Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi Mume gaidi sehemu ya sita (06)



Maiko na kundi lake ndani ya jiji la Mwanza wakimsaka Patrick na Tusa popote pale walipo.

Swala ambalo Maiko hakulijua ni nyumba anayoishi Deborah tu, hata Patrick alimjua kwa namba za simu.

Wakiwa wanatafuta sehemu ambazo wanamashaka nazo, Maiko akapokea simu toka kwa Mashaka.

MASHAKA: Maiko nakuhitaji Arusha mara moja, kuna kazi ya haraka imejitokeza.

MAIKO: Kazi gani? Mi si ndio nipo Mwanza kumsaka Patrick na Tusa.

MASHAKA: Achana nao kwanza, njoo huku tumalize hii kazi bhana.

MAIKO: Poa poa, ngoja nicheki uwezekano wa kurudi basi.

Maiko akakata simu na kumcheki Tulo aliyekuwa na Pamela ndani ya gari.

Ila Pamela hakuwepo tena na Tulo alikuwa mwenyewe.

MAIKO: Vipi Tulo, wapi mama yake Tusa?

Tulo nae akatazama huku na kule bila kumuona.

TULO: Aah alisema anaenda kujisaidia, ameondoka na Rashidi hapa.

MAIKO: Dah nikajua tumempoteza tena.

TULO: Hapana bhana.

Wakakaa kwenye gari wakimngoja Pamela arudi na Rashidi, ila muda nao ukazidi kupita hakuonekana Pamela wala Rashidi, ikabidi Maiko na Tulo waende kumuangalia sehemu za kujisaidia, walipokaribia waliona eneo ambalo watu wamezunguka kushangaa, wakasogea kuangalia wakamuona mtu ameanguka chini, kumuangalia vizuri alikuwa ni Rashidi, ikawabidi wambebe na kwenda kumpakiza kwenye gari yao.

Wakabaki na maswali mengi juu ya nini kimetokea.


Tusa akiwa ametulia pale nyumbani kwa Deborah, akafatwa na Sele.

Sele alikuwa akitamani sana kuwa karibu na Tusa na alitamani kumsikia Tusa akiongea ila Tusa alikuwa akilia muda wote.

SELE: Usilie Tusa mpenzi wangu, kumbuka nipo mimi Sele ninayekupenda sana.

Tusa alijikuta akiongea na kumwambia Sele huku machozi yakimmiminika.

TUSA: Sikufai Sele, mimi sifai kuwa mke wako tena, sifai kuwa mke wa mtu yeyote nimeshaharibika Sele.

SELE: Tusa wangu, unaongea jamani!!

Mara Deborah akawafata,

DEBORAH: Jamani Patrick amechelewa sana na muda umeenda, inabidi tukalale Tusa.

SELE: Mamdogo, nilikuwa nafurahia kuongea kwa Tusa.

DEBORAH: Kumbe Tusa ameanza kuongea, dah ashukuriwe Mungu jamani.

Wakaongea mawili matatu halafu wakaagana na kwenda kulala, ila mawazo ya Deborah yalikuwa ni juu ya mwanae, na Tusa nae alikuwa akiwaza kauli aliyoambiwa na Patrick, kwakweli alikosa jibu.


Kulipokucha Tusa alitamani kumwambia Deborah maneno aliyoambiwa na Patrick,

TUSA: Mama kuna kitu nataka nikwambie.

DEBORAH: Hakuna tatizo, ngoja nikavae nije uniambie, maana ndio nimetoka kuoga.

Wakati Debora ameenda kuvaa mara akatokea Patrick, akamwambia Tusa.

PATRICK: Tusa, ona nilichokuletea!

Tusa akatazama na kumuona mama yake.

TUSA: Khaaa mama!!

Tusa akamfata na kumkumbatia kwa furaha.

Deborah alikuwa anatoka chumbani huku akiongea

"haya Tusa niambie"

Mara akigongana macho na Pamela.

Deborah akajikuta akisema kwa mshangao,

"Pamela!!!"


Mara akagongana macho na Pamela, Deborah alijikuta akisema kwa mshangao,

"Pamela!!!"

Pamela nae alimuangalia Deborah kwa umakini na kusema "Deborah"

Deborah akamsogelea Pamela na kumkumbatia.

DEBORAH: Karibu sana nyumbani kwangu Pamela.

PAMELA: Asante, kumbe hapa ni kwako?

Patrick na Tusa walikuwa pembeni wakiwashangaa, ikabidi Patrick aingilie kati,

PATRICK: Kwani nyie mnafahamiana?

DEBORAH: Ndio mwanangu, Pamela ni rafiki yangu kipenzi sijui umemtoa wapi?

PATRICK: Aaah mama, huyo ni mama yake Tusa.

DEBORAH: Mama yake Tusa? (akamgeukia Pamela na kumuuliza), eti Tusa ni mwanao?

PAMELA: Ndio Tusa ni mwanangu.

Deborah alijihisi kunyong'onyea gafla kwani kuna vitu vilipita katika akili yake.


