Yuda akarudi kwao na kumkuta ndugu yake akiwa ameumizwa sana.
YUDA: Vipi kaka, nani amekutenda hivi?
SELE: Ni Patrick bhana, eti kisa mwanamke tena mwanamke mwenyewe kamuiba toka kwangu.
YUDA: Dah! Pole sana, nadhani Patrick amekuwa na nguvu sana kwasasa.
SELE: Patrick ni jambazi, ila watu wengi hawajui.
YUDA: Dah! Kuna kitu kaka ilitakiwa tukakifanyie kazi, ila kwavile umeumia sitakwambia nitangoja upone. Umesema Patrick ni jambazi?
SELE: Patrick ni jambazi ndio, ila nitapambana nae tu. Siachi kupambana nae hadi nipate haki yangu. Hivi na wewe Yuda, kipindi chote hiki ulikuwa Arusha? Ulikuwa unafanya nini huko?
YUDA: Mambo makubwa kaka, ila sikuwa Arusha kipindi chote. Nilikuwa Mombasa nafanya biashara na baadae nikapata kazi Arusha, ila niliyoyakuta huko!! Mmh nitakusimulia ukikauka vidonda.
Yuda aliendelea kutafakari kauli ya Sele kuwa Patrick ni jambazi, Yuda akaona kuwa anaweza kufanya ushirika mzuri na Patrick ukizingatia baba yao alihusika pia na wakina Patrick.
Patrick hakuwa na baba ila baba yao na wakina Sele ndio alikuwa kama baba yake kwahiyo uchungu wa Yuda na Sele juu ya mzee huyo utakuwa sawa na kwa Patrick, Yuda alifikiria hilo jambo akaona ni vyema akamshirikishe huyo Patrick.
Yuda akaenda kuonana na Patrick sasa ili amueleze kuhusu mzee wao.
Alipofika nje akamkuta Deborah na Pamela wakiongea, akawasalimia na kuongea mawili matatu na Deborah, halafu Deborah akamuelekeza Pamela kuwa Yuda pia ni mtoto wa Mariam yaani mdogo wake Sele.
Baada ya hapo, Yuda akamuulizia Patrick.
DEBORAH: Yupo chumbani kwake, nenda tu utamkuta.
Yuda akaenda chumbani kwa Patrick.
Jambo alilolikuta humo lilimfanya Yuda ashtuke na kutetemeka.
Yuda akaenda chumbani kwa Patrick. Jambo alilolikuta humo lilimfanya ashtuke na kutetemeka.
Alimkuta Patrick ameshika bastola na kuielekezea mlangoni, na kwavile yeye ndo alikuwa anaingia ikawa kama vile amenyooshewa yeye.
Yuda akatetemeka na kuishiwa cha kusema, akajilaumu kwa kitendo cha kuingia bila hodi. Patrick akaishusha ile bastora na kuiweka kwenye mkoba pembeni,
PATRICK: Aaah Yuda, karibu sana.
Yuda alikuwa bado anatetemeka na kuamini maneno ya Sele kuwa Patrick ni jambazi. Akashindwa kumjibu Patrick kwani alikuwa na hofu bado.
PATRICK: Usijali Yuda, acha kufikiria ulichokiona bhana. Mambo ya kawaida tu yale.
YUDA: Mamdogo anajua?
PATRICK: Wee, usithubutu kumwambia.
YUDA: Na kama ni yeye je ndie angekuwa kaingia na kukuta kama mimi nilivyokuta?
PATRICK: Hawezi ingia bila hodi, hata hivyo angeongea ongea hapo kabla ya kuingia. Na wewe jifunze adabu usipende kuparamia sehemu bila hodi.
YUDA: Nimekusoma kaka, nisamehe kwa hilo.
PATRICK: Poa, za siku nyingi?
Yuda alipiga stori mbili tatu na Patrick huku akijaribu kumsoma kwanza kabla ya kumueleza.
Fausta alimuita Tina ili aelezwe kuhusu mume wa Tusa.
FAUSTA: Hivi Tusa yule mwanaume alimtolea wapi?
TINA: Facebook mama.
FAUSTA: Facebook? Mmh! Hata kama ni huko kulikuwa na umuhimu wa kuwajua ndugu zake.
REHEMA: Sema wewe Fausta, mi niliuliza hapa hadi nikachoka. Mwanaume hujui anapokaa, huwajui ndugu zake unamuozesha mtoto wako huko, hivi unampenda kweli mwanao?
FAUSTA: Kwakweli Pamela na Adamu wamefanya kosa ambalo watajutia maisha yao yote. Unajua tulipogundua kuwa Adamu ni ndugu yetu, baba yetu mzee Ayubu alipinga vikali ndoa yao lakini kwavile walishazaa haikuwa na jinsi. Na alitupa onyo kuwa tusiozeshe mtoto bila kujua ukweli wa upande wa pili, licha ya undugu unaweza pia kukuta yule si mtu.
TINA: Mmh! Mama, Patrick ni mtu bhana, acha zako hizo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
FAUSTA: Mi nasemea tu wala sina tatizo.
Fausta aliendelea kuwaza vitu mbalimbali kuhusu huko alipo Pamela.
Deborah akizungumza na Pamela kuhusu Tusa.
DEBORAH: Pamela, jaribu kumuweka sawa binti yako. Alishakosea kuolewa na mtu asiyempenda, asitake kufanya kosa lingine hapa, akitaka apange na Patrick na kuachana kiustaarabu, akilazimisha ataumiza wengine.
PAMELA: Ni kweli mwanangu hayupo sawa, na tatizo lake hataki kusema ukweli. Amekonda sana mwanangu, mwanao anamtesa sana Tusa.
DEBORAH: Kila mwamba ngoma huvutia kwake, utamtetea mwanao na mimi nitamtetea mwanangu. Tusa wako ni mpumbavu, atakuwa vipi na mahusiano na wanaume wawili kwa wakati mmoja tena ni ndugu!
