Rehema aliumia sana kama mzazi wa Maiko alijihisi kuwa na mkosi kama mama wa Maiko hakujua cha kufanya kuweza kuvumiliana na ile hali halisi iliyokuwepo.
DEBORAH: Jamani hii ni khatari sana, tutafanyaje sasa?
REHEMA: Tufanye kama alichosema kwenye barua yake tu.
Adamu na Pamela walishindwa hata kuelewa cha kufanya.
MARIUM: Tusikawie jamani, hali ya huku si shwari kabisa.
Kwa waliokuwepo pale mwenye nguvu ya kufanya chochote alikuwa ni Yuda tu.
Tina na Tusa hawakwenda Arusha, Tusa hakutaka kabisa kukanyaga mji wa Arusha na pia hawakuweza kukaa nyumbani kwa Deborah kwa kuogopa kutokew na Maiko. Wao waliondoka na Sele na kwenda kukaa nyumbani kwa Marium.
TUSA: Sidhani kama mama yangu ana roho mbaya kiasi hiko cha kutupa mtoto.
TINA: Hata mimi sifikirii kama mama yangu anaweza kufanya hivyo.
TUSA: Sasa Patrick ni mtoto wa nani?
TINA: Mimi nadhani mama yake Patrick amesahau tu ila mama zetu hawawezi bhana kutupa mtoto. Hawana roho mbaya kiasi hiko.
TUSA: Na mbona walikuwa wanalia sasa?
Sele akaingilia mazungumzo yao.
SELE: Jamani yote yanawezekana ngoja tuwasubiri warudi waje kutuambia ukweli wote.
Sele alitulia sana tangu amesikia stori nzima kuhusu Patrick. Alikuwa anangoja kujua hatma ya Patrick na Tusa itakuwa ni nini.
Patrick nae hakwenda Arusha alijifungia ndani tu, hakutaka kufanya chochote ingawa mama yake alimsihi sana aende nao.
Patrick akaenda dukani na kuchukua sumu ili ajimalize, kabla hajafanya hivyo mzimu wa mzee Ayubu ukamtokea Patrick na kumsihi asifanye vile.
Mwita nae mawazo yalimjaa sana kwani hakujua cha kufanya, stori ya Maiko ilimpelekea kuamini kuwa Patrick anahusika na vifo vya wale wajeshi kwani aina ya uuaji ilifanana na aina ya uuaji aliokuwa akiufanya Maiko.
Akimfikiria Tulo nae ambaye pia ni ndugu yake alikosa jibu kabisa ya nini cha kufany ukizingatia yeye ni usalama wa Taifa. kauli ya Maiko nayo ilimrudia mara kwa mara kuwa wasimuhukumu Patrick.
Deborah aliwaambia kuwa wanatakiwa kuharakisha kwani wameacha watu wengi muhimu huko nyumbani.
Wakaamua mwili wa Maiko na Mashaka wauingize ndani ya ile nyumba na waichome moto nyumba yote.
Wakasaidiana na baadhi ya watu kufanya hivyo, hakuna aliyetaka chochote toka kwenye nyumba ya Maiko.
Viungo vya binadamu viliwatisha sana mule ndani na hapo wakaamini wote kuwa Maiko alikuwa gaidi.
Walitoa begi moja ndogo yenye mafaili toka kwenye ile nyumba kisha wakaimwagia petroli na kuichima, kwavile ilikuwa mbakli kidogo na maeneo ya watu haikuwapa shida sana kuichoma.
Wakati wanaichoma walisimama mbali kabisa, mara gafla ukasikika mlio mkubwa kama bomu.
Wakati wanaichoma ile nyumba ya Maiko, walisimama mbali kabisa. Mara gafla ukasikika mlio mkubwa kama bomu.
Wote wakaogopa na kutetemeka kwa hofu, moshi mzito ukawa unatoka pale kwenye ile nyumba na gafla mvua ikaanza kunyesha na kuwafanya wakimbie hovyohovyo kutafuta sehemu ya kujificha.
Ubaya wa eneo lenyewe lilikuwa mbali na maeneo ya watu wengine.
Mvua ilikuwa ni kubwa sana, wakabahatika kupata usafiri uliowasogeza kwenye nyumba kidogo ya jirani na pale.
Pale kwenye ile nyumba walikutana na majirani wa Maiko, ambao walishangaa sana kuelezewa kuwa Maiko amekufa tena kwa kujiua. Hawakuelewa kwanini tajiri mkubwa kama Maiko kujiua.
Na walivyoambiwa kuwa ile sauti ya bomu ilitokea nyumbani kwa Maiko napo walishangaa sana na kujiuliza je ni kitu gani, wengine wakajaribu kueleza kuwa kwavile wamechoma ile nyumba na miili ya watu ikiwa mule ndani kwahiyo huenda ile sauti ya kama bomu ni kupasuka kwa kichwa, ikabidi waamini vile wanavyoambiwa.
Mvua nayo ilizidi kunyesha eneo lile bila hata ya kukatika.
Hali ya Patrick haikuwa nzuri bado, Patrick alikuwa anaumizwa sana kwa kuujua ukweli kuwa Deborah si mama yake mzazi, hakutaka kabisa kuamini na kukubaliana na ukweli huo.
Alitamani hata ukweli huo ugeuzwe, hakutamani kuujua ukweli wa namna ile maishani mwake, mzimu wa mzee Ayubu nao haukuacha kuwa karibu yake.
