Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mume gaidi sehemu ya kumi na tisa (19)



Siku nilipokuta kuwa kuna namba ngeni imenipigia ila sikupokea kwakuwa nilikuwa nje nikifanya usafi, nilichukua simu na kupiga akapokea mtoto wa kike huku akilia kuwa yeye ni mke wa Patrick.

Nilipata mpasuko mkubwa sana moyoni, yani Patrick anaoa bila hata ya kunishirikisha? Anaoa kimya kimya kama vile nimemkosea kitu gani?

Ni kipindi hicho nilichomsisitiza Patrick amlete huyo mwanamke hapa nyumbani kwangu.


Siku waliyokuja sijui hata walipatwa na majanga gani huko ila nilishtuka sana kumuona huyo binti, machozi yalinitiririka.

Jamani Tusa amefanana sana na mtoto wangu Jasmine yani wamefanana, sura ya Jasmine ilikuwa hivyo hivyo kama sura ya Tusa, utafikiri Jasmine wangu amekua. Nilitoa machozi sana kumuona kumbe binti mwenyewe alifika na matatizo yake tayari. Alishaharibiwa haribiwa kila kitu na mwanangu Patrick, ila Tusa mwenyewe alikuwa akilia tu huku akihofia kusema ukweli.


Nilimsisitiza Tusa kuwajua wazazi wake kwani nilihisi lazima kuna mahusiano ya karibu kati ya Tusa na mwanangu Jasmine, na wala sikukosea.

Alipofika Pamela na kusema kuwa yeye ni mama yake Tusa, moja kwa moja nikajua baba wa Tusa lazima atakuwa Jumanne.

Katika kumuuliza Pamela ni kweli alikuwa Jumanne ila alibadili jina na kujiita Adamu, sawa sawa ni Adamu kweli sijui alibadili kwa misingi ipi labda hakutaka kukumbuka yaliyopita.


Tangu familia ya Tusa imefika hapa mambo yamekuwa shaghala bhaghala mala limetokea hili mara lile yani mambo hayaeleweki kabisa hadi pale nagundua kuwa Jumanne na Maiko ni mapacha mmh kweli kuna siri nzito hujificha kati ya mtu na mtu.


Pamela alinieleza kitu kilichonishtua sana na pale Fausta naye alivyonieleza nimegundua kuwa wazazi wa Patrick wanatokea humohumo kwenye familia ya Tusa.

Haya sasa Pamela na Fausta kazi kwenu kutambua kati yenu ni nani mama mzazi wa Patrick? Na nyie ndio mtamwambia Patrick je baba yake ni Adamu au Maiko au kuna mwingine. Mimi sina la ziada yangu ni hayo tu. Nadhani sasa nitakuwa huru na mawazo hata kama nikifa nitakufa kwa amani"


Wote walikuwa wakilia na kuomboleza, Patrick alizidi kumkumbatia mama yake huku akisema,

"mama, simtaki mama mwingine nakutaka wewe tu. Wewe ndiye mama yangu mzazi, simtaki mwingine mama"

Patrick alikuwa akitokwa na machozi tu, huku Pamela na Fausta nao wakilia tu kwa yaliyopita na kujilaumu sana.

Adamu nae alipatwa na mshituko usio na maelezo kwani nae alihusika humohumo, si Tusa wala Tina walioacha kulia. Tusa alilia sana kwani kwa vyovyote vile ametembea na kaka yake iwe ni mtoto wa Pamela au Fausta.

Wote walilia mule ndani kama vile kulikuwa na msiba.

Bi.Rehema ndio hakuwa na hali kabisa, alihisi kama vile dunia ikimzomea na kumng'ong'a.


Maiko naye na mfuko wake pale nje alipatwa na mshangao mkubwa sana kusikia kuwa Patrick ni mtoto anayewahusu katika familia yao.

Aliinuka na mfuko wake ili kujumuika na wote wa ndani. Hakujali chochote kwani mengi yalishaharibika.


Hakujali chochote kwani mengi yalishaharibika.

Maiko hakutaka kuendelea kusubiri pale nje, alitaka aingie ndani ili wawezo kumuona. Kuku akijisemea:

"Liwalo na liwe"

Hakutaka hata kujua Patrick ni mtoto wa nani kwani alihisi kwa vyovyote vile Patrick anaweza kuwa mtoto wake au wa Adamu.

Maombolezo yaliendelea mule ndani kwani wengi walijihisi kama vile wanaota au wameamka toka usingizini.

Tusa na Tina nao waliwasogelea mama zao.

