki. Nenda kamuangalie mdogo wangu anaendeleaje.

YUDA: Sawa basi, nitaenda kesho.

Halafu Marium akamfata Tina ili wamjaribishe mama yake ila simu iliita tu bila ya kupokelewa.

TINA: Labda atakuwa mbali na simu, ila akikuta kuwa amepigiwa basi atapiga tu hiyo simu.

MARIUM: Ila usiwe na mashaka sana Tina, jisikie huru.

TINA: Sawa mama, nashukuru.

Tina alijilaumu sana kwa tamaa ya pesa, kwani ndiyo iliyomponza.


Patrick alimpeleka Fausta hospitali ile ile aliyotibiwa Yuda.

Daktari hakutaka mabishano safari hii, alimuhudumia Fausta bila hata ya kuulizia karatasi namba tatu (PF3).

Alimuogopa sana Patrick, alifanya kazi kwa uoga mkubwa.

Baada ya kumfunga bandeji na kumpa baadhi ya dawa akaruhusiwa kuondoka, ikabidi Patrick amchukue hadi alipo yeye.

PATRICK: Je unapajua kwa ndugu zako?

FAUSTA: Kwakweli mimi ni mgeni hapa Mwanza, hata sijui panaitwaje pale tulipofikia.

Patrick akaona kuwa huu sasa ni mtihani, akawa anawaza je ampeleke kwa mama yake au kwa mama yao na wakina Sele.


Pamela na Adamu walipoenda kumsaka Fausta.

ADAMU: Hivi wewe Pamela, kwanini hukuniambia mapema kuwa upo kwa Deborah?

PAMELA: Vipi kwani?

ADAMU: Sikuwa tayari kukutana nae kwasasa.

PAMELA: Kwani bado wampenda?

ADAMU: Maswali gani hayo bhana!! Aaargh.

Wakajikuta wakibishana bila hata ya faida.

Walikuwa wanaendelea kubishana ndipo waliposikia tukio la mwendesha bodaboda.


Hata pale Mwita alipomaliza haja zake, Tusa alikuwa bado kazimia.

Mwita akawaza cha kufanya na yule binti.

"Hivi amezimia kweli au amekufa? Kama amekufa mbona itakuwa ni balaa hili mmh!!

Akimtazama mapigo ya moyo yalikuwa bado yanadunda, ila alikuwa mtu asiyejitambua kabisa.

Mwita alipokuwa anahangaika cha kufanya na Tusa, mara anasikia mtu anagonga hodi.

Kwenda kumchungulia dirishani alikuwa ni Sele.


Mara anasikia mtu anagonga hodi.

Kwenda kumchungulia dirishani alikuwa ni Sele.

Mwita akaona sasa kazi anayo na atamweleza vipi Sele, ikabidi ajiandae namna ya kupanga maelezo halafu akamvuta Tusa pale sebkeni na kumfunika, ndipo alipoenda kufungua mlango.

SELE: Mbona uliniacha Mwita?

MWITA: Nilisahau kama tulienda wote ila nilitaka nikufate wewe.

SELE: Hizo ni porojo tu, haya Tusa yuko wapi?

Ikabidi Mwita amuonyeshe Tusa aliyekuwepo pale chini.

Sele akashtuka sana na kwenda kumfunua Tusa.

Sele aliinuka na kumkunja Mwita.

SELE: Niambie haraka umemfanya nini Tusa?

MWITA: Sijui, nimemkuta hivyo hivyo.

SELE: Muongo mkubwa wewe.

Sele akampiga Mwita ngumi ya tumbo,

SELE: Niambie ukweli Mwita.

MWITA: Unanionea tu ila sijui chochote.

Siku zote mkosaji mwenye hofu huishiwa na nguvu na ndivyo ilivyokuwa kwa Mwita.

Sele akampiga Mwita ngumi nyingine, ikabidi Mwita nae aanze kujitetea na kuanza kupigana, wakapigana sana.

Mara Mwita akachukua kisu kilichokuwa mezani ili kumtishia Sele.


Yuda alienda moja kwa moja hadi kwa Deborah.

YUDA: Nimekuja kukusalimia tu mamdogo na kuangalia unaendeleaje.

DEBORAH: Naendelea vizuri ila ukirudi nyumbani mwambie dada yangu kuwa namwitaji sana, nina matatizo hapo.

YUDA: Sawa, ila je yule bibi pale nje ni nani?

DEBORAH: Ni bibi yenu yule.

YUDA: Kivipi mamdogo?

DEBORAH: Hata nikikueleza hautanielewa, wewe ukienda mtaarifu tu dada yangu.

YUDA: Na huyo Tusa yuko wapi maana namsikia kwenye mabomba tu.