Ulikuwa ukimtazama tu na kuendelea kumsihi kuwa asijidhuru.
"usijiumize Patrick wala usijidhuru, ukweli humuweka mtu huru. Kubaliana na ukweli na usijipe mawazo sana kwa yaliyopita, yaache yapite na mengine mapya yaje. Mimi ni babu yako Patrick"
Sauti ile ya mtu asiyeonekana ilizidi kumliza Patrick, uelekeo wote wa Patrick ulipotea kwani hakuwa kama vile alivyotegemea.
Mvua ilipokatika, bi.Rehema alitoa wazo la kwenda kutazama lile eneo la tukio ila Deborah alipinga na kuwaambia kuwa warudi tu Mwanza kwani hata yeye hakutaka tena kuendelea kuwepo kule Arusha.
AMINA: Nakubaliana na wazo la Deborah, bora turudi Mwanza kuliko kwenda kutazama nyumba ya Maiko huwezi jua ni kitu gani kitatupata tena huko ukizingatia nyumba yenyewe ilikuwa na majini.
FAUSTA: Hata mimi sioni umuhimu wa kwenda kuitazama, tuondokeni tu.
Wakakubaliana kuondoka ila bi.Rehema hakuafikiana nao kabisa.
Alitamani kuona yaliyojiri kwenye nyumba ya mtoto wake, ila hakuwa na la kufanya zaidi ya kufatilizana na wakina Deborah kuwa waende stendi na kuondoka kurudi Mwanza.
Walipokuwa stendi kwaajili ya kuondoka bado roho ya bi.Rehema haikukubali kabisa, alitamani kuona hata majivu yaliyobaki kwenye nyumba ya mwanae, akawaomba na kuwasihi sana. Ikabidi Adamu akubali kumpeleka tena mama yake kupaona nyumbani kwa Maiko na kwavile Yuda ndio anayepajua vizuri ilibidi yeye akubali kuwasindikiza ila Deborah na wenzie wakagoma kurudi na kuamua kwenda zao Mwanza.
Wakati wao wakisafiri kwenda Mwanza, bi.Rehema, Adamu na Yuda walipanga kwenda kwa Maiko kesho yake.
Nia kubwa ya bi.Rehema ni kuona tu jinsi nyumba ya mwanae ilivyoteketea na jinsi mwanae alivyoangamia.
Walipotua Mwanza, Deborah hakutaka kupoteza muda aliwaomba wote na kuamua kwenda moja kwa moja nyumbani kwake kumuangalia Patrick.
Walipofika Patrick alikuwa chumbani ikabidi Deborah amfate na alimkuta Patrick akiwa na hali mbaya sana, hali ya kutokujielewa kabisa.
Deborah alimfata mwanae na kumkumbatia sana.
DEBORAH: Haijalishi mambo yote yaliyotokea, wewe Patrick utaendelea kuwa mtoto wangu mpendwa na wa pekee.
PATRICK: (Akiongea kwa uchungu), kwanini mama? Kwanini mimi nisiwe mwanao wa kiukweli? Nakupenda mama na siwezi kumpenda mama yeyote kama ninavyokupenda wewe.
DEBORAH: Naelewa mwanangu Patrick ila una haki ya kujua ukweli kuhusu wazazi wako. Ni kweli mimi nimekulea na kukunyonyesha ila si mimi niliyekubeba miezi tisa Patrick.
PATRICK: Na kwanini nilitupwa?
DEBORAH: Tulia mwanangu, ukweli wote utaujua.
Wakiwa pale nyumbani kwa Deborah, Fausta na Pamela walijikuta wakikumbuka tena yaliyopita na kuanza tena kulia.
Deborah alitoka na kuwafata,
DEBORAH: Kulia hakuta wasaidia cha muhimu muwe wazi, Patrick ni mtoto wa nani kati yenu ili naye apate kuwajua ndugu zake.
Walikuwa wakitazamana na kushindwa hata kusema.
Tusa na Tina waliposikia wazazi wao wamerudi, nao wakajipanga kwenda nyumbani kwa Deborah lengo lao ni kuujua ukweli na kutambua hatma ya Tusa na Patrick itakuwa ni nini ukizingatia na ndoa ambayo walishafunga.
Mwita alienda polisi kuzungumza na Tulo, na kumtolea dhamana ya kutoka huku kesi ikiendelea.
Tulo hakuelewa kuwa kwanini amepewa dhamana ya kutoka pale polisi tena dhamana hiyo kutolewa na Mwita, wakati ni mtu aliyemgeuka na kumkamata na kumpeleka polisi, hakujua ni kitu gani kilibadilisha moyo wa Mwita.
Kesho yake Mwita na Tulo walienda nyumbani kwa Deborah na Tulo alifurahi sana kumuona mama yake, hata Amina nae alifurahi kumuona mtoto wake.
Wakamueleza Tulo kila kitu kilichotokea, ila walipomwambia kuwa kuna watu wamerudi kuitazama nyumba ya Maiko alishtuka sana na kusema wapigiwe simu na kuzuiliwa, wote wakashangaa ni kwanini.
Bi.Rehema, Adamu na Yuda wakaenda kutazama nyumba iliyoungua, kufika pale wote wakapigwa na mshangao kuona ile nyumba ikiwa nzima kabisa.