TUSA: Mama tafadhari, Patrick si kaka yangu jamani.

Pamela alizidi kulia kwani maelezo hakuwa nayo ya kutosha.

Bi.Rehema akadakia kusema,

"Jamani, tuambieni basi huyo Patrick ni mtoto wa nani na kwanini mlimtupa ili tuweze kuokoa jahazi hili."

Mara Maiko akaingia ndani na mfuko wake na kuwafanya wote washtuko kwani matendo ya ajabu waliyoelezwa juu ya Maiko walihofia na wao kudhuruka.


Maiko alisimama katikati yao huku akizungumza.

MAIKO: Jamani, mazungumzo yote nimeyasikia. Deborah amewaeleza matukio ya ukweli tena ukweli mtupu, hakuna alichowaongopea. Mimi kweli ni mwanaume wa ajabu nisiyefaa katika jamii inayonizunguka"

Wote wakashtuka na kumuangalia tu kwani ilikuwa ni vitu vya kushangaza na ajabu.


Tulo alibanwa sana kule kwenye kituo cha polisi ila aligoma kusema.

Badae ikabidi Mwita aende kuzungumza nae tena.

MWITA: Tulo, ukweli humuweka mtu huru. Ni bora useme ukweli tu.

TULO: Ukweli humuweka mtu huru?? Hujielewi wewe, kuna ukweli wa kumuweka mtu huru ila ukweli mwingine unafanya ufungwe maisha. Siko tayari kufungwa, siko tayari kuozea jela.

MWITA: Sina nia mbaya Tulo, ninachotaka ni wewe kubadilika.

TULO: Unahitaji mimi kubadilika? Kabla hujanibadili mimi unatakiwa ukawabadili ndugu zako kwanza.

MWITA: Kivipi? Mbona sikuelewi?

TULO: Mimi ni rafiki tu ila kumbuka kuwa mapinduzi huanza ndani kwanza. Mimi Tulo kuna kazi naifanya inayoniingizia pesa na kunifanya nionekane tayari. Ila kazi yangu mimi sio kubwa sana kama ya baba yako Maiko, tena pia kuna ndugu yako Patrick. Nenda ukaanze na hawa kwanza kisha ndio urudi kwangu.

Mwita alimshangaa sana Tulo, kwani alikuwa tayari hata kufa kwaajili ya kuficha ukweli halisi.

Mwita akaona itakuwa vyema kama akimtafuta baba yake bwana Maiko na nduguye Patrick kuwahoji kidogo na kama akishindwa basi atumie nguvu ya dola.


Mwita aliondoka pale polisi na kuanza kuelekea kwakina Patrick kwanza kwani Maiko hakuwa na mahali pa kusema kuwa utamkuta moja kwa moja ndiomana Mwita alienda moja kwa moja kwakina Patrick.

Alipofika akasikia kuna mtu akizungumza ndani huku wengine wakisikika na vilio vya chini kwa chini.

Mwita akategesha masikio yake kujua kuna nini ila matone ya damu yalimshangaza sana pale nje na akajua tu kuwa mule ndani kuna matukio yasiyo ya kawaida, akategesha sikio dirishani ili kujua kinachoongelewa.


Maiko aliendelea kuongea bila ya kuogopa kitu chochote na bila kujali kama anawatisha watu waliopo mule ndani.

"Jamani, sijapenda kuwa kama hivi nilivyokuwa leo. Roho inaniuma sana, nimepoteza maisha ya watu wengi mno. Kinachoniuma zaidi ni kifo cha baba yangu, roho imeniuma sana kwa kummaliza baba yangu kisha viungo vyake kuvipatia kwa pesa nyingi za kutosha.


Sikuwahi kumuona wala kumjua baba yangu, nilikuwa natoa oda tu. Kwa mama naye nilishapotezwa, sikuweza tena kukutana na mama yangu ila laiti kama ningekutana na mama kama Deborah nina hakika ningekuwa na chembe kidogo ya huruma.

Jinsi Patrick alivyompa shida Deborah wakati mdogo sikufikiria kabisa kama Patrick si mtoto mzazi wa Deborah.

Mateso mengi ambayo Deborah ameyapata ni sababu ya Patrick, roho imeniuma sana kuona kumbe Patrick ni sehemu ya familia yangu.

Nilichukizwa sana kumuona Deborah ana mtoto tena mtoto mwenyewe ni kutoka kwa mwanaume aliyeng'ang'ania kuolewa naye na kuniacha mimi.