DEBORAH: Kamuulize kaka yako Sulemani, kwakweli hata sielewi mie jamani na hata sijui akija Patrick nitamuelezaje mwenzenu.

YUDA: Mmh! Khatari kama ndo hivyo.

Yuda ikabidi aage na kuendelea kupewa msisitizo wa kumwambia mama yake.


Adamu na Pamela ikabidi nao waende kwenye eneo la tukio ambako walikuta damu na gari ambayo iliachwa pale, watu walikuwa wanashangaa na kuondoka ila wao walikuwa wanashangaa na kuendelea kubishana kuhusu kupelekwa kwa Deborah.

Wakati wanaendelea kubishana, Adamu akawa amevutwa sana na maelezo ya mwenye bodaboda, akataka kumfata ili aweze kumsikiliza na kung'amua japo kitu kimoja, akamwambia Pamela kuwa wasogee pale kumsikiliza.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

PAMELA: Tufate kilichotuleta, hayo maelezo ya huyo mtu hayawezi kutusaidia kitu.

ADAMU: Huwezi jua Pamela, pengine tutagundua kitu chochote hapo.

PAMELA: Babu wee, nenda mwenyewe.

Pamela alionekana kuchukizwa na zile lawama alizopewa na Adamu pia alihisi kuwa huenda Adamu akawa bado anampenda Deborah.

Adamu alijua ni hasira za muda mfupi tu zile, akaamua kwenda kumsikiliza yule wa boda boda.

ADAMU: Nikukute hapo hapo.

PAMELA: Utamkuta beberu.

Akawa amesema kwa kumtania mumewe humo humo.

Adamu alipokuwa anasikiliza maelezo ya yule kijana wa bodaboda ambapo baadhi ya wananchi walikuwa wakimsaidia, akaona yale maelezo yanaweza kuwa na kitu cha kuwasaidia, akarudi kwa Pamela ili amueleze na ikiwezekana wakasikilize wote. Ila Hakumkuta Pamela, akamtazama kila sehemu hakumuona. Akaanza kujiuliza, "inamaana aliposema kuwa nitamkuta beberu alikuwa anatania au alimaanisha? Kama alimaanisha je amekwenda wapi jamani?"

Adamu akamuangalia sana bila matumaini.

Ikabidi arudi nyumbani kwa Deborah ili kumuangalia kama amesharudi.


Yuda aliporudi kwao alimpa mama yake taarifa aliyopewa na Deborah.

MARIUM: Ana matatizo gani kwani?

YUDA: Sijui, ila ukienda atakueleza mwenyewe vizuri.

MARIUM: Mmh! Mnanitisha sana.

YUDA: Halafu mama, huyu kaka Sele huyu anatafuta matatizo.

MARIUM: kivipi tena?

YUDA: Nini kimemtuma kuondoka na Tusa? Nakwambia mama, Patrick akijua basi ujue Sele atakuwa hatiani.

MARIUM: Jamani jamani nyie watoto, mtaniua kabla ya siku zangu jamani. Mmh! Sele nae kwanini hakubali kushindwa? Hili ni tatizo sasa.

YUDA: Sijui hata itakuwaje kwakweli, hali ni mbaya mama.

Yuda nae alianza kumuhurumia Sele kwani kipigo cha Patrick kilimtisha sana.


Patrick aliendelea kumuhudumia yule mwanamke.

PATRICK: Ukipata nafuu kidogo nitakupeleka kwa mama yangu kama hutojali.

FAUSTA: Hakuna tatizo kijana, nitashukuru sana.

Fausta alikuwa hajielewi kwani mara nyingine kumbukumbu zake zinakuja na mara nyingine zinapotea.


Adamu akarudi bila ya Pamela, akaanza kuulizwa maswali juu ya Pamela na kusema kuwa haelewi alipo.

REHEMA: Una nini Adamu, kwanini kila ukiondoka na mtu unarudi peke yako?

ADAMU: Sielewi tatizo mama, yani sielewi kabisa.

REHEMA: Umempoteza Fausta, na sasa ni Pamela. Naomba uende mwenyewe kituo cha polisi ukaripoti kupotea kwao.

ADAMU: Yani mama hujui tu nilivyochanganyikiwa hapa.

DEBORAH: Kuchanganyikiwa hakutasaidia, fanya kama ulivyoambiwa na mama. Sijui kuna nini Mwanza hapa, mbona mambo ya ajabu haya. Kupotea kwa watu wazima mmh!

ADAMU: Sawa nitaenda basi.

REHEMA: Ila uwe makini maana naona hali ni mbaya kabisa.

ADAMU: Sawa, ila itabidi tungoje kwanza ili niende kesho.

Wakakubaliana kuwa aende kesho kutoa taarifa ili kwa siku hiyo wawe wanaangalia kwanza kama watarejea.

INAENDELEA

Post a Comment

0 Comments