Haikuungua hata nyasi, hakuna aliyeamini kati yao wakati waliiona ikiungua.
Hakuna aliyeamini kati yao wakati waliiona ikiungua.
Kila mmoja alikuwa akishangaa na kubaki wanatazamana tu.
REHEMA: Jamani, hiyo nyumba si tumeiacha inaungua?
ADAMU: Ndio, na moshi mkali ulitoka na kusababisha mvua kubwa.
YUDA: Haya ni mauzauza jamani, tuondokeni tu.
REHEMA: Hapana tusiondoke, tunatakiwa kwenda kushuhudia humo ndani kuna vitu gani kwa sasa.
ADAMU: Hapana mama, hiyo nyuma ni ya maajabu.
REHEMA: Hapana huwezi jua bhana, labda ile mvua iliuzima ule moto sidhani kama kuna miujiza ya namna hii.
YUDA: Kama nyie mnaenda kuingia nendeni ila mimi hapana kabisa, siwezi kuingia nyumba ya maajabu kama hiyo.
Yuda alipinga kabisa, hakutaka kwenda kuingia kwenye nyumba ya Maiko ila bi.Rehema aliendelea kusisitiza kuwa anataka kwenda kuangalia ndani kama kuna vile vitu walivyoviacha mwanzoni, walimpinga sana ila aling'ang'ania ikabidi Adamu aamue kumsindikiza mama yake ndani ya nyumba ya Maiko.
Wakaondoka pale na kumuacha Yuda akiwa amesimama pale pale akiwatizama.
Wakati wanakaribia kuingia kwenye ile nyumba mara simu ya Adamu ikaanza kuita na kumfanya Adamu asimame na kuisikiliza, mwanzoni aliongea na Pamela ila badae alipewa Tulo ili kuwaeleza vizuri.
TULO: Nasikia mnataka kwenda kuitazama nyumba ya Maiko mliyoichoma. Tafadhari msiende.
ADAMU: Umeshachelewa tayari, ndio tupo huku.
TULO: (Akashtuka), mmepakutaje?
ADAMU: Tumeikuta nyumba ya Maiko ipo vile vile hata haijaungua.
TULO: Basi rudini tafadhari.
ADAMU: Tunataka kwenda kuona ndani kuna nini.
TULO: Msithubutu tafadhari, hayo ni mauzauza jamani. Rudini tu tafadhari. Hiyo sio nyumba ni mauzauza tu.
Ile simu ikakatika, Adamu akamtazama mama yake kwa makini aliyekuwa anajiandaa kuingia ndani.
Akamfata na kumshika mkono kisha akamvuta,
ADAMU: Tafadhari mama tuondoke mahali hapa.
REHEMA: Kwanini Adamu, hutaki kuona mwenzio anapatwa na nini humo ndani?
ADAMU: Mama kumbuka kuwa Maiko ni marehemu tayari hatuko nae tena. Hiyo si nyumba mama ni mauzauza tu.
REHEMA: Msinichanganye jamani, mi sioni kama ni mauza uza wala nini. Kama hutaki kwenda niache niende mwenyewe.
Adamu hakumuachia mama yake kwani alijua akimuachia lazima ataenda tu.
Bi.Rehema nae alizidi kung'ang'ania kwenda ila Adamu akazidi kumzuia huku akimvuta waondoke, Yuda kuona vile ikabidi nae asogee ili kusaidiana na Adamu katika kumvuta bi.Rehema.
Alipofika pale, mara gafla ukatokea mlipuko mkubwa sana toka kwenye nyumba ya Maiko na kuwafanya wale watatu wote kutupiwa mbali kabisa.
Nyumbani kwa Deborah bado walitaka kujua kuwa Tulo kwanini ameshtuka sana kusikia habari ya kwa Maiko haswa swala la wakina Adamu kurudi kuangalia ile nyumba.
AMINA: Kwanza mwanangu, huyo Maiko alikupatia wapi na ulimjulia wapi?
DEBORAH: Na pia alijuaje kama nyumba ile ina mambo ya ajabu?
TULO: Si mimi tu ninaejua hili nadhani hata Patrick analijua hili. Ila mimi nimekuwa msiri wa Maiko kwa kipindi kirefu sana, hata anapoondoka pale kwake ni mimi ndiye aliyekuwa ananiacha.
AMINA: Ndio useme huyo Maiko anakujuaje wewe? Kwakweli bado napigwa na mshangao sana tena sana.
TULO: Lazima mshangae ila Maiko huwa akidhamiria kitu lazima afanikiwe. Nitawaeleza mahusiano yangu na Maiko yalikuwaje na kwanini nimewakataza wale kwenda kule.
Muda huo na wakina Tusa nao wakawasili na kuwakumbatia wazazi wote ila wote walisikitika kwa yale waliyoambiwa kuwa kule Arusha wamewaacha ndugu zao wengine ambao hawajulikani kama watafika salama.
Yuda ndiye aliyekuwa wa kwanza kushtuka, kuangalia pembeni anamuona bi.Rehema na Adamu wakiwa hawajitambui kabisa, alisogea na kumshtua Adamu ambaye hakukawia kushtuka.
Na kuanza kumshtua bi.Rehema ila ilikuwa ngumu sana kushtuka kwani alikuwa hoi zaidi, wakaamua kumbeba na kuanza kujikongoja ili wafike japo barabarani kupata usafiri wa kurudi.
