Deborah bado alikuwa na mawazo kuhusu mtoto wake.
DEBORAH: Sijui atafika lini?
SELE: Usiwe na shaka mamdogo atafika tu.
DEBORAH: Lazima atakuwa amepatwa na matatizo tu, najua Patrick hawezi kunifanyia hivi.
SELE: Hata na mimi naelewa mamdogo, tuendelee kumuomba Mungu tu amuepushe na mabalaa.
DEBORAH: Sawa mwanangu.
Sele akaamua kumuaga Deborah na kwenda kumtembelea bibi yake ambaye alikuwa ni shangazi yao na wakina Deborah.
DEBORAH: Utaenda kukaa siku ngapi huko?
SELE: Wiki moja tu mamdogo.
DEBORAH: Mmh! Mbona unaenda kukaa sana jamani? Nitakukumbuka sana.
SELE: Usijari mamdogo, nitarudi tu.
DEBORAH: Sawa basi, nakutakia safari njema.
Sele akajiandaa na kuondoka zake.
Tusa alikuwa akiumwa sana na tumbo njiani kote alikuwa akiugulia maumivu hayo, hakuweza kula wala kufanya chochote. Muda huo maumivu yalimzidia.
TUSA: Patrick, naumwa sana.
PATRICK: Vumilia tu, karibia tunafika Mwanza.
TUSA: Patrick, hata kama una roho mbaya kiasi gani nihurumie kidogo tu. Nipeleke hospitali Patrick, naumwa sana.
PATRICK: Tusa nishakwambia vumilia, mbona unakuwa huelewi wewe? Wangapi huwa wanaumwa matumbo na wanavumilia jamani!
TUSA: Tatizo Patrick huelewi ni jinsi gani naumia, hili ni tumbo la uzazi ndiomana linaniuma sana. Ungenipeleka hospitali nikapate matibabu kidogo.
PATRICK: Tafadhari Tusa, usinipigie kelele kwanza hapa nilipo nina mawazo mengi sana. Ngoja tukifika Mwanza utaenda huko hospitali ila kwasasa uwe mpole kabisa.
Tusa akabaki analia kwa yale maumivu makali ya tumbo aliyoyapata.
Pamela akazinduka na kuendelea kushangaa bila kuamini yanayomtokea.
Mashaka alipomuona Pamela kazinduka akamfata na kumuuliza.
MASHAKA: Unanikumbuka?
PAMELA: (Huku akitetemeka), hapana.
MASHAKA: Umefanana sana na mama yako wewe, yuko wapi sasa?
PAMELA: (Anashindwa kumuelewa huyu mtu amemfahamu vipi), alishakufa.
MASHAKA: Ooh!! Dada mzuri yule alikufa? Nini kilimuua?
PAMELA: Sijui ila alikufa gafla.
MASHAKA: Nikutajie aliyemuua?
PAMELA: (Akazidi kutetemeka), naogopa.
MASHAKA: Wewe na mtu mzima sasa hutakiwi kuogopa, sawa Pamela? Nimepatia eeh.
PAMELA: Ndio mimi ni Pamela.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
MASHAKA: Vizuri sana Pamela, mimi ndiye niliyemuua mama yako na sababu ilikuwa ni ndogo sana, unajua ni ipi?
PAMELA: (Alizidi kutetemeka), sijui.
MASHAKA: Kwasababu alikataa kunitajia wewe na dada yako mlipo. Unajua kwanini niliwatafuta?
Pamela hakuweza kujibu sasa ila alitetemeka zaidi na kupoteza tena fahamu.
Tusa alikuwa amepatwa na usingizi mzito na ulala, hata walipoingia Mwanza hakuweza kushtuka hadi pale aliposhtuliwa na Patrick.
PATRICK: Tusa, hatimaye tumeingia Mwanza sasa.
Tusa alikuwa ametoa macho tu bila ya kuelewa chochote.
Patrick akafikisha gari hadi nyumbani kwao, akashuka na Tusa huku amemshika mkono, akaamua apite nae mlango wa nyuma ya nyumba yao ambapo aliingia nae hadi jikoni kisha akamuacha hapo na yeye kuingia sebleni, akamkuta mama yake akiwa na mama yake mdogo Anna wakizungumza, Patrick akaita "mama"
Deborah hakuamini macho yake kumuona Patrick, akamkumbatia kwa furaha kisha Anna nae akaenda kumkumbatia Patrick, halafu Patrick akawaambia.
PATRICK: Nimekuja na surprise mama.
DEBORAH: Nini tena mwanangu?
Patrick akarudi jikoni na kumvuta Tusa mkono hadi sebleni.
Cha kushangaza, Deborah alipomuona Tusa akapatwa na mshtuko mkubwa sana, akajikuta akitokwa na machozi mengi huku akilia kwa kwikwi wote wakabaki kumshangaa Deborah.
Tusa nae akaanguka chini na kupoteza fahamu.
Tusa nae akaanguka chini na kupoteza fahamu.
Wote wakabaki wakistaajabu.
ANNA: Kwani vipi jamani! Huyu binti ana nini? Na wewe Deborah unalia nini?
DEBORAH: Nimemkumbuka mwanangu tu.
ANNA: Maana sijaelewa, wewe unalia na gafla huyu binti kazimia jamani loh!
PATRICK: Hata hivyo huyu binti ni mgonjwa.
DEBORAH: Basi tumpeleke hospitali jamani.
Wakasaidiana kumnyanyua na kutoka nae nje, kisha kumpakiza kwenye gari ya Patrick, na safari ya kwenda hospitali ikaanza.
Adamu bado hakuelewa namna ya kumpata mkewe, aliendelea kuwaza sana.
REHEMA: Punguza mawazo mwanangu, atarudi tu.
ADAMU: Kwakweli mama, simuelewi kabisa huyu mwanamke.
REHEMA: Ni vigumu kuelewa ila tambua yule ni mama, anauchungu na mwanae ndomana kamfuata.
ADAMU: Vipi wewe hukuwa na uchungu na mwanao ulipomuacha kwa mumeo? Na vipi huyo mtoto wako wa Mombasa, huna uchungu nae?
REHEMA: Laiti ungejua mwanangu, ungetambua ninavyojisikia. Nakumbuka watoto wangu mapacha wawili wa kiume tena wa kupendeza na kuvutia machoni, nikawapa majina yanayofanana na kuendana lakini wewe umebadili jina nililokupa, ilikuwa bado kidogo nikukose mwanangu.
ADAMU: Majina yapi hayo unayoyazungumzia mama?