Nilikuwa namfanyia mambo mengi ya ajabu ili kumfanya Deborah ajutie kitendo cha kuolewa na mume mwingine na pia ajutie kutelekezwa na mtoto ambaye alikuwa hataki kumuweka chini.


Nakiri wazi kumuua mume wa huyo dada (akionyesha kidole kwa Marium ambaye alikuwa ameangalia chini tu akikumbuka mumewe alivyouwawa kwani kila amuonapo Maiko hukumbuka kifo cha mumewe.)

Nikweli nilimchinja, ila sababu kubwa ni kuwa nilimuona na Deborah kipindi hiko nikimsaka Deborah kwa lengo la kurudisha alivyovichukua kwangu, kweli nimeamini pesa haina mwisho.

Mimi nina pesa nyingi sana, kwa pesa aliyochukua Deborah wala sio ya kuniathiri ila nilimsaka kwa kila njia aweze kunilipa mali zangu.

Ndipo siku hiyo nilipomuona ameongozana na huyo mwanaume na kwa vyovyote vile nilijua kuwa lazima yule atakuwa mwanaume wake na nikapanga kumkomesha.

Nikaanza kumfatilia yule mwanaume, siku niliyomkuta alikuwa nje nikamfata na kumuuliza mahusiano yake na Deborah akanijibu kuwa ni shemeji yake nikahisi ananificha tu. Nikamuuliza alipo Deborah akagoma kusema, nikamvizia anapoelekea.

Aliingia kwenye chumba, nami nikaingia kwa njia za panya hakuona kama nimeingia.

Nikamuona amekaa na yule dada (akimuonyesha tena Marium) ila sikufikiria kama ni mumewe kwani walikuwa wamekaa mbali mbali, nikajitokeza mule ndani, nikambamiza na gongo nililobeba yule mwanaume akaanguka chini, mwanamke akataka kupiga kelele na kukimbia, nikamuwahi kwa kumpiga na gongo nae akazimia kisha nikachukua kisu changu na kumchinja na kuondoka na kichwa chake.

Kwakweli nilifanya tukio la ajabu sana kwa yule baba, kichwa chake nikakitunza na ninacho hadi leo nyumbani mwangu nilitaka siku Deborah akija kwangu aje kukishuhudia.


Kijana yule pale aitwaye Yuda nae pia alikuwa mfanyakazi wangu (wote wakashangaa kusikia kuwa Yuda nae yu chini ya Maiko.)

Niligombana nae baada ya kuona kile kichwa ndani kwangu kumbe alikuwa ni baba yake. Nisamehe sana Yuda ila ndio ishatokea tayari.

Tukiacha yote hayo niliyofanya kwa hiyari yangu ila mengi nilishinikizwa na mtu mmoja aitwae Mashaka.


Mashaka ni mtu mbaya sana, alinijengea kuwa na roho mbaya kupita maelezo na nimefanya mengi mabaya kwa ajili yake, yeye ndiye alikuwa shinikizo kubwa kwangu.

Najua mimi hamnielewi kama mlivyomuelewa Deborah wakati anawaelezea, mimi nishachanganyikiwa kwa mengi mabaya niliyofanya. Sina amani tena moyoni mwangu.


Kisasi changu kimemrudia Mashaka, ngoja niwaambie nilichomfanya Mashaka. Kabla ya yote, ngoja niwaonyeshe hivi vitu."


Maiko aliingiza mkono kwenye mfuko wake wa suruali kisha akatoa barua na kuiweka mezani kisha akasema,

"Hakikisheni mnaisoma hiyo barua"

Kisha akainua ule mfuko wake, akaingiza mkono na kutoa kitu.

Kilikuwa ni kichwa cha Mashaka, Maiko alikuwa amemuua Mashaka.

Kila mmoja alianza kupiga kelele mule ndani na kuogopa.


Kila mmoja alianza kupiga kelele mule ndani na kuogopa.

Maiko hakuwa na wasiwasi wowote na kile kichwa mkononi na hiyo ikawathibitishia na kufanya waamini kuwa kweli Maiko ni muuaji.

Patrick hakushangazwa sana kumuona Maiko ameua ila kitu kilichomshangaza ni kuwa Maiko amempata wapi Mashaka.

Patrick akainuka na kuanza kumsogelea Maiko.

PATRICK: Umempata wapi Mashaka?

MAIKO: Tafadhari usinisogelee.

