Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Mwanamke jini sehemu ya pili (02)

 


Nikagundua kuwa kulikuwa na vifungulio vingine vilivyokuwa chini ya na juu ya mlango. Nikapeleka mkono wangu juu na kupapasa. Nikapata kifungulio kimojawapo nikakivuta chini.

“Amour umeona nini?” Sauti ya Zena sasa ikasikika kutokea mlango wa uani.
Bila shaka alikuwa akinichungulia kupitia mlango huo. Sikutaka hata kugeuka nyuma kumtazama. Nikainama chini ili nifungue kifungulio kingine kilichokuwa chini.
“Amour usiondoke!” Zena aliendelea kuniambia.
Aliposikia nafungua kile kifungulio cha mlango cha chini akaniambia.
“Hebu nisubiri”
Sasa nikazisikia hatua zake akinifuata kwa mwendo wa haraka. Kwa vile miguu yake ilikuwa na kwato, kwato hizo zilisikika kama za farasi wa kwenye sinema, “Kwa…kwa…kwa…”
Mwili ukanisisimka. Nikajiambia sasa nakufa.
Nikauvuta mlango. Licha ya kufungua vifungulio vya juu na chini. Mlango haukufunguka.
Kwato za Zena zilikuwa zimeshanikaribia. Akili yangu iliunda picha nikikabwa na mwanamke huyo wa kijini na kunifyonza damu yangu kupitia kenye tundu za pua yangu…
Mkono wa Zena wenye kucha ndefu ukanishika kwenye bega. Nikaukutua…
“We Amour nini…?” akaniambia kwa hamaki baada ya kuukutua mkono wake.
Niliuvuta tena ule mlango kwa nguvu. Safari hii ukafunguka. Zena alikuwa ameshanishika shati kwa nyuma. Nikapiga hatua kutoka nje. Zena akaliachia shati.
“We Amour…utaona!” akaniambia.
Nilikuwa nimeshavuka kizingiti cha mlango.
“Hutakwenda popote” Sauti ya Zena iliyokuwa na hasira ikasikika nyuma yangu.
Wakati napiga hatua kutoka nje niliona nimetokea nje ya ile nyumba lakini Zena aliponiambia “Hutakwenda popote” nikaona nimetokea kwenye eneo jingine ambalo sikulielewa. Lile jumba la Zena sikuliona tena. Nikajiona kama nimo ndani ya pango la kutisha lenye njia nyembamba ya kupita.
Vile nilivyokuwa nakimbia niliendelea kukimbia ndani ya hilo pango nikiifuata ile njia nyembamba. Kwenye kuta za mawe za lile pango kulikuwa kumewekwa mishumaa iliyokuwa inawaka.
Kadiri nilivyokimbia nilikutana na njia zingine zilizonichanganya. Sikuweza kujua nishike njia ipi. Kadhalika kulikuwa na mashimo yaliyokuwa yakifuka moshi. Wakati nakimbia niligundua nilikuwa nikizunguka tu ndani ya pango hilo
kwani nilikuwa nikitokea mahali pale pale nilipoanzia kukimbia.
Nikajaribu kushika njia nyingine ambayo nilihisi ingeweza kunitoa ndani ya pango hilo, nikajikuta nimetokea kwenye mlango kama mlango wa nyumba. Nikaufungua ule mlango na kuchungulia ndani. Nikaona kumesakafiwa na kulikuwa na kuta kama za nyumba. Kuta hizo zilikuwa zimepakwa rangi ya samawati.
Nikaingia ndani na kukutana na hewa safi yenye harufu ya mawaridi. Sasa nilikuwa kwenye ukumbi mpana ambao haukuwa na kitu chochote. Nilitembea kwenye ukumbi huo uliokuwa kimya huku nikiwa nimejaa hofu.
Sikujua nilikuwa nimetokea katika nyumba gani na inayoshi nani. Mazingira yaliyonifikisha hapo yalinifanya nipate hofu. Nilikuta mlango uliokuwa wazi, nikaingia katika huo mlango. Nilimkuta mzee mmoja aliyevaa shuka nyeupe akiwa ameketi kwenye mswala.
Alikuwa amejifunga kilemba kirefu kama muarabu. Mwenyewe pia alionekana kama muarabu. Alikuwa na ndevu ndefu na sharafa.
Wakati naingia katika hicho chumba alichokuwemo, mzee huyo alikuwa ameinama akisoma kitabu. Kitabu chenyewe kilikuwa ni kile nilichomuazima Zena.
Nikasimama mbele yake na kumtazama. Mzee alikuwa akiendelea kufungua karasa.
Nikamuamkia.
“Shikamoo mzee”
Mzee akainua kichwa na kunitazama. Macho yake yalikuwa madogo ya kijivu.
“Marahaba” akaniitikia. Sauti yake ilikuwa na lafidhi ya kiarabu.
“Mzee samahani, naomba msaada wako” nikamwambia.
“Msaada gani?”
“Mimi sijui nilivyofika hapa, ninaomba unioneshe njia ya kutoka nje”
“Unasema hujui ulivyofika hapa?”
“Sijui, nimejiona tu nikitokea katika nyumba hii”
“Kwani unatoka wapi?”
“Ninatoka katika nyumba ya msichana mmoja ambaye nilimuazima kitabu changu, wakati ule natoka nikaona nimetokea kwenye pango. Baadaye tena naona nimetokea kwenye nyumba hii”
“Wakati unatoka ulimuaga mwenyeji wako?”
“Sikumuaga”
“Kwanini hukumuaga?”