Tulo aliwakalisha wote ili kuwaeleza alivyofahamiana na Maiko na jinsi gani alikuwa mtu wake wa karibu.
TULO: Sikutakiwa kutoa siri hii ila nitaitoa kuyakomboa maisha ya ndugu zangu waliopo huko Arusha.
PAMELA: Inamaana wamepatwa na matatizo?
TULO: Inawezekana, kwajinsi walivyonieleza inawezekana kabisa wamepatwa na matatizo ila siri hii itaweza kuwakomboa.
DEBORAH: Tueleze basi hiyo siri.
Tulo akaanza kwa kuwaelezea namna alivyofahamiana na Maiko.
"Ilikuwa ni Dar es salaam, kwa mara ya kwanza nilionana na Maiko nikiwa ufukweni, eneo maharufu kabisa lijulikanalo kama Coco beach, kwa mimi nilijua kuwa ile ndio mara yangu ya kwanza kufahamiana nae ila yeye aliniambia kuwa ile ni mara ya pili kwa mimi na yeye kuonana na kusema kuwa amenifahamu mimi tangia mdogo na amewahi kumwambia mama yangu kuwa anatamani siku moja afanye kazi na mimi.
Nilimshangaa sana, ila sikupinga alinikaribisha kufanya nae kazi ambayo alisema itakuwa na kipato kikubwa sana.
Nilijiuliza sana aina ya kazi ila sikujari sana kwavile nilisikia kuwa ina kipato kikubwa.
Nikazoeana sana na Maiko na kuamua kumuaga shangazi kisha nikatokomea Arusha, kazi za Maiko lazima ule kiapo na kiapo anachokulisha anakuwa na maana kubwa sana, kwavile nilitaka pesa sikuwa na maswali mengi.
Maiko akaniweka kama msiri wake namba moja na hapo ndipo nilipogundua siri kubwa sana iliyojificha kwa Maiko"
Wakati Tulo akielezea hayo, Yuda na Adamu huku wakiwa wamembeba bi.Rehema walifanikiwa kufika kwenye barabara, wakaona gara likija na wakalisimamisha ili wafike mjini.
Gari likasimama na wakapanda, ile kumtazama dereva wakapambana na sura ya Maiko.
Gari likasimama na wakapanda, ile kumtazama dereva wakapambana na sura ya Maiko.
Wakapatwa na mshtuko mkubwa sana huku ile sura ikiwachekea, walitamani kuteremka ila walishindwa kwakuwa gari lilikuwa kwenye mwenye.
Adamu na Yuda hawakutambua kabisa cha kufanya, bora bi.Rehema aliyekuwa bado amezimia.
Wakiwa ndani ya lile gari, likafika mahari na kusimama na gafla lile gari likapotea na kujikuta wote wakiwa nje bila hata ya kushuka. Walikuwa mbele ya nyumba ya Maiko.
Hakuna aliyeamini lile tukio kati yao, mara gafla bi.Rehema nae akazinduka na kuwaona Yuda na Adamu wakiwa kwenye mshangao na mshtuko wa hali ya juu. Akabaki akiwashangaa, kuangalia mbele anamuona mtu kasimama mbele yao, bi.Rehema hakuamini macho yake akayafikicha sana na kutazama tena akamuona ni mwanae Maiko tena Maiko yule yule aliyejiua mbele yao na kukaa monchwari karibia wiki nzima kwa uchunguzi leo hii yupo mbele yao tena akiwa mzima kabisa.
Bi.Rehema alijikuta akiropoka,
"Hivi naota au ni kweli jamani?"
Wote wakakaa kimya kuona atakachofanya Maiko pale mbele yao.
Ndani ya nyumba ya Deborah waliendelea kusikiliza maelezo ya Tulo kuhusu Maiko.
DEBORAH: Ndio useme hiyo siri basi maana hatujui huko wapo kwenye hali gani ili kama kuna uwezo wa kuwasaidia tuwasaidie.
PAMELA: Kweli kabisa Tulo, endelea kutueleza ili tujue la kufanya.
Tulo akaendelea kuwaeleza habari za Maiko.
"Ukianza kazi kwa Maiko lazima ule kiapo, kiapo cha kutokutoa siri wala kukiuka malengo ya kazi yake. Kiapo ambacho unalishwa na Maiko kinakufanya uwe mtumwa wake na mara nyingi unafanya kitu anachotaka yeye na sio unachotaka wewe.
Mimi pia nililishwa hicho kiapo na nikawa mfanyakazi wake hodari na shupavu, nimefanya kazi nyingi kwa Maiko kama vile kusambaza madawa ya kulevya na viungo vya watu.
Katika hali ya kawaida ya ubinadamu lazima mtu utaogopa kusambaza vitu kama viungo vya binadamu ila kiapo cha Maiko kinakupa ujasiri na kukuondoa uoga kabisa.
Mashaka alikuwa mtu wa karibu sana na Maiko, yeye alikuwa akichukua viungo vya binadamu na kupeleka nje ya nchi na akirudi huko anakuja na pesa nyingi sana na kuchukua mzigo mwingine, kwakweli hadi leo sijui huwa wanafanyia nini viungo vya binadamu ingawa nimefanya nao kazi kwa muda wa kutosha tu.