Deborah kusikia vile akainuka na kuanza kumvuta Patrick kwani alihofia nae kupatwa na matatizo kama yale. Ila Patrick alikuwa mbishi, bado alihitaji kujua Maiko kamtoa wapi Mashaka.

PATRICK: Nataka uniambie ulipomtoa Mashaka.

MAIKO: Yote nitasema ila usinisogelee.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Deborah akazidi kumvuta mwanae na kumuomba warudi kukaa. Ndio Patrick akarudi kwani hata yeye hakujua hatma yake ni nini.


Mwita pale nje hakutaka kujiuliza mara mbili mbili akachukua simu yake na kuwapigia maaskari kisha akawaelekeza eneo la tukio ili waje kumkamata muharifu yule halafu akaingia ndani, alitamani hata muujiza utokee kuwa muongeaji wa yale maneno asiwe baba yake, alitamani hata awe ni mtu mwingine.

Mwita alipoingia tu ndani, Maiko aliweza kumsikia na kumuona.

Maiko akatoa bastola na kumuwahi nayo Mwita kuwa akae chini, Maiko hakuwa kama binadamu wa kawaida. Wote walibaki kushangazwa na ile hali.

Mwita aliamua kukaa huku akivizia namna ya kumnyang'anyanya silaha hiyo baba yake kwani alijua wazi kuwa kitendo cha kumsogelea ni kuhatarisha maisha yake.


Maiko akawaelezea tena vile anavyojielewa yeye.

"Sikufikiria kama ninachokifanya ni kitu kibaya na kuwa ipo siku itanigharimu, kuhusu kukamatwa na polisi sikuwa na shaka nao haswa kwa vijana wanaopenda rushwa kama Taifa letu.

Sitaki mtu anisogelee kwavile nataka kueleza niliyonayo jambo kwa ufupi na kwa kuruka ruka ili wote mpate kunielewa.


Mtoto wa Deborah huyo Jasmine ni mimi kweli niliyetoa oda kwa vijana wakammalize mtoto huyo, sio kwamba nilikuwa na ugomvi na mume wa Deborah au Deborah mwenyewe hapana!! Ila nilifanya kwa kuifurahisha nafsi yangu, ila mwanzoni sikujua kama mtoto huyo ni wa Deborah, nilitoa sifa za mtoto na badae nikaletewa. Nilikuja kugundua wakati mtoto mwenyewe tushamteka ila nikaamua kuipotezea tu, Laiti kama ningejua kuwa Jumanne ni ndugu yangu nisingethubutu kufanya vile.

Vijana wangu walinipa taarifa juu ya kukamatwa kwa yule binti aliyetuletea mtoto, nikafanya mpango hadi yule binti akawa huru kabisa hakuwa na kesi tena hapo pesa yangu ndio iliyoongea.


Nilipomkuta Deborah tena na mtoto nilishangaa sana nikajua labda kipindi tunamteketeza mwanae alikuwa mjamzito. Sikuhisi hata kidogo kama Patrick si mtoto wa Deborah.

Huyu mwanamke ana moyo wa kijasiri sana anahitaji kuigwa.


Ni kweli mimi ni mume gaidi, Deborah hajakosea kuniita hivyo sikuwa na huruma kwa mke wala mtoto.

Nilimtenda vibaya Fausta tena bila hata ya kujua ni dada yangu. Halafu kibaya zaidi ni kitendo cha kumbaka mwanangu Tina.

Sifai kuigwa na yeyote, nilipandikizwa roho mbaya na ya kikatili moyoni mwangu ila hadi nitakapoingia kaburini nitakuwa namlaumu huyu mwenye kichwa hiki.


Msimuhukumu Patrick kwa chochote, najua vyote alivyofanya mimi ndiye chanzo. Nimemuharibu sana Patrick kimawazo na kitabia.

Ni mimi niliyempa mbinu za kumpata Tusa kwa urahisi na kumfanya atakavyo.

Patrick si mtu mbaya kwani kuna kipindi huwa anajirudi.


Patrick alimteka Mashaka, mimi nilikuwa nikimfatilia.

Patrick alimfunga Mashaka huko porini nami nimeitumia nafasi hiyo kummaliza Mashaka kwani tushamaliza watu wengi sana ila Mashaka hakuacha kutamani kuendelea kumaliza watu wasio na hatia.

Mashaka hafai tena hafai kabisa, najua hapa hakuna wa kumsamehe Mashaka wala mimi.


Narudia tena msimuhukumu Patrick, akili yake ilivurugwa.

Deborah ni mwanamke mwema, yani mateso yote yale hakuthubutu kumtupa Patrick.