Hapo nikanyamaza kimya, sikuwa na jibu. Nilishindwa kumueleza niliyoyaona kwa sababu yule mzee naye sikujua alikuwa ni nani.
Pakapita kimya cha sekunde kadhaa. Yule mzee alikuwa akinitazama akisubiri jibu langu na mimi nilikuwa nikimtazama uso wangu ukiwa umenywea ukionesha sikuwa na jibu.
“Ulifanya kosa kutomuaga mwenyeji wako na ndio sababu unahangaika. Siku nyingine usirudie kosa kama hilo” Yule mzee akaniambia.
Akanyamaza kimya kisha akanimabia.

Akanyamaza kimya kisha akanimabia.
“Mlango huu hapa, nenda zako”
Alinionesha mlango uliokuwa ubavuni kwake.
“Asante sana, nashukuru” nikamwambia huku nikivuta hatua kuelekea kwenye mlango huo.
Mzee alikuwa akinitazama.
Niliufungua ule mlango nikatazama nje na kutoka. Nilipotoka nikajiona niko nje ya nyumba ya Zena! Jambo hilo lilinipa mshangao lakini nilishukuru nikaanza kutoka mbio nikiwa pekupeku. Sikukumbuka tena ile pikipiki yangu.
Nilikimbia kwa miguu nikiwa peke yangu usiku ule katika njia iliyokuwa na vichaka vinavyotisha. Vivuli vya miti iliyokuwa ikitikiswa na upepo vilizidi kunitisha lakini sikuwa na la kufanya, nilikuwa nimeshajitolea.
Baada ya nusu saa nikawa nimefika kwenye barabara ya lami nikakata kushoto na kuendelea kukimbia. Nilipokuwa ninakikaribia kituo cha polisi cha Mabawa nikaanza kuchoka. Nguvu zilikuwa zimeniishia kabisa.
Nilisimama huku nikitweta. Nikatazama nyuma. Kulikuwa kimya. Kile kituo cha polisi kilinipa matumaini nikaanza kutembea taratibu. Nilikipita kituo hicho nikaendelea kutembea hadi nikafika nyumbani kwangu.
Nilifungua mlango nikaingia nyumbani kwangu. Mwili wote ulikuwa unaniuma. Shati langu lilikuwa limeloa kwa jasho. Nilivua nguo nikaenda kuoga. Niliporudi chumbani kwangu nikasikia dirisha langu linagongwa.
Nilikuwa nimeshazima taa na kupanda kitandani. Nikatega masikio yangu kusikiliza. Dirisha liliendelea kugongwa.
“Amour! Amour!” Sauti ya kiume ikawa inaita jina langu.
Nilijaribu kuifikiria ilikuwa sauti ya nani lakini sikuweza kutambua ilikuwa sauti ya nani miongoni mwa watu niliokuwa nawafahamu. Nikaamua kunyamaza kimya.
Sauti ile ikaendela.
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Amour fungua mlango nimekuletea viatu vyako na funguo za pikipiki yako”
Nilishituka niliposikia maneno yale nikajua mtu aliyekuwa akiniita alitoka kule kwa Zena ambako niliacha pikipiki yangu na viatu vyangu.
Nikajiambia kwa vyovyote vile atakuwa si mtu bali ni jini. Hofu yangu ilianzaa tena upya. Moyo ukaanza kunienda mbio.
Dirisha liliendelea kugongwa na ile sauti ikaendelea kuniambia nifungue mlango nichukue viatu vyangu pamoja na funguo za pikipiki yangu niliyoiacha kwa Zena.
Sikujibu chochote, nikaendelea kubaki kimya.
Baada ya muda kidogo ile sauti ikapotea, kukawa kimya. Nikasubiri kuona kama kutatokea kitu chochote, sikuona kitu. Nikaendelea kuwa macho huku hofu ikiwa imenitawala hadi nikapitiwa na usingizi.
Nilichelewa sana kuamka asubuhi. Nilishukuru kuwa ilikuwa ni jumapili siku ambayo ni ya mapumziko, vinginevyo ningechelewa kufika kazini.
Mara tu niliposhuka kitandani nilitazama saa. Ilikuwa saa mbili na robo. Nikatoka nje nikiwa nimejifunga taulo. Wakati nafungua mlango wa mbele nikaona viatu vyangu nilivyoviacha kwa yule msichana, vimewekwa mbele ya mlango wangu pamoja na funguo za pikipiki yangu. Nikashituka.
Wakati huo mpangaji mwenzangu wa upande wa pili alikuwa anatoa pikipiki yake. Nikamuita.
“Alphonce!”
Alphonce akanifuata na kunisalimia.
“Kuna tatizo limenitokea” nikamwambia.
“Tatizo gani?” akaniuliza.
“Unaviona hivi viatu?”
“Ninaviona”
“Sasa njoo ndani nikueleze mkasa ulionitokea jana usiku”
Alphone akiwa amepatwa na mshangao aliigesha pikipiki yake karibu na mlango wangu akaingia ndani. Nilimkaribisha sebuleni kwangu. Vile viatu na funguo za pikipiki yangu nilikuwa nimeviondoa pale mlangoni.
“Haya nieleze kuna nini?” Alphonce akaniuliza.
Nikamueleza ule mkasa ulionitokea usiku uliopita uliosababisha nirudi nyumbani kwangu usiku nikiwa pekupeku.