PAMELA: Tusa si mpumbavu ila alipumbazwa na Patrick, Deborah huyajui yaliyojificha kwa mwanao, siwezi kumponda kwani ameniokoa toka kwenye mikono ya simba watu.
DEBORAH: Ndio wakina nani hao?
PAMELA: Ni majangili flani watu wa Arusha, hata tunaishi hapa sijui kama tuko salama.
DEBORAH: Majangili? Kivipi na wanafanya kazi gani?
PAMELA: Nadhani wanafanya kazi za kigaidi, nahisi hata mwanao Patrick ni mwenzao, naye atakuwa jangili tu.
DEBORAH: Ugaidi kama wa kuteka watu?
PAMELA: Ndio, na mengineyo ambayo magaidi hufanya. Hata Patrick alimuoa mwanangu kigaidi tu.
Deborah akaanza kuchezesha akili yake baada ya kusikia Arusha na kazi za ugaidi, wazo lake likaenda moja kwa moja kwa Maiko.
Fausta akiwa nyumbani kwa Adamu alijikuta akiwaza vitu vingi sana.
FAUSTA: Mama, mbona mimi kama najawa na mashaka moyoni juu ya huko Mwanza.
REHEMA: Mashaka gani tena?
FAUSTA: Labda Pamela na Tusa wametekwa, hivi ni kitu gani kinachoweza kuwazuia kurudi.?
REHEMA: Sijui maana wamedai wana matatizo tu.
FAUSTA: Nadhani huyo mtu nia yake itakuwa ni kaka Adamu tu.
REHEMA: Kwanini Fausta? Mbona sisi hatuna maadui kabisa?
FAUSTA: Mama, tusikubali kabisa Adamu kwenda mwenyewe. Lazima tumsindikize wote kwa usalama wake.
REHEMA: Mmh! Unanitisha Fausta. Kwanini unawaza hivyo?
FAUSTA: Mama, yule mke wa kwanza wa Adamu kwao ni Mwanza. Unajua kitendo alichofanya kabla ya kuondoka Dar?
REHEMA: Kitendo gani?
FAUSTA: Huyo mwanamke anaitwa Deborah, ukimuona ni mpole sana na mkarimu. Hata mimi sikuamini kama ni yeye alifanya kitendo cha kikatili kiasi kile.
REHEMA: Mmh! Alifanyaje?
FAUSTA: Alichukua upanga na kumkata binti flani hivi miguu na yule binti ni mlemavu hadi leo hana miguu kabisa. Mmh huyo Deborah ni mkatili mama.
REHEMA: Una uhakika alifanya yeye hicho kitendo? Mbona huo ni ukatili mkubwa jamani, loh anataka kufanana na kaka yangu Mashaka.
FAUSTA: Hata mimi namfananisha na Maiko, mama kuna wanawake makatili sana na yule Deborah ni mmoja wao. Nina hofu kama akawa yeye amewateka Pamela na Tusa na sasa anamtaka Adamu akalipe kisasi.
REHEMA: Mbona unanichanganya sasa, Adamu alifanyaje hadi alipe kisasi?
FAUSTA: Adamu alimsaliti Deborah na kuwa na Pamela kipindi hicho hatukujua kama Adamu ni ndugu. Ila mama hizi ni hisia zangu tu maana hakuna ajuaye kama huyo Deborah bado yupo hai au alikufa.
REHEMA: Ila hata Adamu aliniambia anajutia kitendo cha kumsaliti huyo mkewe, ila nadhani kama alifanya ukatili huo basi alikuwa na sababu maana Adamu kuna siku alinieleza kuwa mwanamke huyo alikuwa mpole sana. Mmh ila kama ndio hivyo alikuwa katili sana.
FAUSTA: Hata nashangaa leo nimemkumbuka mama, ila sitaki kumuwazia mabaya ila pia sidhani kama huko Mwanza ni kwema Adamu kwenda peke yake.
Ikabidi wapange mipango ya wote kwenda huko Mwanza.
Maiko na Mashaka waliendelea kunoa vijana wao kwaajili ya kuwapeleka kupambana na Patrick.
MAIKO: Ila kuna haja kweli ya kwenda na vijana wengi?
MASHAKA: Wengine tutaenda nao kwaajili ya madili mengine tu huko Mwanza.
MAIKO: Hapo sawa, maana Tukiwa wengi sana atatupotea yule. Ila tutachek na madili mengine pia, hiyo nzuri sana.
Wakapanga kusafiri na vijana wanne kwaajili ya madili mengine watakayo yapata huko Mwanza, vijana wawili wa kuwasaidia na wawili wa madili.
Yuda akaamua kumueleza ukweli Patrick baada ya kumsoma.
YUDA: Kaka, hivi unajua mzee wetu yule sisi huku tulizika mwili ila kichwa chake hadi leo kuna mahali kipo.
PATRICK: Kipo? Kipo wapi?
Yuda akaanza kumueleza Patrick jinsi alivyogundua jambo hilo.
Akamkuta Patrick akitikisa tikisa kichwa.
PATRICK: Umesema ni Arusha?
YUDA: Ndio ni Arusha kaka.
PATRICK: Huyo jamaa anaitwa Maiko na mwenzake Mashaka?
YUDA: Ndio hao hao kaka.
Patrick akapatwa na hasira sana, akajikuta akifumba macho kwa dakika kadhaa huku akitafakari hilo jambo.
PATRICK: Unataka tufanyaje Yuda?
YUDA: Nataka tukalipize kisasi, hiyo ndio shida yangu.
PATRICK: Hakuna tatizo, cha msingi tujipange twende huko Arusha.
YUDA: Ila tutaweza kaka?
PATRICK: Kujiamini ni ishara ya ushindi wewe jiamini tu.
YUDA: Sawa, hakuna tatizo basi.
Yuda akaondoka huku akitegemea kuanza kujipanga na Patrick kwaajili ya kwenda kulipa kisasi Arusha.