Laiti kama ningerudi ujanani basi ningemfanya Deborah kufurahia maisha yake duniani.


Kifo cha baba yangu mzazi kimeniumiza sana, ni mengi nimeyafanya bila huruma. Kwangu mimi mwanamke hakuwa na thamani yoyote.

Pole mama yangu bi.Rehema najua hukutarajia kitu cha namna hii ila ndio hivyo mwanao sio mtu wa kawaida kabisa.

Mkienda Arusha mtaweza kuona uajabu wangu humo ndani.

Pole na wewe Deborah kwani uliponitoroka niliitumia nafasi hiyo kummaliza baba yako mdogo. Mimi ndiye niliyemuua.

Wote niliowaumiza nawaambia pole, poleni sana kwa kuumizwa na Maiko.

Sitaki kufungwa na siko tayari kwenda jera.


Najua hakuna wa kunisamehe, ila nawaomba kitu kimoja.

Patrick anakujua nyumbani kwangu Arusha.

Mwende huko, mkateketeze kila kitu cha ndani haswa viungo vya binadamu na mali zangu zote nawaachia nyie mtajua cha kufanya ila nawaomba myasikilize mawazo ya Deborah.

Najua kuna maswali bado mnayo ya kuniuliza ila hiyo barua itawajibu kila kitu. Nimemaliza ila sitaki mtu wa kunisogelea"


Akachukua bastola yake, mara gafla mule ndani mkavamiwa na kundi la maaskari ambao Mwita aliwapigia simu.

Wakataka kumsogelea Maiko, akawanyoonyea bastora.

MAIKO: Atakayenifata nakwenda nae na maji, siko tayari kwenda jela. Kweli nimeamini, mwisho wa ubaya ni aibu.

Wale mapolisi wakikazana kutafuta mbinu ya kumkamata Maiko hakupoteza muda, akaweka ile bastora kichwani mwake na kusema neno moja tu.

MAIKO: Kwaheri mama.

Kisha akajifyatua kwenye ubongo na kuanguka chini huku kichwa cha Mashaka kikiwa mkononi.

Ilikuwa ni tukio la kushtua sana mule ndani.

Polisi wale wakamfata Maiko pale chini aliyeonyesha kuwa bado hajakata roho vizuri,

Polisi mmoja akainama ili amsikilizie akashangaa akivutwa kwa chini.


Polisi mmoja akainama ili amsikilizie akashangaa akivutwa kwa chini.

Yule askari alizidi kuvutwa pale chini na Maiko, wote ndani ya nyumba wakastaajabu na wote wakaogopa kumsogelea.

Askari alianza kuhangaika pale chini kwani alishikwa kwa nguvu sana na Maiko, alihangaika hadi alitia huruma ila waliogopa kumsogelea. Baada ya muda roho ya Maiko ikaachana na mwili na kumuachia yule askari ambaye alikuwa amelowa damu ya Maiko na kuumia pia.

Yule askari alivyoweza kuinuka pale alijikuta akikimbia na kuwaacha maaskari wenzie mule ndani, hakutaka kurudi tena kwani aliona kuwa ni kitu cha kushangaza.

Mvua kubwa ikanyesha, hadi ikawashangaza wote mule ndani, wakajikunyata ili ikatike na haikuchukua muda mrefu ikakatika.


Mule ndani wakawa wanashauriana jinsi ya kubeba mwili wa Maiko na kichwa cha Mashaka kwenda kuzika.

Ilikuwa ngumu kwa kila mmoja kumsogelea Maiko pale chini, maaskari waliokuwepo wakaamuru mwili wa Maiko uachwe pale kwa muda kwaajili ya uchunguzi na upelelezi, na sababu zingine za kiusalama.

Wanausalama zaidi wakapigiwa simu na kufika eneo la tukio, muda huo familia nzima ilikuwa nje wakingoja kutolewa kwa mwili wa Maiko, na walioutoa walilalamika kuwa ule mwili wa Maiko ulikuwa ni mzito sana kuliko marehemu wote waliowahi kuwabeba.


Nyumba ya Deborah ikawa inatisha sana, wakajipanga namna ya kumzika Maiko.

Deborah akawa anaongea na dada yake kuhusu kifo cha Maiko.

DEBORAH: Kifo cha Maiko hakijanisikitisha hata kidogo, amekufa kirahisi sana ukiangalia na makosa aliyoyafanya.

MARIUM: Ila bora amekufa, kwani angeendelea kuwa hai angezidi kutuumiza wengine hapa.

