Ticker

6/recent/ticker-posts

Ad Code

Responsive Advertisement

Simulizi: Uchawi wa mama mkwe sehemu ya kumi (10) MWISHOOO


Akaendelea: “Cha kushangaza ni kwamba yule mchawi aliyekuwa amenasa kwenye nyumba ya jirani yenu hatukumkuta mahabusu!”

“He! Ina maana askari aliyekuwa zamu kamtorosha?” nilihoji.

“Sisi tumeshangazwa, askari wote waliokuwa zamu usiku tumewaweka ndani baada ya kuwahoji lakini wote wanasema, hawakula njama za kumtorosha na sisi tunaamini kwamba ametoka kishirikina,” alisema yule kamanda.

“Sasa itakuwaje?”


“Itabidi asakwe na akamatwe, kwa sababu ni dhahiri kwamba ametoka mahabusu kishirikina,” alisema kamanda huyo.

Alinyamaza kidogo, akachukuwa kiwiko cha simu kisha kubonyeza vitufe.

“Haloo, hebu nipe kiongozi wa hapo kaunta,” alisema kamanda lakini aliyekuwa akizungumza naye hakuweza kusikika.

“Niletee lile jalada lenye maelezo ya askari wetu tuliowaweka ndani.”

Baada ya kutoa amri hiyo alifika askari mmoja ambaye alionekana ni sajenti kwa kuwa alikuwa na V tatu kwenye mkono wake kwa juu karibu na bega.

Askari huyo alishindilia guu chini, akapiga saluti, “Jambo afande?” akasema.

“Jambo,” akapokea jalada na kugeuza kutoka alikotoka. Kamanda alituangalia huku akipekua makaratasi yaliyoambatanishwa ndani ya jalada hilo.


“Humu ndani yule mchawi haijaelezwa anakaa wapi, kati yenu kuna mtu anajua anakaa wapi?”

Mimi na mume wangu tuliangaliana, tulitikisa kichwa kuashiria kuwa hakuna kati yetu anayejua nyumbani kwa mchawi yule, mume wangu akajibu:


“Hatujui anakaa wapi, lakini katika maelezo yake aliyoyatoa kwenu hakutaja anakokaa?”

“Alaaa, hilo sikulitambua lilinipita, ngoja tuone.”

Alifungua jadala lile alilopewa na yule askari na kusoma. Alikuwa kila akisoma anatikisa kichwa kama vile kaambiwa jambo na kulikubali.


“Kumbe ameandikisha hapa kuwa anakaa Wapiwapi, itabidi nitume askari kule wakafuatilie, umenikumbusha jambo zuri sana.”


Sisi kuhusu huyo mchawi tuliona ni jambo ambalo halituhusu. Tulimuaga yule kamanda na kutoka nje ya ofisi yake. Habari zilizagaa mjini kwamba mama mkwe amefariki dunia.Kulikuwa na maelezo ya kutofautiana kati ya kundi moja lililokuwa likijadili tukio hilo na lingine. Kuna waliokuwa wakisema aliteswa sana na askari na ndiyo maana akaaga dunia na wapo waliosema kwamba hakufa, ametoka selo na watu kuona kama amefariki dunia.


Hata hivyo, hoja hiyo ilikuwa inapingwa na baadhi ya watu ambao walisema kama ni kutoka angetoka akiwa hai kama alivyotoweka mchawi mwenzake.Hoja hizo tulikuwa tunazisikia njiani wakati tunarudi nyumbani, tulikuwa tunakuta makundi ya watu wanajadili, bahati nzuri ni kwamba hakuna hata mtu aliyekuwa akijua sisi tulikuwa wahusika wakuu.


Naamini kama wangejua waliyekuwa wanamjadili alikuwa mama mkwe wangu, naamini safari yetu ya kurudi nyumbani ingekuwa ngumu kwani tungesumbuliwa ili tuwape ufafanuzi. Tulifika nyumbani na kukuta tayari ndugu na majirani wamefurika.


Moja kwa moja kikao cha wanandugu kilianza na mume wangu aliwapa taarifa rasmi ya nini kimetokea kule kituo cha polisi. Wengine wakiwa na hamu ya kuona maiti ya mama mkwe kwa kuamini kuwa atakuwa siye.