Yuda aliaga na kuondoka zake, Patrick akamsindikiza kidogo Yuda.
Nje kwao alimuona mama yake na Pamela wamelala kwenye mkeka, Patrick akaingia ndani, kuna kitu kikaanza kujichora katika hisia zake, akasimama mlangoni kwake mara Tusa akapita akiwa anatokea chumbani akitaka aende sebleni na kutoka nje walipo mama zake.
Alipokuwa anapita kwenye mlango wa Patrick, alishtukia akivutwa chumbani na Patrick, Tusa hakuweza kupiga kelele kwani alizibwa mdomo na Patrick.
Tusa hakuelewa ni kitu gani atafanywa na Patrick humo ndani, alijikuta machozi yakimtoka tu.
Tusa hakuelewa ni kitu gani atafanywa na Patrick humo ndani, alijikuta machozi yakimtoka tu.
Patrick akiwa kamziba mdomo Tusa, akaanza kumwambia.
PATRICK: Hivi kwanini hutaki kunipa haki yangu Tusa? Leo nahitaji, hii ni haki yangu kama mumeo kwahiyo utake usitake utanipa tu.
Tusa akaendelea kuhangaika, Patrick akajua kwa vyovyote vile Tusa atapiga kelele tu, akachukua kitambaa alichokuwa amepulizia dawa na kumfunika nacho Tusa usoni, kitu hicho kilichofanya Tusa alale.
Patrick akatumia muda huo kumuingilia Tusa kimwili bila ya Tusa kujitambua.
Kitu hicho kilikuwa ni ushindi sana kwa Patrick, aliendelea kufanya mambo yake mengine kwa uhuru, huku akijisemea "Anataka nisimfaidi wakati naondoka, aje yule mjinga Sulemani kumfaidi wakati mi ndo nimemgharamikia mtoto aah!"
Deborah na Pamela wakiwa nje wakashangaa hadi jioni Tusa hajatoka ndani, Deborah akaingia ndani kumuangalia Tusa ila hakuwepo ndani, akashangaa na kujiuliza alipo Tusa.
Mara Patrick akatoka chumbani kwake, ndipo Deborah alipomuuliza.
DEBORAH: Umemuona Tusa?
PATRICK: Ndio, yupo chumbani kwangu.
DEBORAH: Chumbani kwako!! Anafanya nini?
PATRICK: Mama, Tusa ni mke wangu sasa unapouliza anafanya nini chumbani kwangu nakushangaa sana. Kwasasa amelala.
DEBORAH: Mmh makubwa haya.
Deborah akatoka nje na kumfata Pamela alipo.
DEBORAH: Eti Tusa yupo chumbani kwa Patrick, mbona mambo!!
PAMELA: Hata hivyo ni mumewe yule, hatutakiwi kuhoji sana.
DEBORAH: Pamela unakuwa kama vile hujui kumuangalia mwanao, hivi unavyomuona Tusa hapa unafikiri anafurahia ndoa yake na Patrick?
PAMELA: Sijui, ila Tusa angekuwa hafurahii angesema. Mbona anakaa kimya muda wote! Anashindwa hata kunieleza mama yake! Kwa upande wangu namuona Patrick ni mume bora kwa Tusa.
DEBORAH: Kwanini?
PAMELA: Anajua kumlinda mkewe, si unaone hata Sele ameshindwa kutoroka na Tusa kwasababu ya Patrick. Na pia Patrick ameniokoa.
DEBORAH: Binti yako nae hana msimamo, yani mi namtetea yeye anatoroka na Sele na leo je kilichompeleka chumbani kwa Patrick ni nini? Dah hata simuelewi kwakweli, eti kalala na kulala loh!
PAMELA: Kwa upande wangu sina shaka sana sababu najua Patrick ni mtu mzuri, mwanzo nilikuwa na mashaka nae, ila sasa nimemuona Patrick anafaa kwakweli.
Pamela alijivunia kitu kimoja kwa Patrick, ni kile kitendo cha kuokolewa nae toka mikononi mwa wakina Maiko, kwahiyo alimuona Patrick kuwa mtu mzuri kwake, hakujua kama kuna mambo maovu yanayofanywa na Patrick.
Tina alipoona safari ya kwenda Mwanza imenoga ikambidi aende kumuaga rafiki yake Vene.
TINA: Kesho ndo tunaenda kwenye ile safari yetu ya Mwanza. Nimefurahi kweli maana itakuwa ni mara yangu ya kwanza kufika huko.
VENE: Mmh Tina, Mwanza kuna mapedeshee huko balaa. Na nikujuavyo wewe lazima utawapagawisha tu.
TINA: Mapedeshee siwataki Vene, mdogo wangu Tusa tangu ameolewa na lile pedeshee la Arusha sijawasiliana nae hadi leo. Ndio wanasema yuko huko Mwanza.
VENE: Itakuwa amepatwa na mambo mazuri, yani Arusha na Mwanza ni hatari shoga yani, halafu wana hela hao balaa.
TINA: Ila siwataki hao mapedeshee bhana Vene.
Tina alikuwa akiuwaza mji wa Mwanza kwani akienda ndio itakuwa mara yake ya kwanza kufika Mwanza.
Wakiwa wanajiandaa nyumbani kwao,
TINA: Eti mama wanaume wa Mwanza wana pesa eeh!
FAUSTA: Nani kakwambia mwanangu? Mnapenda kuongopeana sana wewe na mwenzio.
TINA: Nambie ukweli bhana mama.
FAUSTA: Wapo Kawaida tu hawana lolote. Ngoja tujiandae hapa kwa hiyo safari ya kesho.
Wakaendelea kufanya maandalizi ya hapa kwaajili ya safari yao.
Tusa alipozinduka na kutazama huku na kule ndipo alipokumbuka kitu kilichotokea, akaamua kushuka pale kitandani ili aweze kutoka nje. Wakati akifanya hayo, mara Patrick akaingia chumbani.