Deborah alifurahia kwa Maiko kuamua kujiua mwenyewe na mabaya yake kudhihirika.


Kama familia wakaamua kupanga mahali ambako patafaa kumzika Maiko baada ya uchunguzi kukamilika.

REHEMA: Nadhani itakuwa vyema kama mwanangu akienda kuzikiwa alipokuwa anaishi, yani huko huko Arusha.

ADAMU: Hapana mama, itabidi tukamzike Morogoro karibu na kaburi la baba.

DEBORAH: Nawahurumia sana, kuacha kuongelea mambo ya msingi na kukazana pa kumzika Maiko. Yani jinsi Maiko alivyokuwa, bado mnapata nguvu za kumsafirisha sijui Arusha sijui Morogoro, ingekuwa amri yangu ningemtupa kwenye mto wa mamba ili mamba wamtafune na mwili wake usibaki hata chembe.

MARIUM: Kweli kabisa mdogo wangu.

Wengine wote walikuwa kimya kwani hawakujua hata waseme nini ila wakaona kuwa kumzika Morogoro itakuwa vizuri zaidi, ukizingatia Maiko alikuwa na pesa kwahiyo wakaona kuwa watatumia pesa yake hiyo na kumsafirisha kwa ndege.


Pamela alipigiwa simu na wifi yake wa Morogoro Amina, alikuwa anamtaarifu wifi yake huyo kuwa na yeye yupo Mwanza.

AMINA: Wifi dada, mimi niko Mwanza. Kwani nyie bado hamjarudi Dar?

PAMELA: Bado ila tumepatwa na matatizo, wewe umefata nini Mwanza?

TULO: Mwanangu kanipigia simu kuwa yupo huku kashikiriwa na polisi, ndio nimekuja kumuona.

Pamela hakuelewa ni mtoto yupi wa Amina, ikabidi ampe maelekezo Amina ya kufika walipo ili pia akamueleze kuhusu Maiko na undugu wao.


Nyumba ya Deborah ilikuwa inatisha sana, kama vile kulikuwa na maruweruwe ndani ya nyumba.

Tusa na Tina ndio waliogopa kabisa kukaa ndani ukizingatia wakikumbuka jinsi Maiko alivyokibeba kichwa cha Mashaka.

Rehema na Adamu wakamuomba Patrick awapeleke mahali alipomuacha Mashaka ili kuangalia mwili wake ikiwezekana kuuzika.

Waliondoka na maaskari kwenda eneo la tukio, waliukuta mwili wa Mashaka ukiwa umenyofolewa nyofolewa na ndege na kunguru pamoja na mmbwa.

Wale maaskari wakabeba viungo vilivyobaki na kupiga picha kwa uchunguzi zaidi.

Ile kesi hata haikujulikana itaendeshwa vipi ila maaskari walihitaji kupata uchunguzi wa kutosha tu.


Amina alifika hadi alipoelekezwa na Pamela, halafu akaenda nae nyumbani kwa Deborah.

Amina alishangaa sana kumuona Deborah aliyekuwa wifi yake mwanzoni, akamfata na kumkumbatia kisha kusalimiana nae.

AMINA: Deborah!! Hata sijui ulipoteaje jamani, nilishangaa tu kaka kutuletea wifi dada.

Wakaongea ya hapa na pale na kukumbuka mambo mengi yaliyopita.

Pamela akamueleza Amina juu ya tukio lililotokea na kifo cha Maiko.

AMINA: Alikuwa anaitwa nani?

PAMELA: Maiko ndio jina lake, alikuwa anaishi Arusha.

AMINA: Mungu wangu, umesema ni ndugu yetu?

PAMELA: Ndio, hata sisi wenyewe tumemjua tulivyofika Mwanza. Kwani unamjua?

Amina alikaa muda kwa kimya, kisha akaanza kutoa maelekezo ya Maiko anayemjua yeye.

PAMELA: Ndio huyohuyo, hata hujakosea.

AMINA: Yule Maiko kajiua mwenyewe? Halafu mnapanga mipango ya kumsafirisha? Hata kama ni ndugu yangu, siko tayari kumsafirisha yule shetani. Nadhani hamumjui vizuri nyie, yule Maiko si mtu wa kawaida kabisa. Mkimsafirisha mnajitafutia matatizo tu.

PAMELA: Sasa tutafanyaje?

AMINA: Hakuacha maelekezo yoyote juu ya kuzikwa kwake?

PAMELA: Kuna barua alitukabidhi ila bado hatujaisoma.

