Walijitaidi kuogelea kwa alaka sana, mpaka walipofika chini, huku PAPA nao walikuwa nyuma wakiwa winda, ili watakapo
wapata, kiwe ndicho kitoweo chao cha siku hiyo, basi binti BERALITA na kijana MWAIPAMBA, wali weka ushirikiano kati yao ili
hali waweze kutoka kwenye janga hilo, basi walipo ona PAPA wakiwafata kwa kasi, nao walizidi kutafuta njia za kuwakwepa,
lakini PAPA hao walikuwa wanavutia harufu, kuwakimbia ilikuwa kazingumu sana, na ndipo binti alipofikiria jambo, akatumia
ishala kumpatia kijana MWAIPAMBA, nae aliafiki alichokuwa akikusudia binti huyo basi, nao walianza kupanda juu, huku
wakitizama juu, kuangalia kama kuna chombo chochote, kati ya vile walivyo kuwa wakisfiri navyo, watakapo ibukia ili iwe
vyepesi kuingia ndani nakunusulika na wadudu hawa, basi walizidi kutupa macho na kuona kitu kikiwa kina enda kwa kasi kidogo
juu yao, na ndipo walipoongeza kasi ili kuwai kile walicho kuwa wamekiona nakuzani ni chombo chao, basi walipiga maji
kwakasi kuelekea juu ya uso wa bahari, na walipo karibia tu! waliona ni PAPA, basi hofu iliwatanda, wakati huo yule PAPA
ndipo alipogeuka na kuwaona binti pamoja na kijana, wakiwa kwenye mshangao, na ndipo alipo wafata kwa speed, huku akiwa
kafungua mdomo wake, kwani ulikuwa na uwezo wa kuwala wote wawili.
BERALITA pamoja na kijana MWAIPAMBA walipoona hivyo hawakuwa na ujanja na kushikana mikono na kufumba macho, wasione wavyo
tafunwa, walikuwa wameshakata tamaha kabisa, baada ya kuona kabakisha hatua chache kufika walipo na kuanza kusali,kila mtu
sala anayaijuwa yeye, Wakati wakiendelea kusali huku wamefumba macho, walishangaa kuona PAPA huyo anachelewa sana
kuwafikia, na walipo fungua macho, walishuhudia yule PAPA aikwa amerushwa juu hukuakiwa ametapakaa damu, akionyesha kukatwa
na kitu kikali sana, YOROBI alishituliwa nabinti mmoja, mle kwenye jahadhi akimwambia atazame upande ule, ile kutazama
baharini, alishangazwa na alichokiona, PAPA mmoja alirushwaa juu, na kuchanjwa chanjwa, na vitu vyenye ncha kali sana, kwani
waliona alivyo kuwa akipiga piga mkia na bawa zake, YOROBI nae kuona hivyo, akajuwa kuna hali ya hatari ina wawinda,
alichukua siraha yake na kuiweka mkao wa vita, kwani hali alioiona hapo ilikuwa ya vita tu! na kuamini binti pamoja na
kijana MWAIPAMBA hawako nao tena, katika dunia hii ya tatu, yaani wameliwa na PAPA wa baharini.
Basi vijana wote walikaa mkao wa vita, ni kwaamri ya kiongozi wao, ali waambia wawe tayari kwalolote nao waliitika, sasa
waliweza kuwaona jinsi PAPA wa baharini walivyo chachamaa, wakajikusanya sehemu ile yenye damu ya mwenzao, lakini kitu cha
hajabu, walionekana kuzidi kushambuliwa na kitu kisichoonekana, machoni kwawakina YOROBI, hapo wote waka duwaa, nakushindwa
la kufanya, hakuna alie wafikilia wakina BERALITA maana waliamini wamesha kufa......
Ndipo walipoanza jitiada za kuweka sawa vifaa vyao, na kujiimalisha kwaajili ya mapambano hayo, ambayo hawa
kuyatarajia, kwani pindi walipo pita njia hiI wakati wakuja, walikuta iko safi bira buguza yoyote.