“Wakati nimerudi niko chumbani kwangu, nikasikia sauti ya mtu kwenye dirisha akiniambia ameniletea viatu vyngu na funguo za pikipiki. Kwa kweli sikumjibu. Nilinyamaza kimya”
Wakati ninamueleza Alphonce alikuwa ameshangaa kweli kweli.
“Halafu ikawaje?” akaniuliza.
“Baada ya kunyamaza kimya ile sauti sikuisikia tena, sasa hii leo asubuhi nafungua mlango nakuta viatu vyangu na funguo za pikipiki yangu vimewekwa mbele ya mlango wangu”
“Una maana yule mwanamke alikuwa ni jini?”
“Alikuwa jini”
“Na huyo aliyekuletea hivyo viatu na funguo ni nani?”
“Sijui, lakini watakuwa ni wamoja”
“Unajua mimi huwa nazisikia habari za majini lakini siamini kama kuna viumbe hao. Unaonaje kama tutakwenda mimi na wewe kwenye hiyo nyumba?’
“Mimi nilikuwa nimepanga kwenda polisi kwa sababu ya pikipiki yangu”
“Twende huko Mikanjuni kwanza, kama pikipiki yako hutaipata ndio utakwenda polisi kwa ajili ya kupata msaada zaidi”
“Sawa. Subiri nivae tutoke”
“Nitakusubiri”
Nikanyanyuka na kuingia chumbani kwangu. Baada ya nusu saa nikatoka nikiwa nimeshavaa.
“Twende” nikamwambia Alphonce.
Tukatoka. Alphonce alinipakia kwenye pikipiki yake tukaelekea Mikanjuni. Nilimuelekeza mahali ilikokuwa ile nyumba ya yule msichana, tukaenda hadi mahali hapo lakini jambo la ajabu lililotokea ni kuwa ile nyumba hatukuiona. Badala yake tuliona eneo lote lilikuwa makaburi matupu ya watu wa zamani.
Nikapatwa na mshangao. Wakati naangalia angalia nikaiona pikipiki yangu ikiwa kando ya mti. Mti huo ndio ule uliokuwa uani mwa nyumba ya Zena. Kando yake palikuwa na kisima ambacho yule msichana na mwenzake walikuwa wakioga.
Wakati ule kile kisima hakukuwepo tena, badala yake tuliona dimbwinl maji ya mvua.
“Pikipiki yangu ile pale!” nikamwambia Alphonce ambaye naye alikuwa ameshangaa.
“Sasa mbona iko kwenye makaburi na hapana nyumba?” akaniuliza.
“Na mimi ndio nashangaa. Ile pikipiki niliiweka uani mwa hiyo nyumba niliyokwambia. Ule mti unaouona ulikuwa uani na lile dimbwi la maji kilikuwa ni kisima”
“Hebu twende pale karibu”

Tukaenda hadi pale ilipokuwa pikipiki yangu. Karibu yake palikuwa na kaburi la zamani. Lilikuwa limejengewa kiukuta kilichoandikwa jina la Zena binti Ashraf.
Tarehe aliyokufa pia iliandikwa pamoja na tarehe aliyozikwa. Alikufa tarehe kumi mwezi wa kwanza mwaka 1920.
“Yule msichana aliniambia anaitwa Zena na hili kaburi lina jina la Zena, sasa hata sielewi” nikasema.
Nikamsikia Alphonce akitoa mguno. Hakusema chochote. Nikaiangalia pikipiki yangu.
“Ichukue tuondoke, huku Tanga kuna mambo ya ajabu sana”
Nikatia ufunguo na kuikokota hadi kwenye barabara ya vumbi. Nilipoiwasha ikawaka.
“Twenzetu” Alphonce akaniambia huku akipanda pikipiki yake.
Nikapanda pikipiki yangu, tukaondoka.Tukiwa njiani tunarudi tulikuwa tunazungumza.
“Jana ulikunywa pombe?” Alphonce akaniuliza.
“Mimi situmii ulevi wa aina yoyote”
“Sasa ilikuwaje, wewe umeniambia uliingia katika nyumba lakini pale ni makaburini?”
“Yaani pamebadilika. Ilikuwa ni nyumba. Yale makaburi hayakuwepo, ndio nayaona sasa”
“Ni miujiza mikubwa lakini shukuru Mungu umenusurika na pikipiki yako umeipata”
“Aisee nashukuru sana. Na yule mwanamke nikimuona nitamkimbia mbali sana. Sitataka anikaribie, anaweza kutoa roho yangu”
“Mimi sasa naamini kweli majini wapo na wanajigeuza binaadamu”
Tulipofika Mabawa mimi nilielekea nyumbani kwangu, Alphonce akaenda kwenye shughuli zake.
Siku ile nilishinda nikiwa na mawazo ya yule msichana. Kwa kweli alikuwa amenitia hofu sana. Sikutaka nikutane naye tena. Ili kujiondoa wasi wasi niliwaeleza mkasa ule watu mbali mbali niliokuwa nawafahamu akiwemo kaka yangu. Wote walinipa matumaini wakaniambia hakutakuwa na madhara yoyote yatakayonitokea.
Baada ya wiki mbili nilikuwa narudi nyumbani kwangu kutoka kazini. Nilikuwa naendesha pikipiki yangu taratibu. Tukio lile la wiki mbili zilizopita nilikuwa nimeshaanza kulisahau.
Wakati nikiwa katika barabara ya Pangani nikikaribia kwenye mzunguko wa barabara nne uliokuwa eneo la mabanda ya papa nikamuona msichana amesimama kando ya barabara akinipungia mkono. Nilipomtupia macho mara moja nikatambua alikuwa ni Zena! Moyo ulinishituka sana.