AMINA: Maiko hakuwa mtu wa kawaida, kwa ushauri wa bure tu. Someni hiyo barua yake ndipo mkamzike. Maiko hakuwa kama binadamu wengine, mi sikujua kama ni ndugu yangu ila kumbuka mimi ni daktari nishaonana na Maiko mara nyingi sana, hakuwa binadamu wa kawaida kabisa yule.

Pale nyumbani wakaafikiana kuisoma barua ya Maiko kwanza.


Amina akawapa taarifa kuwa kilichomleta Mwanza ni juu ya mtoto wake kwani amesikia kuwa amekamatwa, walipomdadisi vizuri wakagundua kuwa Tulo ni mtoto wa Amina, wote wakashangaa.

Hadi Mwita akajikuta akiuliza kwa mshangao.

MWITA: Inamaana Tulo nae ni ndugu yangu!!

ANNA: Ndio, atakuwa nduguyo.

MWITA: Sasa nimeamini maneno ya Patrick, kweli huu ukoo una laana. Kesi ya Tulo nimeishikilia mimi.

Amina akauliza kwa mshangao kuwa ni kesi gani kwani hakujua kuwa mtoto wake alikuwa na mambo ya ajabu.

Ukoo haukueleweka na kila mmoja alibaki kushangaa tu.


Nyumbani kwa Deborah ilikuwa ni gumzo tu, hakuna kulala wala nini muda mwingi walijikuta wakizungumza na kutafuta chakula tu.

Patrick aliporudi kuonyesha mwili wa Mashaka, alienda moja kwa moja na kumfata mama yake Deborah.

Alimuita na kwenda kuongea nae.

PATRICK: Mama, mimi si mtoto mzuri tena. Mama sidhani kama nastahili kuwepo kwa maisha ya sasa, najua ukishajua maovu niliyotenda utanichukia pia.

DEBORAH: Siwezi kukuchukia Patrick hata mara moja, ondoa kabisa fikra za kuchukiwa na mimi mwanangu. Ngoja tumalize haya mambo ya kina Maiko na tuanze kujenga familia yetu upya kabisa mwanangu.

Patrick alishukuru kwa kauli ya Deborah kwani hakuwa na raha wala na amani moyoni mwake.


Tusa hakuwa na raha kabisa kwani hakujua hatma yake na Patrick ni nini, Patrick nae hakuwa na raha kabisa na bado aliendelea kujishangaa kuwa kwanini aliangukia kimapenzi kwa dada yake. Kwakweli wote walikuwa na mawazo sana ndani ya familia na hawakuelewa cha kufanya.

Mwita hakuelewa afanyeje na Tulo kwani kesi ile alikuwa ameishikilia yeye na sasa anagundua kuwa Tulo ni ndugu yake anajikuta hana la kufanya.


Waliamua kusoma zile barua kama familia, ila walikuta barua mbili moja ikiwa na maelezo mengi sana na nyingine iliandikwa kwa kifupi tu.

"Nitakapokufa, naomba mwili wangu uchomwe na kuzikwa pamoja na viungo vyote vya binadamu ambavyo vipo kwenye nyumba yangu"

Familia iliangaliana na kukubali kuwa kweli Maiko hakuwa mtu wa kawaida, alikuwa ni zaidi hata ya gaidi.


Wakasafiri wote na kwenda Arusha ili kujishuhudia kila kitu kuhusu Maiko.

Kufika nyumbani kwa Maiko walikuta ukuta wa upande mmoja wa nyumba yake umeanguka, walipojaribu kuuliza mambo hayo yametokea lini, wakatajiwa siku na saa aliyokufa Maiko.

Ni familia ile nzima ndiyo iliyokuwepo hapo kustaajabu mambo ya Maiko.

Wakiwa wanashangaa, ukatokea upepo mkali sana na kuwapuliza pale nje.

Mara kuna kitu kikatoka nje ya nyumba ya Maiko.


Mara kuna kitu kikatokea nje ya nyumba ya Maiko.

Upepo mkali nao ukazidi kuvuma nje ya ile nyumba, watu wote wakaanza kuogopa hofu ikawatanda kwenye mioyo yao.

Wakatazamana bila hata kuelewa nini kinaendelea, kile kitu cha ajabu kiliwazunguka na kwenda kuishia nyuma ya ile nyuma na upepo nao ukakatika gafla.


Wakasogea pembeni na kuanza kujadiliana ile hali iliyowatokea na waliyoiona.