Basi nae YOROBI aliamuru vijana kukaaa tayari, na alipoamlisha kwa mara ya.mwisho vijana walianza kupambana na hao
PAPA.waliokuwa wametapakaaa kote na ndipo vijana kutupa mishare na kila siraha, ilionekana itawazuru maadui zao (PAPA).
Hawakuamini kilichokuwa kikiendelea, kwani PAPA hao walionekana kuwa kama wametumwa, pengine walihisi ndivyo sivyo, lakini
mawazo yao yote yalikuwa hapo, pindi walivyoona mapambano yamekuwa na changamoto kali, walipokuwa wakiendelea na mapambano
hayo, waliona kwa mbali watu wakiwa wana piga maji, huku wakiomba msahada, walionekana wamechoka sana, ndipo YOROBI alipo
weka macho kwenye lenzi kali, na kuwaona binti BERALITA na kijana MWAIPAMBA wakiomba msaada, basi nae aliwaonyesha wenzie
waliokuwa nao pembeni yake, na kuamuru chombo kielekee mahali walipo, nao kuona hivyo vijana waliongeza kasi, ili kuwawai
wasije kuzulika na PAPA hao, jitiada zilionekana pale walipo wakaribia, nao waiongeza kupiga maji ili kufikia chombo, binti
BERALITA alionesha juhudi kali huku akimsaidia kijana MWAIPAMBA kumkokota, kwani kwa kile kichapo alicho mpa, kilikuwa cha
huakika, kilimlegeza sana nakumfanya achoke mapema, kwakweli alikuwa mwingi wa huruma na utu binti huyo, walifika mpaka
kwenye chombo walimokuwa wenza, lakini kabla kupanda kwenye chombo hicho, waligeuka wote wawili na kuutazama msitu wa PAPA waliokuwa wakiwakizidi kuangamizwa na kitu kisichoonekana, ndipo
binti BERALITA alipo toa pumzi ndefu kama ameshusha mzigo mzito, alitazama tena walipotoka na kuto amini kilicho tokea huku
wakiwa salama, tena bila hata majeraha mengi, sana maana aliye umia sana, alikuwa ni kijana MWAIPAMBA.
Basi nao waliingia ndani ya chombo, huku kwa mbali, wakianza kuona kiumbe flani wakiona, kikiwasurubisha wale PAPA, kila
mmoja wao kwenye chombo, alibaki akiwa na butwaa, kwani baada ya muda mchache, PAPA wote walionekana kutulia wakielea juu ya
bahari hiyo, wakiwa hawana uhai, huku wakiona maji yakiendelea kuchemka kuonyesha kuna kuvumbi bado kinaendelea, watu wote
wakatulia kusubiri kuona, kitu kitachoibukia pale, huku vjina wawili hawa BERALITA na MWAIPAMBA, wakipewa huduma ya kwanza,
watu hawawakiwa wame kodoa macho yao, waliona na kitu cha hajabu kwenye maji, kila mmoja alistuka...
