Ad Code

Responsive Advertisement

Chombezo: Kitumbua Cha Nani Sehemu Ya Kumi Na Nne (14)



Wakati akiwa anaendelea na mapishi yake Stella akamwona Pross anakuja kule jikoni, akiwa na simu yake mkononi, ambayo ilikuwa ina ita, alipotazama jina la mpigaji, ilikuwa ni namba ngeni, akaipokea, “hellow” aliita Stellah, na hapo akakutana na sauti ya mtoto wake wakike, “shikamoo mama” alisalimia binti yake, na hapo ghafla Stellah, hakiri ikamkaa sawa kuwa, leo ndiyo siku ambayo, watoto wake wanatakiwa kurudi nyumbani, ni baada ya kusherehekea chrismass, “hoo mwanangu umesusa, yani leo siku ya kurudi ndio mna nikumbuka, “ alisema Rose, huku Pross akisikiliza kwa pembeni, “lakini mama siunajuwa atuna simu, nime azima ili nikuambie kuwa sisi tuna karibia mbezi, uje utupokee na gari lako” alisema mtoto wa Stelllah, kwa sauti iliyo jaa uchangamfu, wala msiwe na wasi wasi, wanangu, tena mkifika tutapika zinga la pilau, alafu yule kijana washambani mnamkumbuka?” aliuliza Stellahm “ndiyo mama, si yule kijana alie tuangulia nazi, amefanyaje” aliuliza binti wa Stellah, kwa bashasha, leo anakuja kututembelea, nazani mtamkuta” alisema Stellah, akasikia sauti ya binti yake akimweleza kaka yake, “kaka yule Pross wakisalawe leo anakuja nyumbani” hapo akasikia wote wakifurahia, ni sababu siku ya kwanza kuonana nao, aliwafanyia fadhira kubwa sana, na aliwakaribu vizuri sana, “alafu mama hivi nasikia baba alikutwa amezimia huko guest, ume ona video zake mtandaoni?” aliuliza mtwa kike wa Stellah, alie zaa na Kipanta, “kwahiyo na wewe umeziona?” aliuliza Stellah, kwa sauti iliyo poa, maana alizikumbuka vizuri sana zile video nakama binti yake ameziona, basi ilikuwa ni aibu ya mwaka, siyo kwa kipanta pekee ata yeye pia, kwa kuonekana kwa dudu iliyo mwingia mala kadhaa, “haku sija ziona” alijibu mtoto huyo, lakini kwa mama mtu mzima kama Stellah, alijuwa kuwa, binti yake anakataa kuuwa soo, “ok! basi nita kuja kuwapokea hapo mbezi mnisubiri” hapo ndipo maongezi yalipoishia, Stellah alikata simu na kumtazama Pross, “watoto wametuaribia picha yetu, sasa leo tuta lala shamba” alisema Stellah huku anampatia simu Pross, na yeye kuendelea kupika, “lakini kule shamba bpss wangu amehamia kule, maana jana amekuja na begi kabisa” alisema Pross kwa sauti ya kiunyonge, “wala usijari tuta tafuta gust tuta lala kwa leo, alafu kesho na wasafirisha tabora kwa babu yao, wataondokea huko huko kwenda shule” alisema Stellah, alie onekana kukolezwa na penzi la kijana huyu. ******


Kipanta alifanikiwa kifika pale kwenye kuosha magari, ambako alikuta watu kadhaa, wakiendelea na uoshaji wa magari huku wengine wakichotelea maji, toka kwenye mto wa jirani, karibu na daraja la barabara ya malamba mawili, lakini kila alipotazama pengine ange mwona ata mmoja ambae ange mwuliza, alikosa imani na watu awa asa kutoka na mwonekano wao, licha ya kuwa wengi wao ni vijana pia walikuwa wamechakaa, lakini alipo taka kuondoka, akamwona mmoja wawa watu awa mwenye mwonekano wa uzee, akija maali pale huku amebeba dumu la maji, “habari yako mzee” alisalimia bwana Kipanta, baada ya yule jamaa kuweka maji chini, “safi vipi una inshu?” aliuliza yule mzee kwa lugha flani ya kiuni, tofauti na umri wake, hapo Kipanta akababaika, yule mzee kuona hivyo akaachana nae, na kumfwata kijana kijana mmoja, “hiyo dumu la kumi ilo, niandalie jelo lango, nikapate supu ya alaghe alisema yule mzee ambae kiukweli ungeshangaa anafanya nini mjini, baada ya kurudi kijijini, au atulie nyumbani acheze na wajukuu, “oya Feruz, una wasi wasi gani, we piga kazi, si unaona mwenyewe ndio kwanza tunaanza kazi” alijibu yule jamaa alie kuwa anaosha gari, “tatizo nikileta dumu nyingi, uchelewi kuzingua” alijibu yule mzee huku ana chukuwa lile dumu la maji na kwenda kumimina kwenye kipisi cha jaba, kisha akaelekea tena mtoni, hapo Kipanta akaona kuwa pale akukuwa na dili, hivyo akaondoka zake, kurudi stendi, na kuanza safari ya Kiluvya.


Kipanta alifika Stendi na kuingia kwenye basi ziendazo kibaha, gari alikuchelewa kuondoka, lakini wakati lina anza kuondoka, akamsikia kondakta, akisema, ebwanae ebu cheki yule mtoto alie ongozana na yule kijana, sijuwi dada yake au demu wake, ni mkali kinyama” hapo siyo kipanta pekee alie geuka kutazama nje yagari kuangalia alicho kuwa anakisifia kondactor, ile kutazama akakutana macho kwa uso na wanae, akazania kuwa wakumwona, maana awakuonyesha kuwa na habari nae, akamwakazia macho, ndio kwanza akaona wanaonyesheana vidole kuja kwake Kipanta, ikionyesha mmoja wakiume alikuwa anamshtua dada yake kama amemwona baba yao, Kipanta akajitabasamulisha, na wote waka mtazama, kisha wakakunja sura alafu wakatazama pembeni, hapo kipanta aliumia roho vibaya sana, “yani wananifanyia hivyo mimi baba yao” aliwaza Kipanta, ambae alijaribu kuwaza na kukumbuka katika ubaba wake, alifanikiwa kuwafanyia nini watoto awa, ambao mwonekano wao wa watoto wa kishua, ni kwanguvu za mama yao, akagundua kuwa zaidi ya kumpa mimba baba yao, akukuwa na kingine cha zaidia alicho toa, hivyo akatulia na kuacha gari likiondoka pale mbezi, huku yeye akiwa ndani yake.*****


Mama Pross pia alipata habari za kukamtwa kwa mschana alie mleta sikuile nyumbani, ikiwa pamoja na kumnunulia soda, habari ile ilimuuzunisha sana mama Pross, mke wa bwana Feruz, ilimuuzunisha kwa maana mbili, kwanza kabisa, Rose kuwepo Jella, maana ni binti mbae yeye binafsi alimwona kuwa mwenye moyo safi, pili mkasa wa huyu mwanaume, ambae ameitelekeza familia na kwenda kufumaniwa, na mahawara, “mh! kweli wanaume awawezi kubadirika” aliwaza mama Pross, ambae yeye alisha jikatia tamaa juu ya mume wake, ambae mpaka sasa kuwa anajuwa yupo wapi,”huyu mtoto leo alikuja mapema sana, hivi alilala huku, au likuja mala moja” ilo swali lilimjia mama Pross mala baada ya kumkumbuka Pross.*******


Hapo ndipo patamu, unajuwa ni utamu hupi, baada kutoka pale mbezi, huku akijisikia vibaya baada ya kuchuniwa na watoto wake, bwana Kipanta, alitulia kwenye gari mpaka aliposhtuliwa na kodakta, kuwa walisha fika gogoni, yani Kiluvya, njia panda ya kawawa, akashuka na kueleka kwenye kito cha polisi, ambako kwanza alikutana na gari moja matatasana, aina ya BMW, pembeni yake alikuwepo mfilipino mmoja akiwa na watoto chotara, “wasenge awa wana kula maisha kwenye inchi yetu, wakati sisi tuna pata tabu” alijisemea kimoyo moyo bwana Kipanta, huku akimkata jicho la chuki yule mfilipino, ambae sisi tuna mfahamu kama bwana Mauricio Fernandez, mwanajeshi wa jeshi la Filipino, ndie mume wa Adellah, yani wanamke wa zamani wa bwana Kipanta, ambae nae pia alimtazama Kipanta kwa macho ya utambuzi, akionyesha kama siyo kumwona live, basi alisha wai kumwona kwenye picha, “jambo rafiki” alisalimia Mauricio Fernandez, huku akipunga mkono, kwa Kipanta, “poa! alijibu kikauzu Kipanta kisha akatazama mbele kule uliko mlango wakuingilia ndani, ambako uso kwa uso, macho macho, nusumvae mwana mke mmoja mrembo na wakuvutia kwa sura na umbo la mwili wake, wakajikuta wame tazama usoni, kwa macho ya mshangao, na mshtuko, “Adellah, ni wewe au macho yangu?” aliuliza Kipanta kwa sauti ya kuto kuamini, “ni mimi, au ulizania nie jiuwa baada ya kunitapeli?” aliuliza Adellah kwa sauti tulivu huku akitabasamu…


..