REHEMA: Wewe nilikuita Jumanne na mwenzako nilimuita Juma.
ADAMU: Kumbe jina la Jumanne ulinipa wewe?
REHEMA: Ndio mwanangu, nilitamani siku moja ungekutana na nduguyo. Kwanini ulibadilisha jina mwanangu?
ADAMU: Nilipatwa na maswaibu, ikabidi nibadili jina. Sikutaka tena kuitwa Jumanne, nilitaka kuwa mtu mpya kabisa, mtu wa tofauti. Nikajipa jina Adamu, jina la marehemu babu.
REHEMA: Maswaibu gani yalikukumba?
ADAMU: Mama ni historia ndefu, ipo siku utajua ila yote ni kuhusiana na mke wangu wa kwanza.
Rehema nae akabaki na mawazo na kuona kuwa kuna vitu vingi sana anafichwa na mtoto wake.
Tusa alifikishwa hospitali na kuhudumiwa ipasavyo, kila kitu ni pesa na uzuri ni kuwa Patrick alikuwa na pesa.
Baada ya kuambiwa na daktari kilichomsibu mgonjwa wao, Deborah alimuita Patrick na kumsema.
DEBORAH: Mwanangu, inamaana muda wote unakuja na huyu binti ulikuwa hujui kama anavuja damu kiasi kile?
PATRICK: Mmh! Mama, nilikuwa sijui.
DEBORAH: Acha upumbavu Patrick, utaua mtoto wa watu wewe. Hujui kuwa ni khatari, mimba imetoka, damu inamwagika. Unajua mwanamke anapatwa na maumivu ya kiasi gani? Mwanangu kama ulikuwa unajua halafu ukamtizama tu hiyo ni roho mbaya tena iliyopitiliza.
PATRICK: Hapana mama, sipo hivyo. Nadhani unanijua vizuri.
Hali ya Tusa ilikuwa mbaya sana, ilionyesha kuwa alimwaga damu nyingi sana na aliishiwa damu kwahiyo ikabidi ajitolee mmoja kumchangia damu.
Deborah alijitoa ila damu yake haikuendana na Tusa, ila damu ya Patrick ndiyo damu iliyoendana nae. Ikabidi Patrick atoe damu kutokana na shinikizo la mama yake, na damu hiyo akaongezewa Tusa.
DEBORAH: Yani Patrick ulitaka kukataa kabisa kutoa damu?
PATRICK: Nilijua kuna madhara mama, hata hivyo kuna kitu kimejificha hapa.
DEBORAH: Kitu gani?
PATRICK: Nitakwambia tu mama.
Patrick hakuona sababu ya kumchangia Tusa damu, alitamani anunue damu awekewe kuliko kumchangia damu yake. Sababu kubwa ni kwavile anajua wazi kuwa hapendwi na Tusa, kwahiyo kumchangia damu aliona ni kazi bure.
Bi.Rehema nae akapatwa na maswali zaidi kwenye kichwa chake, ikabidi amuulize Fausta aliyekwenda kumuaga.
REHEMA: Unajua bado siwaelewi Pamela na mwenzie jamani!
FAUSTA: Huwaelewi nini mama?
REHEMA: Kwanini Adamu alimuacha mke wake wa kwanza? Na ilikuwaje hadi akamuoa Pamela?
FAUSTA: Mama, hata mimi namfahamu vizuri huyo mwanamke wa Adamu ila sijui walipatwa na nini hadi kuachana, ila ninachokumbuka alizaa nae mtoto mmoja.
REHEMA: Yuko wapi huyo mtoto?
FAUSTA: Kwakweli sijui chochote mama.
REHEMA: Mmh! Kazi ipo.
FAUSTA: Mama, nimekuja hapa kukuaga. Kesho alfajiri nasafiri naenda China kwenye biashara zangu.
REHEMA: Mbona mapema sana? Nitakukumbuka kweli.
FAUSTA: Usijari mama, safari hii sitakaa sana huko.
Fausta akamuaga bi.Rehema ili awahi kujiandaa na safari yake.
Pamela alipozinduka tena alikutana na macho ya Mashaka yakimtazama, Pamela akaongea kwa uoga huku akitetemeka.
PAMELA: Tafadhari naomba usinidhuru.
MASHAKA: Sina nia hiyo, ila unachotakiwa kufanya ni kuniambia dada yako Fausta yuko wapi?
PAMELA: Kwani mimi na Fausta tumefanyaje?
MASHAKA: Mama yako sikutaka kumuua ila ikatokea tu nimemuua, najutia ndio. Ila ninayemtaka ni Fausta, nikimpata kichwa chake kitakuwa mali yangu.
Pamela alihisi baridi na kutetemeka sana.
MASHAKA: Unachotakiwa kufanya Pamela ni kunitajia alipo dada yako, vijana wangu wakileta kichwa chake hapa ndipo na wewe utakuwa huru.
PAMELA: Kwani wewe ni nani? Na umetujuaje?
MASHAKA: Mimi ni ndugu wa mama yako, mimi na mama yako ni mtoto wa baba mkubwa na mdogo. Mimi ni Mashaka.
Aliposema hivyo moyo wa Pamela ulilia paaa, alihisi kuwa amesikia kitu cha ajabu ambacho hakuwahi kufikiria maishani mwake.
Tusa akasafishwa kizazi na hali yake kuwa na unafuu, Tusa alikuwa na maumivu tu moyoni mwake, tena maumivu yaliyopitiliza.
Wakaruhusiwa kurudi na mgonjwa wao nyumbani.
Deborah hakuacha kumuangalia Tusa, muda wote macho yake yalikuwa juu ya Tusa hata Tusa mwenyewe akajishtukia.
Hata walipokuwa nyumbani, Deborah aliendelea kumtazama Tusa kwa ukaribu zaidi. Deborah alijikuta akimuita Tusa.
DEBORAH: Binti!!
TUSA: Abee.
DEBORAH: Kuna kitu nataka nikwambie, kitu kilichonifanya nilie nilipokuona.
Tusa alibaki kushangaa kuwa anataka kuambiwa nini na mama yake Patrick.
Tusa alibaki kushangaa kuwa anataka kuambiwa nini na mama yake Patrick.
DEBORAH: Unaitwa Tusa, si ndio?
TUSA: Ndio naitwa Tusa.
DEBORAH: Sawa sawa nilisikia hospitali ukitajwa na Patrick, hivi uliwezaje kuolewa na mwanaume ambaye hujui ndugu zake?