Maiko na Tulo wakiwa wanaendelea kumpatia huduma Rashidi akazinduka.

Alipopumzika kidogo wakaanza kumuhoji maswali mawili matatu.

MAIKO: Kwani imekuwaje Rashidi?

RASHIDI: Hata na mi mwenyewe nashangaa jamani, nilipompeleka yule mmama chooni nilikaa nje nikimngoja atoke mara kuna mtu alikuja nyuma yangu na kunipiga utosini, kilichoendelea sijui ila nahisi ni Patrick tu.

MAIKO: Ndio atakuwa Patrick tu. Patrick anacheza na moto, ngoja turudi Arusha tukija tena huku atajua kwanini watu wananiogopa mwehu sana huyo Patrick.

TULO: Nadhani nia yake ilikuwa ni kumtorosha mama Tusa.

MAIKO: Atanitambua nawaambia, hajui ni kitu gani nilikitaka kwa mama yake na Tusa, nikimpata Patrick nitamfunza adabu na lazima nimpate tu.

Maiko alikuwa na hasira sana juu ya Patrick.


Mashaka akiwa na kijana wake mmoja aliyeitwa Yuda, ambaye alienda nae kule kwa Pamela.

Yuda alimshangaa sana Mashaka kukunjwa na mwanamke wakati anajua wazi Mashaka ni mtu katili na mwenye nguvu.

YUDA: Bosi, yule mwanamke alikushinda nini hadi ukamwachia akukunje vile?

MASHAKA: Dada yangu yule bhana, nisingeweza kumdhuru.

YUDA: Kumbe kuna ndugu zako unaowahurumia?

MASHAKA: Dah! Yani katika familia yetu amebakia peke yake, ana hasira sana na mimi yule ananishutumu kwa vifo vya ndugu zetu. Ila siwezi kumfanya chochote kwani bado ni dada yangu.

YUDA: Na huyo tuliyemfata pale naye si ndugu yako?

MASHAKA: Anaitwa Fausta, nataka nimmalize kabisa, amenitendea mabaya. Ila nitamtuma Maiko akashughulike na yule dada yangu halafu mimi nitarudi kushughulika na Fausta.

YUDA: Maiko atasaidiaje sasa?

MASHAKA: We tulia, utaona tu itakavyokuwa.

Yuda hakuelewa mipango ya Mashaka, siku zote mipango yake inakuwa ni hatarishi.


Fausta alirudi nchini kwa gafla sana bila kutegemewa.

Moja kwa moja alienda nyumbani kwa Adamu.

REHEMA: Kheee Fausta, bila taarifa?

FAUSTA: Mama, kuna jambo muhimu lililonirudisha hapa.

REHEMA: Jambo gani tena?

FAUSTA: Kuna kazi imejitokeza huko yani inalipa vizuri sana, ila kuna kitu kidogo tu kilichonirejesha huku.

REHEMA: Kitu gani hicho?

FAUSTA: Pamela mama, ila nitakaa hapa kwa siku mbili tu kumngoja.

REHEMA: Na asiporudi je?

FAUSTA: Nitajua la kufanya, ila namngoja kwanza. Namuhitaji sana kwasasa.

REHEMA: Sawa basi na mi nitasafiri kidogo, nitaenda Morogoro kutembelea kaburi la Ayubu.

FAUSTA: Sawa mama, hata mi nitakuja kabla ya kuondoka.

REHEMA: Haya, ukija ndio tutarudi wote basi. Sijui hapa atabaki nani maana Adamu kaenda Bagamoyo.

FAUSTA: Hakuna shida mama, Tina yupo.

Fausta alionekana kuwa na mawazo mengi hata Rehema hakumuelewa kabisa.


Deborah akiwa bado hajaridhishwa na ukweli kwamba Tusa ni mtoto wa Pamela.

DEBORAH: Niambie ukweli Pamela, umezaa na nani mtoto huyu?

PAMELA: Nisamehe rafiki yangu Deborah.

DEBORAH: Umezaa na Jumanne, si ndio?

PAMELA: Ndio nimezaa nae.

DEBORAH: Kumbe na wewe ni mmoja kati ya watu waliokuwa wanaombea niachane na Jumanne? Pamela rafiki yangu kumbe ndio wewe msaliti wangu! Kumbe ndio wewe mwenyewe mwizi wangu ambaye nilikuwa nakulalamikia kuwa nahisi naibiwa? Pamela, huu ndio urafiki wetu?

PAMELA: Tafadhari Debo, naomba unisamehe.

DEBORAH: Acha kwanza nitoe dukuduku langu, si wewe uliyeniambia kuwa wanaume hawaaminiki, hawana maana? Si wewe Pamela? Kumbe kubadilika kote kwa Jumanne wewe ndo chanzo? Vipi ndio unaishi nae sasa?

PAMELA: Deborah, yaliyopita si ndwele tugange yanayokuja. Nakubali kweli nilikusaliti ila haikuwa kusudio langu, naomba unisamehe.