Mara nyingi Mashaka ndio alikuwa anatoa oda ya kuua watu wa aina flani na kuchukua viungo vyao ila Maiko akienda kuua mtu ujue ana kisasi nae na atabeba kichwa na kukitunza ndani ya nyumba yake.
Unaweza ukamuona mtu anamuonekano ambao si wa kawaida na wengine labda ana macho makubwa sana au madogo sana, kama umeongozana na Mashaka basi atakupa oda muda huohuo kuwa anayataka macho ya yule mtu, tunachofanya ni kuwaambia vijana wakatekeleze kazi hiyo. Ndiomana Mashaka alipomuona Tusa alitoa oda mapema ya kuhitaji vitu vya mwilini mwake maana alikuwa tofauti kidogo na wengine.
Siri kubwa ya Maiko ni majini aliyoyahifadhi ndani ya nyumba yake, siri hii ni mimi pekee ndiye aliyenieleza na kunitaka niitunze nami nikamuahidi kufanya hivyo.
Maiko aliniambia kuwa aliyapata majini hayo alipokuwa Mombasa kule ufukweni ndipo alikutana nayo na yakamuahidi kumtajirisha atakavyo na kumfanyia chochote atakacho ila tu anatakiwa kuwasikiliza wanachotaka.
Maiko alianza kutajirika taratibu huku Mashaka akisaidiana nae.
Mashaka alimsaidia Maiko kutoka Mombasa na wakaanza kusafiri wote ila yale majini hayakupenda Maiko asafiri safiri mara kwa mara nje ya nchi ndipo yakamtafutia sehemu ya kuishi kule Arusha, ukiangalia ile nyumba ya Maiko ilivyokubwa na muda ambao Maiko ametumia kuijenga huwezi kufikiria hata kidogo kama inawezekana ila aliwezeshwa na yale majini.
Wakati Maiko akiishi Arusha, yale majini yalipendelea sana damu kitu kilichomfanya Maiko kuchinja ng'ombe mkubwa kila baada ya miezi mitatu kama kafara yake kwa majini hayo, haikuwa kazi kubwa kwavile Maiko ni mtu mwenye pesa tofauti na watu wengine ambao hawana pesa.
Kulikuwa na chumba maalum kwaajili ya kuchinjia ng'ombe hao.
Kiukweli wakati ananieleza kuwa ile nyumba ina majini niliogopa sana, hata kulala niliogopa ila badae nikazoea.
Majini yale yalimpa Maiko sharti moja kubwa sana kwa Maiko ila ni dogo kulingana na hali ya kawaida tena ni sharti zuri sana.
Maiko alipewa sharti la kutokuthubutu kumdhuru baba yake mzazi.
Aliponiambia hilo sharti nilimwambia ni sharti dogo sana ukizingatia babake anaishi nae vizuri hapo nilijua Mashaka ndiye mzazi wake.
Maiko akaniambia kuwa Mashaka si baba yake mzazi ila nisimwambie Mashaka na kwa kifupi alikuwa hamjui baba yake mzazi si kwa jina wala sura, aliniambia anamjua mama yake tu ambaye alimuona zamani sana hata hivyo mamake huyo amekwisha kufa.
Maiko aliona lile sharti kuwa gumu sana kwake, hivyo basi alitoa oda kuwa tukimuona mtu kafanana nae tumpe taarifa huenda akawa baba yake ili awe huru na kazi yake.
Viungo vya binadamu ambavyo Maiko alikuwa anahifadhi ndani kwake alikuwa anayahifadhia majini yake.
Majini yale yalimwambia kuwa akikiuka hilo sharti atajiharibia sana kwani mambo yake mengi yataharibika na mtu asiyemtarajia atamgeuka na nguvu zake zitapungua hataweza kumdhibiti mtu yeyote yule tena na atakosa mwelekeo wa maisha, biashara zake zitayumba, siri zake zitafichuka na maisha yake kudolola hata kuisha kabisa.
Hapo hata mimi nikajifikiria sana na kugundua kuwa mali za majini ni za mikataba ndomana wanakupa sharti ambalo wanajua siku moja utaligeuka tu na kufanya wao wakufilisi kila kitu na kukuacha patupu.
Maiko aliwahi kuniambia kuwa hata atakapokufa lazima apate wafuasi wa kwenda nao na maji.
Mambo ya Maiko yameharibika kwa kifo cha baba yake mzazi, alikuja Mwanza kumsaka Patrick ndipo alipogundua kuwa walimuua baba yake.
Maiko aliporudi Arusha alienda kuyaomba majini yake yamrejeshee nguvu zake kama zamani, Maiko alilia sana na kusema anazidiwa na Patrick. Yale majini yalimwambia kitu kimoja kuwa anatakiwa kwenda na Patrick kule Arusha kwavile yeye na Mashaka walishindwa kumpeleka Patrick kule Arusha ndiomana mimi nikajitoa kuja kumfata Patrick nimpeleke Arusha.
Mashaka alishukuru sana kwani mambo yao mengi yaliharibia ukizingatia Mashaka alimfanya Maiko kama chambo chake kwahiyo akiyumba Maiko na yeye anayumba.
Maiko alipewa onyo la mwisho kuwa hatakiwi kuguswa mwilini mwake na kitu chochote chenye asili ya moto hadi pale atakapompeleka Patrick kule Arusha kwenye majini yake, na kama akiguswa na kitu cha moto ataharibu kila kitu.