Tusa kabla hajajibu akaitwa na Patrick, Deborah akamruhusu Tusa kwenda kumsikiliza Patrick.
PATRICK: Ole wako umwambie mama kuhusu Maiko, hakuna kumwambia jambo lolote la ndoa yetu. Yote nitamwambia mwenyewe, umenielewa Tusa?
TUSA: Ndio nimekuelewa.
PATRICK: Haya nenda kaendelee kuzungumza nae.
Tusa alirudi kwa Deborah akiwa amenywea sana.
DEBORAH: Una umri gani Tusa?
TUSA: Nina miaka 23.
DEBORAH: Bado binti mdogo sana, kwakweli Tusa umefanana sana na mwanangu. Isingekuwa umri wako mdogo ningesema ni wewe, mwanangu alikuwa hivyo hivyo kama wewe. Ingawa ni sura ya utoto ila alikuwa kama wewe Tusa, nadhani hata wewe sura yako haijabadilika toka utotoni.
TUSA: Ni kweli, watu wengi huniambia kuwa sibadiliki sura. Ila huyo mwanao niliyefanana nae ni nani?
Deborah alijikuta akiinuka na kwenda chumbani kwake ambako alilia kwa uchungu sana, alijikuta akitembelewa na matukio ya nyuma kwenye akili yake. Machozi mengi yalimtoka.
Pamela akiwa kwenye himaya ya Mashaka, akaweza kugundua kuwa Mashaka alikuwa ndugu yao wa aina gani.
MASHAKA: Umenikumbuka vizuri Pamela?
PAMELA: Nimekukumbuka ndio, lakini hakuna baya nililowahi kukufanyia mjomba.
MASHAKA: Ni kweli, wewe ulikuwa mpole, mkarimu na mpenda watu tena mwenye moyo wa huruma. Ulinisaidia sana nilipotoka jela ila dada yako ndiye ninayemtaka hapa, anamajivuno na maringo nahitaji kichwa chake.
PAMELA: Ila hakukufanyia baya.
MASHAKA: Nadhani hujui kitu Pamela, nilipotoroka jela nilifikia kwenu, unadhani ni nani aliyeenda kutoa taarifa polisi kuwa mimi nipo pale?
PAMELA: Sijui.
MASHAKA: Ni Fausta, yule binti ni mbaya sana. Ana roho mbaya, alikuwa ananinyima chakula ananifanyia kebehi, alikuwa ananiona kama chizi.
PAMELA: Ila hata mama yetu hakukufanyia vibaya.
MASHAKA: Sina tatizo na mama yenu, alikataa kunitajia mlipo. Namuhitaji Fausta, nina mengi sana na yeye. Mimi ni Mashaka ila si Mashaka yule ambaye mlimzoea mwanzo na kumuita mjomba chizi. Kwasasa sina masikhara wala mzaa, huwa nikitaka kitu lazima nikitimize kupona kwako ni kumtaja alipo Fausta.
PAMELA: Sawa nitawatajia ila ingebidi kwanza mnipe simu ili nimpigie nijue alipo.
Mashaka akaenda kuichukua simu ya Pamela kwa Maiko na kuiwasha.
Safari hii Maiko nae hakumuelewa Mashaka ana mpango gani.
MAIKO: Tatizo ni nini Mashaka? Mbona tangu aje huyu mama yake Tusa umekuwa kama mtu usiyejielewa?
MASHAKA: Damu za watu zinatembea kwenye akili yangu, kwakweli hii kazi ni kama uchawi ukianza kuacha hutaki.
MAIKO: Kwani ulikuwa unataka kuacha?
MASHAKA: Labda nikimpata huyo Tusa.
MAIKO: Mara nyingi nakuona ukizungumza na mama yake Tusa, kwani ni ndugu?
MASHAKA: Hapana si ndugu ila kuna vitu nahitaji toka kwake.
MAIKO: Nikajua ni ndugu, kwakweli kwa mimi nitawatesa watu wote lakini si ndugu zangu.
MASHAKA: Vizuri sana, ila kuna muda hata ndugu unapaswa kumgeuka.
MAIKO: Mmh unamaana gani?
MASHAKA: Sina maana yoyote.
Maiko amekuwa na Mashaka kwa muda mrefu sana ila hakuelewa mambo baadhi anayofichwa na Mashaka.
Patrick alipoona mama yake amekaa kwa muda chumbani, ikabidi amfate na kumkuta akilia sana.
PATRICK: Jamani mama, una nini wewe?
DEBORAH: Mwanangu, alikufa kifo cha kutisha sana. Siwezi hisia ni maumivu gani alipata, je aliliaje? Roho inaniuma kila nikikumbuka. Siwezi kumsahau mwanangu Jasmine.
PATRICK: Khaaa mama, inamaana mimi nilikuwa na dada yangu?
DEBORAH: Tena amefanana kila kitu na huyu mwanamke uliyekuja nae, hadi nahisi kuwa amefufuka na kukua gafla.
PATRICK: Mama, usilie sana kumbuka mimi nipo kwaajili yako mama yangu.
Deborah alijikuta akiinuka na kumkumbatia Patrick kwa nguvu.
DEBORAH: Ni kweli upo kwaajili yangu Patrick, na umeyafuta machozi yangu.
Akajifuta machozi na kurudi tena alipo Tusa. Kwasasa Tusa aliogopa kumuuliza chochote Deborah kwani aliona kuwa ni kumpa mateso.
Tusa akamuomba Patrick ampigie baba yake simu kuwa yupo salama ila Patrick akaona kama vile ni kujitia mashakani ukizingatia hawajaijua bado hali ya mama yake Tusa. Ila Tusa aliendelea kumsisitiza ili aweze kuongea na baba yake, mwisho wa siku Patrick akakubali.
TUSA: Mimi Tusa baba, nakutaarifu kuwa nipo salama.
ADAMU: Na mama yake je? Maana alikufata huko Arusha.
TUSA: Mi siko Arusha baba, mi niko Mwanza.
ADAMU: Mwanza?
Simu ikakatika kabla ya Tusa kujibu.
Adamu akaamua kuijaribu tena simu ya mkewe kama inapatikana.
Akashangaa inaita, alitaka kujua alipo na aweze kumtaarifu habari ya mtoto wao.
ADAMU: Uko wapi Pamela?
PAMELA: Nipo Arusha, nimepatwa na......
Akazuiliwa kusema na Mashaka.
ADAMU: Umepatwa na nini mbona husemi? Nimezungumza na Tusa.