Lakaini ni tabasamu ambalo alikuwa kwa nianjema, lilikuwa tabsamu la dharau, lakini licha ya hivyo Kipanta akajikuta analipukwa na roho yake, ni baada ya kuona jinsi mwanamke huyu, alie wai kuwa mpenzi wake akiwa ame nawili na kuwa mzuri zaidi ya kipindi kile, “hapana Adellah, yani ume nisusa kabisa, akuna kutafutana, akuna kupeana habari za mtoto, sasa hivi si atakuwa mkubwa sana?” aliongea kwa uchanga mfu Kipanta, “sana ni mkubwa sana, yupo na bibi yake Shinyanga, vipi kazi yako ya jeshi bado unaendelea nayo?” aliuliza Adellah, kwa nza Kipanta akatazama kushoto na kulia, kama kuna watu wanawafwatilia maongezi yao, akaona kuwa japo kilikuwa na watu wengi pale nje ya kituo raia kwa askari, lakini akuna mtu anae wafwatilia, zaidi ya yule mzungu na watoto wake, waliokuwa wanawatazama, “nime staafu mwaka huu, mwezi wasita, nikapata mamatizo, nime poteza kila kitu” aliongea kipanta kwa sauti ya kinyonge, hapo Adellah akajifanya ajuwi lolote, akajiweka sura ya uzuni, “pole sana jamani, ilikuwaje?” aliuliza Adellah kwa sauti ya uzuni, hapo kipanta akashusha punzi ndefu, kabla ajaongea, “ukweli ni story ndefu sana Adellah, awa wanawake ni hatari sana, ila yote kwa yote nashukuru mungu ametukutanisha, nitakusimulia vizuri” alisema Kipanta, huku macho yake yakionyesha wazi, kuutazama kwa uchu mwili na sura ya Adellah, pasipo kujuwa kuwa mume wake amesimama pembeni, ana watazama, “basi poa, sijuwi nitakupata wapi na lini?” aliuliza Adellah, ambae alikuwa anapima, kama Kipanta anatambua kuwa yeye na Rose ni ndugu, “kama una muda ata saa hivi, nachukuwa tu RB, alafu tunaweza kuongea, kama una muda lakini” alisema Kipanta kwa sauti flani ya kubembeleza na yakistaarabu, kama unge isikia ungejuwa kuwa Kipanta ni mstaarabu kweli kweli, hapo Adellah akatulia kidogo kama anatafakari jambo, ukweli ni kwamba lile tabasamu alilo kuwa analionyesha usoni mwake mala kwa mala, lilikuwa la kujilazimisha, ila moyoni mwake, alikuwa anamchukia huyu mtu kuliko mtu mwingine yeyote, akainua kichwa chake na kutzama ng’ambo ya barabara, akaiona bar moja kubwa hivi ambayo ilikuwa na watu wengi, kwakifui ilichanga mka kidogo, “au bado una kumbuka mambo ya zamani Adellah” aliuliza Kipanta, kwa sauti flani ya kumshawishi Adellah, ambbae ndio kwanza moyoni mwake alizidi kuchukia, huku moyoni akionyesha tabasamu angavu, “nitaachaje kukukumbuka Kipanta, ila akuna shida nakusubiri” alisema Adellah, na hapo akaliona tabasamu pana kwa kipanta, “poa ngoja nichukuwe RB faster kisha tuongee” alisema Kipanta alafu akaingia ndani ya jengo la polisi, akimwacha Adellah, anamsindikiza kwamacho, “yes huyu mjinga si anajifanya mjuwaji, sasa nime kutana na mama lao, mbona atatafuta sehemu ya kujificha, na nikisha mfirisi Rose, ndio kabisaaaa, ananywea maji kwenye kifuu” alijisemea Kipanta kimoyo moyo, huku akifwata counter, “alafu anaonekana anamawe ya kuelewekana, nita lia lia, mpaka ni vune fedha ya kutosha” alijisemea Kipanta kabla aja eleza shida yake na kupewa RB.


Tukio la kupewa RB lilitumia muda mfupi, ni kama dakika tano, kisha akatoka haraka kumuwai, Adellah, amenona huyo, leo lazima nikale mzigo, kisha miziga inaanza mpaka atajuta kukutana na mimi” alijisemea Kipanta huku akiangaza ngaza macho kumtafuta Adellah, ambae mwisho wake akamwona amesimama pembeni ya BMW, lile lile alilokuwa amesimama mzungu mwenye watoto chotara, “mh! au yupo nae nini?” alijiuliza Kipanta, huku akimtazama Adellah, ambae pia alimtazama na macho yao yalipo kutana Adellah akatabasamu, kilicho mpa moyo kuwa Adellah akuwa na yule mzungu, ni kuto mwona mzungu wala watoto, Kipanta akapiga hatua kumfwata Adellah, pale kwenye BMW, “nazani unaweza kwenda kukaa pale tuongee vizuri” alisema Adellah huku anatoa funguo ya gari, na kufungua milango kwa remote, “hongera sana Adellah, inaonyesha mambo yako siyo mabaya” alisema Kipanta akiwa ndani yagari, huku Adellah akiendesha aratibu, kuelelea kwenye ile bar, ambayo ilikuwa umbali wamita kama mia moja tu toka kituo cha polisi, “sikushindi wewe Kipanta, nasikia uwa mnalipwa vizuri sana, mnapostaafu” alisema Adellah kwa sauti tulivu na iliyo jaa upole na ukarimu, usinge juwa alicho kiweka moyoni, hapo Kipanta alitulia kidogo akishusha kichwa chini, kwa uzuni, japo ilikuwa ya kutengeneza, “yani Adellah, uwezi amini, limenikuta balaha kubwa sana, nime poteza kila kitu” alisema Kipanta kwa sauti iliyojaa uzuni kubwa, huku Adellah akisimamisha gari, na wote wakashuka, “kwanini unasema hivyo Kipanta, inamaana umeibiwa?” aliuliza Adellah huku wanatembea kuingia ndani ya bar, “nitakueleza tu! wala usiwe na haraka” alisema Kipanta huku wanatembea taratibu ndani ya bar, wakikatiza pembeni ya meza za wateja wengine walio kuwepo pale bar, wengi wao walikuwa wana pata supu na vinywaji visivyo na ulevi, wao walikuwa wanaiendea meza moja waliyo iona hipo tupu, “unajuwa kama kuna kitu sikipendi, ni awa watu wanje, yani utakuta wana kaba ajira zote, alafu wananchi wanapata tabu” alisema Kipanta, na hapo Adellah, akamtazama Kipanta, na kumwona amemkazia macho mfilipino wake alie kuwa amekaa kwenye meza moja na watoto wao wawili, Adellah akaishia kutabasamu tu! “nabado utamchukia sana” alijisemea Adellah, kimoyo moyo, huku wanaendelea kutembea kuelekea kwenye meza waliyo ichagua kukaa.


Naam ile kukaa tu, mhudumu akawafwata, na kuwauliza wanaitaji nini, “na soda yoyote ya orange, alisema Adellah, Kipanta yeye akamtazama kwanza Adellah, ambae alitabasamu “agiza chochote, usinionee aibu” alisema Adellah, na hapo Kipanta akatabasamu, “naona mwenzangu unaagiza soda, au aunywi bia?” aliuliza Kipanta, huku akijichekesha chekesha, ambae kiukweli nisiku ya nne leo ajagusa pombe, kitu mbacho kwake ni mwiko, sema uhaba wa fedha ndio ume sababisha, “mh! ulitaka niagize bia asubuhi hii” alisema Adellah, na wote wakacheka kidogo, “niletee bia, itakuwavyema ukiniletea tano ilikuepusha usumbufu, alafu, niitie mtu wa jikoni” alisema Kipanta, wakati sisi tuna kumbuka mtu huyu akuwa na uwezo wa kulipia ata bia moja, “vipi wewe uagizi chakula” aliuliza Kipanta akimtazama Adellah, “hapana nitakula usiku” alijibu Adellah, na mhudumu akaondoka zake, akiwaacha wakina Adellah wanaanza maongezi, “ok! nipe story, nini kilitokea” alisema Adellah, huku akitoa simu yake na kushika mkononi, akiibofya bofya kidogo, *******


Aya sasa, ebu twendeni mbezi stendi, siyo kwa watoto wa bwana Kipanta au Stellah na Pross, ni moja kwa moja mpaka barabara ya zamani, mita chache kwenye njia panda yamalamba mawili, kwenye kijiwe cha kuoshea magari, bado wanaonekana vijana walio valia nguo chakavu, wengine wakiosha magari na pikipiki, wengine wakichotea maji, “oya tayari zimeshafika kumi nyingine, nitoe buku langu” alisema yule mzee anae itwa Feruz, akimweleza mtu mmoja alie kuwa anaosha gari, “Feruzi unajuwa kudai, aya chukuwa buku lako” alisema yule jamaa, na kumkabidhi mzee Feruz buku lake, “sasa je saa tano hii, bado sija pata chai, ngoja nipate wali harage kisha nirudi kazini” alisema Feruz, huku anaondoka zake kuifwata barabara hii upande wa stend ya mbezi, ambapo alitembea kwa mwendo wa mita kadhaa, akashtuka anashtuliwa, “mzee feruz habari za siku nyingi” ilikuwa ni sauti ya kiume, toka nyuma yake, hapo Feruz akashtuka na kumtazama msalimiaji, huku moyoni mwake akishangaa kweli kweli, maana akutegemea kama kuna mtu anaweza akawa anamfahamu huku mbezi, na ndio kisa cha yeye kuja kuishi huku, macho yake yakakutana na askari polisi alie kuwa kwenye sale, za kazi, lakini akuwa anamfahamu kwa sura askari ambae alionyesha sura ya mshangao, “poa za masiku” aliitikia Ferz, ambae kwa mtu ambae amesha msahau mzee huyu, ndie yule yule baba yake Pross, “mzee Fruz, ipi unatoka shamba, mbona hupo hivi katikati ya mji” aliuliza yule askari ambae kama ni muda wakazini, alikuwa na miaka isyozidi sita, hapo Feruz akajuwa kuwa huyu askari anamfahamu toka kipindi yupo kazini, “kijanwa ngu ni maisha tu, siunajuwa fedha mbuzi ambayo tunalipwa, baada ya kustaafu” alisema Feruz, huku anamtazama yule askari kijana, ambae kiukweli alionyesha wazi kuto kulizishwa na jibu la bwana Feruz, na Feruzi alipoona vileakaanza kundoka zake kuelekea stend, akimwacha yule polisi kijana, anamsindikiza kwa macho ya mshangao, “unashangaa nini we mpumbavu, subiri na wewe ustaafu” alijisemea Feruz, huku anaendelea na safari yake.