Wakati mimi niko Mwanza, nilikutana na Patrick ambaye alipogundua dhamira yangu akanipiga sana hadi nikapoteza fahamu.
Patrick ana nguvu za ajabu ambazo zinanifanya nihisi kuwa kuna kitu amepandikizwa.
Nilipopata nafuu niliwasiliana na Maiko aliyeniambia kuwa amemwagiwa maji ya moto na bi.Deborah, hamu yote ya kurudi Arusha ikaniishia hapo niliogopa kuwa huenda yale majini yakanibadilikia mimi kwani sharti limeshavunjwa tayari na Maiko alikuwa akiuguza tu kidonda chake.
Nilijua mambo yameshaharibika ila nilijikaza kiume, ndipo nilipoanza kumtokea Tina ili nipate mwanamke wa kurudi nae kule kwani majini ya Maiko yalijua sana kuwahurumia wanawake ingawa Maiko alikuwa akimchukia mwanamke kuliko mtu yeyote duniani huku akimpachika sifa kuwa mwanamke ni mtu muongo, mlaghai, mwizi, tapeli na hafai kwenye jamii.
Mliponiambia kuwa mmefata maneno aliyoacha Maiko kuwa msimzike bali mkamchome kwenye nyumba yake nikaona si mbaya sana ila ingekuwa vyema kama mngemzika tu.
Mliponiambia kuwa kuna watu wamerudi kutazama nyumba ya Maiko iliyoungua, hapo ndipo pabaya tena nilipowapigia simu na kusema wameshaenda na nyumba haijaungua kabisa hapo ndipo pabaya zaidi.
Nadhani watakuwa na matatizo na tatizo lao linaweza kutatuliwa na kitabu kidogo cha Maiko kilikuwa kwenye begi lake dogo"
Ndipo Deborah akakumbuka kuwa kuna kibegi kidogo chenye mafaili walitoka nacho kwenye nyumba ya Maiko ikabidi aende kuangalia kama kweli lile begi wamefika nalo Mwanza.
Kila mmoja aliombea hilo begi liwepo ili Tulo awaambie cha kufanya na hicho kitabu kuweza kukomboa maisha ya ndugu zao.
Hali iliendelea kuwa mbaya pale nje walipowekwa kwenye nyumba ya Maiko, wakashangaa Maiko akitangulia na wao wakimfata vilevile wakiwa chini kama wanavutwa na sumaku.
Yuda alijilaumu sana kwa kuwasindikiza, alikumbuka maneno ya mama yake kuwa warudi wote Mwanza.
Adamu nae alizidi kumlaumu mama yao kwani walikuwa katika hali mbaya ya bila kutarajia.
Wakiendelea kuvutwa kama sumaku, mara gafla yule mtu aliyekuwa Maiko akageuka kuwa mti mkubwa wa mbuyu.
Kila mmoja alibaki kutaharuki, mara ule mti ukaanza kusogea.
Kila mmoja akaanza kutaharuki, mara ule mti ukaanza kusogea.
Hofu ikazidi kuwatanda, wakashindwa cha kufanya, wakatamani kupiga kelele ila sauti zao hazikutoka.
Kufika mahali ule mti nao ukayeyuka, woga ukawatanda na wakatamani kunyanyuka na kukimbia ila walijikuta wakiwa wazito sana kuinuka, hakuna aliyeweza kunyanyuka walikuwa kama wamegandishwa pale chini.
Mara kuna kuna majimaji yenye asili ya damu yakawa yanawamwagikia pale walipokuwa.
Deborah aliendelea kusaka lile begi, Tulo aliendelea kuzungumza pale haswa na mama yake.
AMINA: Kwakweli huyu Maiko ni mtu mbaya sana, yani mimi kukuhamisha kote kule bado akakupata mmh!
TULO: Hukutakiwa kunihamisha mama, ulitakiwa uwe nami karibu kunikinga nae na hata kunipa onyo. Ila Maiko ni mtu mwenye vishawishi vingi sana, hutumia njia mbadala kumpata mtu yeyote amtakaye.
Deborah alifanikiwa kukipata kile kibegi na kukipeleka kwa Tulo ambaye alichukua na kumwaga vitu vyote kuangalia kama atakiona hicho kitabu, na kwa bahati nzuri alifanikiwa kukiona.
Kilikuwa ni kitabu kidogo sana chenye karatasi kumi tu na kimeandikwa kwa lugha ya ajabu ambayo huwezi kuisoma kama sio mmoja wao.
Tulo alikishika kile kitabu na kupitia kurasa zake za ndani huku akikisoma kwa lugha ya ajabu na wote wakabaki kumshangaa tu, kadri alivyokisoma kikawa kinabadilika rangi na kuwa nyekundu. Alipokimaliza chote kikawa na rangi ya damu ambayo ilienea hadi kwenye mikono ya Tulo.
Kisha Tulo akawatazama wote pale sebleni na kuwaambia,
"Jamani, hiki ambacho mimi nafanya ni khatari sana kwahiyo msishangae kwa chochote kile ambacho kitanipata.
Ni kheri apotee mtu mmoja kuliko kundi la watu wasiokuwa na hatia, najua yale majini hayawezi kuacha hadi siri hii imetoka.
Nimeua watu wengi kwa kushinikizwa na Maiko pamoja na majini yake, nisingependa Patrick awepo katika mlolongo wa watakao angamia.