PAMELA: Aah sawa.
Halafu akakata simu, Mashaka akachukia kwani alitaka aambiwe huyo Tusa yuko wapi halafu Pamela kaishia kusema sawa.
Mashaka akamuangalia Pamela kwa macho makali na kumlazimisha ampigie simu tena mumewe na amuulize alipo Tusa. Tamaa ya viungo vya Tusa ilishamjaa Mashaka, alivihitaji sana viungo hivyo.
Patrick ndiye aliyempokonya Tusa simu.
PATRICK: Kwanini unakuwa na akili fupi Tusa? Unataja ulipo ili iweje? Ili waje? Unadhani akibanwa atashindwa kusema? Tumia akili wewe.
TUSA: Sawa nimekuelewa.
Tusa alikuwa hawezi kubishana na Patrick kwa kipindi hiki, alikuwa anakaa kimya tu.
Mara kuna mtu akawa anagonga mlango, Patrick akaenda kufungua na mtu huyo alikuwa ni Sele.
Mara kuna mtu alikuwa anagonga mlango, Patrick akaenda kufungua na mtu huyo alikuwa ni Sele.
Patrick akafurahi sana kumuona Sele, wakakumbatiana na Patrick akamkaribisha Sele ndani, wakawa wanazungumza huku wanaingia ndani.
PATRICK: Dah ni siku nyingi sana, umerudi lini kaka?
SELE: Kitambo tu ndugu yangu, kuna matatizo yalinipata mjini mwenzio.
PATRICK: Yapi tena?
SELE: Nitakwambia tu ndugu yangu, vipi maisha maana na wewe umepotea sana.
PATRICK: Mi nipo mbona, sema niliweka maisha yangu pande za Arusha ila sasa nimerudi nyumbani.
SELE: Nimesikia umeoa kaka, vipi ndo umerudi moja kwa moja au utaenda tena Arusha?
PATRICK: Inategemea bhana, ila kweli nimeoa na nilimletea mama mke wangu ili nae amtambue. Tena alikuwa hapahapa, nadhani atakuwa chumbani sasa.
Patrick na Sele walikuwa sebleni wakizungumza, kwa kipindi hiki Tusa alikuwa anaogopa sana macho ya watu kwahiyo alipoona Patrick anaenda kufungua nae akainuka na kwenda chumbani, kwahiyo hawakumkuta pale sebleni.
SELE: Bora kaka umemleta tumjue shemeji yetu.
PATRICK: Ngoja nikamuite.
Patrick akainuka na kwenda chumbani kumuita Tusa na muda huo wakaingia ndani Deborah na Anna ambao walikuwa wametoka kidogo, nao wakafurahi kumuona Sele na wakasalimiana vizuri. Patrick nae akarudi,
PATRICK: Anakuja muda sio mrefu.
DEBORAH: Nani tena?
PATRICK: Mke wangu bhana, yupo chumbani ndo nimemuita aje amsalimie shemeji yake.
DEBORAH: Aah kumbe, loh! Umenishtua maana nilikuwa nawaza mengine hapa.
ANNA: Dada nawe mmh!!
Wakaendelea na maongezi ya hapa na pale.
Pamela akalazimishwa kumpigia simu mumewe tena na kumuuliza alipo Tusa, alipewa amri sasa na si ombi.
PAMELA: Ila mjomba bado sijaelewa, unamuhitaji mwanangu Tusa au dada yangu Fausta?
MASHAKA: nimekwambia mpigie mumeo sasa na umuulize.
PAMELA: Kwani mwanangu Tusa amekukosea nini jamani?
MASHAKA: Sihitaji mjadala, ninachotaka ni umpigie mumeo basi.
Pamela alikuwa anasita ila macho ya Mashaka yakamtisha, Pamela alitamani aongee na mumewe kwa njia ya mawazo ili asimtajie alipo Tusa.
Akapiga simu ambayo iliita bila kupokelewa, akajaribu tena na tena ila ikawa hivyohivyo, Mashaka akachukia sana.
MASHAKA: Mumeo nae ana kiburi eeh!
PAMELA: Hapana, hayupo hivyo unavyodhani.
MASHAKA: Na mbona hapokei simu?
PAMELA: Atakuwa mbali na simu.
MASHAKA: Unamtetea eeh! Haya mpigie Fausta sasa.
Pamela akashika simu na kumpigia Fausta ila hakupatikana.
PAMELA: Hapatikani.
MASHAKA: Tafuta mtu wa karibu yake umpigie na uulize alipo.
Ikabidi Pamela ampigie Tina na alifanya hivyo kwavile alijua wazi atapewa jibu kuwa Fausta kasafiri.
PAMELA: Tina, dada yangu yuko wapi?
TINA: Mamdogo, mama ameshasafiri. Vipi wewe uko wapi?
PAMELA: Nipo Arusha mwanangu, nahitaji maombi.
TINA: Vipi tena mamdogo?
Hiyo haikusikika kwani Pamela alishanyang'anywa simu na Mashaka.
PAMELA: Ila unanionea bure tu.
MASHAKA: Nitakuachia nikishajua Tusa alipo.
PAMELA: Ila Tusa ni mwanangu na mimi sijawahi kukufanyia lolote baya mjomba, unakumbuka ulipotoroka jela! Nani alikuhudumia? Nani alijua njaa yako kama sio mimi? Mbona wanipa malipo nisiyo stahili mjomba? Wewe ni ndugu yangu tu hata iweje itabaki kuwa hivyo, nihurumie basi, niache niwe huru. Mwanangu sijamuona na mateso nayapata, nionee huruma ndugu yangu.
MASHAKA: Maneno yako yananiingia vilivyo akilini mwangu, ila ngoja wakati wako bado.
Mashaka akainuka na kutoka nje huku akimuacha Pamela akiwa katika uchungu na lindi la mawazo.
Tusa akaamua kwenda huko sebleni alipoitwa, alipofika hakuamini macho yake kuiona sura ya Sele mbele yake.
Sele nae hakuamini kumuona Tusa, akajikuta akiinuka na kumfata Tusa alipo, alimshika mikono na kumuuliza,
"Tusa ni wewe"
Tusa aliitikia kwa kichwa tu, Sele alimkumbatia Tusa kwa nguvu huku akifurahi kumuona.
Wote pale sebleni walipigwa na bumbuwazi, Patrick akainuka na kuwafata.
PATRICK: Mbona sielewi? Kwani mnafahamiana?