DEBORAH: Unajua nimepitia mangapi baada ya kufukuzwa na Jumanne? Nilijua ni machangudoa wa mjini wamemshika, kumbe ni wewe rafiki yangu kipenzi? Hata siamini.

Pamela alijikuta akilia na kujutia kitendo alichofanya cha kumsaliti mwenzie na kumchukulia mumewe. Hakujua kama angekutana nae tena, alisahau kuwa milima haikutani lakini binadamu hukutana.


Maiko akiwa ndani ya Arusha, akatumwa tena na Mashaka kwaajili ya ile kazi aliyoiachia kiporo.

Kwahiyo Maiko hakutulia, akasafiri na Yuda kwenda Dar es salaam, safari hii ilikuwa ni kumteka bi.Rehema ili Mashaka akafanye kazi yake kwa urahisi zaidi.

Maiko alienda mpaka nyumbani kwa Pamela akiwa na Yuda, kwavile Maiko anajulikana ni mtu jasiri na ana uwezo wa kuongea na mtu hadi kumteka, akaenda yeye kugonga mlango wa Pamela, kwa mategemeo yao atatoka mama wa makamo ambaye ni Rehema ila safari hii alitoka Fausta, yuleyule anayetafutwa na Mashaka.

Fausta alivyofika nje alishtushwa sana kumuona mgongaji, alijikuta akisema kwa taharuki,

"Maiko!!!"


Fausta alivyofika nje alishtushwa sana kumuona mgongaji, alijikuta akisema kwa taharuki,

"Maiko!!!"

Maiko alikodoa macho kwani hakudhani kama angekutana na Fausta mahali hapo, na hakujua kuwa Fausta anayetafutwa na Mashaka ndio yuleyule anayemjua yeye.

FAUSTA: Ona ulivyokodoa macho kama fundi saa, katika wanaume ninao wachukia hapa duniani wewe unaongoza Maiko.

MAIKO: Ni haki yako kusema hayo yote uyasemayo, najua unavyoumia Fausta.

FAUSTA: Unajua maumivu ya mtoto wewe Maiko? Unajua mtoto anavyouma wakati wa kujifungua? Sikufikiria kama wewe ni gaidi kiasi kile na sikudhani kama ungenifanyia unyama ule Maiko.

MAIKO: Yote nakubali Fausta ila huu si muda muafaka wa kuzungumza hayo, napenda kukuokoa sasa.

FAUSTA: Kwenda zako huko, sipendi hata kukuona nahisi kichefuchefu. Na kama umepanga kuniua, nimalize tu sikuogopi wala nini.

Maiko akaanza kuondoka akiwa amenywea sana. Fausta aliendelea kubwabwaja maneno kama vile amemeza kanda, aliongea bila kumeza mate tena aliongea kwa hisia na hasira.

FAUSTA: Wewe Maiko sio binadamu kabisa, wewe ni mnyama tena shetani wa mashetani, narudia tena sikuogopi ukitaka kunimaliza njoo tu unimalize, wewe si gaidi bhana, njoo unimalize. Siwezi kusahau unyama uliofanya kwa mwanangu, Maiko sitakusahau wala kukusamehe hadi naingia kaburini najua ni Mungu tu ndiye atakayenilipia, mabaya uliyoyafanya kwangu hayatasahaulika kamwe. Shetani mkubwa wewe, hata sijui umetokea wapi leo.

Ingawa Maiko alikuwa ameshaondoka, Fausta hakuacha kuongea, aliongea sana na mwisho wa siku alijikuta akikaa chini na kuanza kulia, alikuwa akilia na kuomboleza.


Maiko aliondoka na Yuda, huku akiwa na mawazo mengi sana.

YUDA: Bosi, mbona siwaelewi jamani? Nilipokuja na Mashaka nae akakutana na mtu anayemfahau, leo tena na wewe, vipi tena kwani yule ni nani yako?

MAIKO: Kwakweli nilikuwa shetani sana si uongo wala utani, hata mimi maneno yake yameniingia sana. Ushetani wa Mashaka sasa ulikuwa ndani yangu, nimetesa watu wengi sana, nimeua sana, hadi sasa sina mtoto kabisa. Fausta aliwahi kuwa mwanamke wangu, ila nilimtenda vibaya sana sidhani kama anastahili adhabu ya Mashaka.

YUDA: Inamaana wakati Mashaka anakwambia kuwa anataka kumuua Fausta, wewe hukujua kama ni Fausta yule?

MAIKO: Kwakweli sikujua, na wala sikutambua kama leo ningekutana na yule mwanamke. Yuda, wewe ni mgeni kwenye kazi hizi, tukirudi Arusha nitakupeleka kwenye chumba changu maalum ukaone, hapo utaelewa kwanini yule mwanamke amesema vile.

YUDA: Sawa, na Mashaka je utamwambiaje?