Basi walipokuwa wakiendelea kuwapa huduma huku waliendelea wakishanga, nini kinacho wamaliza wale PAPA, wote walitazama macho kuangalia nini kitatokea pale wanapoona mapambano, lakini hawakujua ni ya baina ya upande upi na upi, basi YOROBI alingoja na kukaa akionyesha umakini mkubwa, kwa hali aliyoiona ndani ya maji, huku akihisi kuna tukio litatokea, ambalo siyo lakawaida,Naam wote wakiwa wanatazama baharini mala wakaona, bahari ikiwa ime tulia na mizoga ya PAPA ikiwa ina elea juu ya uso wa bahari, kisha wakaanza kuona kiumbe kikiibuka toka ndani ya maji, kadri alivyo zidi kuibu ndivyo walivyo zidi kumwona izuri, alikuwa ni binadamu, tena ni wakike, huku akiwa ameshika siraha, mfano wa kisu kilicho jikunja mbele inaitwa mundu, (kuna makabila wanaita chikwakwa) uso wa mwana mke huyu ulionesha kuwa bado ni mwingi wa hasira, walipo mwangalia vizuri ndipo walipo gunduwa kuwa yule wanae mwona hakuwa bina damu ila ni samaki mtu, kwa kiswahili anaitwa NGUVA, kwa ENGLISH anaitwa MAILRMAID, hakuna ambae hakutambua kuwa yule ndie aliekuwa akipambana na wale PAPA, nakuwaokoa wakina BERALITA, binti Nguva alikuwa amesimama akiwatazama nakuwaonyesha ishala flani, ambazo wao hawakuzifahamu, kiukweli nnguva yule alikuwa na nia nzuri kwao na lengo lake ni kuwajulisha kuwa wasi pite kule wanako elekea, Ndipo alipoonekana akinyoosha mkono wake na kuwaonesha kuwa bado kazi ikiendelea, kwani PAPA walikuwa wengi, na alipokwisha kuwaonesha mara gafra PAPA.nao waliongezeka haraka sana, na kuwafanya vijana waliokuwa kwenye JAHAZI wakiongozwa na YOROBI, huku wakihofia sana juu ya kupoteza, uhai wao hapo kila mmoja akajipanga tayari kwa mapambano, pasipo kuogopa kufa au kuliwa na PAPA, hapo bkila mmoja akitumia silaha za jadi, wote walitumia zana zao mpaka zikawaishia. kasolo YOROBI ambae hakutumia bastola yake,
NGUVA huyo kumbe alikuwa akilinda haki za wanyonge, ambao hawakuwa na msaada baharini, sababu iliompelekea mpaka awasaidie watu awa hakutaka kuonakuona wakimwaga damu zao bila hatia yoyote, aliamua kutoa msahada huo, ukweli alifanya kazi kubwa sana, pindi alipokuwa akijitolea kuokoa umati huo.
Basi binti NGUVA alianza kupambana mno, akijitahidi kuwazuia PAPA wale wasiingie kwenye chombo, na kufanya mahafa, kwa watu waliokuwemo ndani ya chombo hicho. kweli tuna fanana nywele, lakini siyo hakili, wakati hayo yakiendelea, YOROBI alikuwa ametulia, akitafakari jambo juu ya yule Binti Nguva, uwezi amini alichokuwa akiwaza YOROBI, mawazo ya ke yalikuwa ni kumzibiti haraka sana BINTI NGUVA, akiamini kuwa atakapo maliza, kuwa angamiza wale PAPA ataamia kwao,......
Pindi alivyokuwa akiwaza hayo kijana YOROBI alijitoa ufahamu na kuanza kuikoki siraha yake na kuirudisha tena sehemu za kiuno chake, kiukweli wenzake hawakujuwa kama alitaka kufanya jambo ambalo halikupaswa, hata kufanya kwa mda huo, basi nae aliendelea kumkazia macho NGUVA huyo, ambae bado aliendelae kupambana na PAPA, huku matazamio yake yalikuwa ni kumpoteza kabisaaa NGUVA huyo. wakatihuo akiwa hajuwi hili wale NGUVA huyo aliendelea kusafisha bahari, huku akiwatembezea visu wale PAPA, basi alijitaidi sana kufanya hivyo huku malengo yake ni yake ni kuokoa jahazi la watu hao, nakuwaelekeza njia yakupita, kwani hakupenda kuona damu ya mtu ikimwagika maeneo hayo, alipo maliza na aligeuka kwenye jahazi walilokuwemo binti pamoja na kijana YOROBI, huku akitaka kuwaelekez njia yakupita, na kuwatakia safari njema.kwani kazi ilikuwa imekwisha aliyokuwa akiifanya, kuangamiza wote waliokuwemo eneo la bahari hiyo. PAPA wote walipotea kwa kichapo alicho wapa NGUVA huyo huku wengine wakikimbilia mbali, ili wasije kulika kwa kitu chochote, nao walitimkia mbali sana.