Sele alijikuta akimuangalia Patrick kwa ghadhabu sana huku akikumbuka maneno aliyoambia na John kuwa itakuwa ni Patrick nduguye, Sele akamgeukia Patrick na kumwambia.
SELE: Huyu ni Tusa wangu.
PATRICK: Tusa wako? Wakati huyu ni mke wangu, vipi wewe?
SELE: Huyu ni wangu mimi na sio wewe Patrick.
Deborah na Anna wakausogelea mzozo.
DEBORAH: Mbona siwaelewi jamani, kwani nini Tatizo? Inamaana wote mmetembea na mwanamke mmoja au ni vipi?
Muda wote Tusa alikuwa akitokwa na machozi na baada ya dakika kadhaa akaanguka na kuzimia.
Ikabidi waache mzozo na kuanza kumuhudumia Tusa.
Maiko akaamua kumfata Pamela ili akamuhoji maswali mawili matatu kuhusu Mashaka.
MAIKO: Kwani Mashaka ni nani yako?
PAMELA: Mashaka ni mjomba angu.
MAIKO: Ni mjomba wako kabisa?
PAMELA: Ndio, yeye na mama yangu ni watoto wa baba mkubwa na mdogo kwahiyo ni kaka wa mama yetu.
MAIKO: Anataka nini kwako kwasasa?
PAMELA: Kaniambia anahitaji kichwa cha dada yangu, na kikubwa anataka nimwambie Tusa alipo.
MAIKO: Mmh! Mambo mengi ya kikatili nimefanya ila hili la sasa ni too much yani kwa ndugu kabisa duh!
PAMELA: Sasa utanisaidia?
MAIKO: Ngoja niongee na Mashaka ili nipime uzito wa maneno yako, ila dah! Ina maana Tusa nae ni ndugu?
PAMELA: Tusa ni mwanangu kwahiyo Mashaka atakuwa babu yake, hata nashangaa kwanini anamchukia mwanangu.
MAIKO: Nitakusaidia kitu dada, ila na wewe unatakiwa kunisaidia sawa?
PAMELA: Sawa niambie tu nami nitatekeleza.
MAIKO: Tulia kwanza, badae nitakufata kwaajili ya kunisaidia hicho kitu ila chunga sana usiseme Tusa alipo kabla sijakuruhusu mimi.
PAMELA: Nimekuelewa ndio.
Hata Pamela alishangaa kuongea vizuri na mtu katili kama Maiko, hakujua ni kitu gani Maiko anapanga kichwani mwake, na hakujua ataombwa kusaidia nini na Maiko ili nae apate kusaidiwa.
Tusa akiwa hospital, Deborah akaamua kumuita kwa pembeni Sele ili apate kuzungumza nae.
DEBORAH: Unajua Sele hali ya leo mmenishangaza sana, kwani na wewe huyu Tusa ni mkeo?
SELE: Hapana mamdogo ila mimi ndio nilistahili kumuoa Tusa na si Patrick.
DEBORAH: Mbona sielewi, kama wewe ndio ulipaswa kumuoa Tusa na mbona akaolewa na Patrick?
SELE: Mamdogo usitake kumtetea Patrick kwavile ni mwanao.
DEBORAH: Unanijua wazi mwanangu, huwa sina upendeleo wa namna hiyo. Hata wewe ni mwanangu pia, cha msingi unieleze ilivyokuwa na Patrick nae nitaongea nae ila kwasasa naomba nianze na wewe Sulemani.
Sele akaamua kumueleza Deborah kuanzia pale ambapo Tusa alienda Arusha kwa mara ya kwanza hadi yeye alipoteswa.
Kwakweli Deborah alihuzunika sana na hakufikiria kabisa kama Patrick anaweza kufanya kitu cha namna ile.
Mashaka alikuwa na simu ya Pamela na akaamua kujaribisha mwenyewe kumpigia mume wa Pamela.
Alipopiga sauti ya kike ikapokea, alikuwa ni bi.Rehema, alipokea kwavile ile simu iliita kwa muda mrefu na nia yake ni kutaka kuwaambia kuwa mwenye simu katoka na kuacha simu nyumbani, na alipoenda kupokea aliona ni Pamela anapiga kwahiyo hakuwa na wasiwasi wowote.
REHEMA: Hallow
MASHAKA: Mpe mwenye simu niongee nae.
Rehema alijikuta akiitikia kama mtu ambaye hajasikia vizuri na Mashaka aliendelea kumsisitiza kuwa ampe mwenye simu.
Ile sauti ilimtembelea kichwani na kugonga kama mwangwi, alijikuta akisema
"Mashaka!!"
Ile sauti ilimtembelea kichwani na kugonga kama mwangwi, alijikuta akisema,
"Mashaka!!"
Mashaka nae alijikuta akikata simu baada ya jina lake kutajwa.
Rehema akaendelea kutafakari sauti ya Mashaka.
"Mashaka na simu ya Pamela? Amemkutia wapi? Sauti ile ni yake au ni mawazo yangu?"
Alijikuta akiwaza sana bila ya kupata jibu.
Tina alimkuta bibi yao huyo akiendelea kuwaza.
TINA: Bibi una nini?
Rehema akashtuka kutoka mawazoni na kumgeukia Tina.
REHEMA: Unajua sauti ya Mashaka naijua sana!
TINA: Mashaka yupi unayemuongelea?
REHEMA: Mashaka ni ndugu yangu kabisa, Pamela kampata wapi?
TINA: Mbona sikuelewi bibi?
REHEMA: Hata na mimi mwenyewe sielewi.
Tina akabaki akimshangaa tu bibi yao huyo aliyeonyesha kuchanganyikiwa kabisa.
Mashaka baada ya kukata ile siku akajikuta nae akijiuliza maswali mengi,
"ni nani huyu aliyeijua sauti yangu na kunitaja jina? Au atakuwa Fausta!"
Akaamua kumfata tena Pamela.
MASHAKA: Yani wewe Pamela unanidanganya kuwa dada yako hayupo kumbe yupo nyumbani kwako!
PAMELA: Nilichokwambia ni kweli, dada yangu hayupo nchini.
MASHAKA: Nani anayeweza kunitambua kwa sauti nyumbani kwako zaidi yake?
PAMELA: Hata yeye hawezi kukutambua kwa sauti, hatukukaa sana na wewe hata hivyo ulituacha tukiwa mabinti wadogo.
MASHAKA: Sasa nani anayeweza kunitambua mimi?
PAMELA: Sijui ni nani.
MASHAKA: Najua unanificha, nitaenda tu nyumbani kwako na kufyeka kicha cha dada yako.