MAIKO: Kuhusu Mashaka usijari, najua jinsi ya kufanya hawezi nisumbua kitu. Ila leo dah, nilikosa cha kusema mbele ya Fausta, sikujipanga kukutana nae, sikupanga kumuona dah!! Nimejikuta roho ikiniuma sana leo sijui kwanini jamani!! Siku zote huwa sijihisi kuwa na hatia, ila leo mmh!!

Maiko alionekana kuguswa sana na maneno aliyoongea Fausta.


Pamela naye alitafakari sana mambo aliyomfanyia mwenzie, alijiona kuwa na makosa makubwa sana.

PAMELA: Debo, nakubali makosa ila naomba unieleweshe kitu kimoja.

DEBORAH: Kitu gani?

PAMELA: Patrick umezaa na nani?

DEBORAH: Hayakuhusu.

PAMELA: Nauliza nikiwa na maana Debo, kama Patrick ni mtoto wa Jumanne basi Tusa atakuwa dada yake.

DEBORAH: Jumanne nilizaa nae mtoto mmoja tu ambaye ni yule Jasmine wangu aliyefanana kila kitu na Tusa, (akainama kidogo kufuta machozi), haya ya Patrick hayakuhusu, niachie mwenyewe na moyo wangu.

PAMELA: Mmh!! Kwani ulibakwa?

DEBORAH: Pamela usitake kuniudhi tafadhari, nishakwambia hayakuhusu sasa chokochoko za nini?

PAMELA: Nisamehe tafadhari, sitarudia tena.

DEBORAH: Sina sababu ya kutokukusamehe mtu kama wewe usiyejielewa, ila kumbuka kuwa chochote ulichomtendea mwingine, utarudishiwa kwa namna tofauti. Wengine husema, what goes around comes around. Mimi sikuhukumu wala nini, ila niliongea kwa hasira tu ukizingatia mapito niliyopitia ni mengi. Sina baya na wewe na wala sina sababu kubwa ya kukuchukia.

PAMELA: Asante Debo kwa msamaha wako.

DEBORAH: Ila kikubwa, nitapenda Jumanne aje kwa miguu yake mwenyewe huku Mwanza kukufata.

PAMELA: Hilo halina tatizo Debo, cha muhimu ni kuishi kwa amani.

Ingawa Deborah aliongea mengi ila kidonda chake moyoni bado kilimuuma sana.

Pamela nae hakumshangaa sana Deborah kuhusu Patrick kwani hata dada yake Fausta hakumjua mtu aliyezaa nae mtoto wake Tina.


Tina aliyekuwa ametoka kidogo, aliporudi pale kwa Adamu, akamshangaa mama yake aliyekuwa chini akilia sana, Tina akamsogelea na kumuita "mama"

Fausta aliinua macho yake na kumtazama Tina, akamkumbatia kwa nguvu huku akiendelea kububujikwa na machozi.

TINA: Una nini mama yangu?

FAUSTA: Tina mwanangu, dunia ni duara na binadamu wote hukutana humo. Leo nimetembelewa na shetani.

TINA: (Aliuliza kwa mshangao), shetani!!

FAUSTA: Ndio, shetani alikuja leo.

Tina alihisi mama yake ameanza kuchanganyikiwa kwani hakufikiria kama mtu unaweza kumuona shetani kwa macho ya kawaida.

TINA: Mama, mbona sikuelewi?

FAUSTA: Nimetembelewa na baba yako Tina, alimuua pacha wako mbele ya macho yangu. Unajua alimfanyaje?

TINA: Mmh!! Alimfanyaje mama?

FAUSTA: Alimuua, alimchukua akam....

Aliangusha kilio kikubwa kabla ya kumalizia kauli yake, alikuwa akilia sana, "mwanangu mimi, mwanangu jamani"

Tina alijikuta akilia na mama yake, alimuonea huruma sana.


Tusa alikuwa bado hajauelewa vizuri uhusiano wa mama yake na Deborah, alipokuwa akitafakari alifatwa na Sele.

SELE: Tusa, hapa ni swala moja tu.

TUSA: Swala gani?

SELE: Inatakiwa tutoroke hapa, sidhani kama hapa ni mahali sahihi pa kuishi.

TUSA: Na mama yangu je?

SELE: Mama yako hakuna tatizo Tusa, yeye yuko salama na mamdogo ila wewe hauko salama Tusa, sidhani kama Patrick ni mtu sahihi kwako.

TUSA: Kwanza futa hiyo kauli kuwa Patrick ni mtu, Patrick si mtu kabisa, Patrick hata sijui nimfananishe na mdudu gani hapa duniani. Amenifanyia mambo mabaya sana sijawahi kufikiria kama ningefanyiwa vile.

Tusa akainama na kuanza kulia, Sele akamsogelea karibu na kuanza kumbembeleza.

Patrick akarudi na kumkuta Sele akimbembeleza Tusa, Patrick akapatwa na hasira za ajabu.