Maiko alikiuka masharti na ndiomana hajamuweza tena Patrick ambaye amekuwa na nguvu za ajabu, napenda Patrick awe mtu wa kawaida sitapenda aangamie kama wengine."
Tulo akamuangalia Patrick kisha akamuita kuwa amsogelee.
Patrick akamsogelea Tulo na kumsikiliza.
TULO: Ulitumia kitabu hiki kula kiapo mbele ya Maiko, sasa nakuomba utumie tena kitabu hiki kuvunja kiapo ulichokula kwa Maiko.
Patrick akachukua kile kitabu na kukishika huku akivunja kiapo kwa kufatiliza maneno anayoambiwa na Tulo, baada ya hapo Tulo akamfanyia kitu ambacho Patrick alifanyiwa mwanzoni wakati wa kula kiapo.
TULO: Swala la kiapo limeisha kwako Patrick, ila kuna kitu cha ziada utakachofanya. Hiki kitabu kitachomwa na wewe ndio utahusika kufukia majivu ya kitabu hiki.
Patrick akaitikia kwa ishara kuwa ameelewa kinachoongelewa.
Tulo akaendelea kuzungumza.
"Jamani, swala kubwa la kuwakomboa wale ni kukichoma hiki kitabu.
Ila katika kukichoma hiki kitabu, kuna mambo ambayo lazima yatokee moja wapo ni mimi kuangamizwa. Napenda kusema tena kuwa ni kheri aangamie mtu mmoja na wengi wapone.
Nimeshamaliza watu wengi sana kwa kusaidiwa na Maiko kwa nguvu za majini yake.
Hiki kitabu kinamaana kubwa sana kwa Maiko na Majini yake ndiomana amekuwa akikitumia hiki kitabu katika kulisha watu kiapo na kuangamiza watu mbalimbali.
Siri ya hiki kitabu ndio ambayo itaniangamiza mimi"
Amina uoga na hofu vikamtanda kuwa huenda mtoto wake nae anataka kufa.
AMINA: Unanitisha Tulo, unamaana gani kusema utaangamia? Inamaana na wewe unataka kufa?
TULO: Mama, kufa ni kawaida ya mwanadamu. Wanadamu kifo tumeumbiwa kwahiyo usiwe na shaka.
AMINA: Nisiwe na shaka kivipi wakati maneno yako yananikosesha amani?
Ikabidi Tulo ampe mama yake maneno ya kumtuliza kisha akaendelea kuwaeleza kuhusu kile kitabu.
"Hiki kitabu ndio kina mambo yote ya majini ya Maiko, tusipokiteketeza hiki kitabu basi tutakuwa na tatizo kubwa sana. Hata Maiko alipopewa hiki kitabu alikula kiapo, na mimi nilipopewa siri za hiki kitabu nililishwa kiapo cha kutokusema siri hiyo ila leo nimeisema na pia naenda kukiteketeza hiki kitabu.
Naomba mniletee kisu, kibiriti na mfuko wa plastiki niweze kufanya hii kazi kiufasaha. Na Patrick ataenda kufukia jivu kwakuwa yeye ni shupavu na ana nguvu sana"
Wakamletea vitu alivyohitaji na kumkabidhi ili afanye ile kazi ya kukiteketeza kitabu.
Upande wa wakina bi.Rehema hali ilikuwa mbaya sana.
Uoga nao ulizidi kuwatawala kwani walikuwa wamelowa damu mwili mzima huku wakitetemeka sana.
Yule mtu wa kufanana na Maiko akawatokea tena mbele yao, safari hii alikuwa amebeba panga linalong'aa sana. Wote wakaogopa, ikabidi bi.Rehema ajaribu kujitetea,
REHEMA: Maiko mwanangu, mimi ni mama yako mzazi na hawa ni ndugu zako tuhurumie tafadhari.
Yule mtu akacheka sana kisha akaongea kwa kejeli tena kwa kutumia sauti ya Maiko.
"Mama mzazi! Huoni fahari kuwa sehemu ambayo mwanao yupo?"
Halafu akanyoosha mkono, kisha ikatua maiti ya Maiko mbele yao tena akiwa vilevile kama alivyojiua nyumbani kwa Deborah.
Wote wakaogopa, kumtazama Maiko maiti na Maiko aliyesimama.
Yule mtu alilishikilia lile panga vizuri kama vile anajiandaa kuwachinja.
Tulo alichukua kisu na kujikata kwenye kiganja na mkono wake huku damu nyingi zikimwagika zikiungana na zile damu za kwenye kijitabu.
Halafu akachukua kiberiti na kuchoma karatasi moja moja za kile kitabu na kumalizia na ganda la nje.
Kisha akakusanya jivu lote na kuliweka kwenye ule mfuko wa Plastiki, akaufunga vizuri na kumpa Patrick akafukie huku akimpa maelekezo ya namna ya kufukia lile jivu ambapo alitakiwa aende pekeyake kufukia.
Wakati Patrick analifukia lile jivu, hali kwakina bi.Rehema ilikuwa mbaya sana mara mvua mara jua, mara mwanga unakuwa na rangi nyekundu mara wa kawaida, mara ile maiti ya Maiko na yule mtu vinatoweka mara vinakuja tena mbele yao.