Naam bwana feruz wakati anakatiza kwenye stend ya Mbezi, mala akawaona watoto wawili wakike na wakiume, watoto ambao umri wao umepishana kidogo, na watoto wake, alio waacha na mke wake, watoto ambao kwa sasa ajuwi wanaishi wapi na mama yao, “ukweli roho ilimuuma sana, alipokumbuka kuwa akuwaachia ata sehemu ya kuishi, “kama Pross, ni bora angebakia kwa mama yake, kuliko amekuja huku, alafu nime mtelekeza na mama wakambo” aliwaza Feruz ambae kiukweli, akuwa anapenda kukumbuka sana mambo ayo, sababu zaidi ya kumuumiza roho, asingeweza kufanya lolote kurudisha muda nyuma na kufuta makosa, “usingoje majuto, ndipo ulekeshe makosa” aliwaza Fruz huku anawatazama wale watoto, ambao kiukweli walionyesha kuwa na maisha mazuri, akawaona wanainuka pale walipokuwa na kuchukuwa mabegi yao madogo, kisha wakaanza kuelekea upande wa karibu na gate la kutokea, huku nyuso zao zikionyesha furaha, “ona walio andaa maisha yao” alijisemea Feruz, huku anatazama kule walikokuwa wanaelekea wale watoto, yani upande wa gate la kutokea.


Naam hapo ndipo bwana Feruz, aliposhikwa na mshangao, ni mala baada ya kumwona mwanae Pross akiwa anashuka toka kwenye gari aina ya Toyota vits, sambasamba na mwana mama mmoja matata sana, “macho yangu au naona wenge?” alijiuliza Feruz huku nashuhudia wale watoto wakienda kukumbatiana na yule mama, kisha kupeana mikono na mwana Pross, ambae kiukweli alikuwa amenawili, licha yakuwaonekana kuzudi kukuwa, pia alionekana kama vile anaishi maisha mazuri, kuanzia mavazi na mwonekano wa mwili na sura.


Feruz alibakia ameduwaa mpaka, akimshangaa mwanae ambae alikuwa mita kama hamasini toka alipokuwepo, “kumbe familia yangu aitakuwa mbali na hapa” aliwaza Feruz, ambae bado alikuwa ameduwaa, akiwatazama mwanafamilia, walikuwa pamoja na mwanae Pross, ambao sasa walikuwa wanaingia kwenye gari na mabegi yao madogo ya mgongoni, ndipo Feruz, alipopata wazo la kumfwata Pross, lakini alisha chelewa, ile anapiga hatua tu! akaliona gari lina anza kuondoka, akaanza kukimbia, lakini aikusaidia, gari lilitoka nje ya stendi na kuikamata barabara ya morogoro, wakielekea upande wa kibamba.******


Ebu turudi gogoni, mita mia moja, toka kituo cha polisi, kwenye ile bar, tunaipita meza ya mfilipino bwana Mauricio Fernandez, ambae alikuwa ana watazama mke wake Adellah akiwa anaongea na mzazi mwenzie Kipanta, ambae ndie alie msababishia matatizo, mdogo wa mke wake, yani mschana Rosemarry, na tukifika kwenye meza ya kina Kipanta tuna mkuta Kipanta alie kuwa amesha kunywa bia nne na anamalizia ya tano na tayari alisha maliza kula na amesha agiza bia nyingine tano, na kila bia ilikuwa ina uzwa tsh elfu mbili.


“unaona Adellah, yani ilikuwa kama lahana yako, mpaka nikajuta kukuacha na kumchukuwa Stellah, tena nililazimishwa tu! ameniletea mikosi mitupu, sina kitu zaidi ya gari, kuna kipindi nilisafiri, nikamwachia mshahara wote, ili ajenge nyumba kwaajili yetu na watoto, yeye akauza kiwanja cha kwanza, na kununua kingine kwa jina lake, alafu akajenga nyumba, kwa jina lake, mwishoe akanifukuza” alisimulia Kipanta, akijitaidi kutengeneza story, ambayo aita mpa lawama, zaidi ya kuonewa huruma, huku anaendelea kufakamia bia, maana ata zile tano nyingine zilisha letwa, “baada ya kunifukuza nyumbani kwake, nika mpata mwana mke mwingine, ambae anaitwa Rose, huyu ndie mshenzi kuliko Stellah, huyu nilipostaafu tume tumia fedha zangu, na marafiki zake, na mwisho wa siku, nimepatwa na matatizo, amenikimbia kabisa” alisema Kipanta, kwa sauti ya uchangamfu wa pombe, “kwani yeye ndie ulie kuwa nae wakati unawekewa dawa kwenye pombe” aliuliza Adellah, ambae mudawote alikuwa ameishika simu yake mkononi, “hapana, huyu alikuwa ameshaanza vituko, siku hiyo nilikuwa na mschanammoja anaitwa Matrida” alisema Kipanta, kwa sauti ya majisifu, utazania ilikuwa ni sifa kubwa, “niliamua kupita nae sababu Rose alijifanya mjanja, lakini ndio yakatokea hayo” alisema Kipanta akimalizia na kicheko cha kilevi, “au Rose ndie alie kuwekea dawa kwenye kilevi, na kukuibia fedha zako?” aliuliza Adellah, kamavile alikuwa anamtilia mashaka Rose, “ndivyo watu wanavyo amini, lakini ukweli ni kwamba, kuna kitui alitaka kukisikia toka kwa Kipanta mwenyewe, “wengi wanaamini hivyo, lakini Rose akuwepo wala akuja pale bar, ila mimi nataka nimfilisi, arudishe kila kitu changu, nilicho mpatia, maana bila ya hivyo nita zalilika” alisema Kipanta, ambae mpaka mwisho wa maongezi yao tayari alisha kuwa amekunywa bia kumina chakula,akiwa anaamini kuwa Adellah ata lipia ghala za chakula na vinywaji, “pole sana bwana Kipanta, ila kabla sija ondoka naomba nikutambulishe watu flani” alisema Adellah, huku anabonyeza simu yake na kuiweka kwenye kibegi chake, kisha akatazama upande aliokuwepo mume wake bwana Mauricio Fernandez, na watoto wao, kisha akawaonyesha ishala ya kuwa wasogee pale walipokuwepo, yeye na Kipanta, huku Kipanya japo alikuwa amelewa lakini alikuwa ametoa macho ya mshangao, akiwatazama wakina Mauricio Fernandez,na watoto wawili wdogo, ambao walikuwa wanatembea taratibu, kupita pembezoni mwa meza zawatu, kuwasogelea wao, “unataka kusema…..?” aliuliza Kipanta akishindwa kumalizia kwa mshangao aliuo upata, na wakati huo tayari, bwana Mauricio Fernandez, na watoto walisha wafikia pale walipo, “Kipanta huyu, anaitwa Mauricio Fernandez, ni doctor mwanajeshi nilikutana nae ngara, akiwa major, na sasa ni cornel (kanali) ni mwenji wa Filipino, ambako sas tunaishi, kwenye mji wa Sun philipe, na wan i watoto wetu” sijuwi kama Kipanta alikuwa anauzinga tia huo utambulisho, ata kama aliuzingatia sidhani kama aliuona una umuhimu kwake, maana alinekana wazi kuduwaa ba kwwa kile alicho kuwa anakiona, na kukisilia, “mume wangu huyu ndie Kipanta mzazi mwenzangu, ambae umesha sikia sana habari zake” alimaliza kutambulisha Adellah, sasa bwana Mauricio Fernandez,akampa mkono bwana Kipanta, ambae aalikuwa amekunja sura kwa hasira, na akuupokea mkono wa bwana Mauricio, zaidi ua kuinuka kwa hasira, na kutaka kuondoka zake, lakini Adellah akamuwai,“samahani bwana Kipanta, kuna kitu ujamaliza hapa mezani” alisema Adellah na hapo Kipanta akasimama na kutazama mezan, ambapo palikuwa na chupa moja ya soda iliyo bakiwa na soda robo, zaidi ya hapo kulikuwa na chupa tano za bia, huku moja wapo ikiwa na bia nusu, wakati huo mhudumu alie wahudumia alisha wafikia nazani bada ya kuona dalili za watu awa kuondoka, hivyo alikuwa ana fwata malipo yake, “sina aja nayo” alisema Kipanta, kisha akageuka na kutaka kuondoka, lakini akasikia Adellah akiongea tena, “simaanishi bia iliyo bakia, sababu umeshha kunywa Tisa, na nusu, nazungumzia malipo ya bia na chakula” maneno hayo ya Adellah, yalimstua sana, Kipanta ambae aligeuka na kumtazama Adellah kwa mshangao, akamwona anatoa shilingi miatano ya kitanzania nakumpatia yule mhudumu, ikiwa ni ghalama ya soda aliyo kunywa, hapo ndipo Kipanta alipoona kijacho chembamba kwenye paji la uso wake, kikichuruliza kuja kwenye pua, na kuwa kama kina mtekenya hivi, huku pombe alizo kunywa zikianza kupotea kichwani kwake, asa alipo kumbuka kuwa zaidi ya bia za elfu ishilini, pia alisha kula kuku nusu na ndizi za kukaanga, ambazo pia thamani yake ni elfu kumi na moja na mia tano, kwa jumla ilikuwa ni elfu therathini na moja ja na mia tano, na hapo mfukoni alikuwa amebakiza nauri ya dala dala kumfikisha kisalawe ambayo ni elfu moja na mia tano.………