Hapo hapo nikaongeza mwendo. Nilitakiwa nisimame kwenye mzunguko huo wa barabara nne uliokuwa mbele yangu. Lakini sikusimama. Gari lililokuwa linakuja kutoka upande wangu wa kushoto ambalo nilitakiwa nilipishe lilinikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme na kisha kuingia kwenye mfereji wa maji ya mvua.
“Nguzo hiyo iling’oka, waya za umeme zikatikisika na kutoa cheche za moto. Mimi nikaendelea kwenda mbio na kushika barabara ya Pangani kabla ya kuingia katika eneo nililokuwa ninaishi.
Nilipofika nyumbani niliingiza pikipiki yangu ndani nikakaa sebuleni na kuanza kuwaza. Nilijua kuwa nilikuwa nimesababisha ajali kutokana na kuvunja sheria za barabarani baada ya kumuona yule msichana.
Kwa vile nilikuwa na hakika kwamba namba za usajili za pikipiki yangu zilionekana, nilijiambia sitaitimia tena pikipiki yangu hadi lile tukio litakaposahalika.
Zikapita tena wiki mbili. Nilikuwa siitumii tena ile pikipiki yangu kwa kuogopa kukamatwa na polisi. Siku hiyo nilikuwa niko kazini nikawaona polisi wawili wa usalama barabarani wakiingia. Mfanyakazi wa kwanza waliyekutana naye niikuwa mimi.
Wakanisalimia na kuniambia walikuwa wanamtaka Amour.
Amour nilikuwa ni mimi.
Nikasita kuwajibu. Badala yake nikawauliza.
“Amour nani?”
“Hatujui anaitwa Amour nani, kwani hapa kuna Amour wangapi?”
“Kuna Amour mmoja tu”
“Yuko wapi?”
“Ni mimi”
“Sasa mbona hutuambii, unatuuliza maswali. Pikipiki yako iko wapi?”
“Mmejuaje kama nina pikipiki”
“Tumeelekezwa. Tafadhali tuambie”
“Iko nyumbani”
“Ina namba hizi?”
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Polisi huyo alinionesha kikaratasi kilichokuwa kimeandikwa namba za usajili za pikipiki yangu.
“Ndiyo” nikamkubalia polisi huyo baada ya kukiangalia kile kikaratasi.
“Tunakuhitaji wewe na hiyo pikipiki yako”
“Mimi nina nini na pikipiki yangu ina nini?” nikawauliza.
“Uliwahi kufanya makosa ya barabarani wiki mbili zilizopita”
“Sijawahi kufanya kosa lolote labda mmeifananisha pikipiki yangu”
“Tutajua huko kituo cha polisi. Kwa sasa tutaondoka na wewe twende nyumbani kwako tuichukue hiyo pikipiki, twende nayo kituo cha polisi”
Sikuwa na la kupinga. Nikakakamatwa. Polisi hao ambao walikuja na gari lao walinipakia kwenye gari hilo, nikaenda nao nyumbani kwangu.
Niliwatolea pikipiki yangu, walipoiona tu wakasema ndiyo waliyokuwa wanaitafuta kwa karibi wiki mbili.
Nikafikishwa kituo cha polisi. Huko ndiko nilikoelezwa kuwa tarehe fulani siku fulani nilisababisha ajali eneo la Mabanda ya Papa baada ya kuendesha pikipiki kwa uzembe na kuvunja sheria za barabarani.
Nikaelezwa kuwa kutokana na uzembe wangu wa kutosimama mahali ambapo nilipaswa kusimama ili nipishe gari lililokuwa linatoka kuliani kwangu, nilisababisha gari hilo aina ya Toyota Landa Cruiser linikwepe na kugonga nguzo ya umeme na kutumbukia kwenye mfereji.
Ingawa nilijitahidi kukana kosa hilo nilifikishwa mahakamani baada ya kulala ndani kwa siku moja. Katika mahakama ya Chumbageni nikashitakiwa kwa makosa matatu.
Kosa la kwanza lilikuwa kuendesha kwa uzembe, kosa la pili kusababisha ajali na kosa la tatu kuharibu mali na kulitia hasara shirika la Umeme iliyokadiriwa kufikia shilingi milioni kumi na mbili.
Niliyakana mashitaka yote na kumuomba hakimu anipe dhamana. Ndugu zangu walikuwa wamejitokeza kutaka kuniwekea dhamana.
Hakimu aliruhusu dhamana iliyokuwa na masharti magumu. Hata hivyo ndugu zangu walimudu masharti yote waliyopewa wakanitoa.
Shauri hilo lilikuwa limeahirishwa kwa wiki moja. Nilipoachiwa kwa dhamana ndugu zangu walinipeleka nyumbani kwa mama yetu ambaye wakati huo alikuwa yuko hai. Nikawaeleza mkasa uliokuwa umenitokea kuanzia kisa kile cha Zena aliponipeleka nyumbani kwake hadi siku ile nilipomuona tena na kusababisha ile ajali.
Mama yangu na ndugu zangu walishangaa waliposikia kisa hicho.
“Inabidi uende kwa mganga, huyo jini atakuletea matatizo” Mama akaniambia.
“Tatizo la Amour nikuwa ana usiri sana, kwanini hakutueleza tangu mapema?” kaka yangu akanilaumu.
“Sikujua kama yangekuwa makubwa kiasi hiki?’ nikajitetea.