PAMELA: Tafahari usifanye hivyo.
MASHAKA: Haina msamaha hii lazima Fausta aangamie.
Pamela alikuwa akitetemeka na kumuhofia dada yake.
Tusa akapata nafuu na kuweza kuruhusiwa kurudi nyumbani.
Deborah hakutaka tena kusikia mabishano ya Sele na Patrick badala yake aliomba kukaa mwenyewe na Tusa, hakutaka tena kuona Tusa akiwa kama sehemu ya ugomvi baina ya Sele na Patrick.
Deborah akawaida dada zake ili waweze kuzungumzia mzozo uliokuwepo.
SELE: Mimi sina tatizo, ila kwakweli Patrick amenitesa sana jamani. Naumia moyoni, kaniibia Tusa wangu na pia akanipa mateso makubwa sana.
DEBORAH: Nasikia uchungu na masikitiko, yani Patrick unamdhuru nduguyo sababu ya mwanamke?
PATRICK: Hapana mama, sikutarajia iwe vile na wala sikufikiria kama Sulemani ndio Sele.
ANNA: Tofauti ya Sulemani na Sele ni nini Patrick? Mbona ni jina moja tu?
MARIUM: Hata hivyo jamani, ingawa amemtesa nduguye bila kujua ila kitendo alichofanya hakistahili kufanyiwa yeyote hata kama si ndugu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Wote walikuwa wakimshambulia Patrick kwa maneno, ambaye alikuwa ameinama tu.
DEBORAH: Kikubwa kinachonisikitisha ni kuwa Patrick ametoa wapi ukatili wa namna hiyo? Ila najua muda ambao Tusa ataamua kusema basi ataeleza mengi tusiyoyajua.
SELE: Ila mngenipa Tusa wangu niende nae mamdogo.
DEBORAH: Huyu Tusa atabaki na mimi kwasasa, si wewe wala Patrick atakayeruhusiwa kumgusa.
Waliona ukatili wa Patrick ni ule wa kumtesa Sele tu, hawakujua kuwa Patrick kuna mambo mengi makubwa kayafanya.
Wakati yote yanaongelewa, hofu ya Patrick ilikuwa sehemu moja tu yani pale Tusa atakapoamua kusema ukweli wa mambo yote.
PATRICK: Naomba mnisamehe ndugu zangu, hasa wewe hapo Sulemani, nisamehe sana kaka. Ila hata hivyo Tusa ni mke wangu, mama unavyonifanyia sio fair.
DEBORAH: Hata kama Tusa ni mkeo, ila kwasasa nitakaa nae mimi. Atalala ninapolala na atakula ninapokula, Patrick unapaswa kuniheshimu kama mama yako, nafanya hivi kwa faida yako na ya wote hapa.
MARIUM: Kwakweli hawa watoto wametudhalilisha sana, wenzao wanatafuta maendeleo eti wao wanagombania mwanamke loh!
ANNA: Deborah endelea na msimamo huo huo hadi pale Tusa atakapoamua mwenyewe.
Deborah alijua lazima kuna kitu kinachomsumbua Tusa ndiomana aliamua kuwa nae karibu ili apate kusema, Tusa hakuweza kusema chochote tangu siku alipomuona Sele na kuzimia, alijikuta machozi yakimtoka muda wote, alikumbuka mambo yote mabaya aliyofanyiwa na Patrick. Machozi tu yalionyesha jinsi gani Tusa alivyo na maumivu moyoni kwakweli Deborah alimuhurumia sana.
Mashaka akamkaba sana Pamela ili ataje mahali ambako anaishi, wazo la Mashaka ni kuwa Fausta yuko nyumbani kwa Pamela.
MASHAKA: Yani usiponitajia kwako, nitaanza kukufyeka wewe.
PAMELA: Nihurumie jamani, kwangu kuna mume wangu na mama mkwe tu, utawaumiza bure hawahusiki na chochote.
MASHAKA: Nahitaji maelekezo ya nyumbani kwako, najua huko ndio nitampata na mumeo ambae atanipa maelekezo ya alipo Tusa.
Pamela alikuwa akikataa kutoa maelekezo ya nyumbani kwake, ila Mashaka akamkaba sana na mwisho wa siku Pamela akataja ilipo nyumba yao.
MASHAKA: Na ole wako maelekezo yasiwe sahihi, nitakufyeka kichwa chako mimi mwenyewe.
Pamela alikuwa akitetemeka tu.
Sele hakuridhishwa na maamuzi ya mamake mdogo wakati anajua wazi kuwa yeye na Tusa wanapendana, akajikuta akiwaza mambo mengi sana na kubwa zaidi ni kumrudisha Tusa kwenye himaya yake.
Alimuhurumia sana Tusa kwani hakuwa Tusa yule aliyemzoea, Tusa huyu alikuwa amekonda, amenyorodoka halafu alionekana kama kupungukiwa na akili, Sele alitambua kwamba yote yatakuwa ni sababu ya mateso aliyopewa na Patrick.
Sele alijisemea,
"Lazima nifanye kitu cha kumuondoa Tusa toka mikononi mwa Patrick, huyu Patrick si mtu mzuri kwasasa. Nitamkomboa Tusa wangu tu kwani bado nampenda"
Hali ya Tusa ilikuwa ni mbaya kwa mtu yeyote aliyemuona mwanzo, akimuangalia sasa anaweza kutokwa na machozi ndomana Sele aliumia sana.
Mashaka akamfata Maiko ili ampe maelekezo aende, safari hii Maiko akagoma ila baada ya kuombwa sana na Mashaka akaamua kukubali kwenda, ambapo alitakiwa kuondoka usiku wake na ndege.
Kabla ya kuondoka, Maiko alimfata Pamela na kumwambia.
MAIKO: Bado unahitaji msaada wangu?
PAMELA: Ndio, naomba unisaidie tafadhari.
MAIKO: Hakuna tatizo, mi ndio naenda nyumbani kwako hivi ila unatakiwa unifanyie kitu kimoja tu, ila ukishindwa nitafikiria cha kukufanya.
PAMELA: Kitu gani?
MAIKO: Nataka unitajie lilipo kaburi la mama yangu mzazi.
Pamela akashtuka na kujiuliza kuwa atalijulia wapi kaburi la mtu asiyemfahamu.
Kwakweli alijiona kushindwa mtihani wa ukombozi wake na hakujua hatma yake ni nini.