Kipanta aka mtazama Adellah kwa jicho kali la mshangao, “inamaana ulinileta hapa kuni zalilisha?” aliuliza Kipanta kwa sauti ya juu iliyo jawa hasira, sauti ambayo iliwafikia baadhi ya watu waliokuwa meza zajirani, “kivipi Kipanta, kwani huku tanzania wanaume ndio wanawapeleka wanawake bar, na kuwa nunulia chakula na pombe, mbona uliweza kukesha bar na wanawake huku ukilipa ghalama zote, au umezowea kuwa mimi ndie mtu wakukulipia ghalama zako?” aliuliza Adellah, huku anasimama, “lakini wewe ndie ulie niambia niagize tu, si eti dada?” aliuliza Kipanta huku akimgeukia yule mhudumu, “mi sijuwi nachotaka ni ela ya vinywaji na chakula” alijibu yule dada wakati huo tayari watu walisha geuka na kuwatazama wakina Kipanta, huku wengine wakiingiza mikono mfukoni, kutoa simu zao, tayari kuchukuwa tukio, hapo Adellah, na mume wake pamoja na watoto wao, wakaondoka zao, wakipishana na manager wa bar,ambaealisha ona dalili zakuto kuelewana, kati ya mfanyakazi wakenamteja Kipanta, hivyo akaamua awasogelee, “samahani ndugu kuna tatizo?” aliuliza manager baada ya kufika pale na kumkuta Kipanta akitokwa na jasho jembamba usoni, “wewe ndie msimamizi wa hapa?” aliuliza Kipanta huku anamtazama manager, “ndiyo mimi ni manager wa hapa” alijibu yule jamaa, na hapo Kipanta akatazama kushoto na kulia, kutazama kama kuna mtu anawafwatilia, ukweli ni karibu barnzima, ilikuwa ina wafwatilia, na mbaya zaidi, wengine walifika mbali zaidi na kuanza kuchukuwa video, huku minong’ono ya chini ikisambaa, “hiyu sindie yule alie wekewa dawa na kuibiwa kila kitu” ayo ni baadhi ya maneno yaliyokuwa yana tembea chini chini, “manager naomba tukaongelee pembeni” alisema Kipanta, kwa sauti ya chini na yakubembeleza, “ok! wewe twende pamoja na huyu mteja” alisema manager akimweleza mhudumu, kisha wakaondoka kwa pamoja wote watatu, kuelekea upande wa ndani, hakika unge mwona leo bwana Kipanta, ndiyo unge juwa kweli alistaafu kiuhalali, maana alionekana kuwa amezeeka kweli kweli, na sasa akuonyesha dalili kuwa amelewa, ilionyesha kuwa pombe imemtoka kichwani.


Naam walielekea moja kwa moja upande wa jikoni, jiko la ndani, ambako shughuli za upishi zilikuwa zinaendelea, “niambie wewe nini kime tokea” alisema manager, akimtazama mhudumu wake, ambae alielezeakuanzia alipowapokea wakina Kipanta, na kuanza kuwa hudumia, kipanta akiagiza bia kwa mafungu ya tano tano, pamoja na kuitaji mhudumu wajikoni, “sasa yule mwanamke alie kuwa nae, amesha lipa, amebakia yeye, anadaiwa elfu therathini na moja na miatano” alimaliza kuongea mhudumu, na hapo manager akamtazama Kipanta, “nikweli mzee umekunywa bia na utaki kulipa?” aliuliza manager, hapo Kipanta akaweka sura ya huruma kidogo, kabla ajaanza kuongea, “siyo kwamba sitaki kulipa, ukweli kabisa mimi nilijuwa yule mwanamke talipa, sasa ameamua kunikomoa, na kuondoka bila kunilipia” alisema bwana Kipanta, na kumfanya manager ashangae kidogo, “mzee inakuwaje una mleta mwanamke bar, ili akununulie pombe na chakula, ungekuwa kijana mdogo tusinge shangaa, lakini wewe ni mzee” alisema Manager, kwa sauti ya kusimanga, hapo Kipanta akabkia ametazama chini, kwa aibu, akikosa jibu wala kitu cha kumweleza kijana yule, ambae ni manager wa bar ile, “mzee kiukweli sisi atuna cha kukusaidia zaidi ya kulipa hizo, bia, bola zingekuwa moja au mbili, lakini kumi, na chakula, hiyo lazima ulipe” aliongea manager akionyesha kuwa akuwa na chembe ata moja ya huruma, juu ya Kipanta, “kijana japo unifahamu, lakini naomba nijiaminishe kwake, sisi wote ni wanaume, naomba nidhamni, nitaleta hizo fedha jumatatu” alisema Kipanta, na kuzidi kumchochea manager, “weee nikudhamini kivipi, kama wamshindwa kukudhamini wale wenzako, nitawezaje mimi?” aliuliza yule manager kwa sauti ya kumruka kwa futi mia, hapo Kipanta aka ajikuta anathema kwa nguvu akivuta pumzi kwa mkupuo na kuishusha kwanguvu, “leo naumbuka tena” aliwaza Kipanta huku akiwa ametazama chini, kama kuna kitu anakitafuta, “yani mzee we toa mkwanja tu, vinginevyo tuna kupeleka polisi” alisema yule manager kwa msisitizo akionekana kuwa akuwa anatania, kwa kile alicho kuwa anakisema, “lakini ndugu yangu, naomba unielewe, hiyo elfu therasini kwa sasa sina, ila nitakuletea ata kesho mapema tu! naomba uni amini ndugu yangu” alibembeleza Kipanta, kwa sauti iliyotia huruma, “ok! unaacha nini kama dhamana ya elfu therasini?” aliuliza Manager, huku akimtazama Kipanta, hapo Kipanta akatulia, siyo kwa kufikilia ataacha nini ila kwa kujuwa kuwa akuwa na kitu, ambacho anaweza kukiacha hapa, kama dhamana, “ebu tuonyeshe simu yako, kama tunaweza kubakiana yo mpaka utakapo leta ela yetu” alisema manager, lakini ndio kwanza Kipanta akashusha tena pumzi, “inamaana ata simu auna, awa ndio wazee wababaishaji” alisema manager, kwasauti ya kumshuku Kipanta, “hapana kijana wangu, mimi siyo mbabaishaji, ila nime patwa na matatizo makubwa sana siku ya chrissmas, ata yule mwanamke niliekuwa nimekaanae pale, nilikuwa na msimulia matatizo hayo” alisema Kipanta na kusimulia kile kilicho mpata, kule luguruni, “nikaibiwa kila kitu, leo nimetoka hospital na kuja huku kuchukuwa RB, nika chukuwe card yangu ya benk, niweze kuchukuwa fedha nika renew line na kununua simu, pamoja na kuja kuwalipa fedha yenu” alisema Kipanta, na hapo manager akaonekana kuelewa somo, “kumbe wewe ndie yule ulie wekewa dawa zakulevya, dah! pole sana, lakini mzee wangu lazima tukaandikishiane kituo cha polisi” alisema yule manager, na wakakubaliana hivyo, maana Kipanta akuwa na ujanja mwingine.*****


Naam mida hii ya saa nane mchana, ndio mida ambayo Sinder aliingia getoni kwao, na kumkuta mpenzi wake waghola, akiwa amejilaza kitandani, lakini akionyesha dalili ya kuwa alikuwa ameingia hapo muda siyo mrefu, maana alikuwa na nguo zake zote mwilini, “mwenzio yame nikuta makubwa” alisema Sinder yule mwana dada mhudumu wa bar, huku ana pembua nguo moja baada ya nyingine, “kuna nini tena, kuna mtu ullitaka kuwibia amekushtukia?” aliuliza Waghora, pasipo kugeuka kumtazama Sinder, “hapana, siyo hivyo, si una wakumbuka wale watu wawili tulio waibia mpaka nguo zao?” aliuliza Sinder, hapo Waghola akainuka na kumtazama Sinder, “ndiyo wamefanyaje?” aliuliza Waghora kwa mstuko.