Jioni ya siku ile nikapelekwa kwa mganga mmoja aliyekuwa akiishi Mnyanjani. Nilikuwa mimi, mama yangu na kaka Abdul.
Tukamueleza mganga tatizo langu. Mganga akatazama ramli kisha akatuambia.
“Amour amekumbwa na jini anaitwa Ummi Subian, ni jini wa kike ambaye amemfanyia vitisho na kumsababishia kukabiliwa na kesi”
“Huyo jini ataendelea kumfuata tena?’ Mama yangu akamuuliza mgamga.
“Alilolitaka huyo jini ameshalipata, hatamfuata tena kwa sababu anajua atafungwa. Hii kesi imemkalia vibaya” Mganga akasema.
“Sasa tunataka kuizima hii kesi, itawezekana?’ Abdul akamuuliza mganga.
“Itawezekana. Hakuna kisichowezekana”
“Tunataka utufanyie hiyo kazi, itagharimu shilingi ngapi?”
“Itgharimu shilingi laki moja na mbuzi mweusi”
“Punguza kidogo. Shilingi laki moja hatuna”
“Sipunguzi. Kama nilivyowambia hii kesi imekaa vibaya. Kazi inayotakiwa ni kubwa”
“Haya, tutatoa hiyo shilingi laki moja”
“Ninataka na mbuzi mweusi na kipande cha kaniki. Siku muafaka wa kazi yenu ni jumamosi”
“Kwa hiyo tuje jumamosi” Abdul akamuuliza.
“Mje siku ya jumamosi saa mbili asubuhi pamoja na hivyo vitu”
“Sawa. Tumekuelewa.
Tukaondoka.
Siku ya jumamosi tukaenda tena kwa mganga huyo. Tulienda na gari aina ya Toyota ya wazi. Tulikuwa tumepakia mbuzi tuliyekuwa tumeagizwa.
Tulipofika, wasaidizi wa mganga huyo walitupokea tukakaribishwa ndani. Baada ya muda kidogo mganga akaanza kazi. Kazi ilianzia pale nyumbani kisha ikahamia makaburini.
Yule mbuzi alichinjwa akavalishwa ile kaniki na kuzikwa kwenye kaburi.
Mganga akatuambia.
“Kesi nimeshaizika”
“Sasa nitaachiwa au..” nikamuuliza.
“Utakwenda kusikia huko huko lakini kwa upande wangu hakuna kesi tena”
“Tunashkuru kama itakuwa hivyo” Mama akamwambia mganga.
Tuliporudi nyumbani kwa mganga tulimpa ile shilingi laki moja aliyotaka tukaondoka.
Nilipata matumaini sana, ingawa sikuwa na uzoevu na mambo ya kwenda kwa waganga. Tarehe ya kesi ilipowadia nilifika mahakamani nikasomewa tena mashitaka yangu, nikayakana.
Hakimu akasema alikuwa tayari kuanza kusikiliza shauri hilo. Upande wa mashitaka ukaeleza kwamba ulikuwa na mashahidi ambao walikuwa tayari kutoa ushahidi wao.
Hakimu akataka mashahidi hao waanze kuitwa ili watoe ushidi wao.
Akaitwa shahidi wa kwanza ambaye ni dereva wa Toyota iliyogonga nguzo ya umeme.
Akaeleza jinsi tukio zima lilivyotokea.
Baada ya kumaliza kutoa ushidi wake ikafika zamu yangu ya kumuuliza maswali.
“Unamjua huyo mtu aliyekuwa akiendesha hiyo pikipiki?” nikamuuliza.
“Ninamjua” akajibu.
“Ni nani?”
“Ni wewe”
“Nani alikwambia kwamba ni mimi?”
“Nilikuona mwenyewe”
“Ulipata muda gani wa kuniona na kunikariri wakati umesema gari lako liliingia kwenye mfereji na mimi nilikimbia?”
“Nilikuona kabla”
“Sasa mimi nakwambia siye huyo mtu, mmenifananisha tu”
“Ni wewe”
Baada ya mtu huyo kutoa ushahidi wake aliitwa shahidi mwingine, muuza machungwa katika eneo la Mabanda ya Papa.
Kumbe yeye ndiye aliyekuwa amewatajia polisi namba za pikipiki yangu. Siku ile ya ajali aliniona na aliiona pikipiki yangu. Akaieleza mahakama kuwa amekuwa akiniona mara kwa mara nikipita na pikipiki katika eneo lile.
Huku akiongozwa na Mwendesha Mashitaka wa serikali shahidi huyo aliiambia mahakama kuwa siku na tarehe hiyo alikuwa akiuza machungwa yake jirani na Barabara ya Pangani katika eneo hilo la Mabanda ya Papa.
“Nini kilitokea?” Mwendesha Mashitaka akamuuliza.
“Ilitokea ajali”
“Ilitokea ajali gani? Hebu tueleze”
“Kulikuwa na pikipiki moja inakuja kutoka barabara ya Taifa. Ile pikipiki ilitakiwa isimame kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo pale lakini haikusimama”
“Baada ya hapo nini kilitokea?’
“Kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruicer likitokea Gofu, lilikuwa linapita kwenye ule mzunguko likalazimika kuikwepa ile pikipiki. Katika kuikwepa pikipiki, gari hilo lilikwenda kugonga nguzo ya umeme”
“Baada ya kugonga nguzo ya umeme lilikwenda wapi?”
“Liliingia kwenye mfereji”
“Ni athari gani ilitokea baada ya nguzo ya umeme kugongwa?”