FAUSTA: Ndiomana mimi sikutaka kabisa kuja huku, niliyajua yote haya. Bora hata ya Tusa na Tina waliobaki nyumbani.

DEBORAH: Huu sio wakati wa kulaumiana jamani kama jambo limeshatokea hakuna jinsi zaidi ya kukubaliana na hali halisi.

REHEMA: Tuzungumzie ya kufanya jamani tusipeane lawama za bure.

AMINA: Kwa kiasi kidogo namfahamu Maiko, hakuwa binadamu wa kawaida kama mnavyodhani. Inabidi ifanyike namna nyingine ya ziada ili kukabiliana na hii hali, hata kilichotokea wakati anakata roho sio kawaida ila kama.

DEBORAH: Basi utuambie unavyomfahamu huyo Maiko, pengine inaweza kutusaidie.

Basa Amina akaanza kuwaeleza vile anavyomfahamu maiko.


"Mimi ni daktari, nilifahamiana na Maiko kipindi nipo hospitali kwenye ofisi yangu mjini Dodoma, alikuja na mgonjwa wake moja kwa moja ofisini na kuniomba nimfanyie operesheni ndogo. Nikamuuliza mgonjwa anaumwa nini, bila kificho aliniambia kuwa mgonjwa yule ana madawa ya kulevya tumboni na alitaka niyatoe.

Kwanza kabisa nikakataa, Maiko akatishia kuniua ikabidi nikubali na kumfanyia yule mgonwa operesheni ila yule mgonjwa alikuwa kachoka sana ilionyesha kuwa amekaa na madawa kwa muda mrefu tumboni na hali yake kiafya haikuwa nzuri ila Maiko hakutaka yule mgonjwa ahudumiwe zaidi badala yake alisema nimmalize kwa sindano kwakweli nilipinga kabisa swala hilo nikamwambia aondoke tu na mgonjwa wake.

Kesho yake nikiwa ofisini nikasikia kuna binti amekutwa kauwawa na kutupwa kwenye mtaro, tulipoenda kumuona alikuwa ni yule yule binti aliyeletwa na Maiko jana yake. Dah nilisikitika sana kwani sikutarajia kabisa tena aliuwawa kwa kuchinjwa.

Baada ya miezi kadhaa nilikuwa mjamzito na Maiko alinitembelea tena pale hospitali, akasema ameutamani sana ujauzito wangu, kwanza nilimshangaa pili nilimuogopa kutokana na yule binti na tatu niliogopa kuwaambia watu kuwa yule jamaa ndiye muuaji wa yule binti.

maiko aliendelea na hoja yake ya kutamani ujauzito wangu, nikaona ni kitu cha ajabu kwa mwanaume kutamani ujauzito inamaana anatamani awe yeye mjamzito au ni nini.

Akaingia nesi fulini mule ofisini, alipomuona Maiko alishtuka sana na kutoka mule ofisini, badae nikamfata na kumuuliza kwanini alishtuka akaniambia kuwa Maiko si mtu mzuri, mi nikahisi kuwa labda nae anamjua Maiko kuwa anahusika na kile kifo cha yule mdada. Halafu akanipa onyo kuwa nisipende kuwa karibu na Maiko.

Siku nyingine Maiko alikuja ofisini na kuniletea pesa nyingi sana za asante, nikashangaa ni za nini ila sikuziacha nikazipokea na siku iliyofuata mimba yangu ilitoka, kwakweli nilihudhunika sana kwani yule angekuwa mwanangu wa pili baada ya Tulo ila bado sikuelewa.

Kuna siku Maikom alikuja na kunikuta na mwanangu Tulo ofisini aliniambia kuwa amempenda sana mwanangu na atafurahi siku akifanya nae kazi moja, nikapatw na uoga na mashaka ndipo nilipoamua kumsafirisha mwanangu Tulo na kumpeleka Dar es salaam akaishi na shangazi yake.

Yule nesi alinifata tena na kuniambia kuwa Maiko si mtu mzuri, anafuga majini nyumbani kwake hata mimba yangu iliyotoka yeye ndio chanzo na hawezi kuacha kunifatilia sababu nimeshaonja utamu wa pesa yake.

Hapo ndipo nilipoamua moja, niliacha kazi na kurudi kwetu Morogoro ili niepukane na balaa la Maiko.

Nadhani hata huyo askari aliyekabwa itakuwa ni hayo majini ya Maiko yalitaka msindikizaji, na hali ya hapa kwake nadhani ni hayo majini"


INAENDELEA...

Post a Comment

0 Comments