Hapo Sinder akamsimulia kila kitu bwana Waghola, tokea alipoitwa na manager kuwa aende ofisini kwake, na kukutana na insp wa polisi, na maswali aliyo mwuliza, na majibu ambayo yeye aliyatoa, “nilimshinda hakili, akaondoka zake” alimaliza Sinder kusimulia, “hapo sawa ila nazani inabidi utafute bar nyingine, vinginevyo tuta kamatwa” alisema Waghora, huku akijilaza tena kitandani, “vipi wewe ulifanikiwa kuiotea password?” aliuliza Sinder, ambae yeye na mpenzi wake, licha ya kukuta fedha kwa kina Kipanta, pia walisha uza simu na vitu vilivyo uzika, walivyo vichukuwa kwakina Kipanta na Matrida, “nime shindwa tena leo, yule mshenzi sijuwi aliweka password gani?” alilalamika Waghola, “duh! hapo tutakosa miela” alisema Sinder huku anapanda kitandani, tayari alisha vua nguo zake na kubakia na nguo za ndani, “siwezi kukubari nikose ela za yule mshenzi, tena inaonyesha kuwa bado ajaibloack, maana ukiichomeka inasoma kama kawaida” alisema Waghola, huku akiendelea kusema kuwa juma tatu anaanza kudili na card hiyo ya bwana Kipanta mpaka apate fedha.******


Yap! video za tukio la kudaiwa fedha pale bar, zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikieleza kuwa yule jamaa alie fumaniwa na kuwekewa dawa kwenye pombe , leo ame kunywa pombe na kushindwa kulipa, video hiyo ilimkuta Stellah akiwamezani na watoto wake pamoja na Pross wana pata chakula cha mchana, ikiwa ni pilau la kuku, alicho kifanya alicheka kidogo, na kusema kwa sauti ndogo, “na bado mbona uta zalilika sana mwaka huu” alisema Stellah, ambae alikuwa muda huu licha ya kupata chakula, lakini walikuwa wanamaongezi makubwa na watoto wake, ambao waligomesha kwenda tabora kwa babu yao, wakiitaji kwanza washerehekee mwaka mpya na mama yao, jumatano inayo fwata, na siku hiyo ilikuwa ni ijumaa, “mama sisi tutaondoka tarehe mbili” alisema mtoto wa kiume wa bwana Kipanta, “lakini mama kwanini usiwaachie wale mwaka mpya hapa hapa, maana Chriss mass akuwa nao” alisema Pross na kuwafanya watoto wa stellah, furahi kwa msaada huo wa Pross, “ok! kaka yenu amewatetea, mtaondoka tarehe mbili” alisema Stellah, na wanae wakashangangilia, kwa nguvu, “alafu mama kesho juma moss twende shambani kwa kaka Pross, alisema mtoto wa kike wa bwana Kipanta, hapo kabla Pross ajajibu, kuwa boss waka yupo, tayari Stellah, alisha jibu, kuna tope jingi sana akuendeki” alipinga Stellah, ambae alikuwa anajuwa kuwa mume wake ameamishia makazi kule shambani, na wakati huo huo simu yake iliita, ile anaitazama ni simu toka kwa Celine, mwalimu mwenzie, akaipokea na kuiweka sikioni, “hallow niambie mwalimu” alisema Stellah, na hapo akakutana na kicheko cha maana, “Stellah, katika maamuzi uliyowai chukuwa juu ya ndoa yako ili la kuachana na yule baradhuri, ni uamuzi wa maana sana, umeona video zake mpya?” aliongea Celine, na apo Stellah akainuka na kusogea pembeni na maongezi yakaendelea.******


Naam Kipanta baada ya kumaliza kuandikishiana pale kituo cha polisi, akaelekea benk, ambako alifanya utaratibu wa kuandikisha kadi nyingine, ambayo alipewa siku kumi na nne aifwate, huku wakiifunga ile ya zamani na kuitrack, popote itakapo tumika ifahamike na mtumiaji akamatwe mala moja, pia alifanya utaratibu wa kuangalia hakiba ya fedha ambayo ilibakia kwenye account yake, akakuta kuna tanzania shilingi elfu themanini pekee, kati ya milioni zaidi ya themanini alizo lipwa kama fedha ya kustaafia, lakini uwezi amini bwana Kipanta aliziona kuwa ni nyingi sana, nikama ilikuwa toka sifuli mpaka mia, hivyo kitu cha kwanza alienda moja kwa moja kwenye ilebar, na kulipa ile fedha, , na kubakia na shilingi, elfu alobaini na tisa na mia tano, kisha akaanza safari ya kuelekea kisalaweakinuna chupa kadhaa za pombe kali, kisha akaelekea kule shambani, akiwa na elfu kumi tu! ambako alikuta akukuwa na dalili ya uwepo wa Pross, “imanaana jana akurudi” aliwaza Kipanta, huku anatoka nje ya kibanda kile, akiwa na chupamoja ya pombe kali, “we mwache tu, nikisha likomboa shamba langu, namtimua, hayupo makini kabisa mpuuzi huyu” alijisemea Kipanta huku anakaa chini ya mwembe pale kwenye gogo, na kufungua chupa moja ya pombe kali, nakuanza kuinywa taratibu, huku akijipa moyo kuwa, siku siyo nyingi ata jipatia mali zote za Rose.


Naam hayo ndiyo maisha ya Kipanta kwa week end hii, alibakia analinda shamba, huku kila siku akiwa anakunywa chupa moja ya pombe kali, akishondia mihogo, ya kuchemsha, sababu akuwa na uwezo wa kutega wala kununua kambale, fedha aliyo kuwa nayo ya kiasi cha elfu kumi aliitunza kama nauli ya jumatatu, kuendea mahakamani, wakati huo Pross alikuwa anaendelea kufaidi kitumbua cha mke wa Kipanta, ambapo kila usiku ulipowadia Pross alitoka na kwenda kusimama mtaa wapili toka kwa Stellah, na baada ya dakika kadhaa Stella, ange washa gari na kumpitia kisha wanaenda kulala kwenye guest flani, ambapo wange lala mpaka alfajili, na stellah kutangulia nyumbani kisha Pross akafwatia.


Ratiba hiyo ilidumu mpaka juma tatu, siku ambayo Kipanta alifika mahakamani mapema, na kukutana na Matrida, ambao walielewana kuwa wampe kesi Rose, lakini wakati wanataka kuingia mahakamani baada ya muda wakusikilizwa kesi yao ulipofika, Matrida akakumbuka jambo, “hivi umekutana na dada yake Rose?” aliuliza Matrida, kwa sauti ya chini, “sija kutana nae, ata simjuwi mtu mwenyewe, kwani ana dada hapa mjini?” aliuliza Kipanta, na wakati huo wakaliona gari aina ya BMW, likiingia pale kwenye viwanja vya mahakama, wote kila mmoja kwa muda wake akalikumbuka, na kulitambua kuwa lima milikiwa na nani.


Naam wakati Kipanta anashangaa, na kujiuliza kuwa, “amefwata nini huyu Malaya” huku Matrida akisema kwa sauti, “tena huyooo! anaingia” hapo Kipanta akamtazama Matrida kwa macho ya mshangao, “kwani Adellah ni dada yake Rose?”………




Aliuliza Kipanta kwa mshangao, “kwani unamfahamu?” aliuliza Matrida kwa mshangao, “ndiyo namfahamu” alisema Kipanta akishindwa kufafanua anamfahamu kivipi, “ni dada yake, tena anaishi na mzungu” alisema Matrida kwa sauti ya kunong’ona, huku wanalitazama BMW ambalo sasa lilikuwa limesha simama na akashuka Matrida pamoja na familia yake, yani mume wake Mauricio Fernandez, na watoto wao, hapo ndipo Kipanta alipovuta picha ya kile anachoelezwa , kuwa huyu ni dada wa Rose, akakumbuka kuwa kipindi yupo na Adellah kule tabora, Adellah, alikuwa na mdogo wake wakike, alikuwa mdogo sana, “Matrida sasa tume tajirika, yeye si anajifanya mjanja” alisema kwa kunong’ona bwana Kipanta, huku akikwepesha macho yake yasi mtazame Adellah, “kivipi kwani wanaela nyingi?” aliuliza Matrida swali ambalo jibu lake analo, maana kwa mwonekano wa Adellah, na familia yake , na usafiri wanao tumia, yani gari aina ya BMW jipya kabisa, “sasa je anaishi Suns philipe uko Filipino, mume wake ni kanali wa jeshi, yani ili mdogo wake aachiwe lazima watulipe fedha ndefu” alisema Kipanta ambae matumaini yake yalizidi kuongezeka, ata Matrida pia aliingiwa na matumaini mengi zaidi, maana alionekana anatabasamu, tena tabasamu la matumaini, “mi ndio napo kupendea hapo, na tukifanikiwa, siku hiyo tuna kasha tunapombeka mpaka asubuhi” alisema Matrida kwa kunong’ona, kisha wakacheka na kugongeana mikono, kabla awaja mwona insp anakuja mbele yao, “salama kaka, pole sana na matatizo ya jana” alisema insp akimsalimia Kipanta, “asante sana kaka, ndio ukubwa huo” alisema Kipanta, kwasauti ya kinyonge, “dah! niliona kwenye mitandao, lakini nasikia ulisha maliza” alisema insp, “ni kweli nilisha maliza” alijibu Kipanta, “ila we ndugu yangu bwana, kwani ukujuwa kama yule ni dada yake Rose” aliuliza Insp, “sikujuwa ila mwache ajifanye mjanja, wakati mimi nimeshikilia makali” alisema Kipanta huku wana tazama kule liliko BMW, yani kwenye mahegosho ya magari, ambako waliweza kumwona Adellah ana agana na familia yake kisha akanza kutembea kuwafwata pale walipo, “Kipanta bwana, lakini ukifanikiwa, nenda nyumbani tabora, usibakie hapa mjini” alisema insp kwa sauti ya chini, “habari zenu jamani” alisalimia Adellah, akiwasalimia wote kwa ujumla wao, lakini aliitikia insp peke yake, huku wakina Kipanta na Matrida wakielekea ndani ya ukumbi wa mahakama, na wakati huo gari la watuhumiwa likiingia pale mahakamani, “insp nina ushaidi naomba unielekeze namna ya kuuwakilisha, mahakamani” alisema Adellah, huku akitoa simu yake, toka kwenye mkoba wake, “niushaidi wa sauti?’ aliuliza insp kwa sauti ya mshangao huku akiachia tabasamu la kustaajabu, “ndiyo insp, nilipngea na Kipanta jana alinieleza ukweli kuwa Rose akuusika na kwenye tukio hilo” alisema Adellah, na hapo insp akatabasamu, “kweli wewe ni mwanamke wa kuigwa, ok! muda mchache japo nilitaka niisikilize, lakini wacha nikakubadhi kwa mwendesha mashataka, ili akupe nafasi ya kuwakilisha ushaidi wako” alisema insp kisha wakaongozana na Adellah, kuingia ndani, “kweli huyu mzee anamikosi” alisema insp pasipo kufafanua.*******