“Kwanza nguzo yenyewe ilivunjika halafu baadhi ya nyaya zilikatika na nyingine zilitoa cheche za moto hali iliyosababisha mfadhaiko mkubwa”
“Wakati tukio hilo linatokea, mwenye pikipiki alisimama”
“Hapana, hakusimama. Alipita moja kwa moja na kuendelea na safari yake”
“Wewe uliiona hiyo pikipiki?’
“Ndiyo niliiona”
“Ilikuwa ni aina gani”
“Kama sikosei ilikuwa aina ya Honda ya rangi nyeusi”
“Namba yake ya usajili uliiona”
“Niliiona”
Akaitaja. Ilikuwa ndio namba ya pikipiki yangu.

“Je aliyekuwa akindesha pikipiki hiyo ukimuona unaweza kumtambua?”
“Naweza kumtambua”
“Yuko hapa mahakamani?”
“Ndiyo yupo. Ni yule pale”
Akaninyooshea kidole mimi.
“Asante sana”
Baada ya mtu huyo kumaliza kutoa ushahidi wake, niliambiwa kama nina maswali nimuulize.
“Unajua hapa Tanga kuna pikipiki ngapi za aina ya Honda?” nikamuuliza.
“Ziko nyingi”
“Ambazo ni rangi nyeusi kama pikipiki yangu?’
“Ziko nyingi”
“Unawezaje kuzitofautisha?”
“Kivipi?”
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nina maana una uhakika gani kama pikipiki ulioiona ni yangu na si ya mtu mwingine?’
“Wewe unapita pale kila siku na pikipiki yako. Pikipiki yako ninaijua na wewe mwenyewe ninakujua”
“Je nikikwambia kwamba sikuwa mimi bali alikuwa mtu mwingine utakataa?’
“Ndiyo nitakataa”
“Sasa mimi nakwambia sikuwa mimi?”
“Alikuwa nani?”
“Sijui”
Yule mtu akanyamaza.
Mwendesha Mashitaka akasimama na kumuuliza yule mtu.
“Mtu uliyemuona siku hiyo ndiye huyo hapo au siye?”
“Ndiye yeye” shahidi akajibu.
Mwendesha Mashitaka kakaa.
Kesi ikaahirishwa kwa juma moja.
Kipindi kile cha kesi ile kilinifanya niwe mnyonge sana. Nilijiuliza kama nitatakiwa nilipe faini au fidia ya uharibifu uliotokea, nitalipa nini? Kwa vile uharibifu ulikuwa mkubwa niliamni fidia yake pia itakuwa kubwa. Nilijiuliza nitapata wapi pesa za kulipa fidia hiyo ambayo kwa vyovyote vile ingekuwa ni mamilioni ya pesa.
Kila wakati nilikuwa nikimlaani yule msichana wa kijini aliyenisababishia matatizo yale. Niliomba nisikutane naye tena milele na milele.
Siku ya kesi ilipowadia nillifika mahakamani. Upande wa Mashitaka uliendelea kupeleka mashahidi. Safari hii aliyesimamishwa kizimbani kutoa ushahidi alikuwa polisi wa usalama barabarani aliyepima ile ajali iliyotokea.
Alitoa vielelezo yake ikiwa ni pamoja na ramani ya ajali aliyokuwa ameichora.
Ramani hiyo ilionesha kuwa nilifanya kosa la kutosimama katika alama ya L iliyokuwa kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo eneo la Mabanda ya Papa.
Ramani hiyo iliendelea kuonesha kwamba wakati nafanya kosa hilo kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser likitokea upande wangu wa kulia ambalo nilipaswa kulipisha lipite lakini sikufanya hivyo.
Hivyo gari hilo lililazimika kunikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme inayomilikiwa na shirika la umeme na kuivunja.
Katika ushidi wake polisi huyo alieleza kwamba nguzo ya umeme niliyoivunja pamoja na nyaya zilizokatika zina thamani ya shilingi milioni kumi.
Akaeleza kwamba ili kurudisha mfumo wa upatikanaji umeme katika eneo hilo shirika la umeme litalazimika kutoa shilingi milioni kumi na tatu ikiwa ni pamoja na gharama ya ufundi.
“Pesa hizo zitapaswa zilipwe na mshitakiwa kwa sababu alifanya kosa hilo kwa uzembe na kutozingatia sheria za barabarani” akasema.
Hapo ndipo moyo wangu ulipotaharuki. Nitazitoa wapi shilingi milioni kumi na tatu za kuwalipa shirika la umeme? Nikajiuliza.
Polisi huyo alipomaliza kutoa ushahidi wake, hakimu aliniambia kama nina swali nimuulize.
Nilikuwa nimefadhaika sana kiasi kwamba sikuweza kuuliza swali lolote lakini niliona kukaa kimya kutaionesha mahakama kuwa kweli nilitenda kosa, nikamuuliza polisi huyo.
“Hiyo ramani uliyoitoa aliichora nani?”
“Niliichora mimi”
“Unapochora ramani ya ajali kama ile unapata maelezo kutoka kwa nani?”
“Kutoka kwa wale wahusika wa ajali na mashahidi”
“Kwa maoni yako mimi ni muhusika wa ajali?’
“Ndiyo”
“Nilikuwepo wakati unachora ramani hiyo?”
“Hukuwepo”
“Je niliweka saini yangu kuonesha kuwa nimekubaliana na ulichokichora?”
“Saini yako haipo”
“Kwa maana hiyo ni kwamba ramani uliyochora sikubaliani nayo”
“Kwanini saini yake haipo?” hakimu akamuuliza polisi huyo.