Kwakweli alijiona kushindwa mtihani wa ukombozi wake na hakujua hatma yake ni nini.
Pamela akamwangalia tena Maiko na kumuuliza.
PAMELA: Nitalijulia wapi kaburi la mama yako mimi?
MAIKO: Wewe ni ndugu wa Mashaka au sio ndugu?
PAMELA: Mashaka ni ndugu yangu ndio.
MAIKO: Sasa utashindwa vipi kujua lilipo kaburi la mama yangu?
PAMELA: Siwezi kujua mimi, hata huyo mama yako simjui.
MAIKO: Mama yako wewe aliitwa nani na yuko wapi?
PAMELA: Mama yangu aliitwa Neema na ameshakufa, aliuwawa miaka ya nyuma huko.
MAIKO: Unajua kaburi lake lilipo?
PAMELA: Ndio najua.
MAIKO: Sasa kwanini hujui na kaburi la mama yangu lilipo? Nataka kuliona.
Pamela alimshangaa sana Maiko kwa kumsisitiza amwonyeshe vitu asivyovijua.
Adamu aliporudi kwake alimkuta mama yake akiwa na mawazo sana, akaamua kumuuliza.
Rehema akamueleza Adamu kuhusu sauti aliyoisikia wakati Pamela akipiga.
ADAMU: Mama, unauhakika?
REHEMA: Kabisa mwanangu nakwambia ukweli, nimeshangazwa sana na hata sielewi nini kinaendelea.
ADAMU: Au ni mawazo yako tu mama?
REHEMA: Si mawazo yangu ila ni ukweli mtupu.
Adamu akaamua kuchukua simu yake na kupiga ila iliita tu bila ya kupokelewa.
Adamu akabaki kushangaa kwanini simu haipokelewi.
ADAMU: Sasa mama hii inamaana gani?
REHEMA: Hata sielewi, tuseme Pamela kapatwa na matatizo Arusha au ni vipi? Na je huyo Mashaka amekutana nae wapi? Kama kweli ni Mashaka mbona akate simu aliposikia sauti yangu? Na je alikuwa anataka kusema nini? Inamaana nimechanganya sauti kweli? Mmh hata sielewi.
ADAMU: Sasa tutafanyaje mama?
REHEMA: Sijui mwanangu, inabidi tuchunguze na kufatilia. Mtafute tena mume wa Tusa labda tupate taarifa kidogo.
Adamu akaanza taratibu za kumtafuta Patrick hewani.
Sele hakuweza kutulia huku akijua Tusa anaumia, akaenda tena kwa mamake mdogo na safari hii akaamua tena kuishi hapo.
DEBORAH: Mbona nakuona na mabegi?
SELE: Kwani kuna ubaya mamdogo? Nimeamua kuishi tena hapa, siku ile niliondoka kwa hasira tu baada ya kurudi kwa bibi.
DEBORAH: Ila hapa hali si shwari, mbona mtanipa mawazo jamani!
SELE: Mamdogo usijari, moyo wangu umekubaliana na hali halisi kuwa Tusa kashaolewa na Patrick, ingawa nampenda Tusa ila sina la kufanya.
DEBORAH: Kama umeridhia hakuna tatizo, ila mimi bado sijaridhika hadi pale Tusa atakaposema.
SELE: Namjua Tusa mamdogo, ataongea tu ila naona sasa amechanganywa na mambo.
DEBORAH: Analia muda wote hadi huruma, sijui Patrick amemfanya nini mtoto wa watu. Amefika hapa akiwa hoi kwani mimba ilitoka.
SELE: Dah ilikuwa ni mimba yangu hiyo mamdogo.
Sele aliumia sana moyoni mwake alipogundua kuwa mimba aliyompa Tusa imetoka, laiti angejua ilitolewa na Patrick angeweza kumchukia maradufu.
Sele aliamua kuishi hapo ili aweze kufanya mpango wa kutoroka na Tusa, na safari hii alipanga kwenda nae mbali zaidi.
Mashaka hakutaka kupokea tena simu ya Pamela, kwani alijua kuwa akipokea atamshtua Fausta na kutoroka.
Mashaka akaendelea kumlazimisha Maiko aende kwenye tukio ila Maiko alionyesha kukawia kwavile alitaka apewe jibu na Pamela kwanza.
Mashaka akachukia na kuamua mwenyewe kupanga safari ya kwenda nyumbani kwa Pamela, nia yake kubwa ni kumkamata Fausta kwa mikono yake mwenyewe.
Maiko akaachiwa jukumu la kumpata Tusa, akamfata Pamela na kumuuliza.
MAIKO: Je unajua alipo binti yako?
PAMELA: Sijui chochote kwakweli.
MAIKO: Mi najua alipo.
Pamela akashtuka na kujua mwisho wa bintiye umefika.
MAIKO: Umekataa kunionyesha kaburi la mama, mimi naenda kukuonyesha binti yako halafu nitamchukua mbele ya macho yako.
PAMELA: Usinifanyie hivyo tafadhari.
MAIKO: Kesho wakati Mashaka anaenda Dar, mimi wewe na kundi langu tutakuwa Mwanza kwaajili ya Tusa.
Pamela akaogopa sana, roho ilimuua alijikuta akimlilia mtoto wake Tusa, na hakujua kwanini hawa makatili wanataka kumchukua Tusa, alijiuliza maswali mengi kuwa Tusa amewakosea nini.
PAMELA: Mwanangu hana hatia.
MAIKO: Mwanao ana tamaa ndio iliyomponza, hukusoma ile methali ya kuwa ukitaka uzuri sharti udhurike?
PAMELA: Hata kama, ila mwanangu inaonyesha ameshateseka sana.
MAIKO: Kiasi tu, hapa tunachomtakia Tusa kwa sasa ni kumuumiza moyo Patrick, ametulaghai, ametusaliti na kutudanganya kwaajili ya Tusa. Lazima Tusa arudi mikononi mwetu ili Patrick atambue umuhimu wetu, hata hivyo Tusa bado hajalipia gharama tulizotoa kama mahari yake, hata na wewe mama yake unahusika. Ila kwasasa tunayemtaka ni Tusa.
Pamela hakuelewa kitu kabisa, jioni yake Maiko na baadhi ya vijana wakajiandaa kwaajili ya safari ya kwenda Mwanza kumsaka Tusa.
Patrick nae alijikuta akijipanga kurudi Arusha ili akakabiliane na wakina Maiko na kuacha kazi rasmi kabla mama yake hajagundua chochote, muda wote Patrick alionekana yuko kwenye mihangaiko, nyumbani alionekana usiku kwa usiku, hakuna aliyejua Patrick anapanga mambo gani au anataka kufanya nini ila alijua yeye na nafsi yake tu.