Wakati hayo yanaendelea pale mahakamani, huku mwana mama Stellah, akiwa nyumbani kwake, pamoja na wanae na kijana Pross, mala akapigiwa simu na Celine, akimweleza kuwa lisaa limoja badae yeye na rafiki zake wakina Suzie na wengine wata kuja pale nyumbani kwake, hivyo Stellah, akawataka watoto wake wafanye maandalizi ya kina, huku Pross akiaga na kusema anaenda kuangalia kule shamba, maana alisha pitisha siku tatu bila kukuona na ukichukulia boss wake alikuwepo kule shamba, “ok! wewe nenda alafubadae uje kama kawaida” alisisitiza Stellah, na Pross akaondoka zake, huku Stellah akiwa amempatia fedha za nauli, ya kwenda kurudi na fedha ya chakula.******


Naam Rose akiwa kwenye kizimba cha mahakama, aliweza kumsikia Kipanta na rafiki yake Matrida wakitoa maelezo, yanayo fanana, juu ya tukio linalosemwa kuwa ni la yeye kuwawekea dawa kwenye vilevi, wawili awa, na kupoteza fahamu, ukweli Rose aliumia sana kuona anasingiziwa hivi hivi, nambaya zaidi, ata Adellah alipotoa ushidi wa wa sauti, ya kipanta akisema kuwa Rose akuusika na lolote, ila ana taka amkomoe na kumfilisi, ukweli ipanta alipinga vikali, huku akieleza kuwa, yeye akuongea mambo ayo na Adellah, ila Adellah, ametengeneza sauti hiyo, kwa lengo la kumkomoa yeye sababu ya visa vya kimapenzi, na pia kumtetea mdogo wake, “kwanza jana atungeweza kuongea mamboyote hayo sababu, mimi na yeye tulikuwa katika ugomvi mkubwa sana, kiasi cha kukataa kulipia vinywaji ambavyo mwanzo alisema angelipia” alieza Kipanta, na kuzidi kuupoteza maboya ushaidi wa Adellah.


Adellah alijitaidi, kutoa ufafanuzi wa ushaidi wake lakini mahakama ulikataa ushaidi ule, kwa madai kuwa kumekuwepo utengenezaji na uigizaji wa sauti za watu, hivyo ushidi wa sauti pekee usingeweza kutosha kumfanya Rose aondolewe hatia, “kesi ina ailishwa mpaka kesho, ambapo mnatakiwa kuleta ushidi wenu, zaidi ya hapo, hukumu ita fwatia” hayo yalikuwa ni maneno ya hakimu, ambayo yalimvunja nguvu, Adellah ata Rose mwenyewe, na rafiki yao Joyce, huku Matrida na Kipanta wakiachia tabasamu la nguvu, liliashilia ushindi.


Nawalipotoka mahakamani, Adellah, aliekuwa anatililikwa na machozi huku anaagana na Rose, akaweza kumwona Kipanta akiwa ana agana na Matrida ambae alimkabidhi elfu therasini, wakiwa na matumaini kuwa kuna fedha zaidi inakuja.


Adellah awakati anaagana na Rose, walijaribu kushauriana mawili matatu, lakini akuna kitu cha kufanya walicho kipata, ambacho kina weza kuwasaidia ili kumtoa Rose kwenye huu mkasa, “lakini ni kweli Kipanta amesema anataka kukusingizia ili akufilisi” alisema Adellah akionekana kuwa mwenye machungu makubwa sana, na mpaka waachana awakuwa wamepata wazo litakalo wasaidia. ******


Mida hii ndiyo mida ambayo Pross alifika kule shambani, na alikuta pamefungwa, na akuna mtu yoyote, alichowaza, ni kuwa boss wake Kipanta ata kuwa amesha rudi mjini kwa mpenzi wake Rose, na kila alipo mkumbuka Rose, alijikuta anaona wivu, maana anakumbuka mschana huyu, alimhaidi mambo mengi sana usiku wa chriss mas, lakini matokeo yake, akapotea moja kwa moja, “au aliona mimi simfai?” alijiuliza Pross, huku anafungua mlango kwa funguo nyingine, na alipoingia ndani akakuta, begi la boss wake bado lipo, hivyo akajuwa kuwa boss wake lazima ata rudi tena, kwamaana yakwamba bado ajarudi mjini, na muda wowote atarudi pale shamba, na zaidi ya hapo aliona chupa kadhaa tupu za pombe kali, akajuwa kuwa boss wale ni mnywaji wapombe pia, “kumbe huyu jamaa anakunywaga pombe” aliwaza Pross ambae alikuwa anapekuwa pekuwa kutafuta mfuko wa kubebea vitu vya kwenda navyo mjini, kuepeleka nyumbani kwao na kwa mwana mama Stellah, na baada ya kuupata aka zunguka mashambani, akikusanya mazaga kibao, alafu akarudi ndani na kujilaza kidogo, ili akiamka aende zake kibamba, lakini kutokana na uchovu, wa kukesha na #kitumbua_chabuku kwa siku tatu, akajikuta akipitiwa na usingizi mzito.******


Kipanta baada ya kuachana na Marida, alie mkuwa amempatia fedha kiasi cha elfu therathini, akaelekea mbezi, kwenda kutafuta dalali, ili aweze kuliuza gari lake, ukweli ni kwamba akupenda kuishi kama anavyo ishi, hivyo aliona akijipatia fedha kupitia gari lake, Toyota IST, akiwa na maana ya kuliuza, sababu aliamini siku siyo nyingi atakuw amrshapata fedha nyingi , leo Kipanta alifanikiwa kukutana na dalali mmoja pale mbezi, huyu ni bwana Mic Mhagama, ni dalali mmoja ambae alisha fanikiwa kuuza magari mengi sana, ya watu alio mletea, “sasa chukuwa namba yangu nitumie picha whatsaap” alisema dakaki Mhagama, huku anatoa simu mfukoni, lakini Kipanta akuwa na simu, na aliona aibu kusema kuwa akuwa na simu, “da simu nimeiacha chaji, niandikie sehemu, nitakutumia baadae” alisema Kipanta, akiwa na uhakika kuwa ata enda kumtafuta mtu mwenye simu yenye uwezo huo, asa Matrida ambae atakutana nae siku inayofwata kwenye mahakama.


Kipanta alipewa namba za simu na kuondoka zake, kuelekea kisalawe,akipitia chupa kadhaa za pombe kali, akiwa na lengo la kwenda kupumzika na kujinywea pombe yake, kama ilivyo kuwa juzi na jana.******


Naam, mambo yalikuwa ni mpwito mpwito, wakati Stellah, alikuwa nyumbani kwake na marafiki zake anajinywea pombe, huku wakisimuliana na kuonyeshana picha na video za whatsaap zilizomwonyesha Kipanta anavyo dhalilika mtaani, huku Matrida alikuwa na rafiki zake wanaendelea kujipatia vinywaji, kwafujo, wakiongea na kupanga ili na lile, katika kumfilisi Rose, lakini Rose mwenyewe alikuwa kwenye chumba cha mahabusu, anamwaga michozi, asiamini kama rafiki yake Matrida anasema kuwa alimwona Rose akiwa anaingia chumbani na kuwa fanyia fujo huku akigusa gusa glass zao, “sijuwi nime mkosea nini, Mat?” ilo swali akuwai kulipatia jibu Rose, ambae ata dada yake Adellah, alishindwa kumsaidia kujinasua, toka kwenye ile kesi, wakati huo, huo Adellah, pia alikuwa amejifungia hotelini, akiendelea kulia kwa muda mrefu, mume wake akishindwa kum bembe leza, kutokana na machungu aliyo nayo, ilimuuma sana, asa alipo vita picha ya jinsi kipanta akatavyo jiona kuwa ni shujaa, kwa kuweza kuiingiza familia yao kwenye matatizo kwa mala nyingine, na mbaya zaidi Adellah, alimsikia Kipanta mwenyewe akisema kuwa anaamua kumsingizia Rose ili amfilisi, kwakweli ulikuwa ni ucungu mkubwa sana.******


Saa kumi za jioni ndio mida ambayo Pross alihamka toka kitandani, huku akihisi njaa ina mchonyota, cha kwanza kabisa alitoa simu yake na kuipiga kwa Stellah, ambae alimweleza kuwa aendelee kusubiri kidogo, ata mstua, “maana wageni bado wapi” hivyo Pross akatoka nje ya kibanda chake, na kwenda kuwasha moto chini mwembe dodo, alafu akaanza kuandaa chakula maana njaa ilikuwa ina mcharaza kweli kweli, hivyo kijana Pross ambae ssa alizidi kunawili, na kupendeza, aliendelea kujipikia chakula chake, ikiwa na kwenda barabarani, kuchukuwa samaki wakavu aina ya kambale, ambao walikuwa wanapatikana kwa wingi eneo ilo, kisha akaja kuwa tengeneza kwaajili ya mboga.