“Ni kwa sababu wakati tunachora ramani, yeye mwenyewe hakuwepo” Polisi huyo akajibu.
“Alikuwa wapi?”
“Alikuwa mafichoni, yaani baada ya kusababisha ile ajali alikimbia. Tulimpata wakati tukiwa tumeshachora ramani”
“Jibu umelisikia?” hakimu akaniuliza.
“Nimelisikia lakini halinihusu mheshimiwa, wananihusisha tu na hiyo ajali lakini sikuhusika mimi”
“Ushahidi umetolewa hapa kuwa ni wewe” Polisi huyo aliyekuwa akitoa ushahidi aliniambia.
“Sikubaliani na ushahidi huo” nikamjibu.
“Wewe mwenyewe umeonekana na kutambuliwa, pikipiki yako imeonekana na kutambuliwa na namba ya usajili ya pikipiki yako pia imeonekana na kutambuliwa, sasa unakataa nini?”
“Kwa vile sikuhusika lazima nikatae”
“Una swali jingine” hakimu akanuiliza.
“Sina swali jingine” nikamjibu.
Hakimu aliandika kisha akaamuru aitwe shahidi mwingine.
Shahidi aliyeitwa baada ya hapo alikuwa afisa wa shirika la umeume.
Ushahidi alioutoa ulihusu uharibifu uliosababishwa na ajali hiyo. Alitoa takwimu za gharama kama alizozitoa shahidi aliyemaliza kutoa ushahidi wake. Alipomaliza kutoa ushahidi huo nilimuuliza.
“Ulimuona mtu aliyesababisha ajali hiyo?’
“Sikumuona” akajibu. Ndilo jibu nililokuwa nalitaka.
“Kwa hiyo hujui ni nani aliyesababisha ajali hiyo?”
“Nimeambiwa kuwa ni wewe”
“Nimeshasema kuwa sikuwa mimi”
“Kama si wewe kwanini walikukamata?”
“Walinikamata kwa makosa. Wao ni binaadamu wanaweza kukosea”
Jibu hilo liliwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo kucheka kimya kimya.
“Mahakama ndio itajua kama ulikamatwa kwa makosa”
“Lakini kwa maoni yako kama mimi sikuhusika bado nitalazimika kulipia gharama uliyoitaja?”
“Suala hilo tunaliachia mahakama”
“Sawa”

“Kulikuwa na pikipiki moja inakuja kutoka barabara ya Taifa. Ile pikipiki ilitakiwa isimame kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo pale lakini haikusimama”
“Baada ya hapo nini kilitokea?’
“Kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruicer likitokea Gofu, lilikuwa linapita kwenye ule mzunguko likalazimika kuikwepa ile pikipiki. Katika kuikwepa pikipiki, gari hilo lilikwenda kugonga nguzo ya umeme”
“Baada ya kugonga nguzo ya umeme lilikwenda wapi?”
“Liliingia kwenye mfereji”
“Ni athari gani ilitokea baada ya nguzo ya umeme kugongwa?”
“Kwanza nguzo yenyewe ilivunjika halafu baadhi ya nyaya zilikatika na nyingine zilitoa cheche za moto hali iliyosababisha mfadhaiko mkubwa”
“Wakati tukio hilo linatokea, mwenye pikipiki alisimama”
“Hapana, hakusimama. Alipita moja kwa moja na kuendelea na safari yake”
“Wewe uliiona hiyo pikipiki?’
“Ndiyo niliiona”
“Ilikuwa ni aina gani”
“Kama sikosei ilikuwa aina ya Honda ya rangi nyeusi”
“Namba yake ya usajili uliiona”
“Niliiona”
Akaitaja. Ilikuwa ndio namba ya pikipiki yangu.
SASA ENDELEA
“Je aliyekuwa akindesha pikipiki hiyo ukimuona unaweza kumtambua?”
“Naweza kumtambua”
“Yuko hapa mahakamani?”
“Ndiyo yupo. Ni yule pale”
Akaninyooshea kidole mimi.
“Asante sana”
Baada ya mtu huyo kumaliza kutoa ushahidi wake, niliambiwa kama nina maswali nimuulize.
“Unajua hapa Tanga kuna pikipiki ngapi za aina ya Honda?” nikamuuliza.
“Ziko nyingi”
“Ambazo ni rangi nyeusi kama pikipiki yangu?’
“Ziko nyingi”
“Unawezaje kuzitofautisha?”
“Kivipi?”
“Nina maana una uhakika gani kama pikipiki ulioiona ni yangu na si ya mtu mwingine?’
“Wewe unapita pale kila siku na pikipiki yako. Pikipiki yako ninaijua na wewe mwenyewe ninakujua”
“Je nikikwambia kwamba sikuwa mimi bali alikuwa mtu mwingine utakataa?’
“Ndiyo nitakataa”
“Sasa mimi nakwambia sikuwa mimi?”
“Alikuwa nani?”
“Sijui”
Yule mtu akanyamaza.
Mwendesha Mashitaka akasimama na kumuuliza yule mtu.
“Mtu uliyemuona siku hiyo ndiye huyo hapo au siye?”
“Ndiye yeye” shahidi akajibu.
Mwendesha Mashitaka kakaa.
Kesi ikaahirishwa kwa juma moja.