PATRICK: Khee, umeamka mke wangu!
Tusa alimtazama tu kusema chuchote.
PATRICK: Usiwe na hasira Tusa, mimi ni mumeo.
TUSA: Hata kama ni mume, hutakiwi kunifanyia hivi.
PATRICK: Ni haki yangu Tusa, unategemea mimi niende wapi wakati wewe upo?
TUSA: Niachie nitoke basi.
Patrick akawa anamzuia Tusa nae aliendelea kuonyesha kiburi cha kutaka kutoka nje, na hapo hapo akashikwa kwa nguvu zaidi na Patrick.
PATRICK: Sasa ole wako umwambie mtu kitu chochote. Hakuna kusema, hutakiwi kusema kitu.
TUSA: Unanionea sana Patrick, laiti watu wangekujua ulivyo wangekuponda na mawe wewe.
PATRICK: Nimekwambia hakuna kusema Tusa.
TUSA: Bhana eeh nishakuelewa, wewe ni mbabe nani atakuweza bhana. Acha niendelee kuteseka ila siku watapoosha maiti yangu watajua ni vitu gani nimepitia. Niachie Patrick sitasema chochote.
Patrick akamuachia na Tusa akatoka mule ndani akiwa amenyong'onyea sana hakuwa na raha yoyote. Aliwaza vitu vingi moyoni mwake haswa mateso anayopewa na Patrick, mateso anayoyajua yeye mwenyewe.
Mashaka na Maiko walikuwa wameshakamilisha safari yao ya kwenda Mwanza.
MAIKO: Lazima tufanikishe safari hii.
MASHAKA: Tutaonekana wajinga kama tukiwakosa.
MAIKO: Vipi Tusa, nae bado tunamuhitaji?
MASHAKA: Tena sana, si unajua kazi zetu karibia zote zimesimama kwaajili yao, dah wametupatia hasara sana hawa watu jamani.
MAIKO: Yule Patrick anajiamini sana na hilo ndo tatizo, safari hii ni kimya kimya hadi tumpate.
MASHAKA: Ndio, nataka kujua jeuri ya Patrick itaishia wapi. Kijana mdogo lakini anajifanya kucheza na akili zetu, ngoja tumpate firauni yule.
MAIKO: Ametusumbua sana Patrick, hata sikufikiria kweli mapenzi hayafai kazini maana mapenzi ndo yamemponza yule hadi kutoroka na Tusa.
MASHAKA: Ila tuache utani bhana, kabinti kanavutia sana kale.
Wakawa wanacheka huku wakiendelea kuweka mambo sawa na kuianza safari ya kwenda Mwanza wakitumai kumpata Patrick na Tusa.
Patrick alienda kwa Yuda na kupanga mpango wa kuondoka mahali hapo kwenda kwenye ile himaya ya kina Maiko.
PATRICK: Jiandae kesho safari, twende huko kupambana.
YUDA: Dah umeishtukiza kaka.
PATRICK: Kushtukiza ni jambo jema kwani inamfanya adui asijipange kwa muda.
YUDA: Poa poa kaka, ila vipi silaha tutakuwa nazo?
PATRICK: Ondoa shaka, kila kitu kipo kwenye mstari.
YUDA: Poa, nami niko tayari tu.
PATRICK: Na Unapoaga nyumbani hapa usiwaage moja kwa moja ya tuendapo, wadanganye vyovyote ili kuokoa safari yetu.
YUDA: Hakuna shaka, lazima tutafanikisha tu.
PATRICK: Ndio hivyo, kuwa makini sana Yuda. Ikiwezekana usiage kabisa.
YUDA: Sawa, nimekuelewa hapo kaka yangu.
Wakaenda kujiandaa na kesho yake safari ya kwenda Arusha ikaanza.
Tusa alijiinamia huku akitokwa machozi.
DEBORAH: Hivi unaliaga nini wewe? Unatutisha sana kwa kilio chako ila husemi.
TUSA: Muda ukifika nitasema tu.
DEBORAH: Mmh! Haya bhana. Huo muda sijui utakuwa ni lini, ila usipende kuficha mambo Tusa utajitesa bure wakati msaada upo.
Deborah alikuwa akimshangaa sana Tusa kwani binti huyu alijua kuficha mateso yake, machozi tu ndo yalionyesha kuwa anateseka.
Muda mwingi Tusa alijilaumu kwa upumbavu wake, alijiona mjinga sana kukubali kuolewa na mwanaume asiyempenda.
Adamu na familia yake walikuwa ndani ya jiji la Mwanza, waliingia Mwanza usiku na kufikia kwenye hoteli wakalala hapo hotelini.
Kesho yake, Adamu akamtafuta Pamela kwa ile namba ila hakumpata hewani kwahiyo akangoja pale watakapofungua simu hiyo.
Tina baada ya kukaa pale kwa muda kidogo.
TINA: Mama, acha nishuke chini nikatembee kidogo.
FAUSTA: Mwanangu, miguu ishakuwasha tayari. Usiende mbali maana hapa tunangoja jibu la mjomba ako.
TINA: Siendi mbali mama, nitakuwa maeneo haya haya ya hotelini tu.
FAUSTA: Sawa mwanangu.
Tina akashuka na kwenda kutembea tembea kidogo pale karibu ili kuiona Mwanza ilivyo.
Muda ulipita sana bila ya Tina kurejea, wote wakaingiwa na wasiwasi kuwa Tina yuko wapi.
Muda ulipita sana bila ya Tina kurejea, wote wakaingiwa na wasiwasi kuwa Tina yuko wapi.
Fausta akaamua kushuka chini kwenda kumuangalia ila hakuwepo kabisa katika maeneo yale, akarudi juu akiwa hata haelewi pa kuanzia.
FAUSTA: Kwakweli huyu mtoto ananieleleza leo mama.
REHEMA: Jaribu kupiga simu yake.