Lakini basi wakati anaendelea kujipikilisha, akamwona Kipanta anaingia kwa mwendo wa uchovu, huku amekumbatia kifurushi cha chupa ya pombe ali, “kumbe we mpuuzi uwa aulindi ili shamba kabisa, kazi yako ni kudhurula mitaani, hivi si utaasababisha watu waje kuiba” alisema Kipanta bila ata salamu, akiwa mita kadhaa kabla ajamfikia Pross alie kuwa chini ya mwembe anaanza kusonga ugari, “shikamoo boss” alisalimia Pross kabla ajaanza kujitetea, lakini akupewa nafasi ya kujitetea, alikutana na lawama nyingi zilizo ambatana na masimango, “sasa kinacho fwata ni wewe kuondoka hapa, maana naona kazi imesha kushinda” alisema Kipanta huku akiwa anasogelea, kwenye gogo, “lakini boss nilikuaga, kuwa naondoka kidogo” alijitetea Pross, “lakini ukuniambia kama utakaa sikuzote hizi” aliongea Kipanta ambae alikuwa amesha fika pale gogoni, na kutupa macho jikoni, akaona sufulia la ugari lina chemka, aka tazama sufuria la pembeni, akaona samaki wanae elea kwenye mchuzi mzito, hapo aka jichekesha, “kumbe umesha fanya mambo, utatutosha kweli huo maana nina njaa” alisema Kipanta huku anajichekesha chekesha, “unautosha, ni mwngi sana huu” alijibu Pross, alie kuwa anendelea kushugulika na mapishi, ila wewe dogo, unaweza kuishi popote na ukaanikiwa, unaonekana unajiuma sana” alisema Kipanta uku akijikalisha kwenye gogoni, ukiwa ni mkao wa kula.*****


Yap, mama Pross alikuwa anaendelea shughuri zake pale nyumbani, kama ilivyo kawaida, aliuliza mboga na vitu vingine vingi vya gengeni kwake, akisaidiana na mdogo wake, na kuna wakati walikuwa wanazama kwenye maongezi, huku wana sukana, mama mdogo siku hizi, alikuwa moto mzuri, akuwa anaenda tena kutafuta wanaume, na kunywa pombe nyingi nyingi, kama alivyo kuwa anafanya zamani, “hivi dada unamkumbukaga shemeji kweli?” aliuliza mama mdogo, akiwa ana msuka dada yake, yani mama Pross, “yani uwezi amini, kuna wakati uwa najiuliza sijuwi alipatwa na nini, mpaka akaamua kutukimbia” alisema mama huyu, kwa sauti ya upole iliyoanza kuingiwa na unyonge, “lakini sawa ni ela zake, ila ange wakumbuka ata wanae basi” alisema mama Pross, kwa sauti ile ile ya masikitiko, “iala dada tushukuru Pross alibakia na sisi, vinginevyo tunge umbuka” alisema mama mdogo, huku wote wakiamini kuwa bwana Feruz anaishi maisha mazuri, huko aliko, “ulitaka kumwagia radhi mtoto wawatu” alisema mama Pross wote wakacheka, “usinikumbushe dada yani pombe siyo chai, nilijuwa nipo na shemeji yako” alisema mama mdogo wakiendeleea kucheka, “na una bahati mtoto ange juwa kuwa umefanya makusudi, lazima ange kutia” alisema dada mtu, “sijuwi ninge mtazamaje siku yapili, ila siku hizi ana nawili anakuwa mzuriiii!” alisema mama mdogo, “alafu anazidisha kutoa fedha nyingi, sijuwi anazipata wapi?” alisema mama Pross, huku wakiendelea kuongea ili na lile, na kusukana.******


Naam mida ya saa kumi na moja na nusu, Pross alikuwa ndani ya kibanda cha bati, ame jilaza kitandani, ni baada ya kuwa alisha maliza kula na kuosha kuosha vyombo, mida hiyo, Kipanta alikuwa amekaa nje ya kibanda, pale chini ya mwembe, ana kunywa pombe taratibu huku anafilia jinsi atakavyo, miliki mali za Rose, “asa lile gari, yani sijuwi nilikuwa nawaza nini, mpaka nikatoa million kumi na nane kumnunulia” aliwaza Kipanta ambae sasa alishaanza kulewa, pia aliwaza juu ya Rose kuwa mdogo wake Adellah, “kwamaana hiyo Rose akujuwa kama nimewai kuembea na dada yake?” alijiuliza Kipanta, ambae akuwaza kama kilikuwa ni kisasi, “alafu na huyu mpumbavu anajifanya kuni record ime kula kwake, sas wote nim wakanyaga, na nina mkomba kila kitu” alijisifu Kipanta, ambae sasa alianza kupata hamu ya kumweleza mtu, kiasi kwamba ata koo lilianza kumpwita pwita.


Wakati Kipanta anawaza juu ya hayo, huku nako Pross alikuwa anaona anachelewa kwenda mjini, maana bado alikuwa ajapigiwa simu na Stellah, kama aende au asiende, “we dogooo!” Pross alisikia sauti ya kilevi ya boss wake, kwanza aliona kama usumbufu, akaachia msonyo wa chini chini, na kukausha kimya, mala ikasikika tena sauti ya Kipanta, “we! dogooo!” safari hii, ilikuwa ya juu zaidi, “naam boss” aliitikia Pross, kwa sauti ya unyenyekevu, “ebu njoo dogo, unakaaje ndani kama utumbo, kijumba chenyewe kama banda la mbuzi” alisikika Kipanta kwa sauti yake ile ile ya kilevi, “nakuja boss” aliitikia Pross, ambae kiukweli akupenda jambo lile na dharau za bwana Kipanta, “haaa! una niwekea usiku bwana, unataka nini?, alafu unadharau hiki kibanda, wakati ume ng’ang’ania huku utaki kaa mjini” alisema Pross kwa sauti ya chini, huku anainuka toka kitandani, na kuvaa viatu vyake, alafu akatoka nje, na kuelekea pale chini ya mti, “ebu kaa hapa dogo, alafu wewe siunakunywa pombe, kwanini usinywe kidogo” alisema Kipanta kwa sauti ya kilevi, “mimi sinywa hizo kali, na kunywa wine” alisema Pross huku anakaa kwenye gogo pembeni ya Kipanta, simu yake ikiwa mkononi, “ok! tuyaache hayo najuwa demu wako atakupigia mkanywe pombe zenu za kichoyo” alisema Kipanta na kuweka kituo kidogo, akinywa funda moja la ile wisk, na kisha kuisikilizia kama vile ina mchoma maini, au utumbo, alafu akaendelea, “dogo nataka niku fundishe kitu, kuusu maisha, siyo unakaa kindezi ndezi” alisema Kipanta kwa sauti ambayo, ata wewe kama ndiyo unamsikiliza hakika usinge mtilia maanani, kwaku juwa ni mlevi tu!, “ujuwe wanawake ni watu wakuishi nao kwa hakiri sana, hivi una juwa demu wangu yupo wapi?” ……



aliuliza Kipanta huku akimtazama Pross, na usowake umechanua kwa tabasamu la kilevi, hapo zaidi ya tabasamu, Pross aliweza kuona ndevu za bwana Kipanta zilizo jawa na mvi, ilionyesha kuwa bwana Kipanta ata usmart wa kunyoa ndevu uli mshinda, “sijuwi alafu siku hizi simwoni kuja huku, na rafiki zake” alisema Pross ambae sasa alianza kupata hamu ya kusikiliza mafunzo aliyo taka kupewa, maana yalionyesha dalili ya kumuusu Rose, mwanamke ambae alisha peana nae dudu, kwa usiku kucha, na wali furahia usiku wao vizuri sana, siku ile ya christimas, “ata wezaje kuja wakati yupo mahabusu” alisema Kipanta kwa kujisifu, na kuanza kuelezea jinsi mambo yalivyo kuwa, “nili mnasa rafiki yake nika enda kutafuna, yeye akaja kujifanya kufumania, nika mtimua, lafu akajifanya kuni fungia vioo, wakati mimi nime mnunulia vitu kibao, mpaka lile gari, nyumba nime mjengea, nime mjengea maflemu kibao, nime mpa mitaji kibao, alafu leo aniache kilahisi hivi, sasa nime msingizia kesi, ya kuniwekea dawa kwenye pombe, na kesho ndiyo hukumu yake” alisema Kipanta kwa sauti ya kilevi, na kumshtua sana Pross, ambae alitambua kwanini akuwa anamwona Rose, kuja pale shambani kama walivyo kubaliana, “nita mfilisi kila kitu, na dada yake amejifanya mjanja, nime mkataa mbele ya hakimu, amebakia analia lia tu!” alisema Kipanta, na kumkumbusha Pross simulizi aliyo wai kusimuliwa na Rose, siku ile ya Christimas, “kwani we boss auna mke na watoto?” aliuliza Pross, swali ambalo lili mshtua Kipanta japo alikuwa amelewa, “yupo … yupo… mke wangu yupo bomba kinyama, yani akipita hapa ata wewe japo moto lazima unge kubari kuwa najuwa kuchagua mademu bomba” alijisifu Kipanta, “ok! sasa yeye anajuwa kama una mwanamke mwingine, na ulimjengea nyumba” aliuliza Pross na wakati huo huo simu yake ikaita, kutazama alikuwa ni Stellah, “demu wako huyooo nakupigia” alisema Kipanta, na wote wakacheka kidogo, huku Pross anapokea simu, “niambie mama” alisema Pross, huku wanatazamana na Kipanta, ambae akusikia maneno ya upande wa pili, ila alimsikia Pross akiuliza, “kwahiyo niende moja kwa moja mpaka pale pale pa jana?” kusikia hivyo Kipanta akacheka kidogo, mtoto hatari wewe” alisema kipanta kwa sauti ya kilevi sauti ambayo ilionyesha kuwa Stellah aliisikia, maana Pross alisikika akisema, “ni boss wangu huyo….. ok! nakuja, nikifika mbezi nitakupigia, …. sawa nakama ninjia ya huku nachukuwa piki piki” hapo Pross alimaliza kuongea na simu ikakatwa, alafu Pross akamtazama boss Kipanta, “sasa Boss wacha mimi nisogee mjini” alisema Pross, “we nenda tu! ila mimi kesho natoka mapema, nawai mahakamani, nikifanikiwa mambo yangu huku sito rudi, tuta wasiliana kwenye simu” alisema Kipanta ambae alimini baada ya kutoka mahakamani kesho, atakuwa na fedha nauwezo mkubwa sana, ikiwa pamoja na kumiliki magari nyumba maduka ya Rose, na kujinunulia simu ya kisasa, “ aina shida boss” alisema Pross ambae alijitwisha furushi, lake na kuanza kusogea barabarani, huku anatoa simu yake nakumpigia bodaboda, ili ake kumfwata.