“Wewe wachawi unawajua? Huyo kajibadili tu, mwenyewe atakuwa katoweka na utasikia yupo sehemu fulani,” alisikika akisema mama mmoja ambaye sikuwa namjua kabisa wala siyo jirani.


Kwa upande wa tulipoketi akina mama mengi yalizungumzwa, wengine wakiwa na hamu ya kuona maiti ya mama mkwe kwa kuamini kuwa atakuwa siye.


“Wewe wachawi unawajua? Huyo kajibadili tu, mwenyewe atakuwa katoweka na utasikia yupo sehemu fulani,” alisikika akisema mama mmoja ambaye sikuwa namjua kabisa.“

Si umesikia yaliyotokea huko polisi?” aliuliza mama mwingine aliyekuwa amejitanda ushungi.

“Sijasikia,”

“Hujasikia kuwa yule mwanaume aliyenasa ile nyumba ya jirani polisi hawakumkuta mahabusu asubuhi?”

“Acha wewe!”“Inasemekena alifungiwa lokapu lakini asubuhi wakakuta hakuna mtu. Waliangalia mlango wao wa chuma, ulikuwa umefungwa na nondo kwenye madirisha zilikuwa nzimaaa.”

“Duh, ikawaje?”

“Ikawaje? Unauliza sharubu kwa Osama, polisi wote waliokuwa zamu usiku wamewekwa ndani.”

“Hee! Kwa nini?”“Eti wakubwa wao wanadhani wamemtorosha.”

“Hawana akili hao wakubwa. Wamtoroshe kisha wapoteze kazi, kisa?”

“Hayo unajua wewe. Hawajiulizi kwa nini alikutwa ndani kwenye nyumba ya watu wakati hakuna mlango wala dirisha lililobomolewa?”

“Unajua wakubwa serikalini wanajifanya hawaamini uchawi lakini wao ndiyo waumini wa uchawi kwelikweli, kila siku wanakwenda kwa waganga wa kienyeji kutafuta kupandishwa vyeo.”

“Una uhakika?”

“Husomi magazeti au kusikiliza vyombo vya habari? Siyo baadhi ya vigogo tu, hata viongozi wa makampuni makubwa, baadhi yao hawakosi kwa waganga hao.”

“Sasa huyo mchawi wanaweza kumpata kweli?”

“Itakuwa kazi kubwa. Baada ya kutoka rumande atakuwa amehama mji huyo, lakini serikali ina mikono mirefu, wanaweza kumtia mbaroni.”

“Lakini huyu ni kiboko. Hiyo dawa wakiipata majambazi tutakwisha wote. Maana wanaweza kuingia benki wakazoa fedha zote wakakimbia nazo.”


“Kweli, lakini nilisikia mtu mmoja akisimulia kwamba masharti yao ni magumu wakiingia ndani ya nyumba kimiujiza.”

“Hukuambiwa masharti hayo ili nasi tuelewe?”

“Niliambiwa kwamba wanapoingia kwenye nyumba, sharti lao ni kwamba, kwa kuwa wanaingia kupitia ukutani, si ruhusa kutoka ndani hata na sindano, ndiyo maana hawaibi benki.”

“Kwa sharti hilo hata mimi naamini kuwa ndiyo maana wachawi hawaibi benki.”

Mazungumzo ya wanawake wale yalikatizwa na tangazo la MC aliyesema kwamba mwili wa marehemu mama mkwe umeshafika pale nyumbani.

Wanaume walibeba jeneza lenye mwili na kuliweka ndani. Kusema kweli waombolezaji walikuwa wachache. Walimlaani mama mkwe kutokana na mpango wake wa kutaka kumroga mume wangu yaani mwanaye.

Hakukuwa na ucheleweshaji, marehemu alipelekwa makaburini na alizikwa na watu wachache sana, wengi walichukizwa kwa tabia yake ya uchawi.

SOMA HAPA JINSI KUJENGA UJASIRI WA KUFANYA JAMBO

Mwisho.

Nakushukuru wasomaji wangu kwa kufuatilia simulizi hii asanteni.   

Post a Comment

0 Comments