FAUSTA: Simu yake haipatikani, sijui hata yuko wapi na mjomba wake akirudi hapa tutamueleza nini jamani dah.
REHEMA: Ila Tina nae, alienda kutafuta nini nje?
FAUSTA: Mama, Tina huwa kama vile anawashwa miguu, alinambia anaenda tu hapo chini kuangalia mazingira ila hadi sasa hajarudi, na hata hapo chini hayupo.
REHEMA: Mmh hebu tuwe na subira kidogo.
FAUSTA: Mama, ingekuwa Dar nisingekuwa na mashaka, sasa huku Mwanza Tina hata hapajui, nahofia atapotea jamani.
REHEMA: Tina ni mtu mzima, hawezi kupotea kizembe. Shughuli akirudi huyo Adam kabla ya Tina.
FAUSTA: Hapo ndio pagumu, sijui kama atanielewa jamani.
Fausta hakuwa na raha kabisa, alipatwa na mawazo tofauti tofauti kichwani.
Tina akiwa hajitambui, akashtuka na kujiona yupo kwenye chumba na vijana wawili. Kumbukumbu zikamjia kuwa alipotoka nje ya hoteli ili kuangalia mazingira akakutana na baba mmoja asiye mfahamu, akasalimiana nae, yule baba alimuomba Tina wakae mahali na kupata bia mbili tatu kwa maongezi, Tina hakuona tatizo akaenda kukaa na huyo baba, anachombuka Tina ni kuwa alikunywa bia mbili tu halafu akapatwa na usingizi wa ajabu, ndipo hapo aliposhtuka na kujiona yupo kwenye chumba.
Tina akawaangalia wale vijana na kuwauliza
"Nipo wapi hapa?"
Wale vijana hawakumjibu kitu, ila mmoja wapo akatoka na kurudi na yule baba aliyekutana nae Tina, ile Tina alipomuona tu.
"umenileta wapi huku? Kwanini umeniweka humu?"
Yule baba alikuwa ni Maiko, alimuangalia Tina kwa jicho la hamasa na kumwambia.
MAIKO: Wow, umeamka mrembo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Tina alikuwa na alama ya kuuliza bado.
TINA: Kwani humu nimefikaje?
MAIKO: Swali rahisi sana, umefika kama ulivyotakiwa kufika.
TINA: Ok, naomba niondoke maana ndugu zangu hawajui nilipo.
MAIKO: Hapa ndio umefika, huna pa kwenda tena.
Halafu Maiko akatoka mule chumbani, Tina akajikuta kwenye mawazo.
Patrick na Yuda wakiwa ndani ya Arusha, Patrick akaamua kumtuma Yuda aende akaangalie mazingira kwanza kabla hawajaanza kufanya jambo lolote.
Yuda akaingia kwenye himaya ya Maiko ili akaangalie kuna nini na nini, akakutana na Tulo, akamsalimia na kujifanya kama vile amerudi kazini.
YUDA: Vipi, bosi Maiko yuko wapi?
TULO: Amesafiri yeye na Mashaka.
YUDA: duh! Wameenda wapi kwani?
TULO: Wameenda Mwanza bhana.
Hiyo kauli ikamchanganya sana Yuda, akaamua kumuaga Tulo na kwenda kwa Patrick kumwambia.
PATRICK: Dah! Wale wapuuzi watakuwa wameenda kunisaka mimi Mwanza wale.
YUDA: Unajuana nao? Sasa itakuwaje?
PATRICK: Itabidi turudi Mwanza, twende tukaokoe familia huko, yale majitu hayafai.
Ikabidi waanze harakati za kurudi Mwanza.
Adamu alirudi akiwa na mawazo.
ADAMU: Pamela hapatikani kabisa kwa ile simu aliyotumia kunipigia, sijui ndo nini sasa.
FAUSTA: Mmh! Haya majanga sasa.
Ikabidi amueleze na kupotea kwa Tina.
ADAMU: Huo ni upumbavu sasa, huyo Tina nae kitu gani kimempeleka kuzurura miji asiyoijua! Sasa tutaanzia wapi kumpata jamani!
FAUSTA: Hata sijui kwakweli, yani huyu Tina huyu dah!!
Wakakaa na kujadili namna ya kumpata Tina kwani hakurudi wala hawakupata taarifa yoyote ya alipo.
Maiko na Mashaka walifurahia sana kumpata mwanamke.
MAIKO: Yule nitamfanya mke wangu.
MASHAKA: Acha ujinga wewe, mke wa nini? Hawa huwa tunawatumia tu, tukiwachoka tunatupa kulee. Hata hivyo yule binti ni mrembo pia, atatufaa kwenye kazi zetu.
MAIKO: Yani wewe kila mwanamke wa kazi, sijui hata unataka nini. Yule ni demu wangu bhana.
MASHAKA: Acha zako bhana, ukiendekeza mademu, utajikuta unafanya mambo kama ya yule mjinga Patrick, cha msingi ni kuwaepuka hawa viumbe. Dawa yao ni kuwatumia tu na kuachana nao ila ukiona ana mvuto zaidi basi tunamchukua kwa kazi bhana.
MAIKO: Ngoja nikamshughulikie kidogo basi, ana mvuto kweli yule binti.
Tina akiwa mule chumbani amejibanza tu, akaingia Maiko na kuwaamuru wale vijana wampishe kidogo.
MAIKO: Mrembo, nataka huduma kidogo.
Tina akawa anakataa kwa kutikisa kichwa, ila kukataa kwake hakukumsaidia Maiko, akaanza kumlazimisha ndio hapo varangati lilipoanza, katika kuhangaika Tina akafanikiwa kumpiga Maiko teke la chini kitu kilichofanya Maiko augulie maumivu, Tina akataka kutumia mwanya huo kutoroka ila vijana wa mlangoni wakamkamata na kumrudisha tena ndani, hapo Maiko alikuwa na hasira sana na Tina.