Kutokana na Patrick kutokupatikana nyumbani ilimfanya Deborah kukosa muda wa kuzungumza nae na pia kuwa na mashaka na mtoto wake huyo kwani hakumuelewa kabisa anapanga vitu gani.
Patrick alikuwa na mawazo mengi kichwani ikiwemo na wazo la kumtoa Tusa mikononi mwa mama yake kwani hakuwa na uhuru nae tena ingawa alikuwa mkewe.
Mashaka aliingia ndani ya jiji akiwa na watu wake wawili aliofatana nao.
Akafata yale maelekezo aliyopewa na Pamela na kweli alifika kwenye nyumba hiyo, wale watu wawili walikaa pembeni kwanza.
Mashaka alienda yeye mwenyewe alitaka aonane macho kwa macho na Fausta.
Akagonga mlango, Rehema akiwa amebaki mwenyewe ndani akaenda kufungua.
Macho ya Mashaka yakagongana na macho ya Rehema.
Macho ya Mashaka yakagongana na macho ya Rehema, kila mmoja akamuangalia mwenzio kwa mshangao.
REHEMA: Mashaka!!
MASHAKA: Rehema, unafanya nini hapa?
Muda huo huo Rehema akamkunja Mashaka kwenye shati lake karibia na koo,
REHEMA: Namtaka mwanangu.
MASHAKA: Nisamehe Rehema, mwanao alishakufa.
REHEMA: Usinitanie Mashaka, yani bila hata aibu unathubutu kuniambia mwanao alishakufa? Namtaka mwanangu Mashaka, usinitanie hata kidogo. Namtaka hivyo hivyo hata kama alikufa.
MASHAKA: Utaniumiza bure Rehema, niachie bhana.
Huku Mashaka akijaribu kujitoa toka mikononi mwa Rehema, mwanamke huyu hakukubali aliendelea kumng'ang'ania Mashaka kwa nguvu.
REHEMA: Leo sikubali, ama zako ama zangu hadi unipe mwanangu, sijui umemtupa wapi mwanangu mwehu wewe.
Mashaka akaanza kutumia nguvu kujitoa kwa Rehema.
MASHAKA: Niachie bhana Rehema.
REHEMA: Sikuachii ng'oooo fedhuli mkubwa wewe, mjaa laana usojua vibaya.
Rehema alizidi kumng'ang'ania Mashaka, alipoona anazidiwa akaanza kupiga yowe "mwiziiiii...."
Ikabidi Mashaka amponyoke Rehema na kumuachia shati lake kabla raia hawajajaa eneo la tukio.
Patrick aliendelea na mipango yake ambayo hakuna hata mmoja aliyeielewa ndani kwani.
Siku hiyo kabla ya kuondoka akaitwa na mamaye.
DEBORAH: Patrick, hivi wewe ni mtu wa aina gani usiyejua kuaga wakati unatoka? Umejifunza wapi mambo hayo? Mbona umekuwa wa ajabu sana siku hizi mwanangu?
PATRICK: Ila nina haraka sasa.
Akaanza kuondoka, mama yake alijikuta akiongea kwa uchungu sana.
DEBORAH: Patrick hata kama unashindwa kuniheshimu kama mzazi, niheshimu kama mlezi wako basi. Umenyonya ziwa langu Patrick, laiti ungejua shida nilizopitia kwaajili yako usingethubutu kunidharau hivyo. Kumbuka mateso yangu Patrick mwanangu.
Patrick uchungu ukamshika ukizingatia ni mwanamke huyu pekee aliyekuwa faraja kwake na ndiye anayemuelewa na kumsikiliza, akajikuta akirudi na kumkumbatia mama yake.
PATRICK: Nisamehe mama, na kuanzia sasa nitajirekebisha.
DEBORAH: Sina tatizo na wewe ila usipende kuniumiza zaidi Patrick, ni sawa na kuchukua msumari wa moto kuugongelea kwenye kidonda, naumia sana mwanangu.
PATRICK: Naelewa mama, nisamehe sana.
Patrick akamuaga mama yake na kuondoka.
Adamu aliporudi kwao alishangaa kuona umati wa watu umejaa nje kwao.
ADAMU: Kuna nini mama?
REHEMA: Shetani lilivamia hapa nyumbani jamani.
ADAMU: Shetani gani?
REHEMA: Ni Mashaka, huyu ni shetani mkubwa sana. Nitaendelea kumsaka, siku nikimpata atakuwa halali yangu.
ADAMU: Kwani huyo Mashaka alikufanya nini mama?
REHEMA: Mashaka ni mdogo wake shetani, ana mambo ya kishetani kabisa. Huyu Mashaka si mtu, yani watoto wangu wawili wote wafe kwaajili yake sikubali.
ADAMU: Nieleweshe mama nikuelewe.
REHEMA: Nitakuelewesha tu mwanangu, ngoja akili yangu ikae sawa.
Rehema alikuwa na hasira sana na Mashaka, hakuweza hata kuongea vizuri.
Patrick alirudi nyumbani akiwa na mawazo tele kichwani mwake.
Kesho yake asubuhi na mapema akajiandaa kutoka, akamuita mama yake ili amuage.
PATRICK: Mama, naomba dakika tano tu nizungumze na mke wangu.
DEBORAH: Sawa hakuna tatizo.
Deborah akamruhusu Patrick kuzungumza na Tusa.
PATRICK: Tusa mke wangu, najua nitaongea hapa bila kujibiwa ila najua utaelewa nitakachosema.
Tusa alimuangalia tu Patrick bila kusema chochote.
PATRICK: Leo nakuaga kuwa kuna mahali naenda, sijawahi kukuaga hata mara moja tangu nikuoe kwavile sikuona umuhimu wa kufanya hivyo. Ila leo nimeamua kukuaga kwavile imenilazimu kufanya hivyo. Tusa, naondoka leo naenda mahali, nikirudi basi ujue nimerudi na furaha yako na nisiporudi kumbuka kusema aliyetoa ndiye aliyetwaa. Kwaheri Tusa.
Patrick akambusu Tusa kwenye paji la uso tena kwa ustaarabu. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Tusa kufanyiwa hivyo na Patrick, halafu Patrick akaondoka.
Ila kauli ya Patrick ilimshtua sana Tusa ingawa hakuelewa cha kufanya.

0 Comments