Hali ilikuwa mbaya sana, upepo mkali ukavuma na kuwafanya wapatwe na kizunguzungu pale chini.
Mara gafla wakainuliwa juu kabisa wote watatu yani bi.Rehema, Adamu na Yuda kisha wakabwagwa chini kama mzigo wa kuni halafu wote wakapoteza fahamu.
Patrick alitumia ujasiri wa hali ya juu katika kufukia lile jivu kwani alipolitua pale chini lilikuwa zito kama vile kitu kikubwa ila kwakuwa Patrick alikuwa na nguvu sana, aliweza kulifanikisha lile zoezi halafu akarudi ndani.
Kufika ndani akawapa taarifa kuwa ameshafanikiwa kufukia lile jivu na hapo hapo Tulo akaanguka chini na povu kumtoka mdomoni.
Tulo akaanguka chini na povu kumtoka mdomoni.
Tulo alitapatapa kama vile mtu aliyekunywa sumu tena sumu kali.
Wote wakamsogelea na kujaribu kumpa huduma ya kwanza kisha kumuwahisha hospitali.
Amina alikuwa akiyakumbuka maneno ya mwanae tu kuwa lazima aangamie, alikosa imani kuwa Tulo atarudi tena katika hali ya kawaida.
Pale hospitali kila mmoja alikuwa na wasiwasi, hakuna aliyekuwa na amani kabisa.
Bi.Rehema na wenzie walizinduka na kujikuta wote wapo hospitali, kumbe wasamalia wema waliwasaidia na kuwapeleka hospitali.
Yuda ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzinduka baada ya kupata unafuu kiasi, kisha akafatiwa na Adamu na badae bi.Rehema.
Walikuwa wamechoka sana kama vile wamefanya kazi ngumu.
Baadhi ya wasamalia wema waliowasaidia walikuwepo pale hospitali kuwaangalia hali zao zinavyoenda.
Kwakweli waliwashukuru sana na kuwauliza walipowatoa.
Mmoja wao akawaambia ilivyokuwa,
"Kwakweli tulishtuka sana kuwaona pale kando kando ya barabara tena wote mkiwa hamna fahamu, ikabidi tuwabebe na kuwawahisha hapa hospitali. Sijui mlipatwa na nini jamani!!"
Ikabidi wajifanye wamesahau kitu ambacho kiliwatokea hapo kabla.
Hawakuwa na kitu chochote si pesa wala simu, vyote vilibebwa na ndivyo ilivyo upatapo tatizo mwingine anakusaidia na mwingine anashukuru kupata nafasi ya kukuibia kwa urahisi.
http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hali ya Tulo ilikuwa mbaya sana na mwisho wa siku akapoteza maisha.
Ikawa uchungu na simanzi kubwa ndani ya familia, kilio kikatawala sana uchungu na masononeko ya kumkosa Tulo.
Kila mmoja alikuwa akiilaumu kazi ya Maiko kwani ndio iliyopoteza watu wengi waliowapenda.
Wakapanga safari na kuamua kwenda kumfanyia Tulo mazishi mkoani Morogoro ili wakamzike karibu na kaburi la babu yake.
Walifika Morogoro na kupokelewa kwa kilio na mazishi ya Tulo kufanyika.
Tulo alikufa kishujaa kwani alikubali kutoa siri ya kuangamiza maisha yake ili kuwakomboa watu wengine.
Ilikuwa ni huzuni sana kwani hakuna aliyetarajia kitu cha namna ile.
Taratibu zote za mazishi zilifanyika na Tulo akazikwa pembezoni mwa kaburi la mzee Ayubu.
Patrick alipiga magoti kwenye kaburi lile, alilia sana tena sana akakumbuka jinsi alivyomzoea mzee Ayubu tena kwa muda mfupi kabisa. Akakumbuka jinsi alivyomlaghai kwa stori za hapa na pale na jinsi alivyomdanganya kwa pombe.
Akakumbuka na siku waliyommaliza kabisa mzee Ayubu, mzee ambaye hakuwa na hatia. Walimkata viganja vya mikono na kumchuna kipara chake, uchungu ulimshika sana Patrick na machozi mfululizo yalimtoka, ndipo mama yake bi.Deborah alipomsogelea na kumshika huku akimbembeleza atulie, hadi pale walipotoka makaburini.
Tusa nae alilia kwa mengi sana, alimlilia babu yake kwa uchungu uliopitilize alitamani siku zirudishwe nyuma apate kumuona tena akiongea na kutabasamu kwa ucheshi wake ila haikuwezekana kwani mzee Ayubu alishaoza mule kaburini.
Walipopata unafuu wakina bi.Rehema walihitaji kurudi Mwanza ila hawakuwa na chochote kile, wakaamua kutafuta mawasiliano ya ndugu zao na uzuri ni kuwa Yuda alikuwa anakumbukumbu ya namba nyingi kichwani.
Yuda akakumbuka moja wapo ya namba alizokuwa nazo kisha wakaazima simu na kujaribu kupiga, Deborah alipokea simu ile na kuongea nao.
Kwakweli alishukuru kusikia kuwa wamepona, ikabidi afanye mpango wa kuwatumia nauli ili wakakutane nao moja kwa moja Dar es salaam kwani nao walishapanga mipango ya kuondoka kule Morogoro na kwenda Dar es salaam ili kumaliza swala zima linalohusu wazazi wa Patrick.

0 Comments