Akampiga ngumi nyingi nyingi hadi Tina akazimia halafu akambaka.
Alipomaliza, akatoka nje huku akijisemea.
"Eti mtoto wa kike anishinde mimi!! Nitakushikisha adabu mpenda ofa wewe."
Deborah alikuwa akijiuliza kuhusu mwanae Patrick.
DEBORAH: Hivi Tusa, Patrick alikuaga kuwa anaenda wapi?
TUSA: Hapana hajaniaga.
DEBORAH: Hivi huyu mtoto ana kichaa! Kuchukua simu yangu na kuniachia yake ndio nini jamani.
Wakati Deborah akiongea hayo Tusa akawa anajisemea kimoyomoyo "Inamaana siku zote hakujua kama amezaa chizi mmh!!"
Akajikuta akiropoka kabisa.
TUSA: Mwanao ni kichaa ndio.
DEBORAH: Unasemaje Tusa?
Tusa akawa amejiinamia chini tu.
DEBORAH: Hivi Pamela huyu mwanao ana matatizo gani?
PAMELA: Hata na mimi sielewi, ila hebu tujadili mambo ya maana kwanza. Umesema Patrick ameondoka na simu yako na kukuachia yake? Sasa akija huyo babake Tusa atatupataje?
DEBORAH: Duh! Hapo ndipo pabaya, na ubaya ni kuwa simu yake yenyewe ameiacha bila hata line mmh mtoto huyu!!
Deborah alishindwa kabisa kumtafakari mwanae Patrick na matatizo yake.
Patrick na Yuda walishaingia tena Mwanza, walianza msako wa kuwatafuta wakina Maiko kabla ya kuonwa wao kwanza haswaa Patrick.
Hapo ndipo Patrick alipoamua kumtumia Yuda kama chambo.
Katika harakati za kutafutana, Patrick na Maiko wanakutana mjini kwa kugongana vikumbo.
Walipogeukiana na kuonana ana kwa ana, kila mmoja alikuwa na ghadhabu na mwenzie.
Walipogeukiana na kuonana ana kwa ana, kila mmoja alikuwa na ghadhabu na mwenzie.
Patrick akaanza kurudi akimfata Maiko akiwa amejiaminisha kabisa, Maiko akajua hapo si mahala pema kwani aliweza kuiona vizuri hasira ya Patrick.
Ndipo Maiko alipoanza kukimbia, ila hakufika mbali akawa amepigwa mtama na Patrick, Maiko akaanguka chini.
Patrick akamnyanyua Maiko kwa nyuma na kumgeuza huku akimpiga ngumi usoni, Maiko akaona kuwa ataonekana mzembe asipo pambana na Patrick, alichofanya ni kumpiga teke Patrick. Hasira ikamzidi Patrick, akainuka na kumrukia Maiko akampiga teke ambalo Maiko alikwepa, nae akarusha ngumi ambayo Patrick aliikwepa.
Pambano likaanza sasa, walipigana sana na kuumizana ila Maiko ndiye aliyeumia zaidi, alikuwa chini na Patrick juu huku akishambuliwa kwa ngumi, akabahatika kumpiga Patrick teke sehemu za siri, hapo ndipo akapata upenyo wa kukimbilia gari lake na kuondoka.
Patrick alionekana kuwa na hasira sana hadi mishipa ya sura ilimsimama.
Mashaka akaingia kwenye kile chumba alichowekwa Tina, akamkuta Tina akiwa amelala.
Akamfata karibu na kuanza kumpapasa, Tina akashtuka na kuanza kuogopa huku akitoa mikono ya Mashaka ila hakuacha, aliendelea kumpapasa papasa Tina.
Akataka kumuingilia, Tina akawa anakataa na purukushani kati yao zikafatia, ikawa kama mtafutano wa jogoo na kuku jike.
Mashaka akaona asisumbuliwe sana na huyu binti, akaamua kutumia nguvu sasa. Naye akampiga na kumbaka.
Alipomaliza akamuangalia Tina na kumwambia "asante kwa huduma ingawa nimetumia nguvu kuipata" halafu akatoka nje.
Tina akalia sana, akajiuliza maswali mengi "yani ofa ya bia mbili ndio nafanyiwa hivi! Jamani mimi! Maskini Tina mie. Mungu nisaidie nitoke humu."
Tina akawa analia tu bila msaada wowote.
Maiko aliondoka moja kwa moja hadi kwa wenzie walipo.
Mashaka akamshangaa Maiko kuwa na damu na alama za kupigwa mwilini.
MASHAKA: Vipi tena Maiko?
MAIKO: Hivi tumekuja huku Mwanza kumtafuta Patrick au Patrick kututafuta sisi?
MASHAKA: Kivipi Maiko?
MAIKO: Nimekutana na Patrick na ndiye aliyenifanya hivi, alikuwa na hasira sana hata nashangaa kwanini amekuwa vile.
MASHAKA: Dah! Yani Patrick ndo kakufanya hivi!! Hako ka Patrick nikikapata nakanyonga kabisa, yani yeye ndo mwenye makosa halafu anatuletea hasira sisi!
MAIKO: Umeona hapo! Hata mi namshangaa, angekuwa mwingine angekimbia kuniona eti yeye ndo akanikimbilia na kuanza kupigana nami.
MASHAKA: Madai yake imemuuma sana hiyo ya Tusa, ngoja sasa tutamchinja huyo Tusa mbele ya macho yake. Nimechukizwa sana kwakweli.
Maiko alishindwa kumuelewa kabisa Patrick kuwa ana matatizo gani hadi kumvamia yeye kiasi kile.
Deborah bado aliendelea kumtafakari Patrick.
DEBORAH: Nashindwa kumuelewa mwenzenu, kaondoka kimya kimya hadi leo hajarudi.
PAMELA: Ninachowaza mimi ni kuwa, kama Adamu amefika Mwanza basi itakuwa tabu kwamaana hanipati kwenye ile simu yako.