Ndipo kijana YOROBI kuona nguva akiwatazama, uoga ukamshika akijuwa kuwa zamu yao imewadia, hakutaka hata kupoteza mda, nae alitoa mguu wa kuku (bastora) nakuielekeza alipo binti NGUVA, ile kuona viele binti BERALITA, kitendo cha YOROBI kumuoneshea NGUVA huyo aliye angaikia uhai wao walipokuwa ndani ya maji, basi alitoka speed mahari alipokuwepo na kumfata alipokuwepo kijana YOROBI, kuzuia kitendo hicho, lakini mbio zake hazikuzuia kile alicho kusudia YOROBI, kwani alipokuwa akikimbia binti huyo na alipofika tu! alikuta kaisha fyatua risasi, ambayo ilienda moja kwa moja mpaka kwenye bega la NGUVA huyo, huku nae NGUVA alishangaa sana kwa kile kitendo alichofanya kijana YOROBI, kiukweli hakikumpendeza, alishikwa na gasira kali sana, akajiuliza "nawafanyia haya yote kwaajili yao, bado wana nitendea haya"
Basi binti BERALITA alipoona hivyo, alimsukuma kijana YOROBI pembeni na kumtazama sana NGUVA, kama ame dhurika kiasi gani, alimwona akipiga kelele kuashiria risasi ile imempata barabara. Binti BERARITA alimlaumu sana kijana YOROBI, kwa kitendo hicho huku kijana YOROBI, akijiona kafanya jambo la kishujaha, ndipo alipokaa chini akimsikiliza binti BERALITA akifoka sana juu ya tukio, yeye hakumjari zaidi aliwaimiza vijana wake wazidi ku piga makasia nakuinuwa tanga ili jahazi liongeze mwendo, haya sasa ni atuwa gani atachukuwa Binti Nguva? isome kisha nijulishe ili nikujuze kuamuzi alio chukuwa Binti Nguva
Vijana nao walifanya kile alicho sema kiongozi wao YOROBI, kwa kuchochea chombo kile na kuanza safari, huku binti BERALITA akimsihi YOROBI japo amwonyeshe yule binti NGUVA aliye wasaidia, ishala ya kumuomba samahani kwa kile kilichotokea, lakini YOROBI hakuwa tayri kufanya hivyo kwani alijihisi yupo sahii kumtandika risasi, binti NGUVA, ndipo binti BERALITA yeye pekee ndie aliye inuwa mkono wake nakuupunga kwa binti NGUVA, kumuaga na kumpa ishara nzuri ambayo hata NGUVA yule nae alijibu kwakunyoosha mkono juu ana kuupunga.
binti NGUVA alishindwa kuwatahadhalisha juu ya huko waendako, alibaki akitazama mabaki yalio salia kwani alihisi kazi bado ya kupambana na PAPA wale, lakini alipoona hali iko shwali wala hakutaka kuangaika, na ndipo alipo jitizama kidonda chake, ambaacho kilianza kuhuma kwanguvu akashikilia jelaha, na kuangalia JAHAZI kwa machungu, kwani alipata tabu ya kupambana nao lakini hawakuona kazi aliyokuwa kafanya, na kumzawadia kidonda ambacho hakusitahiri kukipata, basi nae hakutaka kuonesha kinyongo kwao, alibaki akijisemea moyoni, "hawa ndiyo binaadamu, nilikuwa nawasikia tu," alimkumbuka sana binti BERALITA kwani ndie aliye onesha kuwa anafahamu mchango wake alioutoa wakati huo.
kwenye jahadhi nako, BERALITA alibaki akimlaumu sana YOROBI, kwa kitendo alichofanya kwa binti NGUVA, alimkumbusha kuwa ndiye aliye wasaidia yeye pamoja na MWAIPAMBA, na kumuelezea vizuri juu ya alichofanya, mpaka sasa wao ni wazima, YOROBI alichoshwa na kelele za binti huyu, akamtazama kwa mcho makali sana, hakutaka kuongea mengi, zaidi ya kumuomba asirudie tena kuobgea upuuzi wake, akidai yeye anaamini vipi kuwa yule bint alikuwa nimwema kwao, "mtu akikusaidia japo na wewe muoneshe shukrani" maneno hayo aliyatamka binti BERALITA, kwasauti ya upole yenye hisia kali, huku akimtaka sana YOROBI kuacha visa na pindi aonapo msahada, asitie jeuri zake maana alionekana kuwa kama BEPARI, kumzidi mpaka kiongozi wao chifu.