Kipindi kile cha kesi ile kilinifanya niwe mnyonge sana. Nilijiuliza kama nitatakiwa nilipe faini au fidia ya uharibifu uliotokea, nitalipa nini? Kwa vile uharibifu ulikuwa mkubwa niliamni fidia yake pia itakuwa kubwa. Nilijiuliza nitapata wapi pesa za kulipa fidia hiyo ambayo kwa vyovyote vile ingekuwa ni mamilioni ya pesa.
Kila wakati nilikuwa nikimlaani yule msichana wa kijini aliyenisababishia matatizo yale. Niliomba nisikutane naye tena milele na milele.
Siku ya kesi ilipowadia nillifika mahakamani. Upande wa Mashitaka uliendelea kupeleka mashahidi. Safari hii aliyesimamishwa kizimbani kutoa ushahidi alikuwa polisi wa usalama barabarani aliyepima ile ajali iliyotokea.
Alitoa vielelezo yake ikiwa ni pamoja na ramani ya ajali aliyokuwa ameichora.
Ramani hiyo ilionesha kuwa nilifanya kosa la kutosimama katika alama ya L iliyokuwa kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo eneo la Mabanda ya Papa.
Ramani hiyo iliendelea kuonesha kwamba wakati nafanya kosa hilo kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser likitokea upande wangu wa kulia ambalo nilipaswa kulipisha lipite lakini sikufanya hivyo.
Hivyo gari hilo lililazimika kunikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme inayomilikiwa na shirika la umeme na kuivunja.
Katika ushidi wake polisi huyo alieleza kwamba nguzo ya umeme niliyoivunja pamoja na nyaya zilizokatika zina thamani ya shilingi milioni kumi.
Akaeleza kwamba ili kurudisha mfumo wa upatikanaji umeme katika eneo hilo shirika la umeme litalazimika kutoa shilingi milioni kumi na tatu ikiwa ni pamoja na gharama ya ufundi.
“Pesa hizo zitapaswa zilipwe na mshitakiwa kwa sababu alifanya kosa hilo kwa uzembe na kutozingatia sheria za barabarani” akasema.
Hapo ndipo moyo wangu ulipotaharuki. Nitazitoa wapi shilingi milioni kumi na tatu za kuwalipa shirika la umeme? Nikajiuliza.
Polisi huyo alipomaliza kutoa ushahidi wake, hakimu aliniambia kama nina swali nimuulize.
Nilikuwa nimefadhaika sana kiasi kwamba sikuweza kuuliza swali lolote lakini niliona kukaa kimya kutaionesha mahakama kuwa kweli nilitenda kosa, nikamuuliza polisi huyo.
“Hiyo ramani uliyoitoa aliichora nani?”
“Niliichora mimi”
“Unapochora ramani ya ajali kama ile unapata maelezo kutoka kwa nani?”
“Kutoka kwa wale wahusika wa ajali na mashahidi”
“Kwa maoni yako mimi ni muhusika wa ajali?’
“Ndiyo”
“Nilikuwepo wakati unachora ramani hiyo?”
“Hukuwepo”
“Je niliweka saini yangu kuonesha kuwa nimekubaliana na ulichokichora?”
“Saini yako haipo”
“Kwa maana hiyo ni kwamba ramani uliyochora sikubaliani nayo”
“Kwanini saini yake haipo?” hakimu akamuuliza polisi huyo.
“Ni kwa sababu wakati tunachora ramani, yeye mwenyewe hakuwepo” Polisi huyo akajibu.
“Alikuwa wapi?”
“Alikuwa mafichoni, yaani baada ya kusababisha ile ajali alikimbia. Tulimpata wakati tukiwa tumeshachora ramani”
“Jibu umelisikia?” hakimu akaniuliza.
“Nimelisikia lakini halinihusu mheshimiwa, wananihusisha tu na hiyo ajali lakini sikuhusika mimi”
“Ushahidi umetolewa hapa kuwa ni wewe” Polisi huyo aliyekuwa akitoa ushahidi aliniambia.
“Sikubaliani na ushahidi huo” nikamjibu.
“Wewe mwenyewe umeonekana na kutambuliwa, pikipiki yako imeonekana na kutambuliwa na namba ya usajili ya pikipiki yako pia imeonekana na kutambuliwa, sasa unakataa nini?”
“Kwa vile sikuhusika lazima nikatae”
“Una swali jingine” hakimu akanuiliza.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Sina swali jingine” nikamjibu.
Hakimu aliandika kisha akaamuru aitwe shahidi mwingine.
Shahidi aliyeitwa baada ya hapo alikuwa afisa wa shirika la umeume.
Ushahidi alioutoa ulihusu uharibifu uliosababishwa na ajali hiyo. Alitoa takwimu za gharama kama alizozitoa shahidi aliyemaliza kutoa ushahidi wake. Alipomaliza kutoa ushahidi huo nilimuuliza.
“Ulimuona mtu aliyesababisha ajali hiyo?’
“Sikumuona” akajibu. Ndilo jibu nililokuwa nalitaka.
“Kwa hiyo hujui ni nani aliyesababisha ajali hiyo?”
“Nimeambiwa kuwa ni wewe”
“Nimeshasema kuwa sikuwa mimi”
“Kama si wewe kwanini walikukamata?”
“Walinikamata kwa makosa. Wao ni binaadamu wanaweza kukosea”
Jibu hilo liliwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo kucheka kimya kimya.
“Mahakama ndio itajua kama ulikamatwa kwa makosa”
“Lakini kwa maoni yako kama mimi sikuhusika bado nitalazimika kulipia gharama uliyoitaja?”
“Suala hilo tunaliachia mahakama”
“Sawa”
INAENDELEAA

Post a Comment

0 Comments