DEBORAH: Haya majanga mbona mmh! Sijui hata tufanyaje! Au labda niende mjini kununua line.
PAMELA: Nadhani hilo litakuwa jambo la busara sana.
DEBORAH: Basi hakuna tatizo nitaenda hata leo au kesho.
Deborah akajipanga kwenda kununua namba nyingine ili aweze kuwasiliana.
Patrick akaenda alipomuacha Yuda.
PATRICK: Nimekutana na Maiko leo, bora hukuwa pamoja nami.
YUDA: Bora tena!! Wakati ndio tungesaidiana kulipa kisasi!
PATRICK: Sitaki ajue mapema hivi kama tunafahamiana, kwasasa wewe unatakiwa ufanye kazi moja.
YUDA: Kazi gani hiyo?
PATRICK: Uwasiliane na wakina Maiko ili ujue walipo, halafu uwafuate. Hapo ndio tutacheza mchezo mzuri bila ya wao kujua. Si wamejileta wenyewe kwenye mji wetu bhana.
YUDA: Na je vipi haturudi nyumbani?
PATRICK: Hakuna kurudi hadi tukamilishe hili swala kwanza.
Yuda akaanza kutambua jinsi gani Patrick anawajua wakina Maiko na kundi lake.
Mashaka akapanga mkakati na Maiko.
MASHAKA: Hakuna kubweteka Maiko, hapa tumtafute Tusa kwa gharama yoyote ile kwanza tutafaidika na pili tutamkomesha Patrick.
MAIKO: Kwahiyo tuanze na msako wa Tusa kwanza?
MASHAKA: Ndio, tuanze na Tusa.
MAIKO: Vipi kale karembo ndani kapo!
MASHAKA: Kapo ndio, kale ndio katakuwa kutuburudisha baada ya kazi.
MAIKO: Yani na wewe unakatumia!
MASHAKA: Ndio kwani kuna ubaya gani?
MAIKO: Tafuta wako bhana, hapa Mwanza wamejaa kibao. Yule mrembo niachie mimi. Tafadhari sana sitaki tuingiliane kwa warembo, nawe tafuta wako bhana.
MASHAKA: Tujadili ya maana hapa, tukianza kujadili kuhusu hao wanawake tunaweza kugombana bure mwanangu. Hebu achana nao kwanza tuwaze ya muhimu hapa.
MAIKO: Hata na yao ni muhimu, sawa bhana. Tujadili sasa namna ya kumpata Tusa.
Wakaanza kupanga mipango ya kuweza kumpata Tusa.
Adamu alishakata tamaa kabisa.
ADAMU: Hivi tutakaa hapa Mwanza hadi lini jamani?
FAUSTA: Hata sielewi, Tina ametuletea mambo jamani.
ADAMU: Yani huyo Tina angekuwepo tungesharudi Dar. Ametuchanganya kweli huyo Tina.
FAUSTA: Mdogo wangu Pamela nae ni magumashi tu, tangu tuingie Mwanza kile kinamba chake hakipatikani wala namba aliyokupigia haipatikani hata sijui anafikiria nini.
ADAMU: Kwakweli wananichanganya sana hawa watu, alianza Tusa, akaja mama yake na sasa ni Tina. Wote namba zao hazipatikani tunabaki kukadilia tu kuwa ni wazima, ila haya ni mateso kwakweli.
FAUSTA: Sasa kaka itakuwaje?
ADAMU: Kama hadi kesho mambo hayaeleweki basi turudi tu Dar tukatafute njia ya kuwapata. Hapa Mwanza hatuna makazi wala nini, kwa kifupi hapatufai, asije akapotea na mwingine bure.
Adamu akatoka tena kwenda kujaribu kuwatafuta hawa watu wa tatu kama atapata taarifa zao zozote.
Adamu akiwa mjini anashangaa kumuona mtu ambaye hakumtarajia kabisa.
Adamu akiwa mjini anashangaa kumuona mtu ambaye hakumtarajia kabisa.
Akajaribu kumtazama vizuri, akaona ni yeye na wala hata hajamfananisha. Akaona ni vyema kujificha kwani hakupanga kukutana na mtu huyo kwa muda huo.
Alikuwa ni Deborah akikazana kununua laini ya simu na kuijaribisha kwa kuiweka hewani, Adamu alijificha kabisa hadi pale Deborah alipoondoka eneo lile.
Adamu akaona hajielewi kwasasa, akaamua kurudi alipowaacha wakina Fausta.
Deborah akarudi nyumbani kwake na kumuita Pamela.
DEBORAH: Nishanunua line na nimeshaweka na vocha, unaweza kumpigia sasa huyo mumeo.
PAMELA: Kwakweli Deborah unanifanyia mambo mengi sana hadi naona aibu kwakweli.
DEBORAH: Huna sababu ya kuona aibu sasa Pamela, kama aibu ungeona kipindi kile wakati mimi nakulalamikia kuwa nahisi naibiwa mume na mwizi mwenyewe ukiwa makini kunisikiliza huku ukionyesha kusikitishwa na kilio changu.
PAMELA: Nisamehe Deborah, ilikuwa akili ya kitoto ikinisumbua.
DEBORAH: Akili ya kitoto!! Sawa sawa Pamela, ila mimi ndio nilikuwa na akili ya kikubwa na kukueleza matatizo yangu wewe mtoto Pamela.
PAMELA: Sina maana hiyo Deborah, ila mapenzi ni kama shetani anavyompitia binadamu maana unajikuta unafanya kitu ambacho hukukitarajia.