Akaingia ndani bila kuwasemesha, wote wawili hawakujua ni kipi kingewapata Patrick atakapo toka nje, walichofanya ni Sele kuondoka na Tusa kwenda alipo Deborah kwani ndio mtu pekee anayesikilizwa na Patrick.


Walipofika Arusha, Maiko kama alivyomuahidi Yuda, akampatia funguo zake za chumba cha siri aende akatazame.

Yeye alienda kuzungumza na Mashaka ili aweze kuweka mambo sawa kabla Mashaka hajaamua kumdhuru Fausta.

Wakiwa katika maongezi mara Maiko alimuona Yuda akija na ghadhabu nyingi usoni.

Moja kwa moja Yuda alienda kumkaba Maiko huku akiwa na hasira kali.


Moja kwa moja Yuda alienda kumkaba Maiko huku akiwa na hasira kali.

YUDA: Kwanini umemuua baba yangu Maiko?

Maiko kabla hajajibu, alishtukia akipigwa ngumi ya sura.

YUDA: Kwanini Maiko? Kwanini umemuua baba yangu?

Maiko akapigwa ngumi nyingine na kujishtukia akiwa chini, Mashaka akaenda kumshika Yuda, nae akashindiliwa ngumu. Mashaka akapatwa na hasira ilibidi awaite vijana wake wengine kuja kumkamata Yuda, wakafanikiwa kumfunga kamba kwavile walikuwa wengi kwahiyo wakamzidi nguvu.

Mashaka alimfata Maiko pale chini,

MASHAKA: Dah! Pole sana mwanangu, hujaumia kweli?

MAIKO: Nadhani alitaka kuniua huyu.

MASHAKA: Ila imekuwaje kwani?

MAIKO: Sijui, labda kuna kitu kakiona kwenye kile chumba changu cha siri maana nilimpa funguo.

MASHAKA: Hilo ni kosa kubwa sana Maiko, unadhani tufanyeje na mtu huyu?

MAIKO: Ilimradi mmemfunga, hata msiangaike nae, niachieni mwenyewe nitajua namna ya kutatua hili tatizo.

Maiko akajua sasa ameingia kwenye matatizo mengine, ukiachana na yale ya Patrick na Tusa.


Bi.Rehema aliamua kurudi jijini baada ya kuona ukimya toka kwa Fausta.

Alipofika alimkuta Fausta akiwa amenyong'onyea sana, wakasalimiana na kuongea mawili matatu.

REHEMA: Mwanangu nini tatizo kwani?

FAUSTA: Wakati haupo mama, alikuja hapa mwanaume. Mwanaume ambaye ni gaidi, mwanaume ambaye ni shetani, mwanaume ambaye hastahili kuwepo katika jamii.

REHEMA: Mwanaume gani huyo?

FAUSTA: Mwanaume aitwaye Maiko, aliua mwanangu mbele ya macho yangu mama. Siwezi kumsahau mwanaume huyu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Fausta alianza kulia, Rehema alimbembeleza huku akiwaza moyoni kuwa huenda akawa Mashaka ila jina la Maiko lilamchanganya kwani aliona kuwa atakuwa mtu mwingine na si Mashaka.

REHEMA: Yukoje huyo mwanaume?

FAUSTA: Ukimuona unaweza sema ni mtu mstaarabu na mwenye heshima zake ila kiukweli ni shetani.

REHEMA: Au ni Mashaka?

FAUSTA: Mashaka? Hapana anaitwa Maiko, kwani Mashaka ndio nani?

REHEMA: Mashaka ni kaka yangu, ila nae ni shetani kama huyo mwanaume uliyemtaja. Kanipotezea wanangu wawili, hafai hata kuonekana. Ila yeye ukimuona unaweza kuhisi tu kuwa ana roho mbaya, msura wake kama alidumbukizwa kwenye tindi kali, macho yake kama ya mmbwa mwizi kiukweli hafai kabisa. Naye alikuja hapa wakati nyie wote hampo.

FAUSTA: Mama, basi hapa hapafai inabidi tujihadhari jamani. Kama watu wa ajabu kiasi hiki wanafika hapa basi maisha yetu yapo hatarini hasa ya mtoto wangu Tina.

REHEMA: Tufanyeje sasa?

FAUSTA: Tuhamie kwangu, nyumba hii ifungwe tu hadi pale kaka ataporudi.

REHEMA: Mmh!! Tumngoje basi siku mbili hizi arudi ndio tuhame.

Rehema nae akaanza kuingiwa na hofu mahali hapo.


Tusa akiwa mikononi mwa Deborah, Patrick alimfata mahali hapo.

PATRICK: Mama, hivi hii ni haki kweli? Yani mke wangu anakataziwa kukaa na mimi ila Sulemani anakaa nae, anambembeleza na kila kitu.

DEBORAH: Mmh! Acha jazba mwanangu, Tusa ni mkeo usiwe na hasira hivyo.

PATRICK: Mama, sipendi kumdhuru mtu ila msitake nifanye hivyo. Mwambie Sulemani acheze na vyote lakini asicheze na mke wangu, nitamuumiza.