Dakika chache baadae alikuwa tayari amesha kutana na boda boda na safari ya mjini imeanza, akiwa juu ya pikipiki, huku amefunga mzigo wakenyuma kabisa, Pross alionekana kuwaza sana juu yakile ambacho Kipanta alipanga kumfanyia, Rose, na kilicho muumiza zaidi ni kwamba aikuwa mala ya kwanza kwa Kipanta kuitendea uovu familia ya kina Rose, maana Pross alisha simuliwa na Rose kila kitu, ukweli roho ilimuuma sana Pross, mpaka akapanga kumsimulia Stellah, ambae walipokutana dakika alobaini natano mbele, Stellah, aligundua unyonge wa Pross, “jamani mpenzi, umechukia, nilivyo kuambia ukakae kwanza shamba niongee na rafiki zangu” aliuliza Stellah alie kuwa amelewa, huku wakiwa bar, wanapata wine na chakula, kuongeza nguvu na chachu ya kuingia chumbani, “hapana Stellah, ila kuna story moja ina umiza roho mpaka nashindwa nifanyaje” alisema PPross na kuanza kumsimulia Stellah, mkasa mzima juu ya kilicho tokea baina ya Rose na Kipanta, pasipo kujuwa kuwa Kipanta ni mume wa Stellah, huku Pross akitumua hakiri nyingi kuepusha kipengele cha kupeana dudu na Rose.


Ukweli japo Stellah, alikuwa amelwa kwa kiasi chake lakini simulizi ile ilimshangaza sana na kumshtua, “imanaana alitembea na dada mtu na kuzaa nae, kisha akamtelekeza na baadae kusababisha kifo cha kaka yao, na yeye akaoa mwanamke mwingine?” aliuliza kwa mshangao Stellah, “ndiyo na sasa anamsingizia kuwa alimwekea dawa, ili mfilisi kila kitu, na kumkomesha mke wake, ambae anasema anajifanya mjanja” alisema Pross na hapo Stellah, alicheka kidogo, “huyu mshenzi ata dharirika sana mwaka huu” alisema Stellah, pasipoPross kujuwa mama huyu ana maanisha nini, kisha wakatulia kidogo, “Sikia Pross kuna kitu mimi nataka nikushauri, ebu msaidie huyo boss wako” alisemStellah na kuanza kumweleza Pross kitu cha kufanya., ili kumsaidia Rose, maana ukiachilia Stellah, kushtushwa na unyama alioufanya Kipanta kwa Adellah, pia akupenda Kipanta afanikiwe, maana yeye angekuwa katika wakati mgumu, na lengo lake yeye ni kuona Kipanta analipia aliyo yafanya.*******


Naam siku ya pili saa mbili asubuhi, nje ya viwanja vya mahakama, watu walionekana wamefulika vibaya sana, watu wa kawaida kwa waandishi wa habari, kila mmoja alionyesha kuwa alitaka kujuwa tamati ya kesi ile ambayo siku za hivi karibuni, ili tawala sana mitandaoni, kuna wakati waandishi walionekana wakimzonga zonga Adellah, na kumwuliza anatabiri vipi juu ya humu ya mdogo wake,

“kuhusu hukumu tuiachia mahakama ila ukweli mdogo wangu, akufanya kitendo hicho” alisema Adellah, ambae leo alikuwa amevaa miwani meusi, kuzuwia wekundu wa macho yake ambayo alikesha akilia usiku kucha.


Lakini waandishi hao hao walipo mfwata ipanta na kumwuliza mwenendo wa kesi, aliongea kwa majigambo, “nazani ilo siyo la kuuliza, mtuhumiwa tayari amesha kosa la kujitetea, na leo ana ngoja hukumu yake’ alijibu Kipanta kwa sauti iliyojaa majivuno na kujiamini, “unazani ni kwanini mschana Rose, alialiamua kukuwekea dawa kwenye kinywaji” aliuliza mmoja wa waandishi wa habari, “ni visa vya kimapenzi, sababu niliachana nae kutokana na tabia zake mbaya, na yeye akaamua kufanya hivyo, akizania kuwa nitapoteza maisha, ili aweze kubakia na malizangu zote” alisema bwana Kipanta, kwa sautimile ile ya kujiamini, kama unge msikia kwa muda huo unge juwa kuwa kipanta ni mtu mwenye fedha nyingi, na wakati waandishi wanataka kuendelea kuhoji, ndipo watu wakatakiwa kuingia mahakamani, tayari kuanza kusikilizwa kwa kesi ya kwanza ambayo ilikuwa ni ya mschana Rose, kesi ambayo ilivutia watu wengi, kutokana na kuzagaa mitandaoni, wengi wakitegemea kuskia adhabu kali inatolewa kwa mschana Rose, kwa kitendo aliacho kifanya, ambacho wengi walitafthiri kama ni kitendo cha kinyama na cha udharirishaji ambacho kina itaji kukomeshwa.


Hapo watu wakaingia mahakamani, huku wakitaani kuona Rose anapewa adhabu kali, kasolo Adellah na Joyce pekee ndio walikokuwa wanatamani kuona Rose anashinda kesi ile, japo matumaini yalikuwa madogo, hivyo Adellah, akiwa na Joyce wakaingia mahakamani, na kukaa karibu kabisa na Rose, huku muda wote Adellah, akimshika Rose mikono, na kushindwa kuzuwia machozi yao.*******


Upande mwingine mida hii ya saa mbili za asubuhi, bwana Waghora yeye alikuwa amesha toka magetoni, akiongozana na Sinder, mpaka stendi ya mbezi, ambapo waliachana, Sinder akipanda gari za kwenda Kibamba, kwalengo la kushukia, Luguruni, na Waghora akaelekea, upande wa stendi ya malamba mawili,a mbapo aliipita na kuvuka barabara, alafu akaelekea kwenye tawi la benk la NMB, moja kwa moja akajiunga kwenye foleni ya ATM ambayo ilikuwa na watu wachache sana, Waghora alitulia kwenye foleni kwa muda mchache, kisha, ikafikia zamu yake, nae akaingia na kuchomeka card yake kama machine ailivyo mwelekeza, lakini basi ilikuwa ni tofauti na mala ya mwisho alipochomeka card hii, na kushindwa kuipatia password, leo card aikusoma kabisa, akaicancer na kukuichomeka tena, mambo yakawa vile vile, akaicancer tena na kuichomeka kwa mala ya tatu, “kaka vipi, kama kuna jambo lina kutatiza ni bora uombe msaada” alipiga kelele dada mmoja alie kuwa nyuma yake, pamoja na wengine kadhaa, ambao walikuwa nasubiri huduma, “ungekuwa na haraka si ungekuja asubuhi” alisema Wagora huku akicancer tena na kuichomeka card kwa mala ya nne, hapo ata wateja wengine waliingilia kati na kupaza sauti za malalamiko kuwa wanacheleweshwa, lakini ili ni sikio la kifo, Waghora aliendelea kuchomeka na kuchomoa, card ile ambayo ilisha mweleza kuwa inamatatizo.


Kitu ambacho waghora akukijuwa ni kwamba, tayari simu toka makao makuu ya benk hii mkoa wa pwani walisha piga simu kwenye tawi la la mbezi, na kueleza kuwa kuna mtu anatumia card iliyo reportiwa kuwa imeibiwa, na camera zimesha mnasa hivyo haraka sana wawai kwenda kumkamata hapo kwenye ATM, na pamoja na maelezo hayo pia walituma picha za mtu huyo.


“Bwanaeee! kama card inamatatizo, ingia ndani” alisema mmoja wa wateja waliokuwa wana msakama Waghora mbae sasa aliona isiwe shida, alichomoa card na kutoka nayo kwenye izimba cha ATM, huku anapishana na yule dada wakwanza kumpigia kelele, ambae alimkata jicho kali, “samahani kaka vipi card yako inamatatizo?” alishtuka Waghora akiulizwa na mtu mbele yake, ile kumtazama, alikuwa ni kijana mtanashati ndani ya sale za wafanyakazi wa benk, “hapana nazani aina salio” alisema Waghora, huku kiendelea kutembea, kueleka kwenye lango la kutokea nje, ambalo lilikuwa na polisi wawili wenye silaha aina ya smg, maana alijuwa kuwa akiambiwa aonyeshe ile card na ikionekana siyo yak wake, lazima ata kamatwa.


Lakini alisha chelewa, maana yule mfanyakazi wa NMB, ambae alipanga kutumia ujanja kumwingiza ndani, kisha kuwaita polisi, alipoona Waghora anatoka na kuna dalili za kumkosa,a akaona isiwe shida, akawatazama wale polisi, na kuwapa ishala kuwa wamkamate Waghora, ambae sasa alikuwa anakaribia, lango la kutokea nje ya uzio wa eneo la benk, “simama hapo hapo” ndivyo alivyo sikia Waghra, hapo akajuwa kuwa tayari amekwisha, na akuwa na ujanja, akasimama mala moja, huku akiwatazama wale polisi, wenye silaha zao mikononi, “huyu bwana anatumia card ya wizi, hivyo tunaomba asachiwe, na hivi tunavyoongea tayari kuna polisi wa kituo cha mbezi, wapo njiani wanakuja, kumchukuwa” alisema yule jamaa mwenye kuvalia sale za benk, ma hapo aikuwa na haja ya kusachi bwana Waghora, maana card alikuwanayo mkononi.******

INAENDELEA

Post a Comment

0 Comments