DEBORAH: Mapenzi eeh!! Mapenzi ya kupendana na mume wa mtu! Tena ni mume wa rafiki yako wa damu!! Ama kweli ni mapenzi, nadhani wewe ni mke sahihi kwa Jumanne na pia hamtojutia kamwe kitendo cha kuichanganya akili yangu. Nakubali nilifanya tukio la kusikitisha yote sababu ya mapenzi, mapenzi kwa mume na mtoto wangu. Sawa, yaliyopita si ndwele tugange yajayo mpigie mumeo ili ajue mlipo, ajue kuwa mwanamke yule mwenye roho mbaya ndiye aliyewapokea, nataka anione hapa kwa macho yake kuwa sikufa sababu nina ushuhuda mkubwa wa kuishuhudia dunia.
PAMELA: Maneno makali sana hayo Deborah mmh!!
Akachukua simu na kuanza kupiga akashangaa kuona haipatikani kumbe alikosea namba moja.
Patrick aliendelea kupanga mipango yake na Yuda.
Kama alivyopanga nae Yuda, ikabidi ampigie simu Maiko ili ajue walipo na aweze kwenda.
Yuda akafanikiwa kuongea na Maiko, halafu Maiko akamuelekeza Yuda mahali walipo huku akifurahi kuongezeka kwa jeshi lao hapo Mwanza.
YUDA: Kila kitu safi kabisa kaka, ndio nataka nianze safari ya kuwafata.
PATRICK: Ukifika huko usiwaeleze kabisa kama unanifahamu, jifanye hujui chochote. Nataka maelezo yote wakupe wao, sawa!
YUDA: Hakuna tatizo kaka, we niaminie tu. Mi nitahakikisha mambo yao yote yanakuwa wazi.
PATRICK: Wewe nenda huko halafu na mimi niandae mambo mengine hapa.
Yuda akaianza safari ya kwenda kwenye himaya ya kina Maiko.
Adamu alirudi pale hotelini akiwa na mawazo sana.
ADAMU: Huwezi amini Fausta, nimemuona Deborah akiwa mjini leo.
FAUSTA: Deborah!! Sasa ikawaje?
ADAMU: Nikajificha, sikuwa tayari kuzungumza nae kwakweli.
FAUSTA: kwanini? Au bado unamuogopa kwa alivyomtenda Vero?
ADAMU: Hapana si hivyo ila sidhani kama Deborah anaweza kuongea vizuri na mimi.
FAUSTA: Ila kumbuka alikuwa mkeo yule Adamu!
REHEMA: Na bora angebaki na huyo, si kwamba simtaki Pamela hapana ila wewe hukustahili kuishi na Pamela kama mke na mume, nyie ni kama ndugu na unaweza hata kujitafutia laana bure.
ADAMU: Lakini mama, mimi na Pamela si ndugu kivile, yeye ana wazazi wake na mimi nina wangu.
REHEMA: Ni vigumu kunielewa Adamu, ila kwa maelezo niliyopewa ni kwamba mzee Ayubu alimchukulia Pamela kama mwanae pia, halafu wewe ndo umemfanya mkeo mmh! Ila hata hivyo maji yakimwagika hayazoleki, vilevile sijaona sababu ya wewe kumkimbia huyo mkeo wa kwanza.
ADAMU: Mama, sikujiandaa kukutana nae. Yule ni mshtakiwa anaetembea huru halafu pia namuonea aibu mama yangu, jaribu kunielewa.
FAUSTA: Ila kesi yake si ilishaisha?
ADAMU: Ni kweli iliisha, muda mrefu sana umepita. Kipindi hicho alikuwa binti mdogo sana, ila sasa ni mmama kabisaa.
FAUSTA: Miaka inakwenda na watu hubadilika Adamu.
Mara simu ya Adamu ikaanza kuita, alikuwa ni Pamela baada ya kupatia namba ya simu sasa.
Adamu alifurahi sana kuongea na Pamela, halafu Pamela akawaelekeza mahali pa kwenda.
ADAMU: Mmh! Afadhari maana nishauchoka mji huu.
FAUSTA: Na mwanangu je itakuwaje?
ADAMU: Twendeni tukaonane kwanza na hawa watu wawili halafu ndio tuanze na harakati za kumtafuta Tina.
FAUSTA: Mmh! Mwanangu, sijui amekumbwa na janga gani jamani.
Sele alikuwa na mawazo mengi sana juu ya Tusa, akaamua tena kwenda kwa mamake mdogo.
SELE: Mamdogo, unajua Tusa anakuficha mambo ya Patrick, mwambie akwambie ukweli kuwa Patrick ni nani.
DEBORAH: Ukweli gani tena jamani? Eti Tusa, hebu niambie.
TUSA: Mmh! Sele! Hakuna ukweli wowote mama, mi sijui chochote.
SELE: Acha uongo Tusa, mwambie ukweli mamdogo. Mwambie kazi anayofanya Patrick.
DEBORAH: Mbona mnanichanganya sasa! Mnaniweka njia panda mjue! Eti Tusa!
TUSA: Hapana mama, mi sijui kazi ya Patrick.
DEBORAH: Utashindwa vipi kujua kazi anayofanya mumeo Tusa? Patrick ni mume wako na umeishi nae sana huko Arusha, kwanini usijue kazi yake.
TUSA: Kweli mama, sijui chochote.
SELE: Tusa sema ukweli, sema ukweli kama Patrick ni jambazi.
DEBORAH: Patrick ni nani?http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
SELE: Patrick ni jambazi mamdogo.
DEBORAH: Mungu wangu! Yani Patrick ni.... Hapana, hapana haiwezekani kabisa. Mwanangu Patrick hawezi kuwa jambazi.
Deborah akainuka pale na kwenda chumbani, hawakuelewa ameenda kufanya nini.
TUSA: Umeona Sele, unasababisha makubwa bure.
SELE: Tatizo ni wewe Tusa hupendi kuongea ukweli. Unaposema ukweli unakuwa huru, na ukweli huo utakuponya toka mikononi mwa Patrick.
TUSA: Sasa hapa umeponya au umeongeza tatizo Sele?
Wakawa wanatupiana mpira wa lawama tu. Sele alifanya hayo ili kumponya Tusa toka mikono ya Patrick.
ITAENDELEA

0 Comments