Deborah alikuwa na wakati mgumu sana juu ya kusuluhisha hili swala.

Kwavile Tusa alikuwa kawaida sasa ikabidi amuulize,

DEBORAH: Niambie maisha ya Arusha Tusa.

TUSA: Yalikuwa kawaida tu mama.

DEBORAH: Kawaida! Kweli? Mbona unamuogopa sana Patrick? Nakuona kila muda anapokuja huwa unakosa raha, kwanini?

TUSA: Hakuna tatizo mama.

DEBORAH: Hutaki kusema sio! Mmh! Mficha maradhi kifo humuumbua, unaijua hiyo methali?

TUSA: Ndio naijua.

DEBORAH: Kwanini unanificha Tusa? Niambie ukweli, mi namjua sana Patrick, ukiniambia nitajua cha kufanya, niambie mama. Acha kuficha ficha.

Tusa aliinama na kuanza kulia, Deborah akafanya kazi ya kumbembeleza.

DEBORAH: Niambie ukweli nikusaidie mwanangu.

TUSA: Ni mambo ya aibu sana, hayafai hata kueleza.

DEBORAH: Mmh! Mambo gani hayo? Niambie tafadhari.

TUSA: Nitakwambia mama.

Akaendelea kulia tu, Deborah akatambua kuwa ni kitu kizito sana kilichomsibu Tusa, ila Deborah alitaka kujua kwa haraka ili kama ataweza kudhibiti basi adhibiti swala hilo.


Maiko akamfata Yuda kuzungumza nae.

MAIKO: Yuda Yuda, hii ni himaya ya watu wengi tena wenye uwezo mkubwa. Huwezi fanya chochote hapa, kama una roho nyepesi ni bora usingeenda kwenye kile chumba.

YUDA: Sikia Maiko, hata ingekuwa ni wewe ungeumia tu, yani kuona baba yako alichinjwa dah! Nyumbani tulizika mwili kumbe kichwa unacho wewe Maiko!! Dah, sikujua kama kazi zenu zipo hivi jamani.

MAIKO: Sikia Yuda, maji yakishamwagika hayazoleki cha msingi ni kukubaliana na matokeo na kusonga mbele.

YUDA: Poa bhana, mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu. Sawa bhana.

MAIKO: Unatakiwa kuwa mpole tu bwana Yuda.

Ikabidi Yuda awe mpole kweli ili aweze kufunguliwa na kwenda kupanga plan zingine.

YUDA: Nifungueni basi.

MAIKO: Nitakufungua endapo utaahidi kutoleta fujo tena.

YUDA: Ilikuwa hasira tu zile, haitajirudia bosi.

Vijana wa Maiko wakamfungua Yuda kama walivyoamriwa na Maiko.

Kwakweli Yuda aliumia sana na kujiapiza moyoni kuwa lazima alipe kisasi.


Adamu aliporudi nyumbani kwake akasimuliwa mikasa yote iliyowakumba mahali hapo.

ADAMU: Duh hii khatari, lazima tumdhibiti huyo Maiko jamani.

REHEMA: Na Mashaka mwanangu nae anatakiwa adhibitiwe.

ADAMU: Mama, usijali nitatuma wapelelezi waweze kuchunguza hao watu.

REHEMA: Utawezaje mwanangu?

ADAMU: Mama usijari, mimi ni khatari ila watu hawanijui tu. Nitawapata hao mabwege nazi.

FAUSTA: Itakuwa vizuri kaka, hayo majitu yatakuwa mashetani tu.

Fausta alichukizwa sana na Maiko, alitamani hata ampate amchinjilie mbali.


Mpango wa Yuda ilikuwa ni kumteketeza Maiko pamoja na Mashaka ila akajua peke yake hawezi kitu, akaamua kusafiri ili arudi kwao amuombe ndugu yake ambaye aliambiwa kuwa amesharudi, wakashirikiane kumtokomeza Maiko, Yuda alikuwa na hasira sana.

"Haiwezekani, yani tumekazana kumjua aliyemuua baba kumbe ni huyu baladhuri!! Sisi tunazika mwili halafu kichwa anacho yeye!! Lazima nimfunze adabu Maiko, na lazima nae afe tu, kama asipokufa yeye safari hii basi nitakufa mimi, dah! Maiko ni shetani sana jamani"

Yuda alijikuta akimchukia sana Maiko, alimchukia kupita maelezo.


Sele aliandaa mipango yake vizuri na moja kwa moja wazo lake lilikuwa ni kumtorosha Tusa.

Siku hiyo alilala nyumbani kwa Deborah na kama alivyopanga na Tusa, usiku wakati watu wote wamelala, Tusa akatoka na kumuacha Deborah na mama yake wakiwa wamelala na kumkuta Sele akiwa anamngoja sebleni.

Wakautumia muda huo kutoka pale ndani, wakiwa wanatokomea gizani machale yakamcheza Patrick na kujikuta akishtuka kwa nguvu.