waliendelea na safari yao huku ikionekana kuwa yenye mikosi, sana licha ya kila mmoja wao kujipa matumaini juu ya kufika, lakini kukweli hali ilikuwa mbaya kwao, safari ya kurudi kwenye makazi yao ilipo kuwa ikiendelea,lakini akuna ata mmoja aliekuwa anajuwa, wanapo pelekwa na mfalme huyo, maana siunajuwa kwenye maji ataukigeuka ulipo toa wewe uelewi labda uwe na compas,ndipo kijana MWAIPAMBA nae alipo changia juu ya swala alilokuwa akipewa somo YOROBI na binti BERALITA, huku akimwambia kile kilichotokea ndani ya maji, na msaada mkubwa alikuwa ni huyo NGUVA, nae MWAIPAMBA alimlaumu, pia huku akimsihii asije fanya tena hayo, kamaita watokea tena mbele ya safari, basi nae alipoona hayo nae YOROBI alikubaliana nao, na kuwaomba radhi juu ya kile kilicho tokea, basi nao hawakutaka kujibizana basi yaliisha na kila mmoja wao kuelekea kwneye sehemu yake ya kukaa, safari ilikuwa imepambamoto, hivi huko wanakokwenda kuna nini?
Basi kila mmoja wao alurudi mahali pake na kuangalia chombo kikichana maji huku kikisonga mbele, ili kufika hitimisho
la safari yao, Basi kijana.YOROBI aliendelea kuongoza vijana wenzake, kukipa nguvu chombo ili wawai safari, yao ndipo nae
alipo tulia, na kufikilia kile alicho ambiwa na binti BERALITA juu ya kufanya makosa kwa binti NGUVA, ane alifikiria sana
nakukili kimoyo moyo, huku akiapa mwenyewe, hatofanya tendo kama hilo endapo akiona NGUVA yoyote akiwapa msaada.
binti BERALITA alikuwa akitizama sana maji huku yeye akifikiria juu ya safari yao, ambayo misuko suko na vijimambo,
vilivyokuwa vikiwaandama kwenye safari yao, basi alifikilia sana, juu ya hayo yanayotokea, kwani lengo lake ni kufika kwenye
kijiji chake salama, hakufahamu ya kuwa walikuwa wameuzwa na licha ya kudanganywa sana, nae alikuwa na imani ya kufika kwao
basi jioni iliingia kwa kasi, kwani matazamio yao hayakuwa ya kulala kwenye maji, ila vile vikwazo vilivyokuwa vikitokea
njiani vilifanya mpaka giza kuingia wakiwa ndani ya maji,
Waliamuwa kuwasha taa, kwenye jahazi lao, huku nae alikuwa nataa yake ndani ya begi lake, nae alipoona wakiwasha taa, nae
aliwasha ili apate mwanga maeneo yalio mzunguka, huku akilinda usalama wake kwani toka kijana MWAIPAMBA kufanya tukio, lile
hakupenda tena itokee juu yake, binti BERALITA.
Basi nae alikuwa makini sana, kwani hakutaka tena kuamini mtu, bali kujiamini yeye mwenyewe tu, kwani wote walikuwa ni
watumwa, nahakilizao uwa wanazijuwa wenyewe, ndipo kwa mbali aliona kitu kama mwangaza flani, lakini hakutaka kujifanya
kimbelembele, kuwa kaona kijiji chao, basi alikaa kimya, akiamini kuwa nawenzake watakuwa wameona, maana sasa likuwa
zikionekana taanyingi sana walizidi kukisogelea, huku akitafakali ule ni mji gani, kwani kulionekana kuwa ni mji mkubwa na
siyo kijiji kama alivyo zowea, kwani taa ziling'aa sana, na kuwaka kila kona, nae akaamua kutulia, mpaka atakaposikia tamko
kutoka kwa kijana YOROBI,
kijana MWAIPAMBA nae alikuwa amekaa pembeni, nyuma ya mrembo wetu, alibaki akimtizama sana binti BERALITA, akimtafakari
binti huyu maana siyo wa kumchezea, asa kwa kile kichapo alichopatia ,hato kaa na kumsahau binti huyo, alipokuwa akimtizama
alimpa heshima zake, kimoyo moyo huku akitupa huusika aliokuwa kauvaa juu ya binti, japo kuwa ni mdogo kuliko kwakw, lakini
kwake ilionekana tofauti sana, na kuwa kinyume chake,...
alibaki akimtizama sana binti BERALITA, akimtafakari binti huyu maana siyo wa kumchezea, asa kwa kile kichapo alichopatia ,hato kaa na kumsahau binti huyo, alipokuwa akimtizama alimpa heshima zake, kimoyo moyo huku akitupa huusika aliokuwa kauvaa juu ya binti, japo kuwa ni mdogo kuliko kwakw, lakini kwake ilionekana tofauti sana, na kuwa kinyume chake, safari ilizidi kusonga mbele, binti BERALITA alianza kujiliwaza kwa kuimba wimbo ambao hata kijana MWAIPAMBA alipousikia tu alivutiwa nao, lakini cha kushangaza hakuweza kumsogelea zaidi, sababu alitokea kumuogopa sana binti huyo, kwa kipigo ambacho hato sahau miaka nenda rudi, basi alicho amua ni kusaidia kuimba wimboule sambamba na mrembo BERALITA, MWAIPAMBA alizidi kuimba kwa sauti ya chini huku akimfatisha binti BERALITA. YOROBI alizidi kuwa amuru vijakazi wake wafanye haraka kwani safari ilionekana ya kutumia muda mrefu sana, huku giza nalo lilitanda, nakusaidia zile taa wanazoziona mbele yao wazione vizuri, huku kila mmoja wao akiwa na hofu juu ya kulala ndani ya maji, huku wakijionea visa na mikasa inayotokea, walianza kupata matumaini ya kufika mapema sana kwenye kijiji chao, na ndipo YOROBI alichukua kifa chake cha kutazamiambali, ambacho kina uwezo wa kuona kilomita ata 20, kwenye maji, na kujua wamefikia wapi, wahenga wanakiita jicho la jini, basi nae alifanya hivyo hivyo, alipoweka tu jicho lake kwenye kionw mbali, akaona kitu ambacho kilimshangaza sana, hakuamini alicho kiona kwa wakati huo, akapachika tena ilikujilidhisha, ndipo alipoona vizuri tena kwa mara ya pili, taa zikimulika kwakung'aa sana. Ndipo alipo wageukia wenzake nakuanza kuangua kicheko, huku akiwachanganya vijakazi wake, na vijana hao walimuuliza "vipi kiongozi kulikoni? mbona unacheka mwenyewe?, tujuze nasi tucheke pamoja na wewe" nae alijibu kwa kujiamini na kusema "haaaaah nimeona kitu ambacho hata nikiwaambia, mtafurahi sana, kwakifupi lisaa limoja mbele tuna weza tukawa tumefika" kauli hiyo ilifwatiwa na shangwe na Vicheko, vilitawara mahari pote, huku sasa ule wimbo wa BERALITA, ulikuwa ukiimbwa na karbia nusu ya jahazi, safari ilizidi kuendelea nawakazidi kusogea, dakika chache baadae, walianza kuona vizuri kabisa bila kutumia kifaa cha jicho la jini, walifanya sherehe, huku wakisahau yaliopita kuwa bahari hiyo ilikuwa ya mahajabu sana, basi walizidi kuongeza kasi ya kukifata kijiji au mji huo maana ulionekana ni kama mji wakisasa, matazamio yao ni kufika haraka, kwani safari iliwachosha huku chakula nacho ni chashida, walishindia mkate mdogo kutwa nzima, binti BERALITA waki wote, akiyashuhudia, hayo nae alitoa tabasamu, ambalo lilimchanganya akili kijana YOROBI, huku kijana huyo alijionesha yuko bize na shangwe za vijana hao. muda ulizidi kuhesabiwa na kijana YOROBI, huku mkadilio wake ni kufika yalikuwa ni kutumia saa limoja au moja na nusu, huku akijitamba kuwa ataonekana shujaaa pindi washukapo ndani ya JAHAZI hiyo. wakati bado watu wana shangilia huku wakiona kile kijiji au mji wanasogelea kwakasi, lakini YOROBI gunguwa jambo lakushangaza juu ya mji ule, kwanza kabisa..
wakati bado watu wana shangilia huku wakiona kile kijiji au mji wanasogelea kwakasi, lakini YOROBI gunguwa jambo
lakushangaza juu ya mji ule, kwanza kabisa, jinsi awalivyokuwa wanausogelea ulemji, japo mwendowao ulikuwa wakawaida, lakini
walionekana wakiusogelea kwaharaka sana, kingine mwonekano waule mji, nitofauti ya alivyozowea kuuona, Basi walizidi
kukata maji, huku kelele za shangwe, zikichangia kuwapa nguvu ya kuendelea na safari yao, wakiamini inaenda kufika tamati,
kufika mahari walipokuwa wakienda. ndipo binti BERALITA,alipojipa moyo kuwa mambo yako sawa, ile kutazama vizuri, mbele
zaidi, aliona wamezidi kukaribia, alizidi kuimba kwa hisia, akisidiwa na wenzake, huku moyoni mwake akiwa mwingi na shauku
ya kukanyaga aridhi yao, kwani kilikuwa ni kipindi kirefu sana, tangu atoke kwenye aridhi yao,
YOROBI aliendelea kuwaahimiza vijakazi wake, kufanya haraka kufikisha chombo inchi kavu, kulikuwa na wengine wakisita
kufanya upesi kufikisha chombo hicho, lakini akilini mwake alikuwa ikiwaza sana, na huku kichwa chake kikiwa kimejaa sifa,
mpaka kikataka kuonekana kupasuka, kwa sifa alizokuwa akizitaka pindi atakapo shuka na kuwafikisha watumwa kwenye ngome yao.
pindi watakapo fika tu atapandishwa cheo, na kumpa ngazi kubwa sana lakini huku akiendelea kuwaza hayo, alishangaaa kuona
kitu kidogo kikitoka kwenye maji na kufika mahari alipo na kuzama tena, ndani ya maji hilo tukio lilimshangaza kijana huyo,
huku ajui nini afanye kwani tukio hilo aliliona mwenyewe tu!, na kuwaza sana kiashirio cha hilo tukio, lakini alitupa kule
mawazo hayo chini, na aliposikia shangwe zikiendelea, alijawa na furaha tele, huku na kule alisahau hata tukio lilitokea
mda mfupi tu na kubaki akitazama mbele nakuona viashilio vyote vya kuwa wamefika.
Upande wa binti BERALITA, yeye alikuwa akiendelea na nyimbo zake, huku akiwa akimkosha sana kijana MWAIPAMBA mpaka kijana
huyo aliona kuvunja ukimya na kumfata binti huyo, uku akiendelea kuimba, ili apate kufurahia pamoja, kuwa wemefika safari
yao, basi nae alifanya hivyo kwa tahadhari sana, maana alijuwa kitachotokea, endapo atakosea kidogo, lakini hatimaye
alimfata, kumbe binti BERALITA hakuwa na mawazo hayo, aliyokuwa akiwaza kijana MWAIPAMBA, yeye alikuwa kawaida tu, yale ya
nyuma alikuwa ameyasahau, basi nae alipomuona tu kijana MWAIPAMBA ..
ITAENDELEA
0 Comments