Patrick akatoka nje na kuona watu wawili wakipotelea gizani, Patrick akapatwa na wasiwasi. Hapohapo akaamua kuwafatilia kwa nyuma ili kujua ni wakina nani.


Hapo hapo akaamua kuwafatilia kwa nyuma ili kujua ni wakina nani.

Patrick alipowanyatia karibu, moja kwa moja akagundua kuwa ni Sele na Tusa.

Jambo la kwanza alilofanya ni kumkaba Sele kwa nyuma, alipomgeuzia mbele akampiga ngumi ya sura iliyompeleka Sele hadi chini.

Sele akainuka na kupewa ngumi nyingine na hapo kuanza kupambana na Patrick.

Tusa akaona hiyo ni vita kubwa, ikabidi akimbie kuwaamsha Deborah na mama yake, kwakweli nao walishangaa kuwa imekuwaje, wakakimbilia eneo la tukio na kumkuta Patrick akimshambulia Sele kwa ngumi zisizo na idadi.

Debora alijikuta akiweka mikono kichwani,

DEBORAH: Wee Patrick wewe utamuua mwenzako.

Akawasogelea kuweza kuwaamulia, Sele nae hakukubali akampiga ngumi Patrick wakati ameshikwa na Deborah, kitendo hicho kilimkera Patrick na kutaka kuchomoka mikononi mwa mama yake huku Pamela akimuondoa Sele.

PATRICK: Niache mama, niache nimfunze adabu huyu.

DEBORAH: Sikuachi Patrick, ukitaka nipige mimi. Naomba hasira zako zote umalizie kwangu maana nadhani ndio malipo ulioamua kunipa kwa kukulea mwanangu. Nipige baba.

Patrick akajisikia vibaya kwa kilio na maneno ya mama yake, ikabidi atulie na wote wakarudi nyumbani.

Kwavile Patrick alikuwa na nguvu sana, alijikuta amemuumiza sana Sele aliyekuwa akivuja damu.

Patrick alipomuangalia nduguye huruma ilimshika akaamua kumfata na kumuomba msamaha.

PATRICK: Nisamehe ndugu yangu.

Sele alimuangalia tu Patrick bila kusema chochote, humo ndani hawakuweza kulala tena hadi kunakucha wakijadili yaliyotokea, aliyerudi kulala ni Patrick tu baada ya kumuomba msamaha Sele, ila hawakujua kama huyo Patrick amelala kweli au anapanga mipango yake.


Maiko akiwa amefatwa na Mashaka kuhusu Fausta.

MASHAKA: Unajua sikukuelewa mwanangu, umesema Fausta kafanyaje?

MAIKO: Unapenda niendelee kuwa mshirika wako?

MASHAKA: Ndio napenda tena sana Maiko.

MAIKO: Basi achana na Fausta, nakuomba swala la Fausta niachie mimi.

MASHAKA: Kivipi wakati mi nahitaji kichwa chake?

MAIKO: Unaniamini au huniamini?

MASHAKA: Nakuamini mwanangu.

MAIKO: Basi swala la Fausta niachie mimi halafu utaona.

MASHAKA: Hivi yule Yuda alipatwa na nini?

MAIKO: Jinga lile, eti aliona kichwa cha baba yake ndo linaleta fujo zake hapa. Ila lishapotezea kwa sasa.

MASHAKA: Kweli ni jinga, nadhani alikuwa hajui kazi vizuri yule. Sasa vipi kuhusu Tusa.

MAIKO: Dah! Sasa hayo ndio mambo ya kujadili bhana.

Maiko akamueleza Mashaka na jinsi walivyompoteza mama yake na Tusa.

MASHAKA: Dah! Hilo ni kosa ila sio kubwa sana. Tatizo langu sasa ni kuwa, huyu Patrick ni mtu wa aina gani hadi anaweza kucheza na hisia zetu kiasi hiki? Mwanzoni katulaghai wote akatoroka na Tusa, na sasa katoroka na Pamela. Hivi huyu Patrick ni nani haswa!!

MAIKO: Hata na mimi namshangaa.

MASHAKA: Nadhani tufanye operesheni ya kumsaka yeye kwanza, na tukimpata kichwa chake tutakitunza kama kumbukumbu.

Mashaka na Maiko wakaanza kufanya harakati za kumpata Patrick.


Kulipokucha Patrick akamfata mama yake na kuongea nae.

PATRICK: Yote haya mama umeyataka wewe, ungeniachia mke wangu isingekuwa hivi.

DEBORAH: Nitakuachia mwanangu, ila hukupaswa kumpiga mwenzio sababu ya mwanamke.

PATRICK: Yani ulitaka nimuangalie tu wakati anatoroka na mke wangu? Mama, mke anauma sana.

DEBORAH: Hata kama, ila ulichofanya hakistahili kabisa.

Patrick akamuaga mama yake na kutoka, ikabidi Deborah amuulize vizuri Tusa juu ya kilichosibu.

Tusa hakuwa na jinsi zaidi ya kusimulia yaliyotokea usiku uliopita.

DEBORAH: Niambie ukweli Tusa, unampenda Sele au Patrick?

TUSA: Kwakweli mama nampenda Sele.

DEBORAH: Sasa mbona ukaolewa na Patrick? Hukujua madhara ya kuolewa na mtu usiyempenda?

TUSA: Patrick alinilazimisha tu, kwakweli simpendi Patrick mama.

DEBORAH: Unajua sheria za ndoa Tusa? Tatizo mnaolewa mkiwa wadogo jamani, hapo ulipo hata huelewi haki yako ni ipi. Unatakiwa umuheshimu mumeo, umpende na kumjali. Sasa kama wewe humpendi Patrick, siku zote hizo umeishi nae vipi?

TUSA: Mmh! Mama ni aibu.

DEBORAH: Hata kitendo cha kutoroka na mwanaume mwingine wakati mumeo yupo ndani ni kitendo cha aibu, ni bora kuniambia ukweli wa mambo yote.

TUSA: Ila mama, niahidi kuwa utanilinda.

DEBORAH: Usijali Tusa, cha muhimu ni kuniambia ukweli tu na siku zote ukweli huweka huru.

Mara Pamela akawafata Deborah na Tusa kwenye mazungumzo yao, nia ya Pamela ni kupata mawasiliano ya nyumbani kwake ili wasiwe na hofu tena.


Adamu akiwa na familia yake wakijadili.

ADAMU: Na bora haya mambo yametokea wakati watoto wangu wale wadogo wanasoma bording, maana tungepata shida dah!

TINA: Bora kabisa mjomba walivyoenda shule za bweni maana wanavyompenda mama yao sidhani kama wangevumilia kuona hata hakuna habari kuhusu yeye.

ADAMU: Na nimefanya vizuri kweli, maana likizo wanaenda kwa shangazi yao kulekule hadi nikawachukue.

Mara simu ya Adamu ikaanza kuita, kuangalia ni namba ngeni.

PAMELA: Mimi ni Pamela mume wangu.

ADAMU: Pamela! Uko wapi wewe?

PAMELA: Nipo Mwanza na Tusa.

ADAMU: Sasa mbona hamrudi nyumbani.

PAMELA: Kuna matatizo kidogo Adamu, itabidi uje kutufata.

ADAMU: Matatizo gani tena?

PAMELA: Ukija utajua tu, ila unatakiwa uje Adamu.

ADAMU: Sawa, utanipa maelekezo basi.

PAMELA: Hakuna tatizo, ni wewe tu kunitajia kuwa lini utakuja.

Simu ilipokatika kila mmoja ndani alikuwa na hamu ya kugundua ni kitu gani kinaendelea, ikabidi Adamu awaeleze vile alivyozungumza na Pamela.

REHEMA: Inamaana utaenda mwenyewe?

ADAMU: Ndio mama.

REHEMA: Tutaenda wote mwanangu, sitaweza kukungoja hapa. Twende wote hukohuko.

TINA: Hata na mimi mjomba nataka twende wote, nimemkumbuka sana Tusa.

FAUSTA: Halafu hapa mmuache nani? Hata na mimi nitaenda huko Mwanza.

ADAMU: Hebu acheni kunichekesha jamani, mmekuwa kama watoto wadogo bhana. Kwani mama tatizo ni nini? Mi si ninaenda na kurudi nao jamani! Na wewe Tina vipi? Kama Tusa si nitarudi nae! Na wewe Fausta, huko China kwako huendi tena?

FAUSTA: Siwezi kwenda hadi nimpate Pamela, ndomana nataka twende wote huko ili niondokee huko huko.

TINA: Mjomba, mi ndo hata sibaki tutaenda wote tu.

ADAMU: Mmh!! Haya majaribu, na kule tutafikia wapi sasa?

FAUSTA: Hotelini, ila kama huwezi waambie waje wao.

ADAMU: Wamesema wana matatizo jamani, ila nitajaribu kumuelewesha Pamela kama ataelewa.

Rehema ndio hakutaka kabisa kubaki mahali hapo mwenyewe kwani alihisi Mashaka anaweza kurudi tena, na jinsi alivyokuwa na hasira nae anaweza hata akamchoma kisu na kujitafutia kesi ya mauaji bure.


Mashaka na Maiko wakaanza kuandaa vijana kwaajili ya kwenda nao kumshambulia Patrick.

MASHAKA: Patrick anaonekana kuwa ni kijana mjanja sana, inabidi tutumie ujuzi na uzoefu kwa sana kumshika.

MAIKO: Tumepata vijana wa kutosha, sidhani kama atatushinda na kipindi hiki.

MASHAKA: Mazoezi ya kutosha kwa vijana hao, hakuna kumkosa Patrick.

Wakaendelea kupanga mpango kabambe wa kumkamata Patrick, ila hawakujua kuwa Patrick nae ana mipango yake jijini Mwanza.

INAEDELEA

Post a